url
stringlengths
22
161
text
stringlengths
23
18.2k
https://nation.africa/africa?utm_source=menu&utm_medium=drop_down
South African former finance minister Tito Mboweni dies at 65 Tito is a pivotal figure in the nation’s transition to democracy and a champion for labour rights. PRIME East Africa corporate deals dip 18pc on low Kenya activity Deals data compiled by advisory firm I&M Burbidge Capital shows that the count fell to 73 between January and July from 89 in 2023. Uganda selects Turkish firm for Malaba-Kampala SGR In 2013, Uganda, Kenya, Tanzania, South Sudan and Rwanda broke ground on the construction of the SGR to connect member states. When DRC was self-sufficient as a cultural state How 1970s bid to free the people from colonial legacy defines the identity of DR Congo to date. The untold story of Nanyuki’s Mt Kenya Safari Club It’s membership was uber-exclusive; then the FBI started investigations after learning Mafiosi members. On land, Mugabe walked path other African leaders would not But he and his cronies abused the reform process by taking some of the choice parcels for themselves
https://nation.africa/kenya?utm_source=menu&utm_medium=drop_down
PREMIUM Gachagua's ouster: Kenya's 2027 power shift? The fall of a kingpin or the rise of new alliances? PREMIUM AUC chairman: Why this could be Africa’s most important election The African Union should elect a visionary leader capable of transformative change and dramatically reducing poverty. The making of a TikTok sensation: Maureen Kibui's rise as Mama Morin How did a university student's imitation of her mother become a cultural phenomenon? PREMIUM What Kericho governor faces in Senate trial Governor Erick Mutai's fate hangs in the balance as the Senate prepares for a crucial impeachment hearing. PREMIUM How KDF's Somalia incursion changed face of the military Major improvements in training and equipment since October 2011 have boosted the troops' ability to defend the nation from external aggression. PREMIUM Exposed: Kenya’s underworld of gemstone smuggling where foreigners call shots Foreign nationals, some only holding tourist visas, have infiltrated the gemstone market. Is the stock market still a way to make money? Disenfranchised and battered by a decade of disappointing returns, little to no listings and falling share prices, many investors have lost faith in the Nairobi Securities Exchange EXPLAINED: Depression and anxiety—Not what you think You may appear happy yet are depressed. Dr Muthoni Karanja, takes host, Sheryl Blessing on how to identify triggers to help combat depression and anxiety. To sue your doctor or hospital? Health lawyer, Margaret Nyambura takes us through medical negligence from a legal perspective PREMIUM Western Sahara issue threatens Morocco’s business deals The Western Sahara region was initially a colony of Spain but after the colonialists departed, it was administered by Mauritania and Morocco before Morocco claimed its territory. PREMIUM Mutua: Why Gachagua was impeached Mr Gachagua did himself no favours by appearing arrogant and dismissive of his boss President Ruto and MPs. Bureaucrat banned from travelling to South African for lavish Birthday A top government official's extravagant birthday plans in South Africa come crashing down. PREMIUM Kenyan female wine tasters shine at World Tasting Championship Kenyan wine tasters have outperformed traditional wine powerhouses at the Wine Olympics. The making of a TikTok sensation: Maureen Kibui's rise as Mama Morin How did a university student's imitation of her mother become a cultural phenomenon? A weekend in the life of a taxi driver Business begins to peak on Thursdays when those that patronise bars begin to unwind and ease into the weekend. Barry Otieno announces bid for FKF presidency He said his campaign will be anchored on implementing four pillars.
https://www.monitor.co.ug/uganda?utm_source=menu&utm_medium=drop_down
PRIME Atiak Sugar Factory: Billions spent, no production When machines at the factory first started roaring over a decade ago, its senior management pledged to turn the venture into “an engine for development to support the livelihoods of vulnerable... PRIME How wooden houses can transform Uganda's housing crisis Wooden houses can position Uganda for a sustainable future by addressing the housing crisis through cost-effective, eco-friendly construction, reducing carbon emissions, and promoting responsible... Take children to schools you can afford, Nabbanja tells parents Highlighting the government’s commitment to ensuring every child has access to quality education, the Prime Minister emphasised the vital role education plays in shaping the nation’s future Tayebwa lures Manchester United to visit Uganda On September 10, the Indomitable Lions played out a goalless draw with ‘hosts’ Zimbabwe in Namboole and fans chaotically swarmed Onana outside the stadium after the match. Mr President, don’t stop at KCCA. Fire them all Gloria Bugie is the most recent nude video released but while this has evoked public outrage, it seems entirely business as normal at the Ministry of Ethics and Integrity PRIME Museveni wants easy way to buy big chunks of land for industrialists A crowd at a DP rally at the Constitutional Square in Kampala in the 2000s. It was renamed at the launch of the 1995 Constitution 29 years ago. PHOTO/FILE PRIME Uganda's Balagadde builds cargo business in US Mr Anthony Balagadde says Crane Cargo’s biggest advert is word of mouth by happy clients African music platform to pay $1m in royalties By localising content, Mdundo adds incremental value to its advertising clients, who benefit from targeted reach, and to artistes, who gain increased exposure in their communities PRIME Uganda's activists face increasing digital violence Ms Namata says online attacks have a spilling effect on the physical and emotional wellness of online activists Zari leads celebrity cast for hubby’s show at Lugogo Linda couldn’t stop admiring her idol, occasionally stealing shots of Zari smiling, or fanning herself with her veil or piece of paper.
http://www.mwananchi.co.tz/mw?utm_source=menu&utm_medium=drop_down
TAARIFA KWA UMMA Tunasikitika kuwaarifu wasomaji wetu wapendwa kuwa tunalazimika kusitisha uchapishaji wa maudhui mtandaoni kuanzia sasa kufuatia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kusitisha leseni zetu za... Mfanyabiashara wa madini auawa mlima wa maombi, wauaji watuma meseji… Mwili wa mfanyabiashara wa madini ya ujenzi, David Mollel mkazi wa Kata ya Moivaro, umekutwa ukining’inia kwenye mti juu ya Mlima Oldonyowas, jirani na eneo linalotumika kwa maombi. Diwani CCM mbaroni, Bashe acharuka Masasi Fedha hizo ni malipo yaliyopaswa kufanywa kwa wakulima wa korosho wanachama wa Chama cha Msingi cha Ushirika cha Nanyindwa Amcos katika msimu wa 2016/17. Wananchi kushirikishwa mchakato wa kumng’oa Gachagua Spika wa Bunge la Kitaifa la Kenya, Moses Wetang’ula ametangaza ushiriki wa umma katika hoja ya kumng’oa madarakani Naibu Rais, Rigathi Gachagua Ijumaa, Oktoba 4, 2024. Sababu ongezeko wagonjwa wa vifua, mafua Wizara ya Afya imesema kuna ongezeko la virusi wanaosababisha homa kali ya mafua inayoambukiza maarufu influenza, waliyotaja kusababishwa na mabadiliko ya hali ya hewa. Sita washikiliwa Polisi madai ya mauaji mkaguzi wa ndani Korogwe Mkaguzi wa Ndani wa Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga, Jonais Shao, mwanawe na mtumishi wa kazi za ndani waliuawa kwa kuchomwa moto. Benki ya CRDB yasaini mkataba wa Dola 320 milioni na DFC, Citi kusaidia wajasiriamali Tanzania na Burundi Strategis insurance yaungana na Vitality Health International kuhamasisha mtindo bora wa maisha kiafya TAARIFA KWA UMMA Tunasikitika kuwaarifu wasomaji wetu wapendwa kuwa tunalazimika kusitisha uchapishaji wa maudhui mtandaoni kuanzia sasa kufuatia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kusitisha leseni zetu za... Ajali yaua wawili Pemba Kaimu kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, Mussa Mwakasula amethibitisha kutokea ajali hiyo ya gari ya kampuni ya ujenzi wa barabara IRIS baada ya kuacha njia na kuwafuata watu waliokuwa... Fahamu vyama vilivyotoa marais Marekani nje ya Republican, Democrats Marekani inatarajia kufanya uchaguzi mkuu Novemba 5, mwaka huu huku kampeni za uchaguzi zikitawaliwa na vyama viwili vya Republican na Democrats, ambavyo ndivyo vimetoa marais wengi nchini humo... Sekta binafsi, wachumi waeleza ulipo mkwamo ongezeko vituo vya gesi asilia Mkurugenzi wa Mkondo wa Chini wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Emanuel Gilbert wapo mbioni kumaliza kero ya madereva kutumia muda mwingi kusubiri huduma ya gesi. Yanga Princess yaivua Simba ubingwa Ngao ya Jamii, ikitinga fainali Yanga Princess imetinga hatua ya fainali ya Ngao ya Jamii ya Ligi ya Wanawake baada ya kuifunga Simba Queens kwa mikwaju ya penalti 4-3 kwenye nusu fainali ya pili ya mashindano hayo iliyochezwa... Mambo matatu kwa Mondi akiwa na miaka 35 Ikiwa leo Oktoba 2, mwanamuziki wa Bongo Fleva nchini Naseeb Abdul 'Diamond' anasheherekea siku yake ya kuzaliwa akitimiza miaka 35, ndani ya miaka hiyo msanii huyo tayari amefanya makubwa katika... Ruto anavyomchinja Gachagua kwa kisu alichokificha kwenye tabasamu Wakanda ni dola ya kufikirika Afrika Mashariki, ndani ya mfululizo wa vitabu vya Fantastic Four. Shujaa Black Panther ambaye jina lake halisi ni T'Challa, anafanya kila kitu kuhakikisha anailinda... Pre-Form One na msimu wa shule binafsi ‘kupiga fedha’ Baada ya kumalizika kwa mitihani ya kuhitimu darasa la saba, wazazi kote nchini Tanzania wanapata furaha isiyo kifani kuona watoto wao wamevuka hatua hiyo muhimu katika safari ya elimu.
http://www.mwananchi.co.tz/mw
TAARIFA KWA UMMA Tunasikitika kuwaarifu wasomaji wetu wapendwa kuwa tunalazimika kusitisha uchapishaji wa maudhui mtandaoni kuanzia sasa kufuatia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kusitisha leseni zetu za... Mfanyabiashara wa madini auawa mlima wa maombi, wauaji watuma meseji… Mwili wa mfanyabiashara wa madini ya ujenzi, David Mollel mkazi wa Kata ya Moivaro, umekutwa ukining’inia kwenye mti juu ya Mlima Oldonyowas, jirani na eneo linalotumika kwa maombi. Diwani CCM mbaroni, Bashe acharuka Masasi Fedha hizo ni malipo yaliyopaswa kufanywa kwa wakulima wa korosho wanachama wa Chama cha Msingi cha Ushirika cha Nanyindwa Amcos katika msimu wa 2016/17. Wananchi kushirikishwa mchakato wa kumng’oa Gachagua Spika wa Bunge la Kitaifa la Kenya, Moses Wetang’ula ametangaza ushiriki wa umma katika hoja ya kumng’oa madarakani Naibu Rais, Rigathi Gachagua Ijumaa, Oktoba 4, 2024. Sababu ongezeko wagonjwa wa vifua, mafua Wizara ya Afya imesema kuna ongezeko la virusi wanaosababisha homa kali ya mafua inayoambukiza maarufu influenza, waliyotaja kusababishwa na mabadiliko ya hali ya hewa. Sita washikiliwa Polisi madai ya mauaji mkaguzi wa ndani Korogwe Mkaguzi wa Ndani wa Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga, Jonais Shao, mwanawe na mtumishi wa kazi za ndani waliuawa kwa kuchomwa moto. Benki ya CRDB yasaini mkataba wa Dola 320 milioni na DFC, Citi kusaidia wajasiriamali Tanzania na Burundi Strategis insurance yaungana na Vitality Health International kuhamasisha mtindo bora wa maisha kiafya TAARIFA KWA UMMA Tunasikitika kuwaarifu wasomaji wetu wapendwa kuwa tunalazimika kusitisha uchapishaji wa maudhui mtandaoni kuanzia sasa kufuatia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kusitisha leseni zetu za... Ajali yaua wawili Pemba Kaimu kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, Mussa Mwakasula amethibitisha kutokea ajali hiyo ya gari ya kampuni ya ujenzi wa barabara IRIS baada ya kuacha njia na kuwafuata watu waliokuwa... Fahamu vyama vilivyotoa marais Marekani nje ya Republican, Democrats Marekani inatarajia kufanya uchaguzi mkuu Novemba 5, mwaka huu huku kampeni za uchaguzi zikitawaliwa na vyama viwili vya Republican na Democrats, ambavyo ndivyo vimetoa marais wengi nchini humo... Sekta binafsi, wachumi waeleza ulipo mkwamo ongezeko vituo vya gesi asilia Mkurugenzi wa Mkondo wa Chini wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Emanuel Gilbert wapo mbioni kumaliza kero ya madereva kutumia muda mwingi kusubiri huduma ya gesi. Yanga Princess yaivua Simba ubingwa Ngao ya Jamii, ikitinga fainali Yanga Princess imetinga hatua ya fainali ya Ngao ya Jamii ya Ligi ya Wanawake baada ya kuifunga Simba Queens kwa mikwaju ya penalti 4-3 kwenye nusu fainali ya pili ya mashindano hayo iliyochezwa... Mambo matatu kwa Mondi akiwa na miaka 35 Ikiwa leo Oktoba 2, mwanamuziki wa Bongo Fleva nchini Naseeb Abdul 'Diamond' anasheherekea siku yake ya kuzaliwa akitimiza miaka 35, ndani ya miaka hiyo msanii huyo tayari amefanya makubwa katika... Ruto anavyomchinja Gachagua kwa kisu alichokificha kwenye tabasamu Wakanda ni dola ya kufikirika Afrika Mashariki, ndani ya mfululizo wa vitabu vya Fantastic Four. Shujaa Black Panther ambaye jina lake halisi ni T'Challa, anafanya kila kitu kuhakikisha anailinda... Pre-Form One na msimu wa shule binafsi ‘kupiga fedha’ Baada ya kumalizika kwa mitihani ya kuhitimu darasa la saba, wazazi kote nchini Tanzania wanapata furaha isiyo kifani kuona watoto wao wamevuka hatua hiyo muhimu katika safari ya elimu.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/search
Hello Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa Ready to continue your informative journey with us? Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features. Reclaim your full access. Click below to renew. Subscribe for a month to get full access
http://www.mwananchi.co.tz/mw/account
Dhibiti akaunti yako Maelezo ya kibinafsi Badilisha neno la siri Uliyonunua Imesasishwa kwa mafanikio. Name Jina linahitajika Surname Email address Barua pepe inahitajika Tafadhali tumia barua pepe halali Phone Number Tafadhali tumia namba sahihi ya simu I would like NMG to notify me about news, events and promotion Sasisha Current Password NenoLasiri linahitajika Neno Nenosiri lazima liwe na angalau herufi 6 New Password Nenolasiri linahitajika Nenosiri lazima liwe na angalau herufi 6 Confirm Password Maneno ya siri hayalingani Badilisha neno la siri Hakuna ununuzi Tafadhali Ingia
http://www.mwananchi.co.tz/mw/account#maelezo-ya-kibinafsi
Dhibiti akaunti yako Maelezo ya kibinafsi Badilisha neno la siri Uliyonunua Imesasishwa kwa mafanikio. Name Jina linahitajika Surname Email address Barua pepe inahitajika Tafadhali tumia barua pepe halali Phone Number Tafadhali tumia namba sahihi ya simu I would like NMG to notify me about news, events and promotion Sasisha Current Password NenoLasiri linahitajika Neno Nenosiri lazima liwe na angalau herufi 6 New Password Nenolasiri linahitajika Nenosiri lazima liwe na angalau herufi 6 Confirm Password Maneno ya siri hayalingani Badilisha neno la siri Hakuna ununuzi Tafadhali Ingia
http://www.mwananchi.co.tz/mw/account#badilisha-neno-la-siri
Dhibiti akaunti yako Maelezo ya kibinafsi Badilisha neno la siri Uliyonunua Imesasishwa kwa mafanikio. Name Jina linahitajika Surname Email address Barua pepe inahitajika Tafadhali tumia barua pepe halali Phone Number Tafadhali tumia namba sahihi ya simu I would like NMG to notify me about news, events and promotion Sasisha Current Password NenoLasiri linahitajika Neno Nenosiri lazima liwe na angalau herufi 6 New Password Nenolasiri linahitajika Nenosiri lazima liwe na angalau herufi 6 Confirm Password Maneno ya siri hayalingani Badilisha neno la siri Hakuna ununuzi Tafadhali Ingia
http://www.mwananchi.co.tz/mw/account#uliyonunua
Dhibiti akaunti yako Maelezo ya kibinafsi Badilisha neno la siri Uliyonunua Imesasishwa kwa mafanikio. Name Jina linahitajika Surname Email address Barua pepe inahitajika Tafadhali tumia barua pepe halali Phone Number Tafadhali tumia namba sahihi ya simu I would like NMG to notify me about news, events and promotion Sasisha Current Password NenoLasiri linahitajika Neno Nenosiri lazima liwe na angalau herufi 6 New Password Nenolasiri linahitajika Nenosiri lazima liwe na angalau herufi 6 Confirm Password Maneno ya siri hayalingani Badilisha neno la siri Hakuna ununuzi Tafadhali Ingia
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari
TAARIFA KWA UMMA Tunasikitika kuwaarifu wasomaji wetu wapendwa kuwa tunalazimika kusitisha uchapishaji wa maudhui mtandaoni kuanzia sasa kufuatia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kusitisha leseni zetu za... TAARIFA KWA UMMA Tunasikitika kuwaarifu wasomaji wetu wapendwa kuwa tunalazimika kusitisha uchapishaji wa maudhui mtandaoni kuanzia sasa kufuatia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kusitisha leseni zetu za... Mashambulizi ya Iran yapandisha bei ya mafuta Bei ya mafuta ya Marekani imepanda kwa asilimia 3 na kufikia zaidi ya Dola 70 za Marekani (Sh190,750) kwa pipa, huku mafuta ghafi aina ya Brent yakiuzwa kwa Dola 73 za Marekanio (Sh 198,925) kwa...
http://www.mwananchi.co.tz/mw/michezo
### Yanga Princess yaivua Simba ubingwa Ngao ya Jamii, ikitinga fainali Yanga Princess imetinga hatua ya fainali ya Ngao ya Jamii ya Ligi ya Wanawake baada ya kuifunga Simba Queens kwa mikwaju ya penalti 4-3 kwenye nusu fainali ya pili ya mashindano hayo iliyochezwa...
http://www.mwananchi.co.tz/mw/kolamu
Hello Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa Ready to continue your informative journey with us? Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features. Reclaim your full access. Click below to renew. Subscribe for a month to get full access
http://www.mwananchi.co.tz/mw/picha
Hello Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa Ready to continue your informative journey with us? Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features. Reclaim your full access. Click below to renew. Subscribe for a month to get full access
http://www.mwananchi.co.tz/mw/video
Hello Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa Ready to continue your informative journey with us? Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features. Reclaim your full access. Click below to renew. Subscribe for a month to get full access
http://www.mwananchi.co.tz/mw/toleo-maalum
### Mikakati ya GBT katika mapambano dhidi ya mashine haramu za sloti ‘Dubwi’ Michezo ya kubahatisha inajumuisha michezo ya aina mbalimbali ikiwemo Bahati Nasibu ya Taifa, kasino, michezo ya kubashiri matokeo (sports betting), michezo inayotumia jumbe fupi (SMS Lottery) na...
http://www.mwananchi.co.tz/mw/zanzibar
### Tume kuandika wapigakura wapya 14,878 Z’bar, ACT-Wazalendo watoa neno Wakati maboresho ya daftari la mpigakura yakitarajia kuanza Oktoba 7 hadi 13, 2024, wapiga kura wapya 14,878 wanatarajiwa kuandikishwa kisiwani humo ambao watakuwa na fursa ya kupiga kura moja tu...
http://www.mwananchi.co.tz/mw/ajira
Hello Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa Ready to continue your informative journey with us? Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features. Reclaim your full access. Click below to renew. Subscribe for a month to get full access
http://www.mwananchi.co.tz/mw/notisi
Hello Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa Ready to continue your informative journey with us? Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features. Reclaim your full access. Click below to renew. Subscribe for a month to get full access
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa
TAARIFA KWA UMMA Tunasikitika kuwaarifu wasomaji wetu wapendwa kuwa tunalazimika kusitisha uchapishaji wa maudhui mtandaoni kuanzia sasa kufuatia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kusitisha leseni zetu za... TAARIFA KWA UMMA Tunasikitika kuwaarifu wasomaji wetu wapendwa kuwa tunalazimika kusitisha uchapishaji wa maudhui mtandaoni kuanzia sasa kufuatia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kusitisha leseni zetu za... Mashambulizi ya Iran yapandisha bei ya mafuta Bei ya mafuta ya Marekani imepanda kwa asilimia 3 na kufikia zaidi ya Dola 70 za Marekani (Sh190,750) kwa pipa, huku mafuta ghafi aina ya Brent yakiuzwa kwa Dola 73 za Marekanio (Sh 198,925) kwa...
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kimataifa
Hello Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa Ready to continue your informative journey with us? Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features. Reclaim your full access. Click below to renew. Subscribe for a month to get full access
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/biashara
Hello Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa Ready to continue your informative journey with us? Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features. Reclaim your full access. Click below to renew. Subscribe for a month to get full access
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/makala
Pre-Form One na msimu wa shule binafsi ‘kupiga fedha’ Baada ya kumalizika kwa mitihani ya kuhitimu darasa la saba, wazazi kote nchini Tanzania wanapata furaha isiyo kifani kuona watoto wao wamevuka hatua hiyo muhimu katika safari ya elimu. Yafahamu anayopitia mtoto asiyemjua baba Majuzi nilikutana na Salome (si jina lake halisi) akinielezea masikitiko yake ya kutokumfahamu baba yake. Salome (23), mwanafunzi wa chuo kikuu, ana maumivu makali ya kutafuta kumfahamu baba yake... Hekaya za mlevi: Kijana elimu haijakufunza kuajiriwa Kuna wakati kila kijana alitamani kuwa msanii. Hii inatokea baada ya akili ya kijana kumwonesha mjomba wake akisota na shahada zake bila kupata kazi. Lakini pia masikio ya kijana yaliwanasa wale... Fahamu msongo unavyochangia magonjwa yasiyoambukiza Msongo wa mawazo ‘stress’ ni hali ya shinikizo la kiakili au la kihisia linalotokana na mahitaji yanayofikiriwa. Pombe, energy ni balaa kwa ogani “Nimeshazoea, kwa sasa siwezi kufurahia kunywa pombe kali bila kuchanganya na energy drink (kinywaji cha kuongeza nguvu), pasipo kufanya hivyo ninahisi kama kinywaji changu kinapungua ladha,”... Miwani mpya inayotarajiwa kuleta mapinduzi duniani Kampuni ya Meta ipo mbioni kuja na miwani mpya yenye teknolojia ya hali ya juu ambayo inatajwa kuwa na uwezo wa kuunganisha ulimwengu wa kidigitali na ulimwengu wa kweli. Upungufu watalaamu wa dawa ngazi ya msingi watajwa kufikia asilimia 81 Tanzania inakabiliwa na upungufu wa wataalamu wa kada ya famasia na wateknolojia dawa kwa asilimia 81 katika ngazi ya msingi, hali inayotajwa na wataalamu kuchangia wagonjwa kutopata huduma... Tahadhari yatolewa matumizi vidonge vya P2 Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya watu (UNFPA), limeeleza matumizi ya vidonge vya P2 sio njia ya uzazi wa mpango, bali hutumika kwa dharura. ‘Wanaume washirikishwe kikamilifu uzazi wa mpango’ Imeelezwa ushiriki wa wanaume katika masuala ya uzazi wa mpango ni muhimu na utakuwa na manufaa zaidi ukionekana. Kama unadhani ni mate ya nyoka, unajidanganya Ni kawaida kuona povu linalofanana na mate kwenye mimea hasa asubuhi au kipindi cha masika. Povu hilo wengi huamini ni mate ya nyoka na kusababisha kuogopa kuyashika Walimu kufeli mitihani ya wanafunzi, shida walimu au mfumo? Katika hali isiyo ya kawaida, walimu wanaweza kufeli mitihani ileile waliyowatahini wanafunzi wao? Michepuko janga lingine kwa wanandoa Umedumu kwa muda gani kwenye ndoa au uhusiano wako? Katika maisha yote umewahi kuchepuka? Nini kilisababisha ufanye hivyo? HEKAYA ZA MLEVI: Kiswahili cha waswahili changamoto Hivi haikushangazi kuona asilimia kubwa ya wanafunzi wanafaulu masomo ya kigeni kuliko somo la Kiswahili, lugha waliyozaliwa kwao na wanayoitumia wakati wote? Kiswahili ni kigumu sana PRIME Huyu ndiye Prof Manji, bingwa aliyeokoa maelfu ya watoto wachanga Profesa Karim Manji (65) wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), amechaguliwa kuwa mmoja wa washindi wa tuzo ya Mhitimu Bora wa Chuo Kikuu cha Harvard. Atolewa uvimbe kwenye kizazi uliomtesa kwa miaka 10 Jopo la madaktari bingwa wa upasuaji, wamefanikiwa kutoa uvimbe wenye uzito wa gramu 800 kwenye kizazi cha mwanamke mwenye umri wa miaka 49 alioishi nao kwa miaka 10, katika Hospitali ya Rufaa ya... Wadau kutoa mapendekezo ya kisera afya ya utengamao Mchango wa huduma za utengamao ni kuimarisha mifumo ya afya Fahamu mambo ya kuzingatia, kuepuka unapokuwa mgonjwa Wataalamu wa afya wameeleza mambo anayopaswa kufanya mgonjwa na yasiyopaswa ili kuimarisha usalama wake hospitalini na nyumbani PRIME Mikoa hii balaa kwa kuwa na mbumbumbu wengi Chini ya mti wa mwembe amekaa Rose Daniel akiwa ameshika simu ya mkononi, akiangalia ujumbe mfupi wa maneno aliotumiwa na mwalimu wa mwanawe. Kijana unafanya mazoezi au unasubiri ‘Six Pack’ baa? Ingawa kwa baadhi yetu mazoezi ni jambo la kila siku, wale wenzangu na mie angalau ifanye leo iwe siku itakayouchangamsha mwili wako kwani ndiyo maalumu kwa ajili ya mazoezi. PRIME Madhara wanayopata wanaokaa karibu na wavuta shisha, sigara Tafiti za kisayansi zinaonyesha moshi wa sigara una kemikali zaidi ya 400 zenye athari kubwa kwa afya ya binadamu
http://www.mwananchi.co.tz/mw/notisi/zabuni
Hello Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa Ready to continue your informative journey with us? Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features. Reclaim your full access. Click below to renew. Subscribe for a month to get full access
https://nation.africa/africa
South African former finance minister Tito Mboweni dies at 65 Tito is a pivotal figure in the nation’s transition to democracy and a champion for labour rights. PRIME East Africa corporate deals dip 18pc on low Kenya activity Deals data compiled by advisory firm I&M Burbidge Capital shows that the count fell to 73 between January and July from 89 in 2023. Uganda selects Turkish firm for Malaba-Kampala SGR In 2013, Uganda, Kenya, Tanzania, South Sudan and Rwanda broke ground on the construction of the SGR to connect member states. When DRC was self-sufficient as a cultural state How 1970s bid to free the people from colonial legacy defines the identity of DR Congo to date. The untold story of Nanyuki’s Mt Kenya Safari Club It’s membership was uber-exclusive; then the FBI started investigations after learning Mafiosi members. On land, Mugabe walked path other African leaders would not But he and his cronies abused the reform process by taking some of the choice parcels for themselves
https://nation.africa/kenya
PREMIUM Gachagua's ouster: Kenya's 2027 power shift? The fall of a kingpin or the rise of new alliances? PREMIUM AUC chairman: Why this could be Africa’s most important election The African Union should elect a visionary leader capable of transformative change and dramatically reducing poverty. The making of a TikTok sensation: Maureen Kibui's rise as Mama Morin How did a university student's imitation of her mother become a cultural phenomenon? PREMIUM What Kericho governor faces in Senate trial Governor Erick Mutai's fate hangs in the balance as the Senate prepares for a crucial impeachment hearing. PREMIUM How KDF's Somalia incursion changed face of the military Major improvements in training and equipment since October 2011 have boosted the troops' ability to defend the nation from external aggression. PREMIUM Exposed: Kenya’s underworld of gemstone smuggling where foreigners call shots Foreign nationals, some only holding tourist visas, have infiltrated the gemstone market. Is the stock market still a way to make money? Disenfranchised and battered by a decade of disappointing returns, little to no listings and falling share prices, many investors have lost faith in the Nairobi Securities Exchange EXPLAINED: Depression and anxiety—Not what you think You may appear happy yet are depressed. Dr Muthoni Karanja, takes host, Sheryl Blessing on how to identify triggers to help combat depression and anxiety. To sue your doctor or hospital? Health lawyer, Margaret Nyambura takes us through medical negligence from a legal perspective PREMIUM Western Sahara issue threatens Morocco’s business deals The Western Sahara region was initially a colony of Spain but after the colonialists departed, it was administered by Mauritania and Morocco before Morocco claimed its territory. PREMIUM Mutua: Why Gachagua was impeached Mr Gachagua did himself no favours by appearing arrogant and dismissive of his boss President Ruto and MPs. Bureaucrat banned from travelling to South African for lavish Birthday A top government official's extravagant birthday plans in South Africa come crashing down. PREMIUM Kenyan female wine tasters shine at World Tasting Championship Kenyan wine tasters have outperformed traditional wine powerhouses at the Wine Olympics. The making of a TikTok sensation: Maureen Kibui's rise as Mama Morin How did a university student's imitation of her mother become a cultural phenomenon? A weekend in the life of a taxi driver Business begins to peak on Thursdays when those that patronise bars begin to unwind and ease into the weekend. Barry Otieno announces bid for FKF presidency He said his campaign will be anchored on implementing four pillars.
https://www.monitor.co.ug/uganda
PRIME Atiak Sugar Factory: Billions spent, no production When machines at the factory first started roaring over a decade ago, its senior management pledged to turn the venture into “an engine for development to support the livelihoods of vulnerable... PRIME How wooden houses can transform Uganda's housing crisis Wooden houses can position Uganda for a sustainable future by addressing the housing crisis through cost-effective, eco-friendly construction, reducing carbon emissions, and promoting responsible... Take children to schools you can afford, Nabbanja tells parents Highlighting the government’s commitment to ensuring every child has access to quality education, the Prime Minister emphasised the vital role education plays in shaping the nation’s future Tayebwa lures Manchester United to visit Uganda On September 10, the Indomitable Lions played out a goalless draw with ‘hosts’ Zimbabwe in Namboole and fans chaotically swarmed Onana outside the stadium after the match. Mr President, don’t stop at KCCA. Fire them all Gloria Bugie is the most recent nude video released but while this has evoked public outrage, it seems entirely business as normal at the Ministry of Ethics and Integrity PRIME Museveni wants easy way to buy big chunks of land for industrialists A crowd at a DP rally at the Constitutional Square in Kampala in the 2000s. It was renamed at the launch of the 1995 Constitution 29 years ago. PHOTO/FILE PRIME Uganda's Balagadde builds cargo business in US Mr Anthony Balagadde says Crane Cargo’s biggest advert is word of mouth by happy clients African music platform to pay $1m in royalties By localising content, Mdundo adds incremental value to its advertising clients, who benefit from targeted reach, and to artistes, who gain increased exposure in their communities PRIME Uganda's activists face increasing digital violence Ms Namata says online attacks have a spilling effect on the physical and emotional wellness of online activists Zari leads celebrity cast for hubby’s show at Lugogo Linda couldn’t stop admiring her idol, occasionally stealing shots of Zari smiling, or fanning herself with her veil or piece of paper.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/account/subscribe
### Account Subscribe # Subscribe Hello Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa Ready to continue your informative journey with us? Hello Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features. Reclaim your full access. Click below to renew. ## Nation.Africa For corporate packages please contact us directly. Call +254(0)20-328-8033 # Forgot your password? Please fill in your email address. ### You can also pay using **Lipa na MPESA** by using the following instructions: 1. Go to the M-PESA menu 2. Select Lipa na M-PESA 3. Select the **Paybill** option 4. Enter business number: 5. Enter your account number: 6. Enter the amount: 7. Enter PIN and press OK to send 8. You will receive a confirmation SMS with your payment ## Kwa nini ujisajili? Asante kwa kujiunga nasi! Dhamira yetu Mwananchi ni kukuwezesha msomaji wetu kupitia uandishi huru wa kina unaoakisi dunia yako. Unapoendelea kutuamini, unatuwezesha kutekeleza dhima yetu ya Kuwezesha Taifa. Tupo kwa ajili yako! Kwa taarifa ama msaada zaidi, wasiliana nasi kupitia [email protected] ama +255 754 780 647. ## That's it. You are all set! Thank you for becoming part of our journey. You will be redirected back to the article in ** seconds ** ### We have noticed that the amount you paid is less than the expected total amount. Your payment has been received, but there is an outstanding balance. Please follow the following instructions to clear the balance. 1. Go to the M-PESA menu 2. Select Lipa na M-PESA 3. Select the **Paybill** option 4. Enter business number: 5. Enter your account number: 6. Enter the amount: 7. Enter PIN and press OK to send 8. You will receive a confirmation SMS with your payment
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/taarifa-kwa-umma-4784382
# TAARIFA KWA UMMA Tunasikitika kuwaarifu wasomaji wetu wapendwa kuwa tunalazimika kusitisha uchapishaji wa maudhui mtandaoni kuanzia sasa kufuatia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kusitisha leseni zetu za utoaji wa huduma ya maudhui mtandaoni kwa siku 30 kutokana na kuchapisha maudhui yaliyozuiwa yanayokiuka Kanuni za Maudhui ya Mtandaoni za 2020. Mwananchi Communications Limited (MCL) inaahidi kuwaletea wateja na wasomaji wetu habari, taarifa na maudhui bora yanayowezesha taifa kupitia magazeti yetu, na huduma zetu nyingine zisizo za mtandaoni wakati tukiendelea kuzungumza na mamlaka husika ili kupata muafaka. Tunawashukuru sana kwa kuendelea kuwa nasi. Imetolewa na *Victor A. Mushi Kaimu Mkurugenzi Mtendaji na Mhariri Mtendaji Mkuu* *Mpoki Thomson Mhariri Mkuu Mtendaji Msaidizi na Mhariri Mtendaji, The Citizen*
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/uchaguzi-chadema-boni-yai-kushinda-akiwa-gerezani--4783260
# Uchaguzi Chadema: Boni Yai kushinda akiwa gerezani? ## Muktasari: **Jumamosi ya Oktoba 5, 2024, Kanda ya Pwani ya Chadema yenye mikoa ya Dar es Salaam na Pwani itafanya uchaguzi wa viongozi wake huku mmoja wa wagombea nafasi ya uenyekiti, Boniface Jacob, maarufu Boni Yai atakuwa gerezani.** **Dar es Salaam**. Meya wa zamani wa Ubungo, Boniface Jacob, maarufu Boni Yai atalazimika kupigiwa kura ya nafasi ya uenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kanda ya Pwani akiwa gereza la Segerea jijini Dar es Salaam. Endapo atashinda uchaguzi huo uliopangwa kufanyika Jumamosi Oktoba 5, 2024 Kibaha mkoani Pwani, atakuwa kada wa pili wa Chadema kushinda akiwa gerezani baada ya Ameri Nkulu kushinda udiwani mwaka 2015 huko Sumbawanga akiwa gerezani. Ingawa chaguzi zinatofautiana, lakini Nkulu aliyekuwa akiwania udiwani katika Kata ya Lusaka, Oktoba 23, 2015 alihukumiwa kwenda jela miezi sita ikiwa ni siku mbili kabla ya uchaguzi mkuu, lakini wananchi wakaamua kumchagua. Boni Yai yuko katika Gereza la Segerea kutokana na dhamana yake kusubiri hatima ya dhamana yake ambayo imepangwa kutolewa Jumatatu Oktoba 7, 2024 na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, baada ya kusogezwa hadi tarehe hiyo. Hata hivyo, taratibu za Chadema zinaruhusu kupigiwa kura kwa staili hiyo. Boni Yai ambaye ni mfanyabiashara, mwanaharakati na mwanasiasa wa upinzani anakabiliwa na kesi ya kuchapisha taarifa za uongo mitandao ambapo upelelezi wake bado haujakamilika. Awali, uchaguzi huo ulipangwa kufanyika Septemba 29, 2024 wilayani Bagamoyo, lakini ulisogezwa mbele na waratibu wa uchaguzi huo wakisikiliza uamuzi wa mahakama wa kumpa dhamana Boni Yai ambaye ni mgombea anayechuana na Gervas Lyenda. Septemba 27, 2024, Katibu wa Chadema Kanda ya Pwani, Jerry Kerenge aliliambia Mwananchi: "Ngoja tuone siku hiyo (Oktoba Mosi) kutakuwa na ishu gani kuhusu mgombea huyu. Kufanya uchaguzi halafu mgombea mmoja yupo ndani (mahabusu), inawezekana hatumtendei haki, tumeamua tujipe muda kidogo.” “Hizi ni siasa wakati mwingine unaweza ukafanya jambo kwa faida, lakini likatengeneza ugumu, tusubiri tarehe moja,” alisema Kerenge. Hata hivyo, Jumanne Oktoba Mosi baada ya uamuzi wa mahakama kuhusu dhamana ya Boni Yai, uongozi wa Chadema Kanda ya Pwani umeamua kuendelea na uchaguzi kama ilivyopangwa ukitarajiwa kufanyika Njuwen Hoteli Kibaha badala ya Chuo cha Sanaa Bagamoyo (Tasuba). "Inatulazima tuendelea na mchakato kama ilivyopangwa maana hatuwezi kujua uamuzi wa mahakama utakuaje, Boni Yai atakosa fursa ya kujinadi na kuomba kura tu, kazi ambayo itafanywa na watu wake wa kampeni," alisema mratibu huyo. Mmoja wa wajumbe wa kamati kuu aliyezungumza na Mwananchi akiomba hifadhi ya jina amesema: “Tunalazimika kuendelea na uchaguzi kwa sababu tukiacha kuufanya unavuruga ratiba za chaguzi. Lakini kama mgombea anakubalika anakubalika tu, wapiga kura wataamua wenyewe kwani wanawajua wagombea wao wote.” “Kitu ambacho Boni atakikosa labda ni kuulizwa maswali tu pale lakini mambo mengine yatakuwa sawa na hii kwetu si mara ya kwanza uchaguzi kufanyika na mgombea kutokuwapo, imewahi kujitokeza huko nyuma na chaguzi ziliendelea.” Hata hivyo, si mara kwa wagombea wa nafasi mbalimbali Chadema kuombewa kura pasipo wenyewe kuwepo ndani ya ukumbi kama ilivyotokea kwa Chacha Heche aliyeibuka kidedea katika uchaguzi wa uenyekiti wa chama hicho, mkoa wa Mara, ingawa hakuwepo kwa kuwa alikuwa nje ya nchi kwa dharura. Siyo huyo tu bali hata mbunge wa zamani wa Mikumi, Joseph Haule, maarufu Profesa Jay amefanikiwa kutetea kiti chake cha uenyekiti wa wilaya hiyo, wiki iliyopita baada ya kuchaguliwa tena hata hivyo hakuwepo katika ukumbi wakati mchakato huo ukiendelea kutokana na changamoto anazozipitia za kiafya. **Meneja kampeni 'Boni Yai' ** Wakati hayo yakijiri, Meneja Kampeni wa Boni Yai, Ernest Mgawe ambaye pia ni mwenyekiti wa Chadema Jimbo la Kibamba amesema hawana wasiwasi hata mgombea asipokuwepo watamwakilisha vema katika kiny'anganyiro hicho. "Tuendelea na maandalizi, hatuna wasiwasi hata kama chama kikiamua kuitisha uchaguzi leo, kesho tutashiriki na kumpigia kura mgombea wetu Boni Yai aliyepo gerezani. "Tunaendelea kunadi vipaumbele vyake tangu alivyopitishwa na chama kuwania nafasi hii, tuna uhakika ataibuka kidedea katika uchaguzi huu," amesema Mgawe aliyewahi kuwania ubunge wa Kibamba katika uchaguzi wa mwaka 2020. **Lyenda atamba ** Wakati Mgawe akieleza hayo Lyenda amesema: "Maandalizi ya kumaliza kampeni yanakwenda vizuri kwa sababu timu yangu ya kampeni inafanya kazi nzuri tangu mwanzo, kama ambavyo timu ya Boni Yai inavyofanya." "Hizi kampeni zetu zinaongozwa na timu, maana hali ya siasa ya Tanzania wagombea hamuwezi kuwa mbele bali tunatanguliza timu," amesema. Lyenda amesema timu yake na Boni Yai zimesambaa mtaani kusaka kura kwa wajumbe wanaowaunga mkono, akisema kitendo cha mpinzani wake kusalia mahabusu hakuathiri chochote ndani ya timu yake. "Tunamwomba Mungu tumalize salama viongozi wapatikane ili tukijenge chama kwa ajili ya maandalizi ya chaguzi zijazo za serikali za mitaa na uchaguzi mkuu 2025," amesema Lyenda ambaye ni Ofisa Habari wa Chadema kanda ya Pwani. Uchaguzi huo utahusisha kumpata makamu mwenyekiti ambapo mchuano upo kati ya Sheikh Ally Mohamed ‘Kadogoo’ na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Kisarawe. Pia, wajumbe wa kanda hiyo watawachagua viongozi wa mabaraza ya wazee (Baraza la Wazee la Chadema- Bazecha), Baraza la Wanawake la Chadema (Bawacha), Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha) pamoja na mhazini wa kanda. Kwa miaka minne, Kanda ya Pwani yenye mikoa ya Pwani na Dar es Salaam, imekuwa chini ya Kaimu Mwenyekiti, Baraka Mwago, baada ya Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye aliyekuwa mwanachama wa Chadema kabla ya kurejea CCM kushindwa katika uchaguzi uliofanyika Novemba 19, 2019. Katika uchaguzi huo, Sumaye mbunge wa zamani wa Hanang' na Waziri Mkuu 1995 hadi 2005 alikuwa mgombea pekee lakini akapigiwa kura ya hapana 48 na ndio 28 huku moja ikiharibika. Katika hatua nyingine, Aden Mayala amechaguliwa kuwa mwenyekiti mpya wa Kanda ya Kusini yenye mikoa ya Mtwara, Ruvuma na Lindi, huku Belle Ponera akiibuka makamu mwenyekiti katika uchaguzi uliofanyika Septemba 29, 2024.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/siasa/simulizi-ya-saa-24-kabla-ya-kifo-cha-sokoine-4783080
Prime # Simulizi ya saa 24 kabla ya kifo cha Sokoine Imepita miaka 40 tangu aliyekuwa Waziri Mkuu, hayati Edward Sokoine alipofariki kwa ajali ya gari mkoani Morogoro wakati akitoka mkoani Dodoma kuelekea Dar es Salaam. Sokoine alifariki Aprili 12, 1984 baada ya gari lake kugongwa na gari lingine katika eneo la Dakawa, Wilaya ya Mvomero, mkoani Morogoro. Sokoine anatajwa kuwa miongoni mwa viongozi walioonyesha uwezo wa hali ya juu kwa kutatua kero za wananchi na kutafuta suluhu kwa mambo magumu yaliyoikabili nchi. Mapema wiki hii, kitabu cha “Edward Moringe Sokoine, Maisha na Uongozi Wake” kilizinduliwa na Rais Samia Suluhu Hassan. Kitabu hicho cha tawasifu ya maisha yake, kimeandikwa na Taasisi ya Uongozi kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (Sua). Makala haya yanachambua maisha ya kiongozi huyu kama yalivyosimuliwa kwenye kitabu hiki, ikiwemo uongozi wake, haiba yake, uamuzi alioufanya na hata kifo chake kilivyotokea na kusababisha majonzi kwa Watanzania. **Kifo chake** Kitabu hicho kinaeleza mazingira ya kifo cha Sokoine siku moja kabla ya ajali aliyoipata, kikisema alikataa usafiri wa ndege aliokuwa anaupendelea. “Aprili 11, 1984, siku moja kabla ya kifo chake, mlinzi na mpambe wake Sokoine, Amaan Abihudi Luila, alimweleza Waziri Mkuu kuwa ilikuwapo ndege ya kumrudisha Dar es Salaam kama alikuwa anapendelea usafiri huo. “Sokoine, baada ya kuelezwa kuwa ndege hiyo ilikuwa na uwezo wa kubeba watu saba, aliuliza kama angepanda ndege hiyo, wasaidizi wake ambao alikuwa amekwenda nao Dodoma wangerudi vipi Dar es Salaam? “Alisisitiza kuwa angetaka timu yake irudi pamoja Dar es Salaam kama ilivyokuwa imekwenda Dodoma. Ilikuwa kawaida ya Sokoine kuwatetea wasaidizi wake na siku hiyo utetezi ulihusu maofisa wake wengine watano ambao alisafiri nao kwa njia ya barabara kwenda Dodoma kutoka Dar es Salaam, Aprili 8, 1984.” Kitabu hicho kinaeleza kuwa ilikuwa Aprili na ilikuwa nyakati za masika, hivyo mvua ilinyesha usiku kucha Dodoma, kuanzia saa 4 usiku, ikiwa imeambatana na ngurumo za radi, kama ilivyokuwa kwa nchi nzima. “Mvua ile ilikuwa bado inaendelea kunyesha wakati safari ya Waziri Mkuu inaelekea Dar es Salaam. Sokoine hakujali hayo. Pamoja na mvua hiyo kubwa, saa 2 kamili za asubuhi, msafara wake uliingia kwenye lango kuu la nyuma la ofisi yake mjini Dodoma.” Kitabu hicho kinaeleza kuwa pamoja na mvua iliyokuwa ikinyesha, Sokoine alikwenda ofisini katika jengo la Old Boma, eneo la Uzunguni, karibu na Dodoma Hotel, kama ofisi yake. Kitabu hicho kinasimulia kwamba kama ilivyokuwa kawaida yake, baada ya kuingia ofisini kwake, alikagua majalada na kufanya mashauriano na wasaidizi wake. Saa 4:30 asubuhi, alitoka nje ya jengo la ofisi yake na kumkuta mmoja wa wasaidizi wake, Horace Kolimba (sasa marehemu), kwa masihara, alimkaribisha aingie kwenye gari lake ili wasafiri kwa pamoja kurudi Dar es Salaam. “Kwa heshima, Kolimba akamjibu Sokoine kuwa yeye angesafiri baadaye jioni kwa ndege. Hayo ndiyo yalikuwa maneno ya mwisho ya Sokoine kwa msaidizi wake yeyote, kwa sababu baada ya hapo msafara ulitimka kuelekea Dar es Salaam. “Lakini kabla ya kuanza safari yake kuelekea Dar es Salaam, Sokoine alikutana pia na Mawaziri wa Nchi (watatu) katika Ofisi ya Waziri Mkuu - Paul Kimiti, Gertrude Mongella na Anne Makinda. Alifanya kikao cha mapitio ya kazi za Serikali na Bunge kwa siku nne alizokuwa Dodoma. Sokoine aliwapitisha mawaziri hao kwenye muhtasari wa mambo muhimu aliyotaka yafanyike baada ya Bunge.” Pia, alikutana na watu mbalimbali, ikiwa pamoja na kufanya karamu na wabunge mkoani humo. Ufafanuzi wa Mwanga kuhusu yaliyotokea katika safari ya kwenda Da es Salaam hautofautiani na ule wa Chiledi, ambaye kama alivyo Mwanga alikuwa ni mtu wa lazima kuwapo katika kila msafara wa safari za Wazi Mkuu. **Safari yaishia Wami** Kwa mujibu wa aliyekuwa mwandishi wa Soikoine, Accadoga Chiledi, mwendo wa magari yaliyoandamana katika msafara wa kiongozi huyo ulikuwa wa kawaida, kati ya kilomita 110 na 130 kwa saa kwa sehemu zilizonyooka. “Chiledi alikaa katika gari lake la kawaida mbele ya lile la Waziri Mkuu. Gari lililotangulia, la kusafisha njia, lilikuwa la Jeshi la Polisi, aina ya Peugeot 504, likifuatiwa na gari la maofi wa usalama, na la tatu lilikuwa ni la Waziri Mkuu, Mercedes Benz. Baada ya gari la Waziri Mkuu likafuata gari jingine la maofisa wa usalama, baadaye gari la wasaidizi wengine, akiwamo Mwanga. Chiledi anaongeza, “Hata hivyo, dakika tano baada ya kuvuka Mto Wami, kiasi cha kama kilomita 40 hivi kutoka Morogoro, nilisikia kishindo kikubwa kikitokea nyuma yetu, kishindo cha mgongano wa vyuma. “Gari la Waziri Mkuu lilikuwa limegongana na gari aina ya Toyota Landcruiser la kubeba mizigo. Sokoine hakuchukua muda. “Alipoteza maisha muda mfupi tu baadaye kutokana na majeraha makubwa ambayo alikuwa ameyapata ya kichwani na kifuani.” **Aanza na Katiba mpya** Sokoine aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu siku nane tu baada ya vyama vya TANU na ASP kuunganishwa na kuunda Chama cha Mapinduzi (CCM). Aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu kwa mara ya kwanza mwaka 1977 na alidumu hadi mwaka 1980, akajiuzulu na baadaye aliteuliwa tena mwaka 1983 hadi alipofariki mwaka 1984. Kuunganishwa kwa vyama hivyo kulienda sambamba na mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ambayo ndiyo inaendelea kutumika nchini hadi sasa. Katiba hiyo iliyopitishwa Aprili 26, 1977, siku ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, pia ilichukua nafasi ya Katiba ya Muda ya Tanzania ya mwaka 1965. Kitabu hicho kinaeleza kuwa uongozi wa Sokoine ulijitokeza katika usimamizi wake wa kupitishwa kwa Katiba hiyo. “Katiba hiyo kimsingi ndiyo iliyoimarisha kwa vitendo mfumo na nadharia ya Chama Kushika Hatamu za Uongozi wa nchi, na nafasi ya CCM katika maisha ya Watanzania. “Katiba hiyo ya 1977 pia ndiyo iliyoondoa utata wa kuwapo kwa vyama viwili vya siasa. Kwa mara ya kwanza tangu Muungano, nchi sasa ilikuwa kweli na chama kimoja cha siasa kufuatia kuungana kwa vyama vya TANU na ASP miezi miwili kabla ya kupitishwa kwa Katiba mpya ya mwaka 1977. Aidha, hatua ya kuunganisha vyama hivyo iliimarisha Muungano,” kinaeleza kitabu hicho. **Vita vya Idd Amin** Mafanikio mengine ya Sokoine yanayotajwa katika kitabu hicho ni uongozi na usimamizi wake wa vita dhidi ya Idi Amin vya kukomboa sehemu ya Tanzania iliyovamiwa na mtawala huyo wa Uganda. “Sokoine alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Vita wakati huo. Vita vinahitaji mchango wa watu wengi na hakuna shaka kuwa watu wengi nchini walichangia mafanikio ya Tanzania katika ushindi huo. “Hata hivyo, ushindi huo usingepatikana bila uongozi thabiti wa Sokoine katika vita hivyo. Nyerere alitambua mchango wa Sokoine katika barua ambayo alimwandikia Waziri Mkuu akimkubalia ajiuzulu Uwaziri Mkuu mwishoni mwa mwaka 1980. “Baada ya kummiminia sifa nyingi za uongozi, Nyerere alimwambia Sokoine, ‘Ni lazima nitaje, kwa namna ya pekee, kazi uliyoifanya katika kuendesha na kuratibu juhudi za taifa letu wakati tulipolazimishwa kuingia vitani; binafsi ulitoa mchango mkubwa katika ushindi wetu wa mwisho na mchango wako ni lazima utambuliwe hadharani’.” **Vita dhidi ya uhujumu uchumi** Sokoine pia aliingia madarakani kwa nyakati zote mbili wakati Tanzania inapitia kipindi kigumu kiuchumi. Baada ya kupitishwa Sheria ya Uhujumu uchumi, ukamataji ulianza hata kama ilikuwa katika mazingira ya siri. Kamatakamata ilikwenda kwa kasi sana na Hamad Rashid ananukuliwa kwenye kitabu hicho akisema katika kipindi kifupi, watu wapatao 3,000 walikuwa wametiwa ndani, mali nyingi za mamilioni ya fedha zilikamatwa na vyombo vya Serikali na nyingine hata kupotea katika mazingira ya kutatanisha. Akimwelezea Sokoine katika mkutano wa uzinduzi wa kitabu chake Septemba 30, 2024, Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba anasema Sokoine alisimamia uanzishwaji na utekelezaji wa Sheria ya Uhujumu uchumi ambayo kwa maoni yake aliona kuwa inaweza kuleta shida. “Alisema kesi za uhujumu ya uchumi zisikilizwe katika Mahakama maalumu, halafu ushahidi wa kusikia uchukuliwe, kesi zisikilizwe faragha na kusiwe na dhamana,” anasema. Hata hivyo, Jaji Warioba anasema alipinga sheria hiyo akisema inakiuka utawala bora na haki za binadamu. “Nikamwambia, mimi kwa kuwa ni Waziri wa Sheria na Mwanasheria Mkuu, siwezi kusimamia sheria ambayo siiamini. Kwa hiyo nikamwambia Mheshimiwa Waziri Mkuu, mimi nitakaa pembeni,” anasema. Hata hivyo, alisema Sokoine hakupenda msimamo wake. “Akaniambia wewe umekuwa mstari wa mbele kupambana na rushwa, unataka kuacha kazi kwa jambo dogo hili? “Nikamwambia hapana, sheria zozote zinazotekelezwa kwa operesheni zinakuja kuleta madhara makubwa baadaye na kwa sheria hii, italeta madhara na inavunja utawala bora na inaingilia haki za binadamu,” anasema Jaji Warioba. Anaendelea kusimulia kuwa Sokoine alimchukua hadi Msasani kwa Mwalimu Julius Nyerere kutaka ushauri. “Mwalimu akaamua nusunusu, akasema nendeni mkaondoe hiyo ya kesi kusikilizwa faragha na hiyo ya hearsay evidence (ushahidi wa kusikia), lakini utaratibu maalumu ubaki na dhamana isiruhusiwe na akasema hakuna mtu ku-resign (kujiuzulu) hapa,” anasema. Anasema sheria hiyo ilipitishwa Aprili 1983 na Nyerere aliisaini haraka haraka. “Yaleyale niliyokuwa naogopa yakaanza kutokea, kwa sababu utekelezaji wake ulikuwa na vurugu kubwa. Watu walianza kukamatwa kwa taratibu mbaya, mali za watu zilichukuliwa na malalamiko ya wananchi yalikuwa mengi sana,” anasema. Hata hivyo, kwa mujibu wa Jaji Warioba, baadhi ya watendaji wa Serikali waliosimamia operesheni ya uhujumu uchumi walikwenda kinyume na maelekezo, jambo lililomsikitisha Sokoine. Kwa mujibu wa kitabu hicho, Sokoine hakuwa na ugomvi na ubepari na mabepari kwa sababu aliweka tofauti kati ya mabepari “waaminifu” ambao kazi yao ilikuwa kushiriki katika uzalishaji na shughuli halali, na walanguzi na wahujumu uchumi waliojipatia mali kwa njia za ulanguzi na uhujumu uchumi. “Wakati ule wa vita dhidi ya uhujumu uchumi, Sokoine alitamka hadharani kuwa chama na Serikali havikuwachukia matajiri, bali kuwa kilichotakiwa ni watu kutajirika kwa njia halali za uzalishaji mali. Katika moja ya kauli zake, Sokoine alitoa changamoto za matatizo akisema: “Watuambie nani katika Tanzania amenyang'anywa ardhi yake, mifugo yake na kadhalika.” Ilikuwa vigumu kwa Sokoine, kwa hakika, kutokuamini katika miliki binafsi ya mali kwa kuzingatia kuwa, licha ya kukadiriwa kuwa na ng'ombe kati ya 500 na 600, pia alimiliki maeneo makubwa ya ardhi. Katika kitabu hicho, Profesa wa Sheria, Issa Shivji, mmoja wa wasomi na wachambuzi hodari wa mambo nchini, anasema kuwa Sokoine hakuwa na ugomvi kuhusu ubepari kwa maana ya ubepari au kuhusu mabepari kama tabaka ndani ya jamii.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/mfanyabiashara-wa-madini-auawa-mlima-wa-maombi-wauaji-watuma-meseji--4783428
# Mfanyabiashara wa madini auawa mlima wa maombi, wauaji watuma meseji… ## Muktasari: **Inadaiwa alinyongwa kwa mkanda wa suruali, usoni alifungwa kitambaa chekundu** **Arusha.** Mwili wa mfanyabiashara wa madini ya ujenzi, David Mollel mkazi wa Kata ya Moivaro, umekutwa ukining’inia kwenye mti juu ya Mlima Oldonyowas, jirani na eneo linalotumika kwa maombi. Inadaiwa Mollel mwenye umri wa kati ya miaka 50 na 55, aliuawa na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia Jumanne, Oktoba Mosi, 2024 kwa kunyongwa na mkanda wa suruali. Mwili wake ulifunikwa kitambaa chekundu usoni. Taarifa za awali zinaashiria mgogoro wa kugombea eneo la uchimbaji madini ya ujenzi aina ya moramu ni chanzo cha mauaji hayo. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo amethibitisha tukio hilo akisema uchunguzi umeanza kwa kushirikiana na vyombo vingine vya usalama. Masejo amesema bado chanzo cha mauaji hayo hakijafahamika na wameanza uchunguzi kujua kiini cha tukio hilo kwa kushirikiana na taasisi zingine za usalama mkoani Arusha. Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Mount Meru. Jeshi la Polisi limesema linaendelea na uchunguzi ikiwa ni pamoja na ujumbe wa vitisho uliotumwa kwa familia yake. “Uchunguzi zaidi unafanyika kwa kushirikisha taasisi nyingine za kiuchunguzi kutokana na ujumbe wenye utata uliotumwa kwa ndugu zake watatu Septemba 30, 2024 kabla ya kugundulika kwa mwili wake katika Mlima Oldonyowas,” amesema leo Oktoba 2, 2024 alipozungumza na Mwananchi. Wakati huohuo, jirani na rafiki wa karibu wa mke wa marehemu, Rehema John, amesema Mollel alionekana mara ya mwisho asubuhi ya Septemba 30, 2024. Amesema alimuona saa tatu asubuhi alipokwenda kunywa chai nyumbani kwake na baadaye aliondoka. “Jioni saa 12, rafiki yangu aliniambia anakwenda polisi kutoa taarifa maana anasikia mume wake ametekwa na watu wasiofahamika, hivyo tukaenda kutoa taarifa na kutakiwa kukaa saa 24 ndipo turudi tena,” amesema. “Baadaye saa mbili usiku shemeji yake akampigia simu kumwambia kuna watu wametuma ujumbe kuwa wanaenda kumuua mume wake kwa sababu amekataa kuachia Mlima wa Moramu,” amesema. Amesema familia ilianza msako na asubuhi uligundulika mwili wake katika msitu wa Mlima Oldonyowas. Mjomba wa marehemu aliyejitambulisha kwa jina moja la Mollel amesema alitumiwa ujumbe kabla ya kupigiwa simu na watu hao saa mbili kasoro usiku na kuambiwa wamepewa kazi ya kumuua ndugu yao na watu wanaogombea nao mlima na ndiyo wanaenda kutekeleza. Ujumbe huo ambao Mwananchi umeuona unasomeka: “Unarijua hiri rijamaa renye simu hii, tunaritundika kwenye mti kakataa kuachia mgodi sio madai tu, pesa kitu gani na hiro rimoram aache, tumepewa kazi ya kumuua na watu watatu wababe akiwemo…” “Mimi ni mmoja wa watu watatu niliotumiwa ujumbe usiku saa mbili, nikasoma nikashtuka sana maana hatujawahi kusikia ndugu yetu akiwa na ugomvi na mtu, hivyo nilimtumia kaka yangu naye asome,” amesema. “Wakati huo nikaamua kupiga hiyo namba iliyotuma ujumbe akapokea akasema wako watatu na wamepewa pesa nyingi za kuhakikisha wanamuua ndugu yetu hivyo wanakwenda kumtundika juu ya mti,” amesema Mollel. Steven Joram, jirani mwingine wa Mollel amesema mauaji hayo yana viashiria vya mgogoro wa eneo la uchimbaji moramu ambalo alikuwa akilimiliki. “Alikuwa mtu wa watu sana, sijui hata huo mgodi wahusika wakiupata wataufanyia nini wakati wamedhulumu maisha ya mtu huyu aliyeacha watoto,” amesema.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/diwani-ccm-mbaroni-bashe-acharuka-masasi-4783914
# Diwani CCM mbaroni, Bashe acharuka Masasi ## Muktasari: **Bashe alifahamishwa kuwa wakulima kadhaa hawakulipwa kiasi cha Sh139 milioni katika msimu wa 2016/17 hatua iliyosababisha mali za Amcos hiyo ikiwemo trekta na lori kupigwa mnada kwa amri ya mahakama.** **Masasi.** Diwani wa Chiwale (CCM), wilayani Masasi, Yusuph Mataula amejikuta mikononi mwa vyombo vya dola akitakiwa kusaidia uchunguzi katika sakata la ubadhirifu wa Sh139 milioni. Fedha hizo ni malipo yaliyopaswa kufanywa kwa wakulima wa korosho wanachama wa Chama cha Msingi cha Ushirika cha Nanyindwa Amcos katika msimu wa 2016/17. Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe ametoa maagizo hayo leo Jumatano, Oktoba 2, 2024, alipohutubia mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Chiwale wilayani Masasi, Mtwara, baada ya kusikiliza kero mbalimbali zinazoathiri maendeleo ya kilimo katika kijiji hicho. Katika mkutano huo, Bashe alifahamishwa kuwa wakulima kadhaa hawakulipwa kiasi cha Sh139 milioni katika msimu wa 2016/17 hatua iliyosababisha mali za Amcos hiyo ikiwemo trekta na lori kupigwa mnada kwa amri ya mahakama. "Katika kulipatia ufumbuzi suala hilo, uongozi mpya wa Nanyindwa Amcos, uliamua kulipa Sh10 milioni kila msimu ili kupunguza deni hilo," mwananchama mmoja wa Amcos hiyo amesema mkutanoni hapo. Alipotakiwa kuelezea sakata hilo, Mwenyekiti wa Chama cha Ushirika Nanyindwa, Anania Kamaghe amesema alikuta taarifa za ubadhirifu huo baada ya kuchaguliwa mwaka huu. Amesema jitihada za kuokoa mali za chama ziligonga mwamba baada ya kuelezwa uamuzi wa mali kupigwa mnada ulitolewa na mahakama hivyo hakuwa na uwezo kupinga maamuzi ya kisheria. Alipotakiwa na Waziri Bashe awataje wahusika wa ubadhirifu huo, Kamaghe amesema, "Bodi nzima ya Nanyindwa Amcos, katibu mstaafu wa chama hicho ambaye sasa ni mheshimiwa (diwani) na viongozi wengine 12." Diwani huyo alipotakiwa kueleza upotevu wa fedha hizo, amekiri uongozi wake kuhusika na sakata hilo na kubainisha kuwa wajumbe 13 katika uongozi wake walitakiwa kulipa Sh7.4 milioni kufidia fedha hizo za malipo kwa wakulima. "Siwezi kujua endapo wenzangu wamemaliza kulipa kwa sababu kila mmoja alitakiwa kufanya malipo baada ya kupewa namba ya akaunti. Binafsi, nikipewa muda hadi Jumatatu nitakuwa nimemaliza kulipa sehemu yangu," amesema. Baada ya kusikiliza kwa makini, Bashe ameamuru vyombo vya ulinzi na usalama vimchukue ili kusaidia uchunguzi utakaofanikisha kupatikana kwa fedha hizo na wahusika wote wa ubadhirifu huo. "Fedha zote zipatikane ndani ya wiki na wahusika wajulikane walipo," amesema, akihimiza madiwani kusimamia Amcos badala ya wenyewe kuwa sehemu ya dhulma. Katika hatua nyingine, Waziri Bashe ameamuru kukamatwa kwa Afisa Mtendaji wa kijiji mstaafu Hashimu Pahala anayetuhumiwa kushiriki katika kumtapeli shamba la ekari 30, Fatuma Namkumbo licha ya kulipia Sh1.5 milioni na kupatiwa risiti. Pia, amekiagiza Chama Kikuu cha Ushirika cha Masasi na Mtwara (Mamcu), Bodi ya Korosho Tanzania (CBT), Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC), na ofisi ya mkuu wa wilaya ya Masasi kuchunguza ubadhirifu unaohusisha mamilioni ya shilingi katika Chama cha Msingi cha Lipumbulu (Amcos). Katika ubadhirifu huo, taarifa zinaonyesha wakati baadhi ya wakulima hawajalipwa fedha zao baada ya kuuza bidhaa kupitia chama hicho, wengine wamelipwa mara mbili.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/kabendera-atangaza-kukata-rufaa-dhidi-ya-vodacom-4783800
# Kabendera atangaza kukata rufaa dhidi ya Vodacom ## Muktasari: **Uamuzi wa kukata rufaa dhidi ya Kampuni ya Vodacom Tanzania Ltd, ndiyo unaoonekana kama hatua iunayofuata kwa Mwanahabari Erick Kabendera, baada ya kesi yake kupingwa na kushindwa kuendelea.** **Dar es Salaam**. Mwanahabari, Erick Kabendera ametangaza uamuzi wa kukata rufaa dhidi ya pingamizi lililozuia kuendelea kwa kesi yake anayokabiliana na Kampuni ya mtandao wa simu ya Vodacom Tanzania Ltd. Kabendera aliifungua kesi hiyo, Julai 2024, akiituhumu kampuni hiyo kuhusika na utoaji wa taarifa za mahali alipo hadi kukamatwa kwake Julai, 2019 nyumbani kwake Mbweni jijini Dar es Salaam. Baada ya kufungua kesi hiyo namba (12799/2024), iliwekewa pingamizi lililosababisha Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Dar es Salaam kuifuta. Kabendera alitangaza uamuzi wa kukata rufaa jana Jumanne, Oktoba 1, 2024 alipozungumza na waandishi wa habari kwa njia ya mtandao, akidokeza anafanya hivyo baada ya kushauriana na mawakili wake. Alisema anatarajia kukata rufaa kwenye Mahakama ya Rufaa dhidi za pingamizi lililowekwa kwa kuwa wanaamini kesi hiyo ina mashiko na inastahili kusikilizwa ili wawasilishe ushahidi. “Kutokana na ushahidi tulioukusanya baada ya miaka mitatu ya uchunguzi, tumeona ushahidi ni mkubwa kiasi kwamba unatosha kuishitaki Vodacom Tanzania na kampuni zake tanzu nchini Afrika ya Kusini na Uingereza,” alisema. Sambamba na uamuzi huo, Kabendera alisema wanasheria wake kutoka Uingereza na Afrika ya Kusini wanakamilisha utaratibu wa kufungua kesi dhidi ya Vodacom Group South Africa na Vodafone Group PLC yenye makao yake makuu nchini Uingereza haraka iwezekanavyo. Kabendera anaibuka kutangaza uamuzi huo takribani siku 20 zimepita tangu Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam kuifuta kesi yake aliyokuwa ameifungulia kampuni ya huduma za mawasiliano ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania Public Limited. Uamuzi huo wa kuifuata kesi hiyo utolewa Jumanne, Septemba 10, 2024 na Naibu Msajili wa Mahakama hiyo, Livin Lyakinana kwa niaba ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Salma Maghimbi aliyesikiliza kesi hiyo, kufuatia pingamizi la awali lililowekwa na Vodacom. Katika kesi hiyo ya madai namba 12799/2024, Kabendera aliyewakilishwa na Wakili Peter Madeleka alikuwa anaituhumu Vodacom kufanikisha kukamatwa kwake na namna hiyo anayoiita kutekwa na hatimaye kufunguliwa kesi hiyo ya uhujumu uchumi. Alikuwa anadai kutokana na tukio hilo amepata madhara mbalimbali yakiwamo ya kiuchumi na yasiyo ya kiuchumi, ya kijamii, maumivu ya kiakili na kimaono, ya kutokufurahia maisha, ya maendeleo binafsi na hadhi yake katika jamii na kutokuaminiwa kitaaluma. Hivyo, alikuwa anaitaka kampuni hiyo imlipe Dola 10 milioni za Marekani (takribani Sh28 bilioni) kama fidia ya hasara halisi na riba kwa kiwango cha Mahakama (asilimia) kuanzia tarehe ya hukumu mpaka kumaliza malipo yote. Pia, alikuwa anaiomba Mahakama iamuru Vodacom imlipe fidia ya hasara ya jumla kadri Mahakama itakavyotathmini, gharama za kesi na nafuu nyingine kadri mahakama itakavyona inafaa. Hata hivyo, Vodacom kupitia wakili wake Gaspar Nyika, Julai 9, 2024 kufuatia wito wa Mahakama uliyoitaka kufika mahakamani na kuwasilisha utetezi wake wa maandishi, iliwasilisha mahakamani maelezo yake ya utetezi wa maandishi. Katika maelezo hayo ya utetezi ambayo Mwananchi iliyaona nakala yake, kampuni hiyo ilikana tuhuma zote zilizoelekezwa kwake na mwanahabari huyo kuhusu ushiriki wake kufanikisha hicho alichokiita kutekwa kwake na ikamtaka mwanahabari huyo kuthibitisha tuhuma hizo. Sambamba na maelezo hayo ya utetezi pia kampuni hiyo iliibua pingamizi la awali dhidi ya kesi hiyo ikiiomba Mahakama isiisikilize. Katika pingamizi lake, kampuni hiyo iliiomba Mahakama hiyo iitupilie mbali kesi hiyo bila kuisikiliza ikidai haina mamlaka ya kuisikiliza kwa madai imefunguliwa nje ya muda uliowekwa kisheria. Katika uamuzi huo, Jaji Maghimbi amekubaliana na hoja ya pingamizi la Vodacom kuwa kesi hiyo iko mahakamani isivyo halali kwa kuwa imefunguliwa nje ya muda uliowekwa katika sheria. Jaji Maghimbi amesema sheria inaelekeza kesi za aina hiyo zinapaswa kufunguliwa mahakamani ndani ya muda wa miaka mitatu tangu kutokea kwa jambo linalolalamikiwa, lakini Kabendera alifungua kesi hiyo baada ya muda huo kupitia. **Alivyotiwa mbaroni** Kabendera alitiwa mbaroni na askari polisi nyumbani kwake, Mbweni jijini Dar es Salaam Julai 29, 2019 na kushikiliwa kwa siku kadhaa, kisha akafunguliwa kesi ya uhujumu uchumi. Kesi hiyo ilimalizika kwa utaratibu wa majadiliano na makubaliano ya kukiri makosa baina yake na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) unaojulikana kisheria kama plea bargaining. Aliachiliwa huru Februari 24, 2020 baada ya kulipa fidia ya hasara aliyodaiwa kusababisha kwa kukwepa kodi zaidi ya Sh173 milioni na faini aliyoamuriwa na Mahakama baada ya kumtia hatiani kwa kukiri makosa yake kulingana na majadiliano na makubaliano hayo na DPP. Mwaka 2024, katikati, ikiwa ni miaka mitano baada ya kukamatwa na miaka minne baada ya kesi yake hiyo ya uhujumu uchumi kumalizika, ndipo Kabendera akafungau kesi hiyo ya madai ya fidia dhidi ya Vodacom. Simulizi ya kutekwa, msingi wa madai Kwa mujibu wa hati ya madai katika kesi hiyo Kabendera ameeleza matukio yaliyojiri katika simu yake kabla ya tukio la kukamatwa kwake, kuwa ilianza kupoteza mawasiliano na kumfanya ashindwe kupata huduma ya mawasiliano. Pia, Kabendera ameelezea juhudi alizofanya kujua chanzo cha hali hiyo kwa kufanya mawasiliano na mwakilishi wa huduma kwa wateja na hata kutembelea ofisi za kampuni hiyo lakini hakupata ufumbuzi wa tatizo hilo. Kwa mujibu wa hati hiyo ya madai, hali hiyo ilianza Julai 27, 2019, saa 9:00 alasiri alipoiwasha simu yake ambayo alikuwa ameizima tangu jana yake usiku na kwamba ndipo alipobaini kuwa haikuwa na mtandao. Hivyo, aliazima simu nyingine akampigia mtoa huduma kwa mteja kujua mazingira yaliyosababisha kumkatia huduma katika simu yake bila kumjulisha kwanza. Mwakilishi wa huduma kwa wateja wa Vodacom alimweleza kuwa namba yake ya simu ya Vodacom (+255767456796) ilikuwa na changamoto za kiufundi ambayo ilimhitaji kutoa taarifa katika kituo cha huduma kwa wateja cha karibu kilichopo Tegeta. Kabendera alimtaka mwakilishi huyo kuelezea tatizo ni nini kabla ya kwenda huko kituoni, lakini mwakilishi huyo alikataa akidai ni suala nyeti ambalo linamtaka aende binafsi kituoni hapo. "Hata hivyo (Kabendera alisita kwenda huko kituo cha huduma kwa wateja) kwa kuwa kulikuwa kina matukio kadhaa ya watu kutekwa ama kutiwa mbaroni walipokuwa wakitembelea kituo cha huduma kwa wateja tangu mwaka 2016," inasomeka sehemu nyingine ya hati hiyo ya hiyo na kuongeza: Inaendelea kueleza Jumatatu, Julai 29, 2019 saa 4:00 asubuhi Kabendera alipiga tena simu ya huduma kwa wateja akimlalamikia kuwa alikuwa akihitaji kutoa pesa kwenye simu yake hiyo kwa ajili ya kumnunulia dawa mama yake aliyekuwa mgonjwa. Mwakilishi wa Vodacom aliyemhudumia alimweleza kuwa asubiri kidogo ili amuulize meneja wake na alirejea dakika chache baadaye na kumweleza kuwa kesi yake ilikuwa nyeti na kwamba ilikuwa juu ya uwezo wao kuitatua. Badala yake walimshauri atembelee ofisi zao zilizoko Mliman City asubuhi hiyo. Hata hivyo saa 9:00 alasiri siku hiyohiyo ya Julai 29, ghafla tu simu yake ilianza kufanya kazi, kisha alipoigiwa simu na mwakilishi wa Vodacom ambaye alimtaka (Kabendera) amwelezee tatizo lake na baada ya Kabendera kumuelezea kwa takribani dakika tatu, alikata simu akiahidi kumpigia baadaye kidogo. Baada ya takribani dakika tatu Kabendera alipokea simu iliyopigwa kutoka huduma kwa wateja Vodacom ambayo aliipokea akabaini kuwa ilikuwa ni sauti ya mwanamume, ambaye alimtaka Kabendera aeleze mahali alikokuwa na kwamba simu hiyo ilikuwa ikihanikiza na kukwaruza kama vile ilikuwa inarekodiwa. “Kabla ya simu hiyo kukatwa mteja wetu alimsikia huyo aliyempigia simu hiyo akinong'ona kuwa alikuwa nyumbani kwake na kuongeza kuwa sogea karibu na nyumba yake,” inasomeka sehemu nyingine ya hati hiyo ya madai. Kwa mujibu wa hati hiyo, maelezo hayo yalimstua Kabendera, akakimbia sehemu ya juu ya nyumba yake ambako aliweza kuona magari kadhaa ambayo hakuyafahamu, karibu ya nyumba yake. Kisha lilitokea gari lingine aina ya Toyota Alphard lililoegeshwa mbele ya magari hayo upande wa kulia mwa nyumba yake, halafu wakashuka watu wanne ambao walijitambulisha kuwa maofisa wa polisi lakini walikataa kutoa utambulisho. Walimpiga pingu kumshikilia kizuizini kwa siku mbili. Hati hiyo inaendelea kueleza wakati wa mahojiano, maofisa wa polisi walifika katika chumba cha mahojiano wakiwa na karatasi zilizochapishwa kutoka katika kompyuta za akaunti za pesa ya simu na za namba simu alizokuwa amezipiga kwa mwaka mzima. Hivyo, walimhoji lengo la kila muamala alioufanya kwa mwaka mzima nyuma yake na pia walimhoji uhusiano wake na watu aliokuwa amewasiliana nao miaka kadhaa. Kabendera analalamika polisi na Serikali walitoa taarifa kadhaa zenye mgogoro kwa umma kuhusiana na ‘kutekwa’ kwake na kwamba walimtuhumu kwa kutokuwa raia na kumkashfu Rais (wa wakati huo) John Magufuli. “Hatimaye alishtakiwa mahakamani kwa makosa ya utakatishaji fedha, uhujumu uchumi na ukwepaji kodi na matokeo yake walimuweka chini ya ulinzi mkali katika mahabusu ya Gereza la Segerea,” inasomeka hati hiyo ya madai.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kimataifa/wananchi-kushirikishwa-mchakato-wa-kumng-oa-gachagua-4783456
# Wananchi kushirikishwa mchakato wa kumng’oa Gachagua ## Muktasari: **Bunge la Kenya limeanza mchakato wa kumng’oa Naibu Rais, Rigathi Gachagua kutokana na tuhuma za matumizi mabaya ya Ofisi. Oktoba 8, 2024 atapaswa kujitetea kwa muda wa saa mbili (sawa na dakika 120).** **Nairobi**. Spika wa Bunge la Kitaifa la Kenya, Moses Wetang’ula ametangaza ushiriki wa umma katika hoja ya kumng’oa madarakani Naibu Rais, Rigathi Gachagua Ijumaa, Oktoba 4, 2024. Kwa mujibu wa tovuti ya The Standard, mchakato huo utafanyika katika kaunti zote 47 na Katibu wa Bunge atatoa taarifa kamili kupitia matangazo ya vyombo vya habari kuanzia leo Jumatano Oktoba 2, 2024. Wetang'ula amebainisha kuwa shughuli zote za Bunge kuanzia Alhamisi, Oktoba 3, 2024 hadi Jumatatu Oktoba 7, 2024 zitasitishwa ili kupokea maoni ya umma. Kamati ya Shughuli za Bunge itaweka azimio la kuahirisha kikao cha Bunge kesho Alhamisi na kufanya kikao cha asubuhi Jumanne, Oktoba 8, 2024 kujadili hoja hiyo. Gachagua anaweza kujitokeza ana kwa ana au kupitia uwakilishi wa kisheria. Hatua hiyo inafuatia baada ya Mbunge wa Kibwezi Magharibi, Mwengi Mutuse kuwasilisha rasmi hoja ya kumtimua Gashagua, akisema hoja za kufikia uamuzi huo ni sahihi na zinajitosha kumwondoa ofisini. Wetang'ula alisoma hoja hiyo Jumanne Oktoba Mosi, 2024 na kuthibitisha kuwa wabunge 291 waliiunga mkono hoja hiyo, na kuvuka idadi ya wabunge 117 wanaohitajika ili kuunga mkono hoja hiyo. Mutuse alitoa waraka wa kurasa 100 za ushahidi zinazoelezea sababu zake za kutaka kiongozi huyo atimuliwe. “Ibara ya 145 (1) ya Katiba inatamka kwamba mjumbe wa Bunge akiungwa mkono na angalau theluthi moja ya wabunge wote, anaweza kutoa hoja ya kushitakiwa kwa Rais au naibu wake kwa sababu ya ukiukwaji wa Katiba,” amesema Wetang'ula.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/sababu-ongezeko-wagonjwa-wa-vifua-mafua-4783394
# Sababu ongezeko wagonjwa wa vifua, mafua ## Muktasari: **Wizara ya Afya imetaja sababu ya ongezeko la wagonjwa wanaougua vifua na mafua kuwa ni uwepo wa virusi wapya wa mafua na influenza, wanaotokana na mabadiliko ya hali ya hewa.** **Dar es Salaam**. Wizara ya Afya imesema kuna ongezeko la virusi wanaosababisha homa kali ya mafua inayoambukiza maarufu influenza, waliyotaja kusababishwa na mabadiliko ya hali ya hewa. Homa hiyo ambayo husababisha ugonjwa wa vifua inaongezeka katika baadhi ya maeneo nchini, huku wataalamu wa afya wakitoa angalizo kuacha kutumia kiholela antibaotiki na badala yake wakiwashauri wagonjwa kuhudhuria vituo vya afya na kunywa maji mengi. Akizungumza na Mwananchi jana Jumanne, Oktoba 1, 2024, Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Tumaini Nagu amesema magonjwa ya vifua huongezeka na kupungua kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa. Amesema ikiangaliwa mwenendo wa mwaka jana na mwaka huu hakuna tofauti, lakini mara nyingi ni maambukizi ya virusi na wamekuwa wakifuatilia Uviko19 kote nchini kupitia maeneo ya ufuatiliaji zaidi ya 20 nchi nzima, kupitia sampuli za wagonjwa wanafika vituo vya afya kwa matatizo ya vifua. “Ikiwa mgonjwa ana changamoto za homa na kifua labda kukohoa sanasana maabara hatuoni Uviko19 ni wachache sana na pengine wiki nzima tusipate mgonjwa kama wiki iliyopita. “Lakini kuna virusi tofauti, kwa mfano tumegundua virusi wa mafua na influenza na virusi wengine tofauti tofauti na hii inaendana na mabadiliko ya hali ya hewa, lakini hakuna tofauti ukiangalia mwaka jana na mwaka huu katika magonjwa kama haya,” amesema Profesa Nagu. **Madaktari watoa angalizo** Wakati changamoto hizo zikiwakumba watoto na watu wazima, wataalamu wa afya wameshauri ni vyema tiba ikazingatia ushauri wa daktari na si vinginevyo. Daktari bingwa wa magonjwa ya mfumo wa upumuaji, Elisha Osati amesema mara nyingi magonjwa hayo virusi wake husambaa kulingana na hali ya mazingira kutoka kwenye baridi kwenda hali ya joto ambapo wadudu pia hubadilika. “Wanapobadilika husumbua mwili ni mabadiliko ya hali ya hewa, influenza hii hutokea hali inavyobadilika mfano tumetoka kwenye baridi tunaenda kwenye joto, wadudu wanaathiri njia ya hewa wanaweza kusababisha kutoka sehemu moja kwenda nyingine. Dk Osati ambaye pia ni Mtaalamu na mshauri wa masuala ya afya amesema ni vema kupima afya kabla ya kufanya maamuzi ya kununua dawa na kumeza. “Wengi wanaenda kwenye famasi wanakunywa antibiotiki kwa ugonjwa usiohitaji nguvu hiyo ya dawa matokeo yake ugonjwa unazidi, tunashauri ni mpaka aende apimwe na mtaalamu wa afya apewe dawa inayohusika ili kuzuia usugu wa dawa. “Virusi hivi husababisha maambukizi kwenye njia ya hewa, tunashauri mara nyingi unywe maji ya kutosha, inasaidia na dawa za kikohozi na hutakiwi kutumia antibiotiki,” amesema Dk Osati. Daktari bingwa wa magonjwa ya mfumo wa upumuaji Hospitali ya Aga Khan, Alex Masao amesema virusi hao huleta kero na homa kwa wagonjwa lakini hawana madhara makubwa. “Bahati nzuri virusi hawaendi kwenye mapafu, huu ni msimu wa mafua ni vyema mgonjwa kumsikiliza mtaalamu wa afya amshauri nini cha kufanya. “Kunywa dawa bila kumuona mtaalamu siyo sawa, tunatumia antibaotiki holela, ukipata mafua ukiitumia haisaidii mpaka pale utakapopona. Watu wajifunze, siyo kila unachoumwa unakimbilia kutumia antibiotiki unatengeneza usugu,” amesema Dk Masao.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/sita-washikiliwa-polisi-madai-ya-mauaji-mkaguzi-wa-ndani-korogwe-4783816
# Sita washikiliwa Polisi madai ya mauaji mkaguzi wa ndani Korogwe ## Muktasari: **Septemba 23, 2024, saa 3 usiku, watu watatu walikutwa wamechomwa moto katika msitu wa Hifadhi ya Korogwe Fuel, kijiji na kata ya Sindeni, Wilaya ya Handeni mkoani Tanga ambapo gari ndogo lilikutwa likiteketea huku pembeni yake kukiwa na watu hao waliokuwa wakiungua.** **Tanga**. Siku tisa tangu yalipotokea mauaji ya Jonais Shao, aliyekuwa Mkaguzi wa Ndani wa Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe mkoani Tanga, pamoja na mwanawe na msichana wake wa kazi za ndani, Jeshi la Polisi limesema linawashilikia watuhumiwa sita. Tukio hilo la mauaji ya Jonais (46), mwanawe Dedan Shao (8), mwanafunzi wa darasa la tatu na Salha Hassan (18), msichana wake wa kazi waliochomwa moto yalitokea Septemba 23, 2024 ndani ya msitu wa Hifadhi ya Korogwe, uliopo Kijiji cha Sindeni wilayani Handeni. Jonais na mwanawe Dedan walizikwa Septemba 28, 2024 katika Kijiji cha Maring’a Kondiki, Mwika wilayani Moshi, Kilimanjaro. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Almachius Mchunguzi akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatano Oktoba 2, 2024 amesema uchunguzi na msako wa jeshi hilo umewezesha kuwakamata watuhumiwa hao sita. Amewataja kuwa ni wakulima Bernard Kizughuto (31), mkazi wa Msambiazi Korogwe, Marko Jambia maarufu Rajabu Mhilu (28) wa Lushoto, Peter Jambia au jina lingine Johson (31) wa Msambiazi Korogwe, na Hassan Kitombo ‘Jombi’ (53) mkazi wa Kwamaraha Handeni. Wengine ni James Mkama maarufu Teacher (42), mfanyabiashara na mkazi wa Mtonga Korogwe na Omary Salehe ‘Mwiba’ (20), ambaye ni mkulima na mkazi wa Kwamaraha Handeni. “Upelelezi wa shauri hili unaendelea, ili hatua nyingine za kisheria zifuate. Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga linalaani vikali vitendo vyote vya kihalifu na halitamuonea muhali wala halitasita kumchukulia au kuwachukulia hatua za kisheria yeyote au kikundi cha watu wanaojihusisha na vitendo vya kihalifu,” amesema Mchunguzi. Ametoa wito kwa wananchi kushirikiana na Polisi katika kubaini na kuzuia uhalifu, ili kuendelea kuuweka mkoa huo kuwa salama. Ilivyokuwa Septemba 24, 2024 akizungumzia tukio hilo, Kamanda Mchunguzi alisema lilitokea Septemba 23, saa tatu usiku. Alisema Polisi lilipokea taarifa kuwa ndani ya msitu wa Hifadhi Korogwe kuna gari aina ya Toyota IST lenye namba za usajili T 305 EAL linaungua moto na pembeni yake kuna watu wawili wakiungua. Mchunguzi alisema askari walifika eneo hilo na kukuta kuna gari ndogo likiungua na pembeni yake kukiwa na watu wawili walioungua kwa moto na kufariki dunia wakiwa pembeni ya gari hilo. Alisema baada ya uchunguzi wa awali ilibainika miili iliyokuwa nje ya gari ni ya jinsia ya kike na ndani ya gari kiti cha nyuma ulionekana mwili mwingine ambao nao umeungua moto hadi kupoteza sura na haukubainika ni wa jinsia gani. Akizungumza na Mwananchi wakati huo, Lameck Shao, mume wa marehemu Jonais alisema alikuwa akiwasiliana na mkewe hadi Septemba 23 saa tatu usiku kabla ya mawasiliano kukatika. “Tuliwasiliana vizuri hadi saa tatu usiku kwamba amefika nyumbani baada ya hapo akawa hapatikani, nilijaribu kutafuta namna ya kupata mawasiliano hadi asubuhi ya leo (Septemba 24) nilipomtuma kijana wa shamba aende pale nyumbani. “Baada ya kufika pale, yule kijana hakukuta mtu na alipozungumza na majirani walibaini milango iko wazi. Tulianza kufuatilia ndipo mchana tuliposikia taarifa kwamba kuna watu wameungua kwenye gari,” alisema. Wito wa familia Wakati wa maziko ya Jonais na wanawe Dedan, wito ulitolewa kwa Jeshi la Polisi kuhakikisha watuhumiwa wanapatikana na sheria ichukue mkondo wake. Dainess Shao, mama mzazi wa Jonais alisema alikuwa ndiye tegemeo lake baada ya baba yake mzazi, Edward Shao kufariki dunia miaka michache iliyopita. Aliviomba vyombo vya dola vichunguze tukio hilo, ili mwanaye na mjukuu wake wapate haki zao. Akisoma historia ya marehemu, Mchungaji Jesse Shao, ambaye ni mwanafamilia alidai kina Jonais walivamiwa nyumbani kwao na watu wasiojulikana na kisha kuondoka nao zaidi ya kilomita 50 ambako walichomwa moto msituni. Akihubiri wakati wa ibada ya mazishi, Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Barikiel Panga alilaani tukio hilo la mauaji, akisema hakuna kabila lolote wala dini inayoruhusu mtu kutolewa uhai. Aliitaka jamii kukemea na kuwaombea wote wenye tabia za kinyama wakutane na neema ya Mungu, ili waache maovu na kuwakatili wenzao.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/biashara/sekta-binafsi-wachumi-waeleza-ulipo-mkwamo-ongezeko-vituo-vya-gesi-asilia-4784242
# Sekta binafsi, wachumi waeleza ulipo mkwamo ongezeko vituo vya gesi asilia ## Muktasari: **Kumekuwa na misururu ya vyombo vya moto kwenye vituo vya huduma ya kujaza gesi asilia jijini Dar es Salaam.** **Dar es Salaam. **Wadau wa sekta binafsi na wachumi wametaja mambo yanayokwamisha kujenga vituo vya kujaza gesi asilia kwenye vyombo vya moto, ni kutokuwepo sera na sheria ya kuisukuma sekta hiyo kufanya uwekezaji huo. Wamesema sekta binafsi huitaji kuwekeza eneo lenye kuipatia faida, hivyo vipo vikwazo vya kikodi ya uingizaji wa vifaa vya kubadili mifumo ya vyombo vya moto kutumia gesi asilia. Pamoja na hayo, wamesema hakuna miundombinu rafiki kwa vituo vya mafuta kuanzisha maeneo ya kujaza gesi kwenye magari. Kauli hizo zimetolewa wakati ambao madereva wanaotumia vyombo vya moto vitumiavyo gesi wakilalamika foleni kubwa kusubiri kupata huduma hiyo. Solomon Albert, dereva wa bajaji anayetumia gesi amesema Oktoba Mosi, 2024 alitumia zaidi ya saa sita kusubiri nishati hiyo kutokana na foleni. “Tatizo vituo ni vichache tulikuwa na vituo vitatu, kituo cha TAQA Dalbin kimepata hitilafu, sasa tuna vituo viwili vimebaki ambavyo navyo vimelemewa, ni muhimu Serikali ikaangalia namna ya kutengeneza mazingira kuvutia sekta binafsi kuwekeza kwenye ujenzi wa vituo, kutuepushia adha hii ya kupoteza muda,” amesema. Amesema bajaji yake ameichukua kwa mkopo na anapaswa kurejesha Sh40,000 kila siku lakini imekuwa vigumu kutokana na muda anaoupoteza kusubiri kujaza gesi. **Wanachosema wadau** Mchambuzi wa Sera wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Khadija Ally amesema sababu ya sekta binafsi kutokimbilia kuwekeza kwenye gesi asilia, ni kukosekana msukumo wa kisera na kisheria wa kuifanya sekta binafsi wanapoanzisha vituo vya mafuta miongoni mwa vigezo viwe ni mifumo ya kujaza gesi. “Ukiangalia miundombinu bado si rafiki kwa vituo vya mafuta kupata hiyo gesi, pia hakuna sera au sheria inayoipa sekta binafsi nafasi ya kuwekeza kwenye gesi asilia. “Sekta binafsi inavyowekeza fedha inategemea kupata faida, sasa ni kwa namna gani itapata bado hakuna mwelekeo unaoonyesha kama kutakuwa na faida,” amesema. Khadija amesema kodi kwenye vifaa vinavyotumika kubadili mifumo kwenye magari zinatatiza soko la uhitaji wa gesi kuendelea kupanuka, akisisitiza magari yenye uhitaji yanapokuwa mengi ndiyo wawekezaji huvutiwa kuwekeza. Amesema hata kampuni zilizojitokeza kubadili mifumo ya mafuta kwenda kwenye gesi nazo zinakwama kutokana na kodi ya vifaa wanavyoingiza kutoka nje. “Wananchi wanahitaji huduma lakini gharama ya kubadili mifumo ni kubwa,” amesema. Profesa Anna Sikira wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (Sua) uwekezaji ni mdogo kwenye matumizi ya gesi asilia kutokana na wenye mamlaka kutoamua kutenda yale wanayosema kuhusu sekta ya gesi. “Gesi kama nishati ni muhimu hasa tukiangalia mabadiliko ya tabianchi tunapoelekea ni kubaya zaidi, nchi yetu ina maeneo mengi yaliyoonekana jangwa, watu wanaendelea kutumia kuni na mkaa kama nishati, tungeimarisha gesi kama nishati ingetusaidia,” amesema. Amesema endapo Serikali ingetekeleza mipango kama inavyopanga kungekuwa na hatua katika matumizi na uwekezaji katika gesi asilia. “Serikali itende kama inavyosema kwenye suala la gesi tuone mambo yakifanyika, tupo hapa kwa sababu yale yanayosemwa hayafanyiki,” amesema. Mtaalamu wa masuala ya mazingira, Dk Aidan Msafiri amesema matumizi ya gesi asilia kwenye vyombo vya moto ni muhimu kutokana na kuwa rafiki kwa mazingira. “Kinachotukwamisha kwenye uwekezaji ni Serikali haikuwa imejipanga vya kutosa kisera, kiutawala au kuwezesha upatikanaji wa rasilimali za watu kuwekeza, kutumia gesi asilia ni jambo zuri lakini tulikurupuka,” amesema. Dk Msafiri amesema Serikali na wadau hawakufanya utafiti wa kutosha kuangalia idadi ya vyombo vya moto vitakavyotumia gesi ndipo kuwaita wadau kuingia kuwekeza kwenye gesi. Amesema takwimu za idadi ya vyombo vya moto vilivyopo na vitakavyoingia nchini itatoa taswira ya aina ya uwekezaji unaohitajika kwenye sekta ya gesi. “Tunapaswa kupunguza vigingi vinavyozuia watu kukimbia eneo la gesi kufanya uwekezaji, kwa sababu ni eneo changa tuondoe kodi ambazo zinaweza kuwarudisha nyuma wawekezaji,” amesema. Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu Huruia Tanzania (OUT), Dk Yohana Lawi amesema uwekezaji katika sekta ya gesi ni suala la kisera. “Kama Taifa na Serikali, sera yetu katika matumizi ya gesi asilia inatoa kipaumbele kiasi gani na maelekezo gani kwenye matumizi ya gesi asilia, suala la kupata wawekezaji na kupata vituo ni jambo dogo kwa sababu ili wafungue vituo wanahitaji wateja lakini tuna sera gani?” amehoji. Amesema endapo kuna sera inayoelekeza magari na mitambo viwandani kufikia miaka ijayo ziwe zinatumia gesi asilia kungesaidia kuvutia wawekezaji katika nishati hiyo. Dk Lawi ametoa mfano wa baadhi ya mataifa yaliyoweka sera ya kuachana na magari yanayotumia petroli na dizeli, badala yake watajikita katika matumizi magari yanayotumia gesi. Amesema uwepo wa sera inayoelekeza kuhamisha matumizi kutoka kwenye mafuta kwenda kwenye gesi unavutia sekta binafsi kukimbilia kufanya uwekezaji. “Sekta ya gesi ni eneo linalopaswa kupewa kipaumbele kwani ina uwezo wa kubadili uchumi kwa kiwango kikubwa ndani ya muda mfupi,” amesema. Amesema uchumi wa gesi ni mkubwa na unakwenda kubadilisha mfumo wa nishati hasa kupunguza gharama za uzalishaji na usafirishaji wa bidhaa na kupunguza utegemezi wa Dola ya Marekani. “Matumizi ya gesi ni nafuu kuliko petroli na dizeli na matumizi yake yakiwa makubwa yatakwenda kushusha gharama za matumizi viwandani, usafirishaji wa watu na bidhaa, hivyo watu watakwenda kupata bidhaa kwa gharama nafuu,” amesema. Dk Lawi amesema sababu ya gharama ya bidhaa kuwa kubwa ni kutokana na gharama za usafirishaji na uendeshaji kuwa kubwa, hivyo gesi ikipewa kipaumbele itakwenda kuonyesha mabadiliko kwenye uchumi. **Kauli ya TPDC** Mkurugenzi wa Mkondo wa Chini wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Emanuel Gilbert akizungumza na Mwananchi amesema mkakati wa kumaliza kero ya madereva kutumia muda mwingi kusubiri huduma hiyo ni kukamilishwa kituo kingine cha kujaza gesi eneo la Sam Nujoma mwishoni mwa mwaka huu. “Pia kuna wawekezaji binafsi ambao wanaendelea na hatua za awali za kuanza ujenzi wa vituo zaidi. TPDC itaingiza vituo jongefu ifikapo Juni 2025, kwa ujumla tunataraji kuongeza vituo 13 kufikia mwisho wa mwaka huu wa fedha,” amesema. Kaimu Mkurugenzi wa TPDC, Francis Mwakapalila katika taarifa ya Septemba, 2024 akizungumzia ukuzaji wa matumizi ya gesi asilia nchini alisema hadi sasa wameruhusu kampuni binafsi zaidi ya 30 kujenga vituo vya gesi asilia iliyogandamizwa nchini (CNG) ili kuwezesha matumizi katika maeneo mbalimbali.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/hifadhi-ya-jamii-itakavyonufaisha-wasiokuwa-kwenye-ajira-rasmi-4783982
# Hifadhi ya jamii itakavyonufaisha wasiokuwa kwenye ajira rasmi ## Muktasari: **Uhakika huo wanaupata kupitia skimu maalumu inayotolewa na NSSF, watu hao watapata mafao kama vile pensheni ya uzeeni, bima ya afya na fidia ya ulemavu.** **Dar es Salaam.** Kilio cha muda mrefu cha Watanzania waliojiajiri wenyewe kukosa huduma za matibabu na kinga ya kipato baada ya nguvu kupungua, kimesikika. Uhakika huo wanaupata kupitia skimu maalumu inayotolewa na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), watu hao watapata mafao kama vile pensheni ya uzeeni, bima ya afya na fidia ya ulemavu. Skimu hiyo kwa watu wa sekta isiyo rasmi, inalenga kuwapatia ulinzi wa kijamii wale ambao hawapo kwenye ajira rasmi, kama wafanyabiashara wadogo, wakulima, wasanii hata watumishi wa ndani. Akizungumza jana Jumanne Oktoba mosi 2024 wakati akitambulisha huduma hiyo kwa wahariri wa vyombo vya habari nchini, Mkurugenzi wa Uendeshaji wa NSSF, Omari Msiya amesema skimu hiyo inamlenga mwananchi yeyote aliyejiajiri katika sekta isiyo rasmi kama katika kilimo, ufugaji, uvuvi, uchimbaji mdogo wa madini, sanaa, biashara ndogo ndogo, mama lishe/baba lishe, bodaboda, machinga na wanahabari wa kujitegemea. Amesema lengo la skimu hiyo ni kuimarisha ustawi wa jamii kwa kuweka mifumo inayowakinga dhidi ya majanga kama uzee, ulemavu, urithi, ugonjwa, gharama za matibabu, kuumia kazini, uzazi, ukosefu wa ajira na ukubwa wa familia. Msiya amesema mtazamo na malengo ya hifadhi ya jamii katika umri wa kufanya kazi (miaka 18 hadi 60) ni kwamba kila anayejiunga anajiwekea akiba ya uzeeni, hivyo baada ya kustaafu anapata kinga dhidi ya kushuka kwa kipato. “Hali ya maisha baada ya kustaafu itategemea na jinsi ulivyojiandaa wakati ukiwa kwenye ajira. Maandalizi endelevu na ya uhakika ni kuwa kwenye mpango wa hifadhi ya jamii,” amesema Msiya. **Mafao kwa mnufaika** Skimu hiyo inatoa mafao ya muda mfupi na ya muda mrefu ambayo ni pensheni ya uzee, urithi na mafao ya ulemavu. Mafao ya muda mfupi ni ya uzazi, matibabu, mafao ya kujitoa (sehemu ya michango isiyozidi asilimia 50 au malipo ya mkupuo wa michango yote) na msaada wa mazishi ambayo hapo awali hayakuwahi kutolewa kwa sekta isiyo rasmi. Akizungumzia pensheni ya uzee ambayo awali ilitolewa tu kwa waajirwa wa sekta rasmi, Msiya amesema kwa mwanachama aliyetimiza umri wa miaka 55-59 (umri wa kustaafu kwa hiari) au miaka 60 (umri wa kustaafu kisheria) na aliyechangia mfuko kwa kipindi kisichopungua miezi 180, atapata malipo ya mkupuo wa awali na pensheni ya kila mwezi kama wastaafu wengine. Kuhusu pensheni ya ulemavu, alisema mwanachama anatakiwa awe amepoteza angalau theluthi mbili (2/3) ya uwezo wake wa kufanya kazi kutokana na ulemavu wa kimwili au kiakili na ulemavu huo usiwe umetokana na kazi yake. “Mwanachama huyu anatakiwa asiwe amefikia umri wa kustaafu na awe amechangia katika mfuko si chini ya michango ya miezi 36 (miaka mitatu) na katika michango hiyo, kuwe na michango 12 iliyolipwa ndani ya kipindi alichopata ulemavu.” **Pensheni ya urithi** Akizungumzia pensheni ya urithi, Msiya amesema hiyo hulipwa kwa wategemezi wa mwanachama aliyefariki ambao ni mke/mume na watoto walio na umri usiozidi miaka 18 au 21 ikiwa wanasoma. “Iwapo warithi hao hawapo, mafao yatalipwa kwa wazazi wa mwanachama aliyefariki,” amesema na kufafanua kuwa mwanachama atakayepata pensheni hiyo, lazima awe amechangia michango isiyopungua miezi 180 (miaka 15) kabla ya kufikwa na umauti. Alisema kwa michango chini ya miezi 180, wategemezi husika watalipwa mkupuo maalumu. Kwa mujibu wa Msiya, mgawanyo wa pensheni ya urithi huwa kwa watoto ambao hupata asilimia 60 ya pensheni na mjane au mgane hupata asilimia 40. Eneo jingine la mafao ni kwenye msaada wa mazishi, ambapo wategemezi wa mwanachama hulipwa kwa kiwango kati ya Sh150,000 na Sh600,000 kulingana na kiwango cha mchango wa mwezi cha marehemu. Vigezo vya fao hilo ni kuwa mwanachama anatakiwa awe amechangia walau mara moja na awe amefariki akiwa kazini. “Madai ya fao la mazishi yanatakiwa yafanyike ndani ya siku 60 baada ya kifo cha mwanachama,” amesema. Tofauti na kwenye ajira rasmi, skimu hii inaruhusu fao la kujitoa, ambapo mwanachama ili aruhusiwe anatakiwa awe amechangia kuanzia miezi 12 na kwamba anaweza kutoa asilimia 50 ya michango yake au kutoa michango yake yote. Yapo pia mafao ya uzazi, ambayo ni asilimia 100 ya wastani wa mapato ya siku ya mwanachama kwa kipindi cha miezi sita, kabla ya wiki ya 20 ya ujauzito na hulipwa kwa muda wa wiki 12, hii ni sawa na wastani wa mishahara ya miezi mitatu. “Malipo hufanyika kwa awamu mbili, yaani 1/3 hulipwa mwezi mmoja kabla ya kujifungua na 2/3 baada ya kujifungua. Mwanachama anaweza kuamua kulipwa kwa wiki zote 12 baada ya kujifungua. “Mwanachama awe amechangia miezi 36 (miaka mitatu) na michango 12 iwe imewasilishwa kabla ya wiki ya 36 ya ujauzito. Mafao haya yatalipwa kila baada ya miaka mitatu,” alisema. Akiuliza maswali, Mhariri mkongwe Salim Said Salim, amehoji iwapo mwanachama atajifungua watoto pacha, mfuko unamsaidiaje? Akijibu swali hilo, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Masha Mshomba amesema mwanachama atalipa asilimia 300 ya mshahara wake au kipato chake, hivyo fao hilo linaangalia zaidi uzazi na si idadi ya watoto waliozaliwa. **Mafao ya matibabu** Kwa upande wa mafao ya matibabu, Msiya amesema hayo hutolewa kwa mwanachama na wategemezi wake ambao ni mume/mke na watoto wasiozidi wanne, wenye umri usiozidi miaka 18 na ikiwa wapo shule wasizidi miaka 21. “Mwanachama akichangia Sh30,000 kwa mwezi atatibiwa peke yake na akichangia Sh52,200 atatibiwa yeye, mke/mume na watoto wasiozidi wanne. Mwanachama huyu anatakiwa awe amechangia angalau michango ya miezi mitatu mfululizo karibu na kupata huduma ya matibabu,” amesema. Amesema mwanachama atapata huduma katika hospitali moja atakayochagua kutoka miongoni mwa zilizoorodheshwa na mfuko huo. Ibrahim Yamola, mmoja wa wahariri alihoji iwapo mwanachama atapata changamoto ya kiafya akiwa nje ya mkoa aliosajili hospitali, matibabu yatakuwaje? Akijibu hilo, Mshomba ameeleza kuna utaratibu wa kuchukua kuponi maalumu katika ofisi za NSSF ambako mwanachama amejiandikisha au atakapopata changamoto kwenye mkoa mwingine anapaswa kwenda ofisi za NSSF eneo husika na kupatiwa kuponi hizo kisha kwenda hospitali kupatiwa matibabu. **Vigezo vya kujiunga** Vigezo vya kujiunga ni lazima uwe Mtanzania mwenye umri kuanzia miaka 15 hadi 70, usiwe mnufaika wa mafao ya pensheni kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii nchini. Pia, awe na namba ya NIDA au kitambulisho chochote kinachomtambua (leseni ya udereva/mpigakura) pamoja na picha ndogo moja (passport size).
http://www.mwananchi.co.tz/mw/toleo-maalum/benki-ya-crdb-yasaini-mkataba-wa-dola-320-milioni-na-dfc-citi-kusaidia-wajasiriamali-tanzania-na-burundi-4781930
# Benki ya CRDB yasaini mkataba wa Dola 320 milioni na DFC, Citi kusaidia wajasiriamali Tanzania na Burundi Benki ya CRDB imengia makubaliano ya mkopo wenye thamani ya Dola za Marekani Milioni 320 na Shirika la Fedha la Kimataifa la Marekani (DFC) na Citibank ili kuimarisha uwezo wake wa kutoa mikopo kwa ajili ya biashara ndogo, hususan zile zinazomilikiwa na kuongozwa na wanawake na vijana. Utiaji saini wa makubaliano hayo ulifanyika kwenye Makao Makuu ya Citibank yaliyopo jijini New York, kando ya Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa, na kuhudhuriwa na Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa, Waziri wa Uwekezaji na Mipango, Profesa Kitila Mkumbo, na ujumbe wa viongozi waandamizi kutoka Tanzania. Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, alisema katika hafla hiyo, "*Mkopo huu wa Dola za Marekani milioni 320 utaongeza upatikanaji wa fedha kwa ajili ya ufadhili wa biashara ndogo na za kati zinaozoongozwa na wanawake na vijana nchini Tanzania na Burundi, na kuwawezesha wajasiriamali kuwa wabunifu na hatimaye kuchochea ukuaji endelevu. * *Tuna imani kwamba fedha hizi hazitachochea tu uwezeshaji wa wajasiriamali nchini lakini pia kukuza usawa wa kijinsia, zikiwapa wajasiriamali wanawake msaada wanaouhitaji ili kustawi na kuchangia katika maendeleo ya kiuchumi*.” Mbali na hayo, fedha kutoka DFC na Citibank zitaimarisha juhudi za Benki ya CRDB za kuchechemua ukuaji wa uchumi jumuishi katika ukanda wa Afrika Mashariki, ikiwa ni sehemu ya mpango mkakati wake wa miaka mitano unaolenga kusaidia kundi la wajasiriamali. Nsekela alibainisha kuwa, pamoja na na kuwa na bidhaa za kifedha bunifu, benki hiyo kupitia taasisi yake tanzu ya CRDB Bank Foundation, imeweka msisitizo mkubwa katika kuwajengea uwezo wajasiriamali vijana na wanawake kupitia mafunzo ya elimu ya fedha na ujasiriamali. "*Ushirikiano huu na DFC na Citibank utachochea zaidi juhudi hizi*," Nsekela aliongeza. Mradi huo utasaidia zaidi ya biashara ndogo 4,500 nchini, zikitajwa kuwa miongoni mwa masoko yenye nguvu barani Afrika. Dola za Marekani Milioni 60 zitasaidia biashara ndogo za Kitanzania zinazomilikiwa au kuoongozwa na wanawake ambazo zimekidhi masharti ya Mpango wa DFC wa 2X wa uwezeshaji wanawake, zitakazosaidia kutatua changamoto mbalimbali za kiuchumi ambazo wanawake wanakabiliana nazo duniani kote. Inaelezwa pia kiasi cha Dola za Marekani Milioni 25 zitaenda kusaidia biashara ndogo ndogo nchini Burundi. Nsekela alitoa shukurani kwa wadau wote waliohusika, akipongeza kazi kubwa ililofanywa na Serikali za Tanzania na Burundi katika kuweka mazingira wezeshi kwa ushirikiano huo. "*Sera na mifumo wezeshi iliyowekwa na Serikali zetu imekuwa muhimu katika kuvutia uwekezaji wa kimataifa, ambao ni muhimu katika kuendeleza ajenda yetu ya maendeleo*," Nsekela alibainisha. Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa DFC, Nisha Biswal alisisitiza dhamira ya dhati ya shirika hilo, akisema, "*DFC imejidhatiti kukuza uchumi wa Tanzania, kwa kuzingatia uwekezaji ambao unaleta athari chanya kwa jamii. Mkopo huu utasaidia maelfu ya wafanyabiashara wadogo ambao ni mhimili wa maendeleo ya kiuchumi*." Mkopo huo unaakisi dhamira ya DFC ya kupanua uhusiano wake nchini ili kuimarisha ushirikiano wake uliopo na kutafuta fursa mpya za ushirikiano, kuendeleza usalama wa kiuchumi katika ukanda wa Afrika Mashariki na kote barani Afrika. Mkopo huu ni matunda ya kazi kubwa iliyowahi kufanyika hapo awali kati ya DFC, Benki ya CRDB pamoja na USAID/Tanzania kusaidia wafanyabiashara wadogo wa Kitanzania, ikijumuisha dhamana ya Dola za Marekani milioni 20 kusaidia utoaji mikopo kwa wafanyabiashara wadogo kwa lengo la kutoa huduma za elimu na kuzifikia sekta zisizo rasmi huku Dola za Marekani milioni 4 zikijikita kuongeza upatikanaji wa fedha kwa wanawake na vijana wanaokopa katika sekta ya afya. Afrika ndiyo eneo la kipaumbele la uwekezaji wa DFC duniani kote. Kwa sasa shirika hilo lina zaidi ya Dola za Marekani bilioni 11 zilizoenda katika miradi ya uwezeshaji fedha kwa wajasiriamali barani Afrika, uwiano mkubwa zaidi wa fedha za uwekezaji duniani. Kwa upande wake, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Citi Tanzania na Mkuu wa Huduma za Benki, Geofrey Mchangila alisema kuwa: *"Kama Citi, tunaendelea kupambana kutekeleza ajenda yetu ya uwezeshaji fedha kwa makundi mbalimbali ya kijamii kupitia ushirikiano wenye ubunifu kama huu*. Lengo letu ni kusaidia kujenga thamani halisi ya kiuchumi nchini Tanzania kusaidia malengo ya ujumuishi wa kifedha kupitia uwezeshaji wa wafanyabiashara wadogo kwa kukata kiu ya huduma za kifedha ambayo ilikuwa haijapatiwa ufumbuzi. Makubaliano haya ni sehemu ya ahadi yetu ya uchangiaji Dola za Marekani trilioni 1 kwenye miradi endelevu ya kifedha ifikapo 2030, inayolenga kuongeza upatikanaji wa ajira, fedha, miundombinu ya msingi na huduma kwa jamii zenye kipato cha chini katika masoko yanayokua kwa kasi. Kwa kutambua kuwa kesho iliyobora inategemea uwezeshaji wa wanawake na vijana, Benki ya CRDB imekuwa mstari wa mbele katika uwezeshaji kundi hili nchini Tanzania, ikitengeneza fursa zinazochochea ukuaji wa uchumi wa nchi. Kama taasisi ya fedha inayoongoza nchini, imekuwa nguzo muhimu katika kuzishika mkono Biashara Ndogo Ndogo na za Kati, hususan zinazomilikiwa na wanawake na vijana, kuwezesha kustawi na kuwa vichocheo muhimu vya uimarishaji wa uchumi wa Tanzania. Ikiwa na kampuni zake tanzu nchini Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Benki hiyo pia inawaweka wafanyabiashara wadogo wadogo, wadogo na wa kati wa Kitanzania kutumia fursa mpya za kikanda kupitia Eneo Huru la Biashara barani Afrika (AfCFTA). Kwa kuunganisha biashara za Kitanzania na soko la zaidi ya wateja bilioni 1.3 barani Afrika, Benki ya CRDB inafungua fursa kubwa za kiuchumi kwa wajasiriamali wa Tanzania, ili watimize ndoto zao za kutambulika kama wafanyabiashara wakubwa barani Afrika. Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, Benki ya CRDB imetoa zaidi ya Sh 4 trilioni kuwawezesha wafanyabiashara wadogo wadogo, wadogo na wa kati katika sekta mbalimbali, huku kipaumbele kikienda kwenye biashara zinazomilikiwa na wanawake kupitia huduma yake ya CRDB Malkia. Hatua hii sio tu imeongeza upatikanaji wa mitaji kwa wajasiriamali wanawake lakini pia imewawezesha kukuza biashara zao na kuchangia katika maendeleo ya uchumi wa Tanzania.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/toleo-maalum/ggml-yatoa-sh200-milioni-kudhamini-maonyesho-ya-saba-ya-teknolojia-ya-madini-mkoani-geita-4781440
# GGML yatoa Sh200 milioni kudhamini Maonyesho ya Saba ya Teknolojia ya Madini mkoani Geita Geita Gold Mining Limited (GGML), kampuni tanzu ya AngloGold Ashanti, imeendelea kuonyesha dhamira yake ya kuleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini Tanzania kwa mara nyingine tena, kwa kudhamini Maonyesho ya Saba ya Teknolojia ya Madini Geita kwa kutoa mchango wa Sh 200 milioni. Maonyesho haya yanatarajiwa kufanyika kuanzia Oktoba 2 hadi 13, 2024, na yatatoa fursa kwa GGML kuonyesha uvumbuzi wake wa kiteknolojia, uzingatiaji wa maudhui ya ndani, na uwekezaji wake wa kijamii kupitia miradi mbalimbali ya Uwajibikaji kwa Jamii wa Kampuni (CSR). Aidha, maonyesho haya yatafunguliwa rasmi Oktoba 5, 2024 na Dk Doto Mashaka Biteko (Mb), Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, ambaye ameonyesha uongozi imara katika sekta ya madini nchini. Hafla ya kufunga maonyesho hayo itafanyika Oktoba 13, 2024, ambapo Dk Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi. Maonyesho haya ya kila mwaka yanayoandaliwa kwa ushirikiano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE), yanatazamiwa kuwa jukwaa muhimu la kibiashara linalokutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya madini na sekta nyingine zinazohusiana. Washiriki wa maonyesho haya wanapata fursa ya kujadili changamoto, uvumbuzi, na fursa za kiuchumi zinazojitokeza, huku pia wakishuhudia jinsi kampuni kama GGML inavyochangia maendeleo endelevu ya Taifa kupitia teknolojia na uwekezaji wa ndani. Gilbert Mworia, Meneja Mwandamizi wa Uendelevu wa GGML, alisema, "*GGML imekuwa mdau muhimu katika maonyesho haya ya Teknolojia ya Madini kwa miaka saba mfululizo, na tuna furaha kubwa kushiriki tena mwaka huu. * *Mchango wetu kwenye maonyesho haya sio tu msaada wa kifedha, bali pia tunalenga kuimarisha mahusiano yetu na wadau wakuu kama vile Serikali za mitaa, wachimbaji wadogo, na biashara za ndani. Tunaamini kuwa teknolojia bora na ushirikiano wa kweli vinaweza kuleta mageuzi makubwa katika sekta ya madini*." Kupitia mpango wake wa urudishaji kwa jamii, GGML inatekeleza miradi mbalimbali inayoimarisha jamii za Geita na maeneo jirani. Mradi wa ujenzi wa viwanja vya Maonyesho ya EPZA huko Geita ni mojawapo ya miradi mikubwa iliyofadhiliwa na GGML ambao unalenga kubuni miundombinu inayochochea ukuaji wa kiuchumi katika sekta mbalimbali. Maeneo hayo yatatumika kwa shughuli za kibiashara na teknolojia kwa miaka mingi ijayo, huku yakifungua milango kwa wawekezaji na wabunifu wapya. Kwa mujibu wa dira yake ya muda mrefu, GGML inaunga mkono kikamilifu jitihada za Serikali ya Tanzania za kukuza uchumi wa madini. Hii ni sambamba na lengo la Serikali la kuhakikisha sekta ya madini inachangia angalau asilimia 10 ya Pato la Taifa ifikapo mwaka 2025. Ushiriki wa GGML katika maonesho haya ni ishara ya wazi ya azma yake ya kusaidia kufanikisha lengo hili kwa kutumia teknolojia za kisasa na kutoa fursa za ajira na mafunzo kwa Watanzania. Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2000, GGML imeendelea kuwa mshirika muhimu katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi ya jamii inayozunguka mgodi wa Geita. Kupitia miradi mbalimbali ya CSR, GGML imewekeza katika sekta za afya, elimu, miundombinu, na ujasiriamali, huku ikilenga kuboresha maisha ya Watanzania na kuleta mabadiliko endelevu. Hii inaonyesha kuwa kampuni hiyo inabaki kuwa kielelezo bora cha uwajibikaji wa kampuni na mshirika wa kweli wa maendeleo kwa Tanzania.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/toleo-maalum/sababu-10-1xbet-kuwa-chaguo-bora-kwa-watanzania-4780758
# Sababu 10 1xBet kuwa chaguo bora kwa Watanzania **Dar es Salaam.** Michezo ya Kubashiri nchini Tanzania inazidi kuwa maarufu, na ni muhimu kwa wachezaji kuchagua mtandao unaotoa masharti bora zaidi. 1xBet ni kampuni maarufu ya kimataifa ya Michezo ya Kubashiri inayozingatia usawa wa wateja na inafanya kila juhudi kutoa mchezo kwa masharti bora zaidi. sababu 10 zinazofanya 1xBet kuwa chaguo bora kwa maelfu ya Watanzania. **1. Kampuni ya kimataifa inayoendana na mahitaji ya watanzania** 1xBet ni kampuni ya kimataifa inayotoa huduma duniani kote, ikiwemo Tanzania. Kampuni hii in website inayopatikana kwa lugha zote mbili Kiswahili na Kiingereza, hivyo kufanya kuwa rahisi kwa watumiaji wetu. inatumia shilingi ya Kitanzania kuweza kubashiri, hivyo hutahitaji kubadilisha fedha na kupoteza kwenye kiwango cha ubadilishaji. Ukiwa na 1xBet, huna haja ya kuwa na wasiwasi — hakuna matata! **2. Bonasi ya amana ya kwanza hadi shilingi 600,000** Mchezaji mpya wa 1xBet hapati tu mtandao wenye urahisi bali pia ofa za faida. Bonasi ya amana ya kwanza ni 200% na inaweza kufikia shilingi 500,000, na kwa kutumia “promo code”, kiasi hiki kinaweza kuongezeka hadi Zaidi ya shilingi 600,000 Kwa mteja, hii ni fursa nzuri ya kupata faida ya ziada na kuongeza mtaji wa kuanzia. **3. Usajili wa haraka na rahisi kwa dakika chache** 1xBet inatoa njia kadhaa za usajili, kwa kubofya mara moja, kwa nambari ya simu, kupitia barua pepe, au mitandao ya kijamii. Unaweza pia kujisajili kwa kutumia VPN au moja kwa moja kwenye App. Haijalishi chaguo lako, mchakato huu utachukua dakika chache tu, jambo ambalo ni muhimu hasa kwa wale wanaotaka kuanza kubashiri haraka iwezekanavyo. **4. Aina mbalimbali za michezo ya kubashiri na michezo ya mtandaoni** Wachezaji kutoka Tanzania wanaweza kutabiri michezo maarufu, ikiwemo mpira wa miguu, mpira wa kikapu, au tenisi ya meza, na kufurahia michezo ya gemu kwenye sehemu ya 1xGames. Zaidi ya hayo, 1xBet inatoa nafasi za kubashiri kwenye michezo ya kielektroniki, burudani za kipindi, utabiri wa hali ya hewa, na mengine mengi. **5. Viwango vya juu vya kubashiri vinakupa nafasi ya kushinda kiasi kikubwa zaidi** 1xBet inatoa viwango bora vya kubashiri kwenye matukio makubwa ya michezo. kabla ya mechi na live. Hii inatoa fursa kubwa kwa wale wanaoamini katika bahati yao na wako tayari kuijaribu. **6. Njia za kuaminika za kuweka na kutoa fedha** Kwa Watanzania, kuweka fedha kwenye akaunti na kutoa ushindi lazima iwe njia ya kuaminika na ya haraka. 1xBet inatoa njia rahisi za kuweka amana kwa kutumia mifumo ya malipo ya hapa nchini. Wachezaji pia wanaweza kubashiri kwa kutumia shilingi ya Kitanzania, jambo linalorahisisha na kuharakisha miamala ya kifedha. Huna haja ya kuwa na wasiwasi— 1xBet itakufanyia kila kitu. **7. Fursa mbalimbali na promosheni za ndani** 1xBet haitoi tu matukio mengi ya michezo bali pia hushikilia promosheni maalum. Miongoni mwa promosheni maarufu ni “No Risk Bet” ambapo watumiaji wanaweza kupata faida kwenye mechi kubwa za mpira wa miguu kwa kutoa utabiri sahihi wa matokeo. Machaguo mengine ni promosheni za kawaida kama “Hyper Bonus” hadi 250%, “Goaless Football” n.k. Unaweza kupata orodha kamili kwenye sehemu ya “Promo”. **8. App ya simu ya mkononi yenye urahisi** Watanzania wanathamini urahisi wa kubashiri wakati wowote. Programu ya 1xBet ya simu haihitaji kumbukumbu kubwa, hivyo inawawezesha wachezaji kutoa utabiri, kuweka na kutoa fedha kwa haraka. Programu ya iOS ni rahisi kupatikana kwenye App Store, wakati programu ya Android inaweza kupakuliwa kutoka kwenye tovuti rasmi ya kampuni ya kubashiri. **9. Matangazo ya mechi moja kwa moja na uchambuzi** 1xBet inakupa sio tu nafasi ya kuweka bashiri bali pia kuangalia mechi moja kwa moja kwenye tovuti au programu. Matangazo ya moja kwa moja yanakuruhusu kufuatilia matukio kwa muda halisi (Live) bila kukosa nyakati muhimu. Kampuni ya kubashiri pia inatoa ufikiaji wa data za uchambuzi, jambo linalowasaidia wateja wake kufanya maamuzi bora zaidi ya kubashiri. Hii inatoa thamani ya ziada kwa wale ambao hawataki tu kujaribu bahati bali pia kuboresha ujuzi wao wa uchambuzi wa michezo. **10. Ubora wa 1xBet unathibitishwa na tuzo za kimataifa** 1xBet ni Kampuni ya kimataifa inayounga mkono vilabu na ligi maarufu duniani. Kampuni ya kubashiri ni mshirika rasmi wa FC Barcelona, Paris Saint-Germain, LOSC Lille, Serie A, na Shirikisho la Soka la Afrika (CAF). Mtazamo wa kampuni hii kwenye soko la Afrika umethibitishwa na hadhi ya kifahari ya “Best Sportsbook Operator in Africa” iliyotolewa katika Tuzo za SiGMA Africa 2024. 1xBet siyo tu kubashiri, bali pia ni fursa nyingi za kufurahia na kupata faida. Jaribu mwenyewe na uone kwamba kucheza na 1xBet ni kufurahisha, rahisi, na kunalipa.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/toleo-maalum/strategis-insurance-yaungana-na-vitality-health-international-kuhamasisha-mtindo-bora-wa-maisha-kiafya-4777446
# Strategis insurance yaungana na Vitality Health International kuhamasisha mtindo bora wa maisha kiafya **Dar es Salaam**. Kampuni ya Strategis Insurance imeingia makubaliano na Vitality Health International ya kutoa bidhaa bora ya bima nchini. Ushirikiano huo unalenga kuboresha afya na ustawi wa Watanzania. Bidhaa hiyo ya afya yenye upekee nchini imebuniwa mahsusi kusaidia kampuni na taasisi mbalimbali kuimarisha afya za wafanyakazi wao kupitia sera zao za bima. Pia, utoaji wa huduma za bima ya afya chini ya ushirikiano huo ni wa hadhi ya juu kwa kuwa umejikita kuleta matokeo bora ya afya za watu huku ukiendelea kuboresha na kulinda maisha yao. **Vitality health international ni nani?** Vitality Health International inamilikiwa na kampuni ya bima ya Afrika Kusini iliyoshinda tuzo nyingi, Discovery, ambayo ilianzisha mfumo wa huduma za bima wa ubia huko Afrika Kusini, ambao umeleta mageuzi katika sekta ya bima ambapo umejengwa katika utaratibu wa kuwapa zawadi watu wanaotunza afya zao kwa mtindo wa maisha yenye afya, na kujenga ushirikiano wenye mafanikio duniani kote na kampuni kubwa za bima. Leo, Kampuni ya Discovery inaendesha shughuli zake katika masoko zaidi ya 40, na kubadili maisha ya zaidi ya watu milioni 35 duniani kote. Tangu k u a n z i s h w a kwake Januari 2022, Vitality Health International imeendelea kujijengea heshima kwa kuleta bidhaa zabima ya afya ambazo ni chachu ya k u i m a r i s h a afya za vikundi vya waajiriwa barani Afrika. Mbali na Tanzania, kampuni hiyo ya bima ya afya tayari imetanua wigo wake kufikia katika nchi za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Ghana, Kenya, Msumbiji, Nigeria na Zambia. Strategis ni mshirika wa bima ya afya nchini wa Vitality Health International, ambaye amekua kinara wa kutoa huduma bora ya bima ya afya kwa waTanzania. Vitality Health International inalenga kutoa bima bora ya afya nchini wakati huo huo ikiendelea na ufikishaji huduma kama hizo katika nchi nyingine barani Afrika. Ikijengwa katika misingi ya ubora, kujitoa na uwajibikaji, Strategis Insurance inatoa huduma zake katika mikoa yote nchini Tanzania, na pia huduma zake zinayafikia mataifa mbalimbali. Kwa pamoja, Vitality Health International na Strategis wamejitolea kuimarisha ubora wa maisha ya watu barani Afrika na kuufanya ushirikiano uliopo uwe na faida kwa pande zote mbili. Mkurugenzi Mtendaji wa Strategis Insurance (upande wa bima ya afya), Dk Malav Manek, anasema: ‘ Tunaamini ushirikiano huu utaleta mabadiliko makubwa kupitia mfumo wake unaotumia teknolojia na kutoa rejesho au zawadi kwa wale wateja ambao watakua wameonesha kiwango kizuri cha mtindo wa Maisha kinachowaepusha na maradhi yasiyo ya kuambukizwa .” Mfumo wa bima ya afya ya pamoja wa Vitality Health International umejikita kwenye mpango wa kisayansi wa kubadilisha tabia ambao umethibitishwa kupitia utafiti huru kuweza kuleta matokeo bora ya afya. Mpango huo tayari umejumuishwa katika mfumo wa bima ya afya wa Vitality Health International. Mpango huu mahiri wa kubadilisha tabia unachanganya chambuzi za data, zawadi na motisha, ambazo huwahimiza watu moja kwa moja kufanya machaguo bora zaidi. Mfumo huo wa bima ya afya ya pamoja huwezesha wafanyakazi, waajiri na kampuni ya Vitality Health International kugawana kwa pamoja thamani na faida za mtindo wa maisha unaozingatia afya kwa kupunguza gharama za huduma za afya kwa waajiri na wafanyakazi, huku ikipunguza hatari za madai ya bima kwa Vitality Health International. Waajiri hurudishiwa hadi asilimia 10 ya fedha zao kwa kuwahimiza wafanyakazi wao kufanya mazoezi na kuishi mtindo mzuri wa maisha, ambao huanza kazi pale wanachama wanapokamilisha Tathmini ya Afya ya Vitality, hatua hiyo inaongeza mafao ya waajiriwa ambao ni wagonjwa wasiolazwa nchini kufikia hadi Dola za Marekani 100, kutegemeana na ukamilifu wa tathmini ya afya ya Vitality na ushirikiano chanya utakaotolewa katika programu za Vitality. Wafanyakazi wa kampuni mbalimbali wanaweza kushinda zawadi kabambe za kila wiki kwa kukamilisha malengo yao ya kila wiki (ikiwa ni pamoja na malengo yao binafsi, yale ya kiakili, siha na mtindo wa maisha), wafanyakazi watajinyakulia zawadi au wanaweza kutumia kiasi cha zawadi walichopata kama mchango wa chanjo za magonjwa kwa wenye uhitaji.. Mkurugenzi Mtendaji wa Vitality Health International, Emma Knox, anasema: “Msingi wa Mfumo wa Bima ya Afya ya Pamoja wa Vitality upo katika kuwatuza watu kwa mtindo bora wa maisha unaozingatia afya zaidi, ambao unaboresha ustawi wao wa kimwili na kiakili, unaokuza uzalishaji na kupunguza hatari za bima ya afya kwa waajiri. Kupitia mfumo huu, Vitality Health International inachangia katika kujenga jamii yenye afya bora kwa kuhakikisha kampuni mbalimbali na wafanyakazi wao wanabaki na mtindo wa maisha unao fanya wawe na afya njema.” Programu ya Vitality pia huwezesha Vitality Health International kuendesha semina mbalimbali kwa waajiri.Wigo mpana wa mafao ya bima za afyaIkijengwa kwa msingi wa mahitaji ya kipekee ya kila soko inakofanyia kazi, Vitality Health International imebuni wigo mpana wa mafao ya bima za afya inayoanzia hapa nchini, barani Afrika na duniani kote (ukiondoa Marekani), iliyopangwa kulingana na mahitaji na bajeti ya kila mwajiri. Vitality Health International inayo machaguo matano ya bima ya afya, yenye vipengele mbalimbali kwa mafao yote. Waajiri wanaweza kuchagua wafanyakazi wao kujumuishwa ndani ya Programu ya Vitality inayowafaa Zaidi. "Kupitia program hii , sio kwamba tumedhamiria kuongeza na kukuza upatikanaji wa bima peke yake bali tunahamasisha mtindo mzuri wa maisha kwa wateja wetu ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za serikali katika kupunguza na kuzuia uongezekaji wa magonjwa yasiyoambukiza’’ anahitimisha Dk Manek Malav
http://www.mwananchi.co.tz/mw/toleo-maalum/dmg-na-mkakati-wa-kuleta-mapinduzi-katika-sekta-ya-bahari-nchini-4776592
# DMG na mkakati wa kuleta mapinduzi katika sekta ya bahari nchini Bahari ni rasilimali muhimu katika kukuza uchumi, husasni kwa nchi zilizo na mwambao. Kuna sekta nyingi zinazotegemea bahari moja kwa moja au kwa njia isiyo ya moja kwa moja kama vile uvuvi, uchukuzi, utalii na nishati ya baharini. Rasilimali hiyo ina mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa dunia, hususani kwa nchi zenye mwambao. Eneo hili la maji lina fursa nyingi za kiuchumi ambazo zinachangia maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa kiwango kikubwa. Uvuvi ni mojawapo ya sekta muhimu zaidi zinazotegemea bahari. Bahari hutoa samaki na viumbe wengine wa baharini ambao ni chanzo cha chakula kwa mamilioni ya watu duniani kote. Hii inachangia kupunguza njaa na kutoa ajira kwa watu wengi, hususani katika nchi zinazoendelea. Bahari ni njia kuu ya usafirishaji wa bidhaa duniani. Karibu asilimia 90 ya biashara ya kimataifa inategemea bahari, ambapo meli zinatumika kusafirisha bidhaa mbalimbali kama mafuta, magari, vifaa vya umeme na bidhaa za kilimo. Utalii wa baharini ni chanzo kingine kikubwa cha mapato kwa nchi nyingi. Miji ya kitalii inayopatikana kando ya bahari huvutia watalii kutoka sehemu mbalimbali za dunia. Vivutio kama fukwe nzuri, michezo ya maji, na maeneo ya kupiga mbizi huvutia watu na kuleta fedha za kigeni. Tanzania ni miongoni mwa mataifa yanayojivunia kuwa na rasilimali hii muhimu ambayo imekuwa mhimili mkubwa katika kuchangia ukuaji wa uchumi. Hii ni kutokana na uwekezaji uliofanyika katika sekta ya bahari. Dar es Salaam Merchant Group (DMG) ni miongoni mwa wadau muhimu katika sekta ya bahari ambapo wamejipambanua kama moja ya kampuni za kizawa zinazofanya vizuri katika sekta hiyo hususan kwenye maeneo ya uvuvi na shughuli za uchukuzi. Ikiongozwa na misingi ya kuanzishwa kwake ambayo ni kuongeza thamani kwa jamii, kuweka malengo ya muda mrefu pamoja na kuwepo kwa manufaa ya pande mbili kwa kila eneo wanalofanya biashara. Mkurugenzi Mtendaji wa DMG, Rayton Kwembe anasema kampuni hiyo ya kitanzania iliyoanzishwa miaka tisa iliyopita inajihusisha na ufanyaji biashara (kununua na kuuza bidhaa), ushauri elekezi katika sekta mbalimbali hususani sekta ya bahari (marine) pamoja na shughuli za bahari (marine activities). Kwembe anasema katika utekelezaji wa majukumu haya wamekuwa wakishirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo Serikali ambayo imekuwa mdau wake mkubwa. “Tumefanya kazi na taasisi mbalimbali ikiwemo za Serikali kama vile; Ofisi ya Waziri Mkuu, Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu, Chuo cha Taifa cha Usafirishaji, Shirika la Huduma za Meli, Mamlaka ya Bandari, Wizara ya Uchumi wa Bluu Zanzibar na wadau wengine wa sekta binafsi “ anasema Kwembe. **Ubunifu, ujenzi na ukarabati wa meli ** Kwembe anasema mwaka 2017 DMG ilianzisha kitengo cha shughuli za bahari (Marine section) ambacho kilipewa jukumu la kufanya ubunifu, kutengeneza pamoja na kufanya ukarabati wa meli. “Sababu ya kuanzisha kitengo hichi ni kutokana na fursa tulizoziona katika sekta ya bahari kwani ni sekta yenye fursa nyingi za kusaidia ukuaji wa uchumi ambazo hazijaweza kutumiwa ipasavyo, lakini mkakati na juhudi za Serikali za kuamua kuipa jicho la kipekee sekta hii ikiwemo kufufua shirika la meli pamoja na kutekeleza miradi ya ujenzi wa meli ni sababu kuu zilizotushawishi kuingia katika sekta hii,” anasema Kwembe. DMG ni kampuni ya pili ya kitanzania kupewa leseni ya kufanya shughuli za ukandarasi wa bahari (marine contractor) nchini. Kwembe anasema kuna mataifa makubwa duniani ambayo uchumi wake umekuwa kutokana na kuwekeza katika shughuli za bahari ikiwemo Korea Kusini. Juhudi za Serikali katika kuhakikisha sekta hii inakua na kuongeza tija katika uchumi iliwasukuma DMG kutafuta wadau mbalimbali wa kufanya nao kazi wenye teknolojia za kisasa na utaalamu wa masuala ya meli na kuingia nao makubaliano ya ushirikiano jambo lililowawezesha kwenda na kasi ya Serikali. Kwembe anasema hatua hiyo iliwawezesha kuwa kampuni ya kitanzania iliyoaminiwa na Serikali kwa kuweza kushiriki katika miradi mbalimbali ya ujenzi na ukarabati wa meli. “Mradi wa kwanza tulioahiriki ulikua wa ujenzi wa meli ya MV Mwanza Hapa Kazi tu ambapo tulipewa kazi na Mkandarasi Mkuu kutoa huduma kwenye mradi ikiwepo kuajili wataalamu wa kizawa, kusimamia masuala ya kiutawala kwenye mradi hasa yanayohisisha maudhui ya ndani (local content). Huu ndio mradi ambao ulitifungulia njia na kuanza kufahamika na wadau wengine,” anasema Kwembe. Anasema wakati wanaingia mwaka 2017 walijewekea lengo la kuhakikisha wanakuwa kampuni namba moja ya kitanzania katika sekta hiyo lakini pia kuliteka soko la Afrika lengo ambalo anaamini wameanza kulifikia kwa kiasi kikubwa. “Katika kipindi cha miaka minne tumeweza kufanya kazi na taasisi zote za Serikali ambazo zinamiliki meli ikiwa ni pamoja na Kampuni ya Huduma za Meli ambayo kwa sasa ni wateja wetu wakubwa. Kampuni hiyo kwa sasa tunatekeleza nayo miradi mitatu ambayo ni; mradi wa kimkakati wa kufufua meli ya MV Liemba mradi huu ni wa kihistoria lakini Serikali imetuamini na kutukabidhi. Kwa sasa mradi umeshaanza na fedha za awali tushalipwa,” anasema Kwembe. Anasema mradi mwengine ni ukarabati wa meli kubwa ya mafuta iliyopo jijini Mwanza pamoja na ukarabati wa tugboat moja kazi ambazo mikataba yake imeshasainiwa na malipo ya awali yameshalipwa hivyo kwa upande wa ukarabati tuna kazi tatu ambazo tunafanya na Kampuni hiyo. Kwa upande wa kazi za usimamizi kampuni hiyo pia imetupa kazi mbili katika miradi ya ujenzi wa meli mbili za mizigo katika ziwa Victoria na Tanganyika ambayo inatekelezwa na Kampuni za Uturuki. Kwembe anasema mbali na kampuni hiyo pia wamefanya kazi na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) katika utekelezaji wa miradi mitano. “TPA tumetekeleza miradi ya ukarabati wa boti ndogo ya kubeba wafanyakazi wa meli (MV Aida Kondo) katika bandari ya Tanga pamoja na kuingia makubaliano ya kuuza boti za fiber, uuzaji wa vipuri vya boti za Mtwara na Tanga, pia tumefanya kazi ya ukarabati wa vivuko vya Temesa ikiwemo kivuko cha MV Tanga, MV Kitunda kilichopo Lindi, MV Kilambo kikichopo Mtwara pamoja na kuanza ujenzi wa meli mpya ya kwenda Mafia na Nyamisati,” anasema Kwembe. Kuhusu uwekezaji katika teknolojia za kisasa za ujenzi wa meli anasema kwa sasa wanashirikiana na Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) pamoja na Chuo cha Bahari (DMI) kwa ajili ya kuchukua wahitimu na kuwakutanisha na wataalamu kutoka Korea kwa ajili ya kupata uzoefu. “Kwa sasa tuna wataalamu watano kutoka kwenye vyuo hivi ambao wanapata mafunzo kutoka kwa mtaalamu kutoka kwa washirika wetu wa Korea ili kuhakikisha tunakuwa na rasilimali yenye uwezo wa kutumia teknolojia hizo. Lakini pia kwa sasa tuna maeneo yetu wenyewe ya kufanyia kazi (facilities) ambayo moja iko Kimbiji na nyingine iko Zanzibar eneo la Mangapwani,” anasema Kwembe. **Uvuvi wa Bahari Kuu ** DMG ni kampuni ambayo ilifanya utafiti kuhusu changamoto zinazowakabili wavuvi wengi nchini kwenda kuvua katika bahari kuu na kugundua kuwa sababu kubwa ni ukosefu wa vyombo ambavyo vinawawezesha kufika bahari kuu pamoja na ukosefu wa taarifa sahihi kuhusu bahari kuu. Katika kuhakikisha inapunguza changamoto hiyo, DMG iliingia makubaliano na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ambapo benki hiyo imetoa kiasi cha Sh 1 bilioni kwa DMG kwa ajili ya kuanza ujenzi wa kisasa wa boti za kufanyia uvuvi wa bahari kuu. “Baada ya kufanya utafiti na kugundua changamoto hizo tulienda kufanya mazungumzo na TADB ma wakakubali kutufadhili Sh 1 bilioni kwa ajili ya kujenga meli nne za uvuvi za kisasa ambapo kati ya hizo meli moja imekamilika na inatarajiwa kuanza kazi hivi karibuni, ya pili inatarajiwa kuanza kazi Desemba mwaka huu ya tatu Aprili mwaka 2025 na ya nne Oktoba, 2025 ,” anasema Kwembe. Tunaamini boti hizi zitaenda kuleta mageuzi makubwa katika uvuvi wa Bahari kuu. **Maadhimisho ya Siku ya Bahari Duniani ** Kama mdau muhimu wa sekta ya bahari, DMG wamejiandaa kuadhimisha siku ya bahari duniani mwaka huu kwa kufanya matukio mawili makubwa. “Tunatarajia kufanya uzinduzi wa boti zetu za kisasa za uvuvi na kufanya safari ya kwanza kwenda bahari kuu lakini pia tutafanya usafi katika maeneo ya bahari tunayofanyia kazi,” anasema Kwembe.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/mchengerwa-aagiza-mchakato-uanze-kuipandisha-hadhi-wilaya-ya-arusha-4783988
# Mchengerwa aagiza mchakato uanze kuipandisha hadhi Wilaya ya Arusha ## Muktasari: **Waziri huyo ametoa maagizo hayo baada ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda kuwasilisha ombi la halmashauri hiyo iliyopo wilayani Arumeru kuomba kupandishwa hadhi.** **Arusha**. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mohamed Mchengerwa ameuagiza uongozi wa Mkoa wa Arusha kuanza mchakato wa kuomba kuipandishwa hadhi Halmashauri ya Wilaya ya Arusha kuwa Halmashauri ya Mji wa Arusha. Mchengerwa ameyasema hayo leo Jumatano Oktoba 2, 2024 wakati akizungumza kwenye ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo baada ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda kuwasilisha ombi la halmashauri hiyo kupandishwa hadhi. Mchengerwa amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa wa Arusha, Missaile Mussa kwa kushirikiana na uongozi wa wilaya, kuanza mchakato kuanzia ngazi ya wilaya, mkoa na wakijiridhisha wapeleke Tamisemi kwa ajili ya kupelekwa kwa Rais Samia Suluhu Hassan. “Nawaagiza Katibu Tawala wa Mkoa na Wilaya, mchakato huo uanzie kwenye wilaya uende kwenye RCC halafu mkoa utatuletea Tamisemi na tukijiridhisha vigezo vimetimia, tutapeleka kwa Rais ipandishwe hadhi na kuwa Halmashauri ya Mji,” amesema. “Anzeni mchakato ili vigezo vilivyowekwa kisheria kama mmekidhi tupeleke kwa Rais. Dhamira ya Rais ni miji ambayo imeshakua kuikuza zaidi kuimarisha mamlaka ya utawala katika miji ili wananchi wasogezewe huduma,” ameongeza. Kuhusu barabara, amesema atawasiliana na Wakala wa Huduma wa Barabara za Vijijini na Mijini (Tarura) ili barabara zinazohitaji udharura zifanyiwe marekebisho, zipitike msimu wote wa mwaka. “Tutapita huko kujionea na kwa kuwa Tarura tutazingalia kwa sababu fedha za dharura zipo na kwa kuwa bajeti kutoka Sh250 bilioni hadi Sh1.5 trilioni,” amesema. Awali, Makonda aliwasilisha maombi mawili ambapo la kwanza alieleza kuwa Wilaya ya Arumeru ni moja ya wilaya zenye barabara mbovu. “Moja ya wilaya ambayo inahitaji msaada na jicho la kipekee upande wa barabara ni wilaya hii ambayo ina halmashauri mbili na kwa namna ya kipekee barabara hizi ziko ambazo zinaenda kwenye kuchochea maendeleo ya wananchi na zikijengwa zitaongeza uchumi,” amesema. Makonda amesema walifanya ziara na timu ya mkoa na miongoni mwa malalamiko waliyopokea ni pamoja na ya migogoro ya ardhi kuibuka katika mamlaka ya mji mdogo. “Halmashauri ya Wilaya ya Arusha wanatamani kama Arusha tuna Jiji, basi na wao wapandishwe hadhi kuwa manispaa,” amesema Makonda.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/tanzania-marekani-kupambana-kichaa-cha-mbwa-watoto-watajwa-kuwa-hatarini-4783996
# Tanzania, Marekani kupambana kichaa cha mbwa, watoto watajwa kuwa hatarini ## Muktasari: **Kichaa cha mbwa bado ni tishio la afya ya umma nchini Tanzania hasa katika jamii zenye uelewa mdogo na upatikanaji hafifu wa huduma za mifugo.** **Mwanza. **Wakati ugonjwa wa kichaa cha mbwa ukitajwa kusababisha vifo vya zaidi ya watu 59,000 duniani kila mwaka, Serikali ya Tanzania na Marekani zimeamua kuungana ili kupambana nao ikiwemo kuelimisha umma juu ya ugonjwa huo. Hatua hiyo inakuja ikiwa kichaa cha mbwa bado ni tishio kubwa la afya ya umma nchini Tanzania hasa katika jamii zenye uelewa mdogo na upatikanaji hafifu wa huduma za mifugo. Shirika la Marekani la Maendeleo ya Kimataifa (USAID), kupitia Mradi wa Breakthrough Action kwa kushirikiana Ofisi ya Waziri Mkuu sehemu ya Afya Moja, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Afya, na Ofisi ya Rais (Tamisemi), wametumia fursa ya maadhimisho ya Siku ya Kichaa cha Mbwa kama sehemu ya juhudi za kimataifa za kupambana na ugonjwa huo. Kupitia kampeni ya kitaifa ya "Holela-Holela Itakukosti," yenye lengo la kuiwezesha jamii kupambana na ugonjwa huo, Usaid na Serikali ya Tanzania inawakumbusha wananchi kuwajibika na kuondoa vikwazo ili kushinda vita dhidi ya hatari ya ugonjwa huo. Awali, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Kichaa cha Mbwa, ambayo hufanyika kila mwaka Septemba, 28 kampeni ya "Holela-Holela Itakukosti," ambayo tafsiri yake ni uzembe ni gharama, ilichukua nafasi kubwa katika kuongeza uelewa kuhusu kichaa cha mbwa, ugonjwa unaosababisha vifo vya zaidi ya watu 59,000 duniani kila mwaka. Tukio hilo la kitaifa liliongozwa na Abdul Mhinte, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ambaye amesisitiza umuhimu wa elimu kwa jamii na mikakati ya chanjo katika kupambana na ugonjwa. Aidha amehimiza kuimarishwa kwa ushirikiano kati ya maofisa wa afya ya umma na jamii za mitaa ili kuimarisha mwitikio wa pamoja. “Kichaa cha mbwa kinaweza kuzuilika. Lengo letu ni kuhakikisha kila mbwa nchini Tanzania anapatiwa chanjo, na kila mwananchi anajua cha kufanya endapo atang’atwa na mbwa. Kila jamii inapaswa kuchukua jukumu lake katika vita hivi.” Msisitizo wake juu ya elimu na ushirikiano ulipeleka ujumbe wa matumaini kwa waliohudhuria. Kampeni hiyo inalenga jamii kwa kutoa ujumbe muhimu kuhusu kichaa cha mbwa, kuwachanja na kutafuta huduma za afya mara baada ya tukio la kung’atwa na mbwa. Watoto, ambao ni miongoni mwa walio hatarini zaidi kuathiriwa na kichaa cha mbwa, wanapewa elimu juu ya kuepuka mwingiliano kama kuwachokoza mbwa hasa wasiowafahamu na wanyama wenye uwezekano wa kuwa na maambukizi. Shuhuda kadhaa zinaonensha umuhimu wa kampeni hii. Revina, mama wa watoto watatu kutoka Mwanza:"Kabla ya kampeni, sikuwa najua hatari ya kichaa cha mbwa. Tulipojifunza kuwa mbwa wetu wanapaswa kuchanjwa, tulichukua hatua mara moja. Sasa, nina amani kuwaacha watoto wangu kucheza nje." Kampeni ya Holela-Holela pia inalenga kupambana na sababu zote zinazochangia kuwepo kwa ugonjwa wa kichaa cha mbwa kama vile uelewa mdogo, juhudi hafifu za chanjo, na usimamizi usio salama wa wanyama.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/simbachawe-ataja-umuhimu-wapinzani-kukosoa-atoa-angalizo-4784020
# Simbachawe ataja umuhimu wapinzani kukosoa, atoa angalizo ## Muktasari: **Waziri Simbachawene amebainisha kwamba wapinzani wanapokosoa wanatimiza matakwa ya kikatiba, hata hivyo amewataka wazingatie sheria katika kutekeleza wajibu wao.** **Rorya**. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene amesema hakuna sababu ya viongozi wa Serikali na wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kukasirika pale vyama vya upinzani vinapowakosoa kwani kwa kufanya hivyo, vyama hivyo vinatimiza takwa la kikatiba. Simbachawene ameyasema hayo leo Jumatano, Oktoba 2, 2024 kwenye mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Utegi wilayani Rorya ambapo vyama vya upinzani vimetengezwa na CCM ili kukupinga hatua ambayo inachochea chama hicho cha CCM kutekeleza wajibu wake ipasavyo. “Katika kutupinga wanatimiza wajibu wa kikatiba, lazima tuwasikilize, lazima tuvilee vyama vya upinzani na wanapotupinga tuwasikikilize na tutekeleze yale Watanzania wanayoyataka na kamwe hawawezi kututoa madarakani,” amesema. Amebainisha kuwa wapinzani siyo watu wabaya, isipokuwa wanawakumbusha kutekeleza yale wanayopaswa kufanya na kwamba pale wanapoyatekeleza kwa ufasaha, wananchi wanazidi kuwaunga mkono, hivyo Serikali inakuwa na uhakika wa kuendelea kushika madaraka huku akiongeza kuwa bila CCM hakuna mpinzani. Hata hivyo, Simbachawene amesema pamoja na uhuru wa kukosa na kupinga, ni vema vyama vya upinzani vikazingatia misingi ikiwemo masuala ya amani, umoja, mshikamano na utulivu na kwamba Watanzania kamwe wasidanganyike na mtu ambaye anataka kuvunja misingi hiyo. “Huwezi kuwa na nchi ya kidemokrasia kama Tanzania bila kuwa na upinzani lakini kazi ya upinzani sio kuvuruga nchi, kwa hiyo niwakumbushe wapinzani kuzingatia misingi ya nchi na mjue uwepo wenu unategea CCM,” amesema. Amesema nchi ya Tanzania ni ya muhimu kuliko vyama vya siasa kwani madaraka na vyeo ni utaratibu tu, hivyo vyama vya siasa havitakiwi kuathiri misingi ya nchi. Katika hatua nyingine, Simbachawene ameuagiza uongozi wa Mkoa wa Mara kufanya uchunguzi kuhusu ujenzi wa jengo la ukumbi katika Halmashauri ya Wilaya ya Rorya baada ya kutoridhishwa na thamani ya fedha katika mradi huo. “Mimi sio mhandisi lakini kwa macho ya kawaida kiasi cha fedha kilichotumika na jengo lenyewe ni vitu viwili tofauti, niuagize uongozi wa mkoa kufanya uchunguzi kujiridhisha kuhusu thamani ya fedha na kazi iliyofanyika hapa kabla ya uzinduzi wa jengo,” amesema. Ametolea mfano wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma ambayo hadi sasa imegharimu takriban Sh1.5 bilioni huku kukiwa na majengo zaidi ya 16 ambayo mengi yamekamilika ikilinganishwa na ukumbi huo wenye thamani ya Sh1.25 bilioni. “Hapa kuna jengo moja hata tukisema tulimege, tutapata majengo madogo manne, kule kuna majengo zaidi ya 16, tena makubwa yenye gharama sawa zilizotumika kwenye hii miradi miwili, ni sawa lakini kwa macho ya kawaida thamani ya fedha hailingani,” amesema. Amesema fedha za utekelezaji wa miradi ya maendeleo inapatikana kwa jitihada nyingi, hivyo ni vyema miradi inayotekelezwa iakisi hali halisi na kwamba suala la ubora wa miradi pia ni la kupewa kipaumbele. Awali, akitoa taarifa juu ya mradi huo, mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya, Ramadhani Mcharo amesema ukumbi huo wa kisasa hadi kukamilika unatarajiwa kugharimu Sh1.25 bilioni. Amesema hadi sasa ujenzi umegharimu kiaisi cha Sh750 milioni ambapo umefikia asilimia 95 ya utekelezaji wake na kwamba jengo hilo likikamilika litatumika kwenye mikutano yote ya halmashauri hiyo ikowepo mikutano ya baraza la madiwani. “Tumepokea Sh750 milioni ambazo ndizo tumepokea na ujenzi huu ulianza Januari 2022 kwa mfumo wa force akaunti, ukumbi ukikamilika mbali na kutumika kwenye mikutano lakini pia utakuwa chanzo cha mapato kwani utakuwa ukikodoshwa kwa shughuli mbalimbali kwa wananchi,” amesema. Mkuu wa Mkoa wa Mara, Evans Mtambi amekumbusha wananchi kuwa tayari kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa, Novemba 27, 2024. “Ili kupiga kura au kupigiwa kura kwenye uchaguzi huu, ni lazima uwe umejiandikisha kwenye daftari la mkazi, niwaombe sote kwa pamoja itakapofika Oktoba 11, 2024 tukajiandikishe tayari kutimiza wajibu wetu wa kidemokrasia na kikatiba ifikapo Novemba,” amesema. Mtambi amesema uchaguzi huo ni wa muhimu katika maendeleo ya nchi, hivyo kila Mtanzania mwenye sifa anapaswa kushiriki kikamilifu.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/wadau-wa-haki-jinai-wabainisha-tishio-la-uhalifu-wa-mtandao-4783884
# Wadau wa haki jinai wabainisha tishio la uhalifu wa mtandao ## Muktasari: **Jumla ya washiriki 60 kutoka taasisi mbalimbali zinazohusika na mfumo wa haki jinai wanahudhuria mafunzo maalumu kuhusiana na tatizo la uhalifu wa kimtandao huku wadau wakionesha unavyogharimu matrilioni ya fedha duniani, Afrika.** **Dar es Salaam**. Wadau wa haki jinai kutoka taasisi mbalimbali nchini Tanzania wamenolewa kwa kupewa mafunzo ya namna ya kukabiliana na tatizo la uhalifu wa kimtandao huku wawezeshaji wa mafunzo wakibainisha hali ya uhalifu huo ilivyo nchini na duniani. Mafunzo hayo ya siku tatu yanayofanyika jijini Dar es Salaam, yamefunguliwa leo Jumatano, Septemba 2, 2024 na Jaji wa Mahakama ya Rufani, Augustine Mwarija kwa niaba ya Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma. Mafunzo hayo yameandaliwa na Chuo cha Uongozi wa Mahakama, Lushoto (IJA) kwa kushirikiana na Sekretarieti ya Jumuia ya Madola kwa ufadhili wa Serikali ya Uingireza. Mkuu wa Utawala wa Sheria wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola, Dk Elizabeth Macharia, amesema Afrika inapoteza Dola za Marekani milioni 4 ambazo ni karibu na asilimia 10 ya pato lake, kwa mwaka kutokana na uhalifu wa kimtandao. Macharia amesema duniani gharama za uhalifu wa kimtandao zinatarajiwa kufikia Dola 23.84 trilioni kufikia mwaka 2027 kutoka Dola za Marekani 8.44 trilioni mwaka 2022. Akifungua mafunzo hayo, Jaji Mwarija amesema mafunzo hayo yanaakisi juhudi za Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola katika kupunguza kiwango na athari za uhalifu wa mitandaoni katika nchi za Jumuiya ya Madola. Jaji Mwarija amesema uhalifu wa kimtandao unaleta changamoto ambayo inaendelea kukua kutokana na kasi ya ukuaji wa teknolojia na kwamba mafunzo hayo yatawawezesha washiriki kubadilishana maarifa, uzoefu, na namna bora ya ushughulikiaji makosa hayo. Amesema mafunzo hayo yataimarisha maarifa na ujuzi wa majaji, waendesha mashtaka na wapelelezi kuhusiana na maendeleo ya hivi karibuni katika sheria za uhalifu wa kimtandao na namna ya kushughulikia ushahidi wa kielektroniki. Pia, amesema watapanua uelewa wao wa sheria zinazosimamia makosa ya uhalifu wa kimtandao na kujadili changamoto wanazokabiliana nazo katika upelelezi, kuendesha mashtaka na kuamua kesi hizo. Jaji Mwarija amesema ukusanyaji, uhifadhi na upokewaji wa ushahidi wa kielektroniki ni mambo muhimu kuhakikisha mafanikio katika kuendesha kesi na uamuzi wa haki. “Kama mlinzi wa haki, mahakama ina jukumu la msingi kuhakikisha kuwa kesi za uhalifu wa kimtandao zinaamuriwa kwa haki na kwa ufanisi wakati ikizingatia utawala wa sheria na kulinda haki za binadamu,” amesema Jaji Mwarija. Jaji Mwarija amesema wapelelezi wana jukumu la kukusanya na kuchanganua na kuhifadhi ushahidi na waendesha mashtaka wana jukumu la kuhakikisha kuwa wahalifu wa kimtandao wanafikishwa mbele ya sheria. Hivyo amesema wanapaswa kuwa ufahamu sheria za makosa ya kimtandao na uwezo wa kuwasilisha ushahidi tata wa kielektroniki wa kwa namna inayoeleweka kwa mahakama. “Kwa kufanya kazi kwa karibu na wapelelezi, waendesha mashtaka wanafanya jukumu la msingi katika kuhakikisha kuwa kesi za uhalifu wa kimtandao zinaendeshwa kwa ufanisi na kwa haki,” amesema Jaji Mwarija. Kwa upande wake, Naibu Balozi wa Uingereza Nchini, Sally Hedley amesema kuwa kuwa tatizo la uhalifu wa kimtandao halina mipaka na kwmaba ni tatizo kubwa linalohitaji unyumbulifu kutoka vyombo vya utekelezaji sheria vya ndani kikanda na kimataifa. “Uzoefu wetu binafsi nchini Uingereza unaonesha kwamba tishio linalosababishwa na uhalifu wa kimtandao linaendelea kukua na kuleta changamoto mpya za kiusalama”, amesema Hedley. Akizungumzia tatizo hilo katika mataifa ya Afrika, amesema taarifa za Shirika la Polisi wa Kimataifa Interpol) zinaonesha linaendelea kukua kwa asilimia 25 kila mwaka na kwamba hakuna taasisi au mtu binafsi aliye salama. Awali, Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) kilichoandaa mafunzo hayo, Jaji wa Mahakama ya Rufani, Dk Paul Kihwelo amesema mafunzo yanawashikirikisha majaji 15 akiwemo mmoja kutoka Mahakama ya Zanzibar. Amewataja washiriki wengine ni manaibu wasajili wanne, mahakimu wakazi wa mkoa 10, mahakimu wakazi wa wilaya watano na mahakimu wengine wa kawaida, wapelelezi sana na waendesha mashtaka wanane kutoka mikoa mbalimbali. “Tumewaleta hawa wote watatu (wapelelezi, waendesha mashtaka na majaji na mahakaimu) ili wewe na uelewa wa pamoja wa namna ya kushughulikia makosa ya namna hiyo”, amesema Jaji Kihwelo na kuongeza: “Na hi inatokana na kwamba sasa hivi uhalifu kwa kiasi kikubwa zaidi unafanyika katika mtandao kuliko uhalifu unaofanyika kwa njia ya kawaida.” Akitoa mfano wa uhalifu wa wizi wa fedha duniani na bila kutoa takwimu, Jaji Kihwelo amedokeza kuwa kwa duniani fedha zinazoibiwa kwa njia ya mtandao ni nyingi zaidi kuliko kiasi cha fedha zinazoibiwa kwa njia za kawaida. Amesema mbali na wawezeshaji wawili wa ndani, wawezeshaji wengi wa mafunzo hayo wametoka nchi za nje kama Uingereza, Dubai na nchi nyingine za Jumuiya ya Madola ambao watachambua sheria zilizopo nchini tayari. Wakizungumzia mafunzo hayo, washiriki wa mafunzo hayo, Wakili wa Serikali Mwandamiz, Ellen Masululi na Hakimu Mkazi Mkuu Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa wa Iringa, Honorious wamesema kuwa mafunzo hayo yatawaongezea ujuzi na maarifa katika kutekeleza majukumu yao. Wakili Masululi mafunzo hayo yatawasaidia katika hatua mbalimbali za utekelezaji wa majukumu yao kama vile kuamua kama kesi ifunguliwe au isifunguliwe baada ya kusoma majalada ya upelelezi kutoka polisi na uendeshaji mashauri mahakamani. “Kwa hiyo sasa ufahamu huo tutakaoupata kupitia semina hii, utatusaidia kujua kama ushahidi nilionao wa makosa ya kimtandao na ushahidi wa Kielektroniki unatosha kwenda mahakamani au la,” amesema Masululi na kuongeza: “Lakini pia yatawasaidia kuongoza upelelezi kwani sisi mawakili wa Serikali tuna nafasi ya kuongoza wapelelezi na kuwashauri namna ya kufanya katika kesi husika na tutakuwa kwenye nafasi nzuri ya kutoa ushauri kuishauri ofisi.” Hakimu Kando amesema kuwa anatarajia kuwa mafunzo hayo yatawajengea uwezo wa kutoa kuamua kesi wanazokumbana nazo hasa katika kipindi hiki ambacho kuna uhalifu mwingi wa kimtandao na makosa mengi yamekuwa yakifanyika kwa njia ya mitandao. Amesema kuwa kumekuwa na mabadiliko ya sheria ambapo kwa Sasa ushahidi wa kielektroniki unapokewa mahakamani na kwamba kwa kukizingatia kwamba makosa haya ni mapya na Sheria pia ni mpya, mafunzo hayo sasa yatawajengea uwezo namna kuamua kesi bila kukosea hasa. Amesema kuwa uzoefu unaonesha makosa ya mtandao yanatokea ni mengi na sheria bado ni mpya na ufahamu bado ni mdogo kwa watu wengi na kwamba baada ya mafunzo hayo watakuwa wamejengewa uwezo wa pamoja. “Tunategemea wapelelezi watapeleleza kesi zao vizuri kwa mujibu wa Sheria na itamrahisishia pia mwendesha mashtaka kuendesha kesi yake vizuri mahakamani na tunategemea Mahakama itatenda haki kwa mujibu wa mnyororo mzima wa haki jinai Kwa maana ya upelelezi, uendeshaji mashtaka na uamuzi,” amesema.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/jinsia-na-afya
Hello Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa Ready to continue your informative journey with us? Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features. Reclaim your full access. Click below to renew. Subscribe for a month to get full access
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/ongezeko-la-maji-ziwa-tanganyika-maumivu-kwa-wananchi-kigoma-ujiji-4717012
# Ongezeko la maji Ziwa Tanganyika, maumivu kwa wananchi Kigoma Ujiji ## Muktasari: **Baadhi ya wakazi wa eneo hilo wamehama na waliobaki wanaishi kwa hofu kwa kuwa maji bado yanaongezeka.** **Kigoma**. Si ajabu Ziwa Tanganyika kuongezeka kina cha maji kutokana na sababu mbalimbali ikiwamo mvua, lakini hali ni tofauti kwa mwaka huu. Kwa mujibu wa takwimu za mamlaka ya Bonde la Ziwa Tanganyika, mvua zilizonyesha Mkoa wa Kigoma, kiwango cha maji ziwani kiliongezeka kutoka usawa wa bahari hadi mita 777.17 Aprili mwaka huu ikilinganiswa na mita 776.35 Mei 2023 na mita 776.27 Mei 2022. Kuongezeka kwa kina cha maji kulichangiwa kwa kuongezeka kwa kiwango cha mvua kwa wastani wa asilimia 28 hadi kufikia milimita 1,071.9 mwaka 2023/24 ikilinganishwa na milimita 836.8 miaka miwili iliyopita. Kutokana na ongezeko hilo la mvua, maji yalijaa maeneo mengi mkoani Kigoma. Hata hivyo, awali mamlaka husika zilieleza maji yangeweza kufika katika maeneo yaliyo karibu na ziwa hilo, hivyo kuleta athari kwa wananchi. Miongoni mwa maeneo hayo, ni Mtaa wa Mgumile uliopo Kata ya Kagera, Manispaa ya Kigoma Ujiji, uliokumbwa na mafuriko na kusababisha makazi na mashamba ya watu kusombwa. Kata hiyo inayokadiriwa kuwa na wakazi 9,916 kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, robo ya wakazi wake, maeneo yao yalizingirwa na maji. Baadhi ya wakazi wa eneo hilo wamehama na waliobaki wanaishi kwa hofu kwa kuwa maji bado yanaongezeka. Malilo Zaidi, aliyekaa Mtaa wa Mgumile tangu mwaka 1983 anasema, “hali hii haijawahi kutokea kwa zaidi ya miaka 40, Serikali inapaswa kuangalia suala hili kwa undani na kutupatia maeneo mengine ya makazi na kilimo.” Mwaka huu yameshuhudiwa mafuriko yaliyoharibu makanisa, hospitali, shule, barabara, masoko, hoteli na maeneo ya fukwe huku baadhi ya wananchi kukosa makazi. Jalala Shabani, mama wa watoto tisa anayeishi kwenye nyumba ya nne sasa kwa kuhama mara kadhaa, baada ya kukimbia maji yanayoongezeka. Hali hii imemlazimu kupika kwa jirani na kuwabeba watoto wake kwenda kulala usiku huko. “Ninaishi na mume wangu na watoto, maji yalianza kwenye nyumba ya kwanza tukasogea kukimbia maji tukahama lakini kila tukisogea na kuhama maji nayo yanasogea,”anasema Jalala. Anasema maji yameharibu nyumba zao, vifaa vya ndani na mashamba ya mchikichi, mahindi na maharagwe. Jalala anasema kwa sasa anategemea vibarua kuendesha maisha, hali ambayo imerudisha nyuma maendeleo yake. “Kukosa huduma za kijamii kama shule, hospitali na makanisa, kumetuathiri sana na baadhi ya watoto wangu hawajakwenda shule kwa miezi minne sasa. “Ninaiomba Serikali msaada wa makazi na huduma za kijamii ili kukabiliana na hali hii ngumu,” Jalala. Mjumbe wa Mtaa wa Mgumile, Ukiwa Sadi ameathirika na mafuriko yaliyoharibu biashara yake ya chakula maarufu kama mamantilie. Sadi aliyekuwa na kibanda akiuza chakula nyumbani kwake, maji yaliingia na kuharibu mali na bidhaa zake zote za biashara. “Hii ilinilazimu kuhama na kuendeleza maisha sehemu nyingine. Ingawa nimejaribu kujipanga upya na kuanza kupika tena, hali ya kibiashara ni mbaya kutokana na ukosefu wa wateja,” anasema Sadi. Anasema mtaji wake umepungua kwa kuwa amekuwa akinunua mchele kilo tano hadi kumi na kuuza, ikilinganishwa na kilo 100 za awali. **Afya na usalama** Zainabu Sabuni anasema maisha yao yamekuwa hatarini kwa kutumia maji ya visima ambayo si salama. Anasema wamekuwa wakihofia magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu na homa za matumbo. Zainabu anasema wamekuwa wakitumia maji hayo kwa kunywa na matumizi mengine, huku wakihofia magonjwa ya ngozi na minyoo. Anasema visima hivyo, vimechimbwa baada ya kukosa maji kwa muda mrefu. Baadhi ya wakazi wananunua majisafi kwa Sh1,500 kwa ndoo, lakini wengine wanatumia maji ya visima kwa kukosa uwezo wa kununua. Zena Haruna, anasema usalama wao unatishiwa na wanyama wakali kama viboko kuvamia makazi, kujeruhi watu na kuua mifugo. “Tunaishi kwa wasiwasi na kuhofia usalama wetu kutokana na wanyama wanaokuja hasa nyakati za usiku kutafuta chakula na kufanya uharibifu,”anasema Zena. Diwani wa Kagera, Gregory Kebelezo anasema Mtaa wa Mgumile umekumbwa na mafuriko makubwa, yakiathiri kaya 60 kati ya 306 na kusababisha wakazi kuhama. Vitu vilivyoathiriwa anasema ni mashamba ya michikichi, mpunga, mahindi na maharagwe. “Shule pia zimejaa maji, watoto wameshindwa kusoma. Ofisi ya mkurugenzi wa manispaa imepanga eneo lingine kwa ajili ya ujenzi wa shule. Hakuna vifo vilivyotokea, lakini mali na makazi yameharibiwa na wakazi wameathirika kiuchumi,”anasema Kebelezo. Pia, huduma ya majisafi imeathirika kutokana na kujaa kwa Mto Luiche na uharibifu wa miundombinu, inayosubiri kurekebishwa na wataalamu wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Kigoma (Kuwasa). **Uvuvi na biashara** Suala la usafirishaji na biashara katika Bandari Ndogo ya Kibirizi, mkoani Kigoma limeathiriwa na ujazo wa kina cha maji katika Ziwa Tanganyika. Licha ya Serikali kuwahamishia wafanyabiashara wa samaki na dagaa kwenye eneo jipya, lakini wamepoteza wateja na biashara zao kuyumba. Zabibu Hussein, mfanyabiashara wa dagaa anasema pamoja na kuhamia soko jipya mauzo yameshuka. “Tumepoteza wateja, soko hili watu hawajalizoea. Tunapata mawazo kwa kuwa fedha za mitaji zenyewe tulikopa,”anasema Zabibu. Selina Jeremia anasema licha ya kwamba hakuna wateja kwenye soko hilo, anaoimba Serikali isiwahamishe tena kwa kuwa kuhamahama imekuwa kero kwa biashara zao. “Eneo hili lipo kwenye mwinuko, tunaiomba Serikali ituache hapa wateja watazoea,” anasema Selina. Kata ya Katubuka, Manispaa ya Kigoma Ujiji, pia ni moja ya eneo ambalo maji yamejaa na kusababisha mafuriko katika makazi ya watu na vibanda vya biashara. Mfanyabiashara Harrison Kinoni anasema mabucha ya nyama ya nguruwe yameathirika na wateja wamepungua. “Tumehamia upande wa pili wa barabara, lakini biashara imekuwa ngumu, awali tuliuza hadi nyama ya nguruwe watatu kwa siku lakini sasa hata nguruwe mmoja haishi,”anasema Kinoni. Diwani wa Katubuka, Moshi Mayengo anasema nyumba zaidi ya 60 zimezungukwa na maji, hali iliyowahi kutokea mwaka 1989/90. Mayengo anasema Serikali ya mkoa ipo kimya, licha ya jitihada zake za kuwasiliana na Wakala ya Barabara za *Vijijini*na Mijini (Tarura), hakuna hatua zilizochukuliwa. **Kauli ya Bonde la Ziwa Tanganyika** Mhandisi Odemba Kornel kutoka Bonde la Ziwa Tanganyika, anasema mwaka 2024, kipimo cha maji ziwani kimefikia mita 777.22 kutoka usawa wa bahari, kikilinganishwa na mita 747 mwaka 2018, kutokana na mvua kubwa. “Mabadiliko ya tabianchi yanasababisha maji kujaa na kupungua, historia inaonesha hali kama hii ilitokea miaka ya 1960. Tunashauri wananchi kuepuka uwekezaji au shughuli za kimaendeleo karibu na ziwa ili kuepuka hasara,”anasema Kornel. Anasema wawekezaji na wadau wanashauriwa kuchukua takwimu za maji kutoka ofisi za bonde kabla ya kuanza miradi. Kornel anasema Bonde la Ziwa Tanganyika limeweka alama kuonesha maeneo hatarishi na wataendelea kufanya hivyo. Anasema wana mpango wa kuzunguka tena katika mwambao mwa Ziwa Tanganyika baada ya maji kuongezeka zaidi kuliko awali ili kuweka alama na kuwapa tahadhari wananchi. Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Thobias Andengenye anasema Wilaya ya Kakonko nyumba za mitaa 20 ziliharibika kutokana na mvua kubwa. “Serikali ilitoa misaada ya kibinadamu. Pia katika Manispaa ya Kigoma Ujiji, eneo la Kata ya Katubuka limezungukwa na maji na wataalamu bado wanachunguza chanzo cha mafuriko hayo,” anasema Andengenye. Bandari Ndogo ya Kibirizi, Soko la Mwalo wa Kibirizi na Chuo cha Maendeleo ya Uvuvi (Feta) vimeathirika na kuongezeka kwa maji ya Ziwa Tanganyika. Wilaya ya Uvinza pia imeathirika, Kivuko cha Ilagala kimesimama kutokana na mafuriko ya Mto Malagarasi. Andengenye anasema Serikali haina nia ya kupoka maeneo ya wananchi, lakini inawashauri kuepuka kujenga makazi katika maeneo hatarishi. Pia, anawataka wazazi kuwapeleka watoto shule katika maeneo salama wakati Serikali ikiendelea kutafuta suluhisho ili wananchi waendelee na maisha yao kwa usalama. Kama una maoni kuhusu habari hii, tuandikie ujumbe kupitia WhatsApp: 0765864917. **Habari hii imedhaminiwa na Bill & Melinda Gates Foundation**
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/mafuriko-yalivyowaacha-hoi-wajasiriamali-moro-4715556
# Mafuriko yalivyowaacha ‘hoi’ wajasiriamali Moro ## Muktasari: **Machi 12, 2024 usiku kulinyesha mvua kubwa mkoani Morogoro na kusababisha maji kwenye Mto Furuwa kufurika** **Morogoro.** “Nilikuwa nimelala nikasikia upepo mkali, kuweka mkono kwenye neti pembeni ya kitanda, kumbe maji yalikuwa yameshajaa ndani.” Hivyo ndivyo anavyoanza kusimulia Oktavina Komba, mama wa watoto wawili kuhusu mafuriko yaliyotokea eneo analoishi Kitongoji cha Kilolelo, Kata ya Msegese wilayani Malinyi Mkoa wa Morogoro. Machi 12, 2024 usiku kulinyesha mvua kubwa mkoani Morogoro na kusababisha maji kwenye Mto Furuwa kufurika. Baadhi ya barabara zilifungwa kutokana na maji kujaa huku nyumba kadhaa zikibomoka na watu kukosa makazi. Miongoni mwa maeneo yaliyoathiriwa miundombinu na mali nyingine za wananchi zikiwamo nyumba ni Malinyi Mjini, Lugala na Misegese. Hata hivyo, Oktavina alishuhudia mafuriko yakiingia ghafla nyumbani kwake wakati akiwa amelala, hivyo alishtuka na kulazimika kutoka nje haraka ili kuwaokoa watoto wake huku maji yakiwa yamejaa ndani. Kabla ya mafuriko hayo, Oktavina alikuwa mjasiriamali akiuza kuku, lakini sasa hana uwezo wa kuendelea na biashara hiyo. “Nilikuwa nikiuza kuku watatu hadi sita kwa siku, kuku mmoja nilipata hadi Sh7,000 kipato kilichotosha kukidhi mahitaji ya familia yangu kwa siku,” anasimulia Oktavina wakati akifanya mahojiano maalumu na Mwananchi. “Lakini kwa sasa, sina tena uwezo wa kuzalisha baada ya mafuriko kuondoka na kila kitu,” anasema Oktavina. Mkazi mwingine wa Kitongoji cha Kilolelo, Mariam Khalfan ambaye ni mama wa watoto wanne, anasema alikumbwa na hali ngumu kwa kuhama makazi yake baada ya mafuriko. Mariam aliyekuwa akiuza uji kabla ya mafuriko kutokea, anasema amelazimika kusitisha biashara yake kutokana na hali hiyo. Veronica Simbeye, mfanyabiashara wa duka la vifaa vya ujenzi, alikumbwa na changamoto za kusafirisha bidhaa kutokana na barabara kukatika, hivyo kusababisha biashara yake kusimama. “Nilipata shida sana baada ya mafuriko. Usafirishaji wa bidhaa ulikwama, barabara zikakatika na bidhaa dukani zikaisha,” anasema Veronica aliyeshindwa kuongeza bidhaa dukani kwake. Mwenyekiti wa Serikali ya Kitongoji cha Kilolelo, Kata ya Msegese, Baptisti Mandimula anasema: “Mafuriko yalianza Machi mwaka huu, yakawa makubwa zaidi Aprili na kusababisha uharibifu zikiwamo nyumba 10 kubomoka. “Wakazi wengi walipoteza mashamba, vyombo na vyakula. Tunaiomba Serikali kuwasaidia mbegu za muda mfupi ili waweze kulima na kupata chakula.” Asha Khatibu, mkazi wa Ifakara anasema soko la jirani na Mto Lumemo walilokuwa wanalitegemea lilijaa maji hali iliyosababisha kinamama wafanyabiashara kusitisha biashara na wengine waliamua kutembeza bidhaa mitaani. “Mitaji iliyumba na wengine wamefilisika kutokana na maji kujaa,” anasema Khatibu. Mfanyabiashara ndogondogo na mwenyekiti wa Kitongoji cha Mguha, Alfred Alloyce anasema walishindwa kutimiza wajibu wao kutokana na maji kujaa maeneo mengi, mashamba yalisombwa na maji, huku wananchi wachache wakiokoa mali zao. **Huduma za afya, vifo** Katika Wilaya ya Kilombero, mkazi wa Igombati, Kata ya Lumemo, Selecia Madunda alipata majanga baada ya mvua kubwa kunyesha na ukuta kumwangukia. “Maji yalivyokuwa mengi, kufika hospitali ilikuwa changamoto maana ilibidi wanitafutie mtumbwi ndio wakanivusha kufika ilipo barabara kuu kisha nikakimbizwa Hospitali ya ST Francis” anasema Selecia. **Kwa upande wake, **Oktaviana anasema wakati wa mafuriko wanawake kwenye kitongoji hicho walipata changamoto ya ukosefu wa huduma za afya na vifaa tiba. “Ukisema uende hospitali yetu ya wilaya huwezi kufika njia yote ni maji tu, hadi ilipo hospitali badala yake tulikuwa tunanunua dawa tunapohisi maumivu, tunameza na maisha yanakwenda,” anasema Oktaviana. Mkazi wa Ifakara, Asha Khatibu anasema, “hospitali tunayotegemea hapa ni hii ya St. Francis, sasa wanawake wengi hususan wajawazito walikuwa wanashindwa kufika, maana wengine walikuwa wanatoka maeneo ambayo hayapitiki kutokana na maji kuwa mengi, wanawake wengi walilazimika kupanda mitumbwi ili kuwahi matibabu.” Mkazi mwingine wa Ifakara, Zainabu Hassan anasema kipindi cha mafuriko suala la usafi halikuwepo. “Kipindi cha mafuriko maji yalizingira eneo kubwa, sasa uchafu ukawa mwingi vyoo vikajaa na vingine kuzibuka, lakini pamoja na yote hayo hakukutokea magonjwa ya mlipuko,” anasema Zainabu. Familia ya Khatib Makoti kutoka Ifakara, imepata pigo baada ya wajukuu zake watatu kuzama walipokuwa wakivushwa kwa mtumbwi, huku mtoto wa miezi minne akiokolewa. Makoti anasema siku nne baadaye walipata mwili wa mmoja na mwingine bado haujapatikana. **Kauli za viongozi** Alfred Aloyce, Mwenyekiti wa Kitongoji cha Mguha anasema mafuriko yalisababisha vifo vya watu wawili na kuangusha nyumba sita kwenye kitongoji chake. “Wanafunzi walishindwa kwenda shule kwa siku saba hadi 14 kutokana na maji mengi.” Hata hivyo, Kijiji cha Igombati kiliathirika zaidi na familia saba ziliyakimbia makazi yao, huku nyumba 22 zikibomoka. Andrea Elias, Mwenyekiti wa Kijiji cha Igombani anaiomba Serikali kuweka kingo kwenye Mto Lumemo. Anasema mafuriko yalisababisha kaya 255 kupoteza mashamba kijijini hapo. Mshamu Bimbumbi (80) ni mzee wa Makamo mwenyeji wa Malinyi anasema, “mafuriko kama haya yamewahi kutokea mwaka 1974, lakini ya mwaka huu yamekuwa makubwa mno, kuna Mto Fulua ambao uko jirani na hapa, inabidi usafishwe ili tusipate mafuriko maana ule mto ndio unapokea maji mengi ya kuyaleta kwenye makazi ya watu.” Mkuu wa Wilaya ya Malinyi, Sebastian Waryuba anasema barabara zilikatika, madaraja yalisombwa na makazi ya watu yaliharibika. Anasema hadi sasa katika wilaya yake hakuna tathimini ya kina ambayo imeshafanyika kuonyesha ni hasara kiasi gani imesababishwa na mafuriko lakini uharibifu mkubwa umetokea. “Zaidi ya watu 3,000 walilazimika kuondoka makwao, nyumba 1,000 zilibomoka. Uharibifu huo ulisababisha vifo vya zaidi ya watu 30. Serikali imeanza kurejesha miundombinu ya mawasiliano kama madaraja ili kuimarisha upitaji wa maeneo mbalimbali na kuzuia uharibifu zaidi,”anasema Waryuba. Kuhusu elimu anasema, “shule zilizoathirika kwa kiasi kikubwa ni shule za msingi Madibila, Kiwale na Lugala. Shule hizi ziko maeneo ya Tambarare, madarasa yalijaa maji hadi futi nne, hatukuweza kuruhusu wanafunzi waingie na hilo limesaidia kutopata madhara kwa watoto wa shule.” Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Dunstan Kyobya anasema mvua kubwa kuanzia Aprili mosi mwaka huu, zilisababisha mafuriko, ziliharibu maduka, zilisomba mashamba zaidi ya eka 2000 na watu 10 walifariki dunia. Pia, anasema kulitokea maporomoko ya udongo yaliyochangia uharibifu wa reli uliosababisha treni ya Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (Tazara) kukwama na abiria 544 kuokolewa kwa helkopita ya kijeshi. Kyobya anasema Serikali ilitoa tani 189 za mbegu kwa wananchi ili kuzuia njaa baada ya mafuriko. “Barabara nyingi ziliharibika, na bajeti ya ukarabati ipo tayari. Serikali ilitoa zaidi ya Sh400 milioni kwa ajili ya ukarabati wa Mto Lumemo ili kuzuia mafuriko,” anasema. Kiongozi huyo anasema mashamba ya miwa yalisimamisha uzalishaji kwa zaidi ya mwezi mmoja, lakini uzalishaji umeanza tena baada ya maji kupungua. Hata hivyo, anasema shule na hospitali hazikuathiriwa sana kwa kuwa ziko kwenye miinuko. Anasema Serikali inafanya mipango ya kuweka mazingira wezeshi ili mafuriko yakitokea tena yasilete madhara makubwa. Kyobya anasema, “uchumi wa wananchi ulisimama kwa kuwa barabara kubwa ya Ifakara mpaka Mlimba ilikatika na mpaka sasa haijakamilika. “Ifakara ni kama Kariakoo kwa halmashauri za Mlimba, Ulanga na Malinyi, hivyo kitendo cha barabara kukatika uchumi wa halmashauri hiyo ulisimama, lakini kwa ukarabati wa miundombinu tunaamini hali ya kiuchumi kwa wananchi wetu itaendelea kurekebishika kila hatua.” **Kama una maoni kuhusu habari hii, tuandikie ujumbe kupitia WhatsApp: 0765864917.** *Habari hii imedhaminiwa na Bill & Melinda Gates Foundation.* ** **
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/matarajio-ya-harusi-yalivyogeuka-msiba-rufiji-4714542
# Matarajio ya harusi yalivyogeuka msiba Rufiji ## Muktasari: **Mkazi wa Rufiji mkoani Pwani, Jamal Kwangaya asimulia mkasa ulioondoa uhai wa mwanawe na wengine watatu.** **Dar es Salaam**. Waswahili husema, “kisicho riziki hakiliki,” methali hiyo imeakisi uhalisia katika familia ya Jamal Kwangaya iliyopo wilayani Rufiji mkoani Pwani. Familia hiyo iliyokuwa katika matarajio ya harusi, ghafla mpango huo uligeuka huzuni, baada ya aliyetarajiwa kuolewa kupoteza maisha. Bibi harusi mtarajiwa Hanifah Kwangaya ni mmoja kati ya ndugu wanne wa familia moja walipoteza maisha katika mafuriko yaliyotokea mwanzoni mwa Mei mwaka huu na kufuatiwa na Kimbunga Hidaya. Mzizi wa mafuriko hayo ni mfululizo wa mvua kubwa zilizonyesha maeneo mbalimbali nchini kuanzia Oktoba 2023 kama zilivyotabiriwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA). **Ilivyotokea** Akisimulia mkasa ulioondoa uhai wa Hanifah na wengine watatu, Kwangaya ambaye ni baba mdogo, anasema mwanawe alikuwa akiishi Kijiji cha Mope, eneo lililokuwa maalumu kwa shughuli za kilimo. Ingawa kijiji hicho ni hatari kwa maisha ya binadamu hasa nyakati za mvua, Kwangaya anasema walilazimika kuendelea kubaki huko kwa kuwa ilikuwa vigumu kupata mtumbwi wa kuwahamisha. Anasema mafuriko yalikiathiri kijiji hicho, hivyo walilazimika kuhamia ng'ambo katika Kijiji cha Kongoniongo. "Kipindi cha maafa mtumbwi ulikuwa vigumu kupatikana, wale (ndugu) wakakwama kule katika maeneo yaliyopaswa kuhama," anasema Kwangaya. Anasema waliishi eneo hilo hadi mahitaji muhimu ya binadamu yalipokwisha; kwa kuwa walitumiwa fedha kwa njia ya simu, walitakiwa kwenda kuzitoa ili kununua mahitaji hayo. Hawakuwa na namna nyingine zaidi ya kutafuta mtumbwi wa kuwawezesha kufika Ikwiriri, kwa kuwa katika kijiji hicho hakukuwa na huduma za kifedha. "Mahitaji yalishaisha, sasa wakawa wanalazimika waje huku (Kata ya Ikwiriri) wapate mahitaji," anasema Kwangaya. Anasema katika harakati za kwenda Ikwiriri walifanikiwa kupata mtumbwi na walipanda watu wanane wakiwamo sita wa familia moja. "Walipanda hadi walipofika darajani mmoja wao wa kiume, alitaka kushushwa lakini dereva wa mtumbwi aliwataka wote washuke darajani hapo, wakakataa kwa kuwa hawakuwa na fedha ya kutokea eneo hilo hadi Ikwiriri, hivyo waliomba kuendelea na safari ya mtumbwi hadi eneo la jirani na Ikwiriri," anasema Kwangaya. Safari na mtumbwi wenye abiria saba iliendelea hadi walipolifikia Daraja la Rufiji; na hapo ndipo mzizi wa ajali ulipoanza. "Yule dereva hakuwa anajua kama pale kwenye daraja kuna maji ya mzunguko kwa hiyo yakawa yanamvuta, alionekana yamemshinda. "Akawa anashauriwa kupita chini ya daraja naye akatekeleza hilo na alivyofika mbele mzunguko wa maji ulizidi na kusababisha mtumbwi kupinduka," anasema Kwangaya. Baada ya mtumbwi kupinduka, anasema waliozama ni mwanawe na wajukuu zake wanne, lakini mmoja aliokolewa. Anasema baada ya hatua hiyo, hatua za kutafuta miili ya waliozama ziliendelea kwa siku tatu bila mafanikio. Kwangaya anasema siku ya nne kwa kushirikiana na Serikali, ndipo walifanikiwa kupata miili miwili; na siku iliyofuata ulionekana mwili mwingine, lakini uliobaki majini haukupatikana hadi sasa. "Hiyo maiti ya mdogo hatukubahatika kuiona hadi hivi sasa, kwa hiyo tunashukuru kwa Serikali kutusaidia na kushirikiana na wananchi katika yote," anasema Kwangaya. Mbali na kupoteza wapenda wao, anasema mazao mbalimbali ikiwamo ufuta katika mashamba yote yamesombwa na mafuriko. **Kuhusu harusi** Kwangaya anasema hadi mwanawe Hanifah anafariki dunia hakuwa na mume, isipokuwa kulikuwa na matarajio ya ndoa. Anasema kabla ya kufariki dunia, Hanifah alishamwambia kuwa, siku chache zijazo angempa taarifa rasmi juu ya mchumba wake. "Kipindi alichokuwa anakuja huku kulikuwa na taarifa ya ndoa na kwa sababu wakati wake umefika ndoa imeishia hapo. Kwa hiyo hilo tulilijua kwamba kulikuwa na mchumba anayehitaji kumuoa," anasema Kwangaya. **Maisha baada ya msiba** Anasema maisha ya familia nzima yameendelea kuwa magumu kwa kuwa mazao yote waliyotarajia kwa ajili ya chakula pia, yamepotea kwa mafuriko. Hali inakuwa mbaya zaidi kwa kile alichoeleza, hata mahindi waliyoyapanda baada ya mafuriko hayo, yamesombwa tena na maji. "Tulijaribu tena kwenda kupanda mahindi, kwa taarifa niliyonayo ni kwamba kuna maji yameyapitia nusu. Tunaiomba sana Serikali jicho lake liangalie Rufiji hasa Ikwiriri," anasema. **Shangazi wa marehemu** Mtumwa Mbonde, shangazi wa marehemu anasema alipokea taarifa ya msiba kwa simu kwamba ndugu zake hao wamezama majini. Baada ya taarifa hiyo, anasema walitafutwa askari wa zimamoto kwa ajili ya uokoaji ndipo walipofanikiwa kuiona miili ya wawili na baadaye mmoja na mwingine hadi sasa haujapatikana. Anaeleza kuwa, binti aliyefariki dunia alikuwa mkulima na kwamba kifo chake kimeacha majonzi kwa kuwa ni vigumu kusahau. "Ni msiba mzito hatutausahau kwa sababu ni pigo kubwa," anasema Mbonde. **Historia ya mafuriko Rufiji** Ingawa mafuriko yaliyoshuhudiwa mwaka huu yalikuwa na athari kubwa, historia inaonyesha hii si mara ya kwanza kwa Wilaya ya Rufiji kukumbwa na mafuriko. Inaelezwa kuwa, Rufiji imekuwa katika hatari ya kuathiriwa na mafuriko katika nyakati tofauti kama inavyoelezwa na Faraji Maloa, mkazi wa wilaya hiyo kwa miaka 40 sasa. "Nafahamu historia hizi za mafuriko, mara ya kwanza mwaka 1936 kulikuwa na mafuriko makali yaliitwa Lilale na ndiyo yaliyotengeneza mito mbalimbali. "Kwa mfano madaraja ya Ngayonga, Mtanga, Tingetingeni, Ruwoyi yote hayo ni zao la mafuriko hayo," anasema Maloa. Anaelezea historia hiyo kuwa, mafuriko hayo ya mwaka 1936 ndiyo yaliyotengeneza Ziwa la Umwe na mito Lingola, Urungu, Poka na Kingola. Anasema mito na mifereji yote, imekuwa vyanzo vya mafuriko mvua kubwa inaponyesha. Pamoja na eneo hilo kuwa hatari kwa mafuriko, anasema watu wanalazimika kuishi kwa kile alichoeleza, wanafuata rasilimali ardhi yenye rutuba. "Unajua bonde ni ardhi yenye rutuba sana kwa hiyo mtu hawezi kuiepuka hiyo, lazima atakwenda kwenye ardhi yenye rutuba huwezi kwenda kulima kwenye ukame," anasema Maloa. Tangu mvua zilivyoanza Oktoba mwaka jana, anasema hakuna aliyetilia maanani hadi pale Serikali ilipotoa taarifa ya tahadhari. Maloa anasema kuanzia Aprili mwaka huu, tahadhari hiyo ya Serikali ikawa katika uhalisia, wananchi walianza kushuhudia mafuriko huku mashamba na makazi yakisombwa na maji. "Mimi nilikuwa na ekari 12 zote zilijaa mpunga, zimesombwa na mimi ndiyo nilikuwa nategemea hizo tu kwamba nikivuna nitakuwa na fedha na chakula cha kutosha," anasema Maloa. Anaeleza kuwa, hata kama wanahitaji msaada, lakini ni vigumu kupata utakaowatosheleza kwa kuwa idadi ya wanaoishi eneo hilo ni wengi. Maloa anasisitiza umuhimu wa taarifa kutolewa mapema ili wananchi wajipange na hilo lisifanywe na mkuu wa wilaya pekee, bali kila ngazi. "Tumeambiwa tuondoke kule bondeni kwa kuwa limefunikwa kabisa na maji, lakini yanakuja (maji) kwa sababu bwawa la Mwalimu Nyerere limejaa kupita kiasi," anasema Maloa. **Mkuu wa Wilaya ya Rufiji** Akizungumzia vifo hivyo, Mkuu wa Wilaya ya Rufiji, Meja Edward Gowele anasema jumla ya watu tisa wamepoteza maisha. Anasema kabla ya Kimbunga Hidaya walifariki dunia watu wawili akiwamo mwanamke mwenye umri wa miaka 20 na mtoto wa miezi miwili. Vifo hivyo, anasema vilifuatiwa na vingine vinne vya familia moja. "Kwa jumla tulikuwa na vifo tisa vilivyotokana na wananchi kutumia mitumbwi ilhali Serikali ilishakataza, lakini kwa maji kuzingira nyumba hakuna mtu aliyepoteza maisha," anasema Gowele. Hata hivyo, anasema iwapo wananchi wagezingatia miongozo waliyopewa na Serikali ya kuacha kutumia mitumbwi pengine wangeokolewa. Meja Gowele anasema watu 89,000 wameathirika wanaojumuisha kaya 23,360. Anasema nyumba 628 zimeathirika katika kata 12 kati ya 13 zinazopatikana wilayani humo, akisisitiza hiyo ni kabla ya Kimbunga Hidaya. Ili kuepuka janga kama hilo, anasema Serikali iliomba ekari 150 katika msitu wa hifadhi kuanzisha makazi na baadhi ya wananchi wameanza kuingia eneo hilo ili kuepuka athari za mafuriko. Anasema katika Kijiji cha Tungi, viwanja vinaendelea kutolewa kwa wananchi ili wakaishi salama. Kuhusu misaada, anasema Serikali ilipeleka mahema 12, chakula zaidi ya tani 200 kwa ajili ya kuhudumia watu waliopo kwenye kambi na wale waliopo kwa ndugu jamaa na marafiki. Mbali na Serikali, anasema misaada mingine ilipelekwa na mbunge wa Rufiji, Mohamed Mchengerwa, hivyo kutosheleza wakazi wa eneo hilo. "Hivi juzi, ameleta misaada ya mbegu zenye thamani ya Sh40 milioni kutoka kwenye mfuko wake mwenyewe na ametafuta wahisani CRDB (benki) wametuletea mbegu za Sh40 milioni," anasema Meja Gowele. Anaeleza bado usambazaji unaendelea kuhakikisha mbegu zinatosheleza mahitaji. **Kama una maoni kuhusu habari hii, tuandikie ujumbe kupitia WhatsApp: 0765864917. ** **Habari hii imedhaminiwa na Bill & Melinda Gates Foundation**
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/hali-tete-maisha-ya-wakazi-kilwa-baada-ya-mafuriko-4713698
# Hali tete, maisha ya wakazi Kilwa baada ya mafuriko ## Muktasari: **Mei 4 mwaka huu Wilaya ya Kilwa mkoani Lindi ilikumbwa na mafuriko yaliyoambatana na Kimbunga Hidaya, yaliyosomba mashamba, vyombo, nyumba na vyakula vya wakazi hao.** **Lindi**. Mafuriko yaliyotokea nchini kati ya Oktoba 2023 hadi Mei mwaka huu, yameendelea kusababisha maumivu kwa wakazi wa maeneo yaliyoathirika na janga hilo, hasa katika Kijiji cha Myumbu wilayani Kilwa Mkoa wa Lindi. Mei 4 mwaka huu wilaya hiyo ilikumbwa na mafuriko yaliyoambatana na Kimbunga Hidaya, yaliyosomba mashamba, vyombo, nyumba na vyakula vya wakazi hao. Jumla ya kaya 207 kati ya 776 zilizopo Kijiji cha Myumbu zimeathirika, huku matumaini ya kula mara mbili kwa siku au tatu kwa kaya 80 yakiwa yameyeyuka. Mjane Darlin Ngalamba (83) anayeishi na wajukuu zake wanne katika nyumba ya udongo kando ya Mto Wenza, mazao yake yote ikiwamo mihogo na migomba katika shamba la ekari tano, yalisombwa na mafuriko. Darlin anayetegemea kilimo na ufugaji, kuku wake pia walisombwa na mafuriko na kubaki wawili tu, kati ya 30. “Baada ya hapo ndiyo tunaangalia utaratibu wa kununua kuku wengine,"anasema mjane huyo ambaye kwa sasa hawezi tena kulima na anategemea misaada ya wasamaria wema kutokana na umri wake mkubwa pamoja na kusumbuliwa na maumivu ya miguu. Akisimulia ilivyotokea, Darlin anasema: "Tuliamka na mvua ilianza kunyesha kidogo kidogo, mvua iliendelea hadi saa tatu asubuhi maji yakaanza kufurika. Wajukuu zangu wakanambia kuna maji." Kutokana na umri wake, ilikuwa vigumu kwa Darlin kutembea mwenyewe kuyakimbia maji hadi maeneo yaliyokuwa salama. Darlin anasema katika hali hiyo, walitokea wasamaria wema waliosaidiana na mjukuu wake mkubwa kumbeba hadi katika eneo lisilokuwa na maji. Miongoni mwa wajukuu zake, mkubwa ana umri wa miaka 25 anayefanya vibarua ili kupata fedha za kusaidia familia ingawa hazitoshi. Darlin anasema baada ya kupata msaada wa kubebwa hadi eneo lisilokuwa na maji, ilimchukua wiki moja kuishi nje ya nyumba yake, akisubiri maji yaondoke na baadaye alirejea. "Kurudi hapa (nyumbani kwake) vitu vyote hamna; mabeseni na sufuria naletewa na watu kama msaada," anasema Darlin. Mjane huyo anasema anatamani kupata msaada haraka kutoka serikalini hasa wa chakula kwa kuwa ndicho kitu muhimu katika uhai. Mbali na Darlin, mkazi mwingine aliyepoteza kila kitu baada ya mafuriko kusomba nyumba, chakula, vyombo na mifugo yake, ni Abdulrahman Kingoma. Mkazi huyo wa Kijiji cha Myumbu amebaki bila chakula na mavazi huku akitegemea msaada wa majirani. Kingoma aliyenusurika kwa sababu mafuriko yalitokea mchana, anasema ingekuwa usiku huenda asingekuwa hai. "Nilikuwa na ghala la kuhifadhi mahindi na mtama na lilikuwa na mtama gunia moja na nusu limeondoka, banda la kuku limeondoka yaani sina chochote," anasema Kingoma. ** ** **Misaada haitoshi ** Kwa sasa Darlin na Kingoma mategemeo yao ni msaada wa Serikali, lakini ule waliopewa awali kipindi cha mafuriko (Mei mwaka huu) ulitosha kwa mlo mmoja wa siku. Rabii Mbonde, mjumbe wa Kamati ya Maafa, anasema hali hiyo ya uchache wa chakula imesababisha malalamiko kutoka kwa wananchi, wakihisi viongozi wameficha misaada. Mwenyekiti wa Kijiji cha Myumbu, Hamidu Mnola anasema walipokea kilo 100 za unga, maharagwe kilo 400, mablanketi 100, vyandarua 130, ndoo za maji na magodoro sita, ingawa kaya zilizoathirika ni 207. **Elimu na changamoto za mafuriko** Khadija Makalani, mwanafunzi wa darasa la sita katika Shule ya Msingi Myumbu, wilayani Kilwa, anakabiliwa na changamoto ya kuhitimu elimu ya msingi kutokana na ukosefu wa Sh10,000 za kununua sare za shule baada ya alizokuwa akivaa kusombwa na mafuriko. Familia ya mwanafunzi huyo anayeishi na bibi yake Mariam Gumba, ilipoteza mali na kuishi katika hali ngumu. Khadija alikatisha masomo kwa takriban wiki nne tangu sare zake ziliposombwa na maji, na sketi aliyopata kwa msaada ilichanika haraka. **Hali ya familia ya Khadija** Mariam Gumba, bibi wa Khadija, anaeleza jinsi familia yake ya watu saba ilivyopoteza mali nyingi kutokana na mafuriko. Anasema hali hiyo iliwalazimu kulala nje kwa siku tano kabla ya kupata hifadhi kwa muda hadi Oktoba 5 mwaka huu. Hadi sasa, Mariam hajui wapi watakwenda baada ya kumaliza muda huo itakapofika Oktoba kwa kuwa, familia yake inakabiliwa na ugumu wa maisha. Mariam mwenye watoto tisa ambao hawana uwezo wa kumsaidia, anategemea kilimo ambacho pia kimeathiriwa na mafuriko. Mazao yao yote, ikiwamo mpunga na mihogo, yamesombwa na maji, hali hiyo iliyobadili ratiba ya mlo wao kutoka mara mbili kwa siku hadi moja. Hassan Kingoma, jirani aliyewahifadhi Mariam na wajukuu zake, anasema aliwasaidia kuokoa baadhi ya vyombo vyao huku maji yakiwa yamejaa hadi kiunoni. Hata hivyo, athari za mafuriko zimepoteza matumaini ya wakazi hao kupata mazao kutokana na kilimo, kwa kuwa maeneo mengi yameingiliwa na mchanga na hayafai tena kwa uzalishaji. Zubery Utondwe, Ofisa Kilimo wa Kijiji cha Myumbu, anapendekeza Serikali itoe msaada wa mbegu za muda mfupi ili kusaidia wakazi kuotesha mazao na kukabiliana na baa la njaa wanalohisi linalokuja. **Msimamo wa Serikali ** Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilwa, Yusuph Mwinyi, anasema wataalamu wa mazingira wamekwenda kutoa ushauri wa aina ya mbegu zinazohitajika. “Serikali imeanza kuleta mbegu, lakini bado wilaya inahitaji msaada zaidi kutoka kwa wadau,”anasema. Mwinyi anasema uongozi wa wilaya unaomba msaada zaidi wa mbegu za maboga, mahindi na kunde kutoka kwa wadau mbalimbali. Katika Wilaya ya Kilwa, mafuriko hayo yameathiri kata 14 na kaya 1,020 zenye wanafamilia 4,080 na kusababisha vifo vya watu watano. Jumla ya nyumba 525 zimeharibika na nyingine 495 zikihitaji kujengwa upya, huku wananchi wengi wakiwa kwenye kambi tofauti za wilaya. Hata hivyo, Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Julai mwaka jana ilitabiri uwepo wa mvua za El-Nino kuanzia Oktoba 2023. Mvua hizo kwa mujibu wa TMA, zingesababisha athari katika maeneo mbalimbali nchini, yakiwamo mafuriko na uharibifu wa miundombinu. Baada ya utabiri huo, Oktoba mwaka jana, mvua hizo zilianza kunyesha na athari katika mikoa mbalimbali zilijitokeza. Kilwa, Pwani, Morogoro, Mbeya na Dar es Salaam ni miongoni mwa mikoa mingi iliyokumbwa na athari za mvua hizo. **Kama una maoni kuhusu habari hii, tuandikie ujumbe kupitia WhatsApp: 0765864917. ****Habari hii imedhaminiwa na Bill & Melinda Gates Foundation**
http://www.mwananchi.co.tz/mw/zanzibar/ajali-yaua-wawili-pemba-4783932
# Ajali yaua wawili Pemba ## Muktasari: **Mwalimu, fundi ujenzi wafariki kwa kugongwa na gari** **Pemba.** Watu wawili akiwemo mwalimu wa Shule ya Msingi Finya wamefariki dunia na wengine kujeruhiwa kutokana na ajali ya gari iliyotokea maeneo ya Kinazini Wingwi Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba. Daktari wa Hospitali ya Micheweni, Hamad Mbwana Shoka ameieleza Mwananchi Digital leo Oktoba 2, 2024 kwamba wamepokea watu saba ambapo kati ya hao, wawili walikuwa wameshafariki dunia. Amewataja waliofariki dunia ni Mohina Egland Nundu (38) mkazi wa Tanga ambaye ni fundi ujenzi katika Skuli ya Simai Micheweni na mwingine Safia Mohamed Yusuf (45) Mwalimu wa skuli ya Finya ambao wote pamoja na majeruhi waligongwa na gari baada ya kukosa mwelekeo barabarani. ‘’Tulipokea watu hao saa 7:00 mchana huku wawili hao wakiwa wamefariki dunia na katika uchunguzi wetu tulibaini waliumia sehemu za kichwani na wengine sehemu za miili yao,” amesema daktari huyo. Kaimu kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, Mussa Mwakasula amethibitisha kutokea ajali hiyo ya gari ya kampuni ya ujenzi wa barabara IRIS baada ya kuacha njia na kuwafuata watu waliokuwa kando ya barabara wakisubiri usafiri. Amesema Jeshi la Polisi linachunguza chanzo cha ajali hiyo huku akiwataka madereva kufuata sheria za barabarani ili kuepusha ajali zisizo za lazima. ‘’Nikweli watu wawili wamefariki dunia na wengine wamejeruhiwa kwenye ajali hiyo baada ya gari ya Kampuni ya IRIS kuacha njia na kupoteza maisha ya watu hao na wengine kujeruhiwa,’’ amesema. Ofisa Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba, Mohamed Nasor Salum amesema wizara imeguswa na kifo cha mtendaji wao na kueleza kuwa ameacha pengo kubwa kutokana na juhudi alizokuwa nazo katika kuiletea matokeo mazuri skuli hiyo. ‘’Tumeguswa na kifo cha mtendaji wetu Safia Mohamed na fundi wa ujenzi wa skuli hiyo anatokea Tanga, Mwalimu huyo ameacha pengo kubwa kutokana na matokeo mazuri yanayopatikana katika skuli yake," amesema. Ameitaka familia ya marehemu kuwa na subira katika kipindi hichi kigumu cha msiba kwani yote hayo ni mipango ya Mwenyezi Mungu.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/zanzibar/anayedaiwa-kuchukuliwa-na-askari-kwa-mahojiano-akutwa-ameuawa-zanzibar-4783832
# Anayedaiwa kuchukuliwa na askari kwa mahojiano akutwa ameuawa Zanzibar ## Muktasari: **Familia ya Ramadhan anayedaiwa kutekwa, kuuawa kikatili yamlilia Rais Mwinyi. Mama yake asema ana hofu na usalama wake.** “Mwanangu ameuawa, kifo cha kikatili naomba haki itendeke waliofanya hivi wachunguzwe, ni kweli kifo kipo lakini sio cha namna hii…” Hii ni kauli ya Saada Ramadhan Mwendwa mama mzazi wa Ramadhan Idd Shaaban (48) akianza kusimulia jinsi mwanaye alivyochukuliwa na watu waliojitambulisha ni askari wakidai wanakwenda kufanya mahojiano naye lakini aliokotwa akiwa amefariki dunia eneo la Mbuzini Kijichi Unguja. Kwa kipindi cha hivi karibuni matukio ya watu kutekwa, kupigwa, kuumizwa na kuuawa yameshika kasi. Kwa tukio la karibuni zaidi ni lile la Mjumbe wa Sekretarieti ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Ali Kibao ambaye alichukuliwa kwenye gari Septemba 6, 2024 akitoka Dar es Salaam kwenda Tanga na mwili wake uliokotwa Ununio uso wake ukiwa umeharibika kiasi cha kutotambulika. Akisumulia mama huyo huku akitokwa na machozi, Saada ametumia fursa hiyo kumuomba Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama kuchunguza tukio hilo na waliofanya hivyo wachukuliwe hatua. Akisimulia mkasa huo nyumbani kwake Chumbuni Oktoba 2, 2024 Saada amesema mwanaye alichukuliwa Septemba 24, 2024 saa 12:00 jioni lakini mwili wake uliokotwa kesho yake Septemba 25 ukiwa umeunguzwa, jicho moja limetobolewa na ulimi umetoka nje ambapo uchunguzi wa polisi ulieleza kuwa ameuawa. “Siku hiyo mwanangu alikwenda kutembea jioni eneo la Amani Baa, saa 12:00 za jioni walikuja vijana watano wakamfuata alipokuwa amekaa na kumuita kwa jina wakasema wana shida naye waende nje wakazungumze wakidai wao ni askari na wana RB wanamtafuta,. “Walipanda naye kwenye gari wakamwambia wanampeleka polisi Mwanakwerekwe lakini walipofika walipitiliza. Saada anasema mwanaye alikuwa na rafiki yake ambaye aliongozana naye kwenda kituo cha polisi ila baada ya kupitiliza alipohoji mbona wamepita walimshusha. “Walichokifanya ndio hicho kilichotokea, wamempiga mwanangu wamemuunguza moto kwa shoti za umeme na kumtoboa jicho moja la kulia," amesimulia akieleza kifo cha mwanaye wa kwanza ambaye ameacha mjane na watoto wanne. Anasema usiku wa siku hiyo mke wake Shaaban alipiga simu baada ya kuona mumewe hajarejea lakini kuna mtu alipokea simu hiyo akasema asiwe na wasiwasi bado anahojiwa na askari akimaliza atarejea nyumbani. Baada ya kuambiwa hivyo, alitulia lakini kadri muda ilivyoendelea akawa anaingiwa zaidi na wasiwawasi ndipo alinipigia mimi simu akisema kuna muda alimpigia askari wakasema bado wapo naye lakini mpaka sasa hajarejea. “Baadaye mimi nilipiga simu ikawa haipatikani nikaanza kumtumia meseji, mwanangu upo wapi mbona hujarudi baba, simu haipatikani nikajua ujumbe unaingia kumbe matokeo yake wameshampiga na kumfanyia ukatili huo,” amesema. Amesema walipoamka asubuhi Septemba 25 walienda kutoa taarifa katika vituo vitatu vya polisi. Hata hivyo, amesema anashukuru polisi kwani walionesha jitihada za kupiga simu katika vituo vingi kuulizia iwapo kuna mtu wa namna hiyo lakini majibu yalikuwa hapana. Akiendelea kusimulia, Saada amesema ulipofika mchana alipigiwa simu na mwanawe mkubwa kuwa kuna maiti imeokotwa katika njia ya Mbuzini Kijichi akiwa na vitambulisho na limeonekana kuna jina la Ramadhani Iddi na walipokwenda katika chumba cha kuhifadhia maiti Hospitali ya Mnazi Mmoja wakakuta ni yeye. “Mdomo ulikuwa wazi, jicho limetumbuliwa na mwili wote umechomwa chomwa, ila niliwaambia wanangu tufanye utaratibu kuchukua maiti,” amesema. “Kwa kweli kilichotokea kwa mwanangu naomba sana, serikali yangu ni sikivu ya Zanzibar na inatupenda wananchi wanyonge, kwa hili nataka isikie kilio changu waliofanya ukatili huu aliyefanya ukatili huu wapatikane haki itendeke,” amesema na kuongeza. “Mwanagu kaonewa…, kapata mateso ndani ya nafsi yake, kwasababu unapotiwa moto kila mtu anajua, kama ni kifo kila mtu atakufa lakini sio kwa kifo kile, naomba serikali ichukue hatua haina uonevu watu wote ni watu wake, tumeumia familia hatuna pa kulilia serikai ina mkono mrefu itawapata waliofanya kitendo hiki sheria ni kwa watu wote,” amesisitiza. Saada amesema ameshakuwa na woga hata kwa watoto wake wengine kwasababu hajui kilichofanywa mwanaye kuuawa. “Sasa sijui kama litaishia kwa Ramadhan au mimi mwenyewe au watoto wangu wengine hadi wajukuu zangu wangu kwakweli tunakosa amani.” Mama mdogo wa marehemu, Yunes Kitarao amesema jambo hilo lnawasikitisha na kuwaumiza kwanini auawe kwa ukatili wa namna ile. “Kwanini mtu atekwe, anaambiwa anachukuliwa na askari na wanasema yupo katika mikono salama watamrudisha na kwanini hakurudishwa akiwa mzima, dhamira hiyo imeniumiza sana, mtoto wa dada yangu, sijawahi kusikia amegombana wala kutukana na mtu,” amesema Yunes. Amesema mambo hayo yamekuwa yakitendeka maeneo mengine sasa na Zanzibar yameanza. “Haya yanayotukuta ni makubwa, tunachokiomba hawa watu wakamatwe mbona majambazi yanakamatwa, liwe fundisho, bila kufanya hivyo hili jambo litaendelea hata kama sio kwa familia hii lakini kwa wananchi wengine,” amesema huku akipeleka kilio hicho kwa viongozi wakuu wa nchi. Mjomba wa marehemu ambaye hakutaka jina lake litajwe, amesema kinachowasikitisha zaidi watu hao kujitambulisha wametoka kwenye vikosi na simu ilipopigwa wakajibiwa yupo kwenye mikono salama halafu wakaokota maiti. Akizungumza na Mwananchi kuhusu tukio hilo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi, Richard Mchomvu bila kufafanua zaidi amesema wanaendelea na upelelezi wa tukio hilo na ukikamilika zitatolewa taarifa zaidi. “Tukio hilo lipo uchunguzi bado unaendelea, tukikamilisha tutaeleza zaidi,” amesema Mchomvu.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/zanzibar/kwa-nini-zra-imevuka-lengo-la-makusanyo--4783624
# Kwa nini ZRA imevuka lengo la makusanyo ## Muktasari: **Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA) imetosa sababu saba kwa nini makusanyo yameongezeka robo ya kwanza yam waka wa fedha 2024/25.** **Unguja.** Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA), imevuka lengo la ukusanyaji mapato kwa kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2024/25, kuimarika na kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi kati ya Zanzibar na Tanzania Bara vikitajwa kuwa miongoni mwa sababu. Ongezeko hilo pia limeelezwa kuchangiwa na kuimarishwa mifumo na uhusiano mzuri na walipakodi, ikiwamo kusaidia kurahisisha biashara zao na kuwafikia kusikiliza changamoto na kuzitafutia ufumbuzi. Akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 2, 2024 ofisini kwake, Kaimu Kamishana wa ZRA, Said Ali Mohamed amesema katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2024/25, ilikadiriwa kukusanya Sh194.031 bilioni na zimekusanywa Sh200.934 bilioni ambao ni ufanisi wa asilimia 103.56 wa makusanyo ya mapato yaliyotarajiwa. “Kwa kulinganisha na makusanyo halisi ya robo ya kwanza ya mwaka uliopita wa 2023/2024, yalikuwa Sh161.831 bilioni, ambayo yakilinganishwa na makusanyo halisi ya robo ya kwanza ya mwaka huu wa fedha wa 2024/25, yanaonyesha ukuaji wa makusanyo halisi wa asilimia 24.16,” amesema. Said amesema kwa Septemba 2024, ZRA imezidi lengo kwani ilikadiriwa kukusanya Sh74.049 bilioni na imekusanya Sh76.497 bilioni, ambao ni ufanisi wa asilimia 103.31 wa makusanyo ya mapato yaliyotarajiwa. Makusanyo halisi ya Septemba ya mwaka uliopita wa 2023/24, yalikuwa Sh61.694 bilioni, ambayo yakilinganishwa na makusanyo halisi ya Septemba mwaka huu wa fedha wa 2024/225, yanaonyesha ukuaji wa makusanyo halisi wa asilimia 23.99. Said amesema kuimarika kwa matumizi sahihi ya mifumo katika usimamizi wa kodi, ikiwemo matumizi ya mfumo wa risiti za kielektroniki, mfumo wa ukusanyaji wa mapato wa Zidras sambamba na kuongezeka kwa utoaji wa elimu ya kodi kupitia njia mbalimbali kumechangia ufanisi. Amesema mbinu nyingine inayosaidia kufikia makusanyo ni kuzungumza na wadau wa kodi kwa makundi ambayo wamekuwa wakikutana nayo kisha kuzipatia ufumbuzi kero zinazoibuliwa. Utekelezaji wa marekebisho ya Sheria za Kodi kwa mwaka wa fedha 2024/2025, amesema ni hatua iliyosababisha kuimarika kwa ukusanyaji katika vyanzo vya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT), ushuru wa bidhaa, ada za bandari na kodi ya miundombinu. Katika kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya kodi kwa robo ya pili ya mwaka wa fedha wa 2024/25 (Oktoba hadi Desemba 2024), ZRA itaendelea kufanya ziara kukutana na walipakodi kusikiliza na kutatua changamoto zao. “Kushirikiana na jumuiya za wafanyabiashara katika kusimamia walipakodi, kuunganisha mifumo yao ya kibiashara na mfumo wa kutolea risiti za kielektroniki (VFMS) ili kurahisisha upatikanaji wa taarifa sahihi za walipakodi,” amesema. Ofisa Mtendaji Mkuu wa Jumuiya ya Waongoza Watalii Zanzibar (Zato), Hassan Burhan amesema hatua ya kukutana na ZRA kusikiliza kero zao imesaidia watu kuhamasika katika ulipaji kodi. “Mfumo huu umesaidia na utasaidia kwa sababu kuna kero nyingi ambazo zinashughulikiwa kwa hiyo watu wanakuwa wepesi kulipa kodi kwani wanaona mazingira yamekuwa rafiki,” amesema.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/zanzibar/tume-kuandika-wapigakura-wapya-14-878-z-bar-act-wazalendo-watoa-neno-4783370
# Tume kuandika wapigakura wapya 14,878 Z’bar, ACT-Wazalendo watoa neno ## Muktasari: **Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imepanga kutumia siku saba kuanzia Oktoba 7-13, 2024 kuandikisha wapigakura wapya 14,878 visiwani Zanzibar ikiwa ni maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa 2025.** **Unguja.** Wakati maboresho ya daftari la mpigakura yakitarajia kuanza Oktoba 7 hadi 13, 2024, wapiga kura wapya 14,878 wanatarajiwa kuandikishwa kisiwani humo ambao watakuwa na fursa ya kupiga kura moja tu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kutokana na shughuli hiyo, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imetumia siku tatu kuanzia Septemba 29 hadi leo Jumatano, Oktoba 2, 2024 kutoa mafunzo kwa wadau wa uchaguzi na watendaji ngazi ya mkoa namna bora ya shughuli hiyo itakavyoendeshwa. Katika mafunzo hayo, Mjumbe wa INEC, Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Asina Omari amewataka wasimamizi hao kuzingatia taratibu na miongozo kuhakikisha kila anayestahili kupata fursa hiyo haikosi huku akisema wanatarajia upata ushirikiano kutoka kwa wadau. “Twende tukasimamie sheria taratibu na miongozo ili kila anayestahili kuandikishwa asikose huduma hii,” amesema. Mkurugenzi wa INEC, Ramadhan Kailima amesema kwa kipindi cha siku hizo wanatarajia kuandikisha wapigakura 14,878 ikiwa ni ongezeko la asilimia 18 ya wapiga kura 83,197 waliopo kwenye daftari la wapigakura. “Inatarajiwa baada ya uandikishaji itakuwa na wapiga kura 98,075 watakaopiga kura moja tu ya kumpigia Rais wa Jamhuri wa Mungano wa Tanzania,” amesema. Nao baadhi wadau wa vyama vya siasa wamesema ni kama wameshtukizwa katika hatua hiyo kwani walitakiwa kupewa taarifa muda mrefu kwa ajili ya kuwaandaa wananchi na wafuasi wao. Ofisa Uchaguzi wa ACT Wazalendo, Muhene Rashid amesema taarifa hizo zimekuja kwa muda mfupi hivyo inaweza kuathiri wananchi wasipate taarifa mapema. "Hili jambo lilikuwa limepangwa mapema, ila muda umeshakwenda tunatakiwa tujipange na tuhamasishe wananchi lakini kwakuwa muda umeisha inaweza kuathiri na watu wasihamasike zaidi," amesema. Hata hivyo, Kailima amesema ni vyema wakatumia muda uliopangwa kupitia majukwaa halali kuhamasisha wananchi wajitokeze kwa wingi badala ya kuona kama muda hautoshi. Ofisa mwandikishaji Unguja, Amina Saleh amesema:“Tumepata miongozo na sisi tutahakikisha tunasimamia na kuendesha shughuli hii kama ilivyopangwa na malengo ya serikali yafikiwe.”
http://www.mwananchi.co.tz/mw/zanzibar/rais-samia-ataka-ushirikiano-serikali-sekta-binafsi-kuboresha-huduma-za-afya-4782836
# Rais Samia ataka ushirikiano Serikali, sekta binafsi kuboresha huduma za afya ## Muktasari: **Uhaba wa wafanyakazi wenye ujuzi, upungufu wa vifaatiba na uchakavu kwa baadhi ya miundombinu ni changamoto zinazoikabili sekta ya afya** **Unguja.** Rais Samia Suluhu Hassan amesema licha ya jitihada zinazochukuliwa na Serikali kuboresha huduma za afya kwa wananchi bado kuna changamoto ya utoaji huduma, hivyo ushirikiano wa sekta binafsi utasaidia kuziimarisha. Ametaja changamoto hizo kuwa ni uhaba wa wafanyakazi wenye ujuzi, upungufu wa vifaatiba na uchakavu kwa baadhi ya miundombinu. Rais Samia ametoa kauli hiyo leo Jumanne Oktoba mosi, 2024 kupitia hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla wakati wa ufunguzi wa Kongamano la 11 la Afya Tanzania (THS) lililofanyika Fumba, wilayani Magharibi B, Unguja. Kongamano hilo limewakutanisha wataalamu zaidi ya 1,500. “Ni vyema mkafahamu pamoja na hatua zinazofikiwa bado kuna changamoto katika utoaji wa huduma, hivyo Serikali itaendelea kushirikisha sekta binafsi katika kutoa huduma kwa wananchi ambao ushirikiano huo unakusudia kuimarisha huduma bora za afya nchini,” amesema Rais Samia. Amesema Serikali itaendelea kuboresha elimu kwa wataalamu wa afya kwa kutoa kipaumbele na kuongeza ufadhili kwa mafunzo ya ubingwa na ubingwa bobezi katika taaluma za kimkakati. Kuna umuhimu wa kushirikiana na sekta binafsi katika kutoa huduma bora kwa wananchi. Rais Samia amesema Serikali zote mbili zinaendelea kuimarisha matumizi ya mifumo ya utoaji wa taarifa ili iweze kusomana kutoka kituo kimoja cha afya kwenda kingine katika ngazi zote za utoaji wa huduma kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa taarifa za wagonjwa, zikiwamo vipimo na matibabu. Pia, kutoa fursa ya kupata matibabu zaidi katika maeneo yote ya nchi. “Serikali zote (SMT na SMZ) zinaendelea kuchukua hatua za kuimarisha huduma za kinga, kuwekeza katika miundombinu ya afya kwa kujenga na kukarabati hospitali zote na vituo vya afya ili ziweze kutoa huduma bora na za kisasa kwa wananchi wa pande zote mbili za Muungano,” amesema Rais Samia. Ametoa wito kwa taasisi za Serikali na binafsi kushirikiana na THS kuongeza nguvu ya majadiliano katika sekta ya afya na kuboresha utoaji huduma za afya mijini na vijijini. Awali, akitoa taarifa ya kitaalamu kwa niaba ya bodi ya THS, Dk Grace Magembe amesema imekuwa ni chachu ya kuleta mabadiliko endelevu katika sekta ya afya hasa katika kuhamasisha utoaji huduma kwa mifumo ya kidijitali ili kuendana na wakati. Dk Grace amesema THS imewawezesha vijana kupitia programu ya kuwajengea uwezo kwa kuwapatia mafunzo, kuwaendeleza kitaaluma na kuwaunganisha watumishi wa afya na fursa zilizopo nje ya nchi. “THS ina jukumu kubwa la kuendelea kushirikiana na Wizara ya Afya katika kuboresha na kuimarisha sekta hasa katika eneo la kutoa elimu ya afya kwa jamii,” amesema Dk Grace. Waziri wa Afya, Jenista Mhagama amezikaribisha sekta binafsi kushirikiana na Serikali katika kujenga huduma za kibingwa ili kuifanya Tanzania kuwa kituo cha utalii wa tiba. Amesema bado Serikali inahitaji ushirikiano na sekta binafsi katika maeneo mbalimbali. Kuhusu bima ya afya kwa wote, Jenista amesema Serikali inapokwenda katika utekelezaji, sekta binafsi inapaswa kushirikiana nayo kwa kuhakikisha huduma bora na rahisi zinapatikana. “Pamoja na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali lazima kuhakikisha sekta binafsi inaimarishwa ili kulinda usalama wa wananchi,” amesema. Waziri wa Afya Zanzibar, Ahmed Mazrui amesema ubia wa sekta binafsi umekuwa na mafanikio makubwa katika uboreshaji wa miundombinu ya vifaatiba vya kisasa. Amesema hospitali binafsi zimewekeza na kuhakikisha zinatoa huduma bora kwa wananchi. Waziri Mazrui amesema changamoto zilizopo zinaendelea kushughulikiwa hatua kwa hatua hivyo zinazidi kupungua. Amesema wameimarisha vituo vya afya ya msingi 52 na kujenga vipya 96 ili kufikia mwakani huduma za afya ziwe bora zaidi kwa wananchi.
http://www.mwananchi.co.tz/mw/habari/kitaifa/wananchi-wataja-wanayotarajia-kwa-rais-akihitimisha-mbio-za-mwenge-4782506
# Wananchi wataja wanayotarajia kwa Rais akihitimisha mbio za Mwenge ## Muktasari: **Kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu kinatarajiwa kufanyika mkoani Mwanza Oktoba 14 katika Uwanja wa CCM Kirumba** **Mwanza. **Wakati Rais Samia Suluhu Hassan akitarajiwa kuhitimisha mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2024 mkoani Mwanza, baadhi ya wananchi wametaja wanayotamani ayazungumzie, kutolea maagizo, ufafanuzi na kuyatatua. Kilele cha mbio hizo mwaka huu kinatarajiwa kufanyika mkoani Mwanza Oktoba 14 katika Uwanja wa CCM Kirumba. Wakizungumza na Mwananchi, baadhi ya wakazi wa jiji wamesema shauku yao ni kusikia Rais Samia akitatua changamoto ya maji, akisisitiza uwajibikaji kwa viongozi na watumishi wa Serikali, ubovu wa miundombinu ya barabara, ugumu wa maisha, suala la ajira, kauli chafu kwa baadhi ya viongozi, mikopo na migogoro ya ardhi. Mkazi wa Isamilo, Dua Nyauko akizungumzia uwajibikaji kwa watumishi na viongozi wa Serikali amedai kuwa, sasa hivi utaratibu wa kuwaona umekuwa mgumu kiasi cha kushindwa kupeleka kero zao. "Kwa mwananchi wa kawaida ukienda kwenye taasisi za Serikali kumuona bosi wa idara ni ngumu mpaka unajiuliza, je sisi hatustahili? Wakati wewe unaambiwa bosi ana vikao ila wengine wanaingia na kuongea naye na kuondoka," amesema. Hata hivyo, Nyauko ametaja changamoto ya ugumu wa maisha kuwa ni moja ya maeneo ambayo wananchi wanashauku ya kusikia Rais akitoa kauli ya matumaini kwa Watanzania. Mkazi wa Kata ya Kiseke, Mary Msisi amesema, "nitakuwepo na natamani kumuona Rais Samia akiwa kama mlezi wetu, atujali sisi wajane kwa kutupatia mikopo ili tuendeleze maisha yetu, pia aboreshe elimu ya shule ya msingi maana watoto wetu wanasoma lakini tunatoa gharama kubwa sana ya michango midogo midogo mfano watoto wa darasa la nne wana michango mingi sana," amesema Mary. Mkazi wa Buhongwa, Stephano Francis amesema anatamani kusikia kauli ya Rais Samia kuhusu changamoto ya uhaba wa maji na ubovu wa miundombinu katika baadhi ya maeneo jijini Mwanza kuwa inatatuliwa. Ester Eliabu amemuomba Rais Samia kushughulikia changamoto ya ukosefu wa ajira nchini na migogoro ya ardhi kwa kuwa imekuwa tatizo kubwa. Awali, akizungumza leo Oktoba mosi 2024 na waandishi wa habari, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda amesema mwenge huo baada ya kupokewa Oktoba 6, utakimbizwa kilomita 627 katika halmashauri nane za mkoa huo na kilele chake kitahitimishwa na Rais Samia. "Mwenge wa uhuru unaingia Mwanza Oktoba 6 mwaka huu, tunatarajia kuupokea katika Kijiji cha Nyamadoke Halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema ukitokea Geita, kwa hiyo kuanzia siku hiyo mpaka Oktoba 13 utakimbizwa katika halmashauri zote nane za mkoa huu," amesema.
README.md exists but content is empty. Use the Edit dataset card button to edit it.
Downloads last month
5
Edit dataset card