text
stringlengths 44
187k
| timestamp
timestamp[us] | url
stringlengths 16
3.37k
| dup_ids
list |
---|---|---|---|
#TBT: Baby J ft Taqwa - Mapenzi ya Kweli (+Video) | ZNZ_Zenji255
Home Videos #TBT: Baby J ft Taqwa – Mapenzi ya Kweli (+Video)
#TBT: Baby J ft Taqwa – Mapenzi ya Kweli (+Video)
Baby J, wengi humfaham kwa jina hilo. Lakini jina kamili la kuzaliwa anaitwa Jamila Abdallah Ally – ni mmoja ya wasanii kike wakongwe katika muziki wa kizazi kipya ‘Zenji & Bongo fleva’ kutoka visiwa vya Zanzibar.
Msanii huyo mwenye urefu wa kiasi, kwa mara ya kwanza alianza kutambulika kwenye anga ya muziki wa bongofleva kwa wimbo wake uliotwa Mapenzi ya Kweli, aliorekodi ndani ya studio za G Records kwa Omar Saidi Kombo a.k.a KGT Shadeed, na kweli wimbo huo ulikubalika kwa wapenzi na washabiki wa muziki huo ndani ya Zenj na hata bara kwa kiasi kikubwa.
Katika kazi yake muziki Baby J alifanikiwa kutwaa tuzo mbali mbali, mnamo mwaka 2008 alipata tuzo ya ‘Msanii Chipukizi wa kike wa mwaka’ na ‘Msanii wa kike wa mwaka’ na mwaka 2014-15 alipata tuzo ya ‘Mwanamuziki bora wa mwaka wa kike’.
Baby J ambaye alizaliwa takribani miaka 25 iliyopita ndani ya kisiwa cha karafuu, alianza kujiingiza kwenye fani ya muziki tangu mnamo mwaka 2006, baada ya kufanikiwa kuibuka na wimbo wake wa kwanza uliojulikana kwa jina la Mapenzi ya Kweli.
Katika mafanikio yake ya kimuziki Baby J ameshashiriki katika tamasha la ZIFF na maonyesho mbali mbali ya ndani na nje ya nchi. Kwa sasa Baby J pia amechaguliwa kuwa Makamu wa Rais wa chama cha wasanii wa muziki wa kizazi kipya Zanzibar (ZFU).
Angalia Video ya wimbo wake wa Kwanza kuachia akiwa amesmshirikisha Taqwa
| 2019-02-16T13:14:10 |
http://www.zenji255.com/tbt-baby-j-ft-taqwa-mapenzi-ya-kweli-video/
|
[
-1
] |
Je wajua mbwa ana jua tofauti zetu? - BBC News Swahili
Je wajua mbwa ana jua tofauti zetu?
https://www.bbc.com/swahili/michezo/2015/02/150213_dog_men
Image caption Mbwa rafiki
Utafiti unaonesha kwamba watu wanaopenda wanyama hasa mbwa,utafiti unaanisha kuwa binadamu hawezi kuficha hisia zake kwa mbwa ,kwani mnyama huyo anao uwezo mkubwa wa kushuku mambo na tofauti zetu kati ya furaha na taswira yenye hasira.
Wanasayansi wanaofanya utafiti katika kitengo cha Messerli Research Institute , juu ya maabara ya mbwa wenye utambuzi ,mjini Vienna huwafundisha mbwa kung’amua picha mbalimbali ikiwa picha aionayo ni ya mtu mwenye furaha ama hasira .
Katika utafiti uliofanywa mfululizo,wanasayansi walionesha mbwa taswira za watu ambazo hawakuwahi kuziona katika mafunzo yao, kumtambua mbwa kama anaweza kugundua sura na muonekano tofauti kwenye picha hizo.
Utafiti huu,ambao ulichapishwa katika jarida la masuala ya biolojia,ni sehemu ya utafiti mkubwa kujifunza namna rafiki wa mwanadamu ‘MBWA’ wanavyoweza kuchangamana.
Lengo kubwa la utafiti huo ni juu ya swali kubwa la mawasiliano yao, anasema kiongozi wa utafiti huo Profesa Ludwig Huber .Inakuwaje mbwa ajiungamanishe na mwanadamu kwa kiasi hiki? Na nini hutokea wakati wa mchakato wa ndani?
Wanasayansi wamerudia mara ishirini kuwaonesha mbwa nusu picha, ama iwe mdomo wa chini ama sehemu ya juu ya jicho la mtu mwenye furaha ama uso wenye hasira,lakini mbwa waling’amua tofauti.
| 2018-08-16T16:22:52 |
https://www.bbc.com/swahili/michezo/2015/02/150213_dog_men
|
[
-1
] |
Raila atishia kuongoza maandamano mapya kuhusu IEBC ▷ Tuko.co.ke
Made in Kenya Latest Politics Entertainment Swahili FEEDBACK LiveScore Submit Video Fighting Al-Shabaab Raila atishia kuongoza maandamano mapya kuhusu IEBC
3936 Chapisha twitter!
- Viongozi wa chama cha ODM wametishia kuandaa maandamano mapya dhidi ya tume huru ya uchaguzi na mipaka (IEBC) kwa muda wa wiki moja ijaayo iwapo makamishana wa tume hawatakuwa wamelipwa marupurupu yao na kuondoka afisiniViongozi wa upinzani wametishia kuandaa mandamano upya iwapo viongozi wa tume huru ya uchaguzi na mipaka (IEBC) hawatakuwa wameondoka afisini kwa muda wa wiki moja. Waandamaji
Habari Nyingine: Kidero akutana na Kalonzo badaada ya kukosana na kiongozi wa uchaguzi wa ODMWanasiasa hao wa ODM waliilaumu serikali kwa kuchelewesha juhudi hiyo.
Makamishna hao wa tume huru ya uchaguzi na mipaka (IEBC) walikuwa wamekubali kuondoka afisini punde wanapolipwa marupurupu yao.Habari Nyingine: Mbunge wa pili amkwepa Ababu Namwamba; aapa kubaki kwa Raila Hassan speaks
Spika wa Bunge Justin Muturi pia ameilaumu serikali kwa kuchelewesha juhudi hiyo akisema kuwa wizara ya fedha haijashughulikia swala hilo la kuwalipa makamishna hao KSh 164 milioni.Muturi aidha, anahofia kwamba makamishna hao wa tume huru ya uchaguzi na mipaka(IBEC) wanaeza badilisha nia yao na wakatae kuondoka afisini kwa vile hakuna sheria inayowalazimisha kuondoka.Read: ENGLISH VERSION
Isaak Hassan Iebc Voter Registration By Iebc Makamishna Wa Iebs Wajiuzulu Moto:
Akothee house Kenyan socialites Kcse leakage 2016 Kalonzo musyoka children Vincent ateya Habari zingine Uhuru afanya tangazo muhimu kuhusu bajeti ya mwaka huu
Uhuru afanya tangazo muhimu kuhusu bajeti ya mwaka huu Gavana Kidero akumbana tena na UHASAMA wa vijana Nairobi, anyeshewa mvua ya mawe!
Hofu yatanda baada ya wavamizi kufyatua risasi katika mkutano wa William Ruto
Huu ndio wasifu wa marehemu Gavana Nderitu Gachagua-Picha
Wafanyabiashara wamtupia pasta MAJENEZA ya MAITI kwa sababu hii ya kushangaza! (video)
| 2017-02-25T11:16:29 |
https://swahili.tuko.co.ke/205517-raila-atishia-kuongoza-maandamano-mapya-kuhusu-iebc.html
|
[
-1
] |
Harambee Stars yajiandaa kucheza na Taifa Stars – Habari Zao
May 24, 2016 Alli Matala News, Sports Harambee Stars yajiandaa kucheza na Taifa Stars
Wachezaji wa timu hiyo maarufu kama Harambee Stars wakiongozwa na kocha Stanley Okumbi walikusanyika uwanjani Kasarani na kufanya mazoezi ya kwanza Jumanne asubuhi.
Miongoni mwa wachezaji waliofika kambini ni wachezaji wanaosakata soka ya kulipwa katika ligi za nje ya Kenya.
Wachezaji wa timu ya Zesco ya Zambia wakiwemo Jesse Werre, David Owino na Anthony Akumu walikuwa baadhi ya wachezaji waliowasili.
Kiungo wa Southampton Victor Wanyama hakuwa amewasili na anatarajiwa kujiunga na timu hiyo wiki hii.
Kikosi kipya cha Taifa Stars chatajwa Tanzania
Baadhi ya wachezaji walioitwa kwenye kikosi walipewa ruhusa kuziwasilisha timu zao za ligi kwa minajili ya mechi za ligi zinazochezwa wiki hii.
Kenya itaachuana na Tanzania tarehe 29 mjini Nairobi siku chache kabla ya kuialika Congo kwa mechi ya kufuzu kwa kombe la Afcon 2017.
Wakati huo huo, timu ya wachezaji chipukizi wa Kenya wanatarajiwa kucheza dhidi ya Sudan Tarehe 27.
“Tunalenga kucheza mechi za kirafiki za kutosha ikiwezekana, ingawa sio kazi rahisi,’’ rais wa shirikisho la soka nchini Kenya Nick Mwendwa alisema.
Kenya imo katika kundi E ikiwa na alama moja baada ya kucheza mechi nne.
Tagged Featured, Harambe Stars, Taifa Stars Published by Alli Matala
China yakana kuuza nyama ya binaadamu AfrikaHarmonize asema Jackline Wolper alikuwa Single
Kuhusu mkanda wa ngono wa Lil Wayne na atakachofanya ukisambazwa. Picha,Huyu ndio Latiffah Nasibu Abdul mtoto wa Diamond na Zari. Picha,Kingwendu Alivyotikisa Kisarawe Picha: Mayunga akamilisha Collabo yake na Akon, amtumia mrembo aliyewahi kutumika kwenye video ya Chris brown ROSE NDAUKA: NIKO TAYARI KUOLEWA NA YEYOTE Follow Habari Zao on WordPress.com
Visitors 87,858 Visitors
| 2017-04-23T08:03:53 |
https://habarizao.wordpress.com/2016/05/24/harambee-stars-yajiandaa-kucheza-na-taifa-stars/
|
[
-1
] |
NICK WA PILI HATIMAYE AFICHUA MAZITO KUHUSU LORD EYEZ,AFUNGUKA LIVE ~ Blogu ya Wananchi
NICK WA PILI HATIMAYE AFICHUA MAZITO KUHUSU LORD EYEZ,AFUNGUKA LIVE
| 2017-01-17T11:02:34 |
http://www.williammalecela.com/2016/11/nick-wa-pili-hatimaye-afichua-mazito.html
|
[
-1
] |
Wanawake mkiamua, wanaume wote kwisha habari yetu!!!!!! | JamiiForums | The Home of Great Thinkers
Leo umefikiri nje ya Box...........................!
u tell me loh!Click to expand...
Leo umefikiri nje ya Box...........................!Click to expand...
Kusema ukweli as frm last week, nina perception tofauti sana ya wanawake! Mwanamke ni wa kuogopa. Si bure mlivyoamriwa kuwa muishi nao kwa akiliClick to expand...
Hebu fafanua hapa, vinginevyo Nitake radhi, maana baada ya kusoma hapa nimeanza kuhisi kizunguzungu!Click to expand...
Wewe pata tu kizunguzungu, wala huntishi, kwani ni mara ngapi nimeona nyuzi zako zimekaa kimazoea!? leo umeacha kufikiri kimazoea na umetoka nje ya box na ndio maana umeweka huu uzi uliosheheni hekima........... lolClick to expand...
Post yako imenifariji.Click to expand...
Bila shaka ulishafikia hatua ya kuchanganya sumu na pilau!Click to expand...
| 2017-01-17T01:27:19 |
https://www.jamiiforums.com/threads/wanawake-mkiamua-wanaume-wote-kwisha-habari-yetu.192137/
|
[
-1
] |
ENZKREIS -UJERUMANI YATOA VIFAA VYA MICHEZO KWA TIMU YA VOLLEYBALL, MASASI
Posted on: August 21st, 2018 style="text-align: justify;">Halmashauri ya Enzkreis ya Nchini ujerumani yenye ushirikiano na Halmashauri za Masasi imekizawadia kituo cha mpira wa wavu cha mkalapa vifaa vya michezo (Mipira 10 na Net...
Posted on: August 14th, 2018 Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Masasi mkoani Mtwara Mhe Fikiri Lukanga ameishukuru Halmashauri ya Enzkreis ya nchini ujerumani kwa msaada wao wa kuweka mifumo ya umeme Jua katika Zahanati 27 na...
Posted on: August 8th, 2018 style="text-align: justify;">Halmashauri ya Wilaya Masasi Mkoani Mtwara imeibuka mshindi wa kwanza wa maonesho ya Nanenane kanda ya kusini kwa mwaka 2018 kati ya Halmashauri 15 za Mikoa ya lindi...
| 2019-10-23T10:48:57 |
http://masasidc.go.tz/news/11
|
[
-1
] |
Kuchelewesha au kukusanya swalah kwa ajili ya kazi au masomo II | Firqatu Nnajia
Kuchelewesha au kukusanya swalah kwa ajili ya kazi au masomo II
Swali: Tunajua kuwa kuchelewesha swalah kwa wakati wake ni dhambi. Lakini wakati mwingine kunatolea hali ambazo zinaweza kupelekea mtu kuchelewesha swalah kwa wakati wake. Kama kwa mfano mtu ni mchungaji wa kondoo na huku anasikia anadhaana inatolewa. Lakini hata hivyo nachelea kondoo wasije kuharibu vipandwa vya vyetu au vya jiarani yetu. Matokeo yake swalah ikanipita hata kama nitakuwa peke yangu au ukanipita wakati wa Dhuhr kama inavyotokea mtu yuko katika muhadhara au kazini. Ni zipi nasaha zenu?
Jibu: Ni wajibu kwa muumini atilie umuhimu swalah kwa wakati wake. Akiwa yuko katika mashamba ambayo anakhofia juu yake, basi atangulie kwanza kuwaweka wanyama hao mbali na mashamba kabla ya wakati haujaingia ili aweze kuswali kwa wakati wake au kuswali kwa mkusanyiko ikiwa yuko pambizoni na mkusanyiko au msikiti. Mtu asichukulie wepesi kunako jambo la swalah mpaka wakati ukawa mfinyu. Ni wajibu kwa mtu huyo kumcha Allaah na afanye sababu za kuhifadhi swalah kabla wakati wake [haujatoka] ili asitumbukie katika kujifananisha na wanafiki ambao wanaziharibu swalah:
إِنَّ الْمُنَافِقِينَ يُخَادِعُونَ اللَّـهَ وَهُوَ خَادِعُهُمْ وَإِذَا قَامُوا إِلَى الصَّلَاةِ قَامُوا كُسَالَىٰ
“Hakika wanafiki wanamhadaa Allaah na [uhalisia wa mambo] Yeye ndiye anawahadaa na wanaposimama kuswali, basi husimama kwa uvivu.” (04:142)
Ni wajibu kwa waumini kutilia umuhimu jambo hili. Akiwa katika muhadhara au masomo basi asimamishe muhadhara au masomo na asimamishe swalah na aswali pamoja na waislamu katika misikiti yao. Ama akiwa sehemu ambazo si pambizoni na misikiti, bali ni mahali ambapo kunafanywa mihadhara au nad-wah, halafu baada ya hapo wanaswali kwa pamoja papo hapo, kama sehemu ambayo ni mbali na msikiti na karibu yake hakuna msikiti au jangwani au safarini, hali zote hizi hakuna neno. Wakimaliza basi wanachotakiwa ni kuswali kwa wakati na wasicheleweshe nje ya wakati wake. Bali wanachotakiwa ni kuswali kwa wakati wake.
Lakini yule ambaye yuko karibu na msikiti na yuko kijijini au mjini mwake, basi haifai kwake kuchelewesha swalah kwa sababu ya muhadhara, nad-wah, kondoo, ngamia au sababu nyenginezo. Ni wajibu kwake kutilia umuhimu yale yatayomsaidia kutekeleza swalah kwa mkusanyiko hata kama itahitajia kuwaweka kondoo au ngamia hao mbali na mashamba kabla ya kuingia wakati wake ili aweze kuswali swalah kwa wakati wake pamoja na waislamu wenzie. Haifai kwake kuchukulia wepesi jambo hili. Anapata dhambi kwa kufanya hivo.
Marejeo: Fataawaa Nuur ´alaad-Darb http://www.alifta.net/Fatawa/fatawaChapters.aspx?languagename=ar&View=Page&PageID=1239&PageNo=1&BookID=5
Kuchelewesha au kukusanya swalah kwa ajili ya kazi au masomo II Swali: Tunajua kuwa kuchelewesha swalah kwa wakati wake ni dhambi. Lakini wakati mwingine kunatolea hali ambazo zinaweza kupelekea mtu kuchelewesha swalah kwa wakati wake. Kama kwa mfano mtu ni mchungaji wa kondoo na huku anasikia anadhaana inatolewa. Lakini hata hivyo nachelea kondoo wasije kuharibu vipandwa vya vyetu au vya jiarani yetu. Matokeo yake swalah ikanipita hata kama nitakuwa peke yangu au ukanipita wakati wa Dhuhr kama inavyotokea mtu yuko katika muhadhara au kazini. Ni zipi nasaha zenu? Jibu: Ni wajibu kwa muumini atilie umuhimu swalah kwa wakati wake. Akiwa yuko katika mashamba ambayo anakhofia juu yake, basi atangulie kwanza kuwaweka wanyama hao mbali na mashamba kabla ya wakati haujaingia ili aweze kuswali kwa wakati wake au kuswali kwa mkusanyiko ikiwa yuko pambizoni na mkusanyiko au msikiti. Mtu asichukulie wepesi kunako jambo la swalah mpaka wakati ukawa mfinyu. Ni wajibu kwa mtu huyo kumcha Allaah na afanye sababu za kuhifadhi swalah kabla wakati wake [haujatoka] ili asitumbukie katika kujifananisha na wanafiki ambao wanaziharibu swalah: إِنَّ الْمُنَافِقِينَ يُخَادِعُونَ اللَّـهَ وَهُوَ خَادِعُهُمْ وَإِذَا قَامُوا إِلَى الصَّلَاةِ قَامُوا كُسَالَىٰ “Hakika wanafiki wanamhadaa Allaah na [uhalisia wa mambo] Yeye ndiye anawahadaa na wanaposimama kuswali, basi husimama kwa uvivu.” (04:142) Ni wajibu kwa waumini kutilia umuhimu jambo hili. Akiwa katika muhadhara au masomo basi asimamishe muhadhara au masomo na asimamishe swalah na aswali pamoja na waislamu katika misikiti yao. Ama akiwa sehemu ambazo si pambizoni na misikiti, bali ni mahali ambapo kunafanywa mihadhara au nad-wah, halafu baada ya hapo wanaswali kwa pamoja papo hapo, kama sehemu ambayo ni mbali na msikiti na karibu yake hakuna msikiti au jangwani au safarini, hali zote hizi hakuna neno. Wakimaliza basi wanachotakiwa ni kuswali kwa wakati na wasicheleweshe nje ya wakati wake. Bali wanachotakiwa ni kuswali kwa wakati wake. Lakini yule ambaye yuko karibu na msikiti na yuko kijijini au mjini mwake, basi haifai kwake kuchelewesha swalah kwa sababu ya muhadhara, nad-wah, kondoo, ngamia au sababu nyenginezo. Ni wajibu kwake kutilia umuhimu yale yatayomsaidia kutekeleza swalah kwa mkusanyiko hata kama itahitajia kuwaweka kondoo au ngamia hao mbali na mashamba kabla ya kuingia wakati wake ili aweze kuswali swalah kwa wakati wake pamoja na waislamu wenzie. Haifai kwake kuchukulia wepesi jambo hili. Anapata dhambi kwa kufanya hivo. Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziy bin ´Abdillaah bin Baaz Mfasiri: Firqatunnajia.com Marejeo: Fataawaa Nuur ´alaad-Darb http://www.alifta.net/Fatawa/fatawaChapters.aspx?languagename=ar&View=Page&PageID=1239&PageNo=1&BookID=5 Imechapishwa: 15/03/2018 http://firqatunnajia.com/kuchelewesha-au-kukusanya-swalah-kwa-ajili-ya-kazi-au-masomo-ii/
Kuswali nyuma ya imamu anayefanya Qunuut Fajr
| 2018-09-19T07:33:58 |
http://firqatunnajia.com/kuchelewesha-au-kukusanya-swalah-kwa-ajili-ya-kazi-au-masomo-ii/
|
[
-1
] |
SIMBA YAZIDI KUUKARIBIA UBINGWA, YAWACHEZESHA KWATA MAAFANDE WA TZ PRISONS - SUFIANIMAFOTO
Home Michezo SIMBA YAZIDI KUUKARIBIA UBINGWA, YAWACHEZESHA KWATA MAAFANDE WA TZ PRISONS
SIMBA YAZIDI KUUKARIBIA UBINGWA, YAWACHEZESHA KWATA MAAFANDE WA TZ PRISONS
Muhidin Sufiani Monday, April 16, 2018
Washambuliaji wa Simba Emmanuel Okwi (kushoto) na John Bocco, wakishangilia, bao la kwanza lililofungwa na Bocco katika kipindi cha kwanza,wakati wa mchezo wa Ligi Kuu Bara uliomalizika hivi punde kwenye kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Katika mchezo huo Simba wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 yaliyofungwa na John Bocco katika dakika ya 35 na Emmanuel Okwi katika dakika ya 80. Picha na Muhidin Sufiani, (MAFOTO).
Beki wa Simba Shomari Kapombe (kushoto) akiwania mpira na wachezaji wa Tanzania Prisons, Leonsi Mutalemwa (katikati) na Eliuter Mpepo, wakati wa mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam
John Bocco (kushoto) akiwania mpira na beki wa Tanzania Prisons, Leonsi Mutalemwa, wakati wa mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini
Emmanuel Okwi, akijipinda kupiga shuti huku beki wa Tanzania Prisons, Nurdin Chona, akijaribu kuokoa, wakati wa mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini
Asante Kwasi (katikati) akiwania mpira na mabeki wa Tanzania Prisons, wakati wa mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini.
| 2018-07-18T14:54:27 |
http://www.sufianimafoto.com/2018/04/simba-yazidi-kuukaribia-ubingwa.html
|
[
-1
] |
Ufufuo na Uzima GCTC: IBADA YA JUMAPILI NA MCHUNGAJI KIONGOZI JOSEPHAT GWAJIMA KUTOKA KAWE,DSM TAREHE 10.11.2013
IBADA YA JUMAPILI NA MCHUNGAJI KIONGOZI JOSEPHAT GWAJIMA KUTOKA KAWE,DSM TAREHE 10.11.2013
BAADA YA MCHUNGAJI KIONGOZI, JOSEPHAT GWAJIMA,ALIYEKUWA AMEONGOZANA NA MAELFU YA WATENDA KAZI WALIOKUWA KATIKA MIKOA YA ARUSHA NA MOSHI HATIMAYE AREJEA KATIKA NYUMBA YA UFUFUO NA UZIMA KAWE, DSM.
Maelfu ya watu wa Mungu waliokusanyika katika viwanja vya Ufufuo na Uzima, kawe, wakifurahia na kumsifu Mungu kwa Kumtumia vyema Mchungaji Kiongozi Josephat Gwajima katika mikoa ya Arusha na Moshi na kuikomboa mikoa hiyo Kwa jina la Yesu.
Nyuso zilizojaa furaha na kumtukuza Mungu kwa kuwa ametenda mambo Makuu, kupitia kwa Mchungaji kiongozi Josephat Gwajima.
Waimbaji wakiwa na nyuso za furaha ambayo ni kubwa sana kiasi wakawa wameshindwa kuielezea baada ya kummpokea Mchungaji Kiongozi, Josephat Gwajima.
SOMO: KUSUDI LAKO LA MILELE
Na Mch.Kiongozi, Josephat Gwajima
Kila mtu alie hai Mungu amepanda ndani yake (moyoni mwake) ambalo ni kusudi lake la milele.
Waefeso 3:11
“…Kwa kadri la kusudi la milele alilolikusudia katika Kristo Yesu…” Inatufundisha hapa kwamba kila mtu alie hai ana kusudi la milele limeandikishwa ndani ya moyo (maelekezo yako ndani ya moyo yameandikishwa ili utakapo kuwa mkubwa, ndio yanatengeneza uwewe na mambo kadha wa kadha), hatma ya maisha yako inauhusiano mkubwa sana na moyo wako.
Nini maana ya moyo?
Kazi ya moyo ni kupeleka minerals (madini), ndani ya mwili kupump (kusukuma) oksijeni, mwili mzima na kusukuma uchafu nje ya mwili. Mara moyo wa mtu utakapo acha kufanya kazi mtu anakufa hapo hapo, sababu moyo ndiyo centre inayofanya mtu aishi.
Kuna utu wa ndani ya mtu ambao ni roho, na nje ya mtu ambao ni mwili, na mtu wa ndani (ambaye ni roho) naye ana moyo pia, ndio maana Mungu ni Roho lakini ana moyo Mwanzo 8:21 “Bwana akasikia harufu ya kumridhisha; Bwana akasema moyoni sitailaani nchi tena”.
Mwanzo 17:17 “Ibrahimu akaanguka kifudifudi akacheka, akasema moyoni…” Mwanzo 18:12 “Sara Moyo wake ukacheka Mwanzo 24:45.
Mungu anapotaka kupanda kusudi la maisha ndani ya mtu hupanda moyoni, ndio maana moyo wa mtu ukiwa mzito mambo yake hayawezi kufanikiwa, atakuwa anaona uzito katika kila jambo analolifanya.
Mwanzo 27:41, “…Esau akasema moyoni mwake...” Kutoka 4:14 “… naye atakapokuona atafurahi moyoni mwake…”
Kumbukumbu la torati 2:30 “..akamtia ukaidi moyoni mwake..” tunajifunza unapotiwa ukaidi moyoni mwako, ukaidi huo unajidhihilisha mwilini, unakuta mtu hupendi kuwa mkaidi, lakini ndio unakuwa ushatiwa ukaidi. Ndio maana mtu utamsikia anasema nakupenda kutoka moyoni mwangu, hapo cha kujiuliza je huo moyo anaouzungumzia ni wa kwake, maana watu hutiwa mioyo tofauti na kusudi la Bwana.
Mithali 4:23 “..linda sana moyo wako kuliko vyote ulindavyo maana huko ndiko zitokako chemichemi za uzima..” Biblia ya kiingereza inasema “Keep thy heart with all diligence; for out of it are the issues of life” Tunajifunza hapa mambo yote za maisha ya mtu huanzia moyoni, matatizo yanayowakumba watu au mafanikio ya mtu huanzia moyoni mwa mtu, “ISSUES OF LIFE”
Kutoka 35:35 “…Amewajaza watu hao akili za moyoni ili atumike katika kazi ya kila aina...”
kutoka 35:34 “…nimemtilia moyoni mwake ili apate kufundisha..”
Siku hii ya leo, ninaomba Mungu apande jambo moyoni mwako, ili kutimiza kusudi la nchi yetu Tanzania. “Utamkuta mtu mwingine anatenda jambo kwa ufanisi ulio wa juu mpaka watu wanashangaa wanamuuliza hivi ulisoma wapi, kumbe hata hajasoma lakini ndio kusudi la moyo wake.
Mungu amepanda kitu ndani ya moyo wako ili kupitia kile uwe na mafanikio, shule haiwezi kukuletea mafanikio, kile kilichopandwa ndani ya moyo wa mtu ndio mafanikio yake. Ufufuo na Uzima imepandwa ndani ya moyo wa Yesu, ndio maana hatuhitaji mtu atuelekeze njia ya namna ya kwenenda.
Kumbukumbu 4:9 “..mambo uliyoyaona yakaondoka moyoni mwako…”, Kumbukumbu 8:2 “…kuyajua yaliyo moyoni mwako…” Hata Mungu kuwapitisha wana wa Israel jangwani ni ili Mungu ajue yaliyo mioyoni mwao, kama watashika amri zake ama sivyo.
“Issues za maisha zipo mioyoni mwa mtu” Nataka nianze biashara, nataka nisome shule, nataka niache kazi vyote hivyo huanzia moyoni. Moyoni mwangu nikimtumikia Mungu najisikia vizuri, nikimuimbia Mungu njisikia vizuri, nikimtolea Bwana moyoni mwangu najisikia vizuri sana, ndio maana mtu anasema nasema kutoka moyoni Mwangu. Na ukisimamia kusudi hilo utafika pale Mungu alipokukusudia.
Shetani ana tabia ya kuiba mioyo ya watu yenye kusudi la Mungu, anaandikia maelekezo yake yeye ambayo ni tofauti na maelekezo ya Mungu, anakutole kusudi la Mungu anaandika maelekezo yake ili uelekee upotevuni, utasikia najisikia nikaibe kabisa, najisikia niwe mwana mziki, najisikia nivute bangi, napenda ukahaba, kumbe ndio maelekezo yaliyonakiriwa na shetani ndani ya moyo wako.
Unakuta mtu alivyokuwa mtoto mdogo, alikuwa anampenda Mungu, anasema nataka nimtumikie Mungu, niwe mchungaji, niwe mwimbaji, lakini mtu huyo akishakuwa mtu mzima anakuwa tofauti kabisa “ukiona upo hivyo ujue umebadilishiwa moyo”.
Unakuta mtu ameokoka anaolewa na mganga wa kienyeji, mnamuuliza mnamwambia unawaza nini wewe anakwambia Mchungaji nampenda toka moyoni mwangu, nampenda huyu kaka toka moyoni, ukiangalia kaka mwenyewe ni mvuta bangi, hata haeleweki. Kumbe moyo wako uliibiwa na shetani na huyo kaka mvuta bangi akaandikishwa ndani ya moyo wako, bila wewe kujua.
Mtu umeokoka lakini unakuta unampenda binti/kaka wa kiislamu, kumbe umebadilishiwa moyo, wamenakiri kwenye moyo wako kuwa utaolewa ana kuoa muislam. Leo tunarudisha mioyo yote uliyobadilishiwa, lazima kusudi la Bwana litimie, kusudi la Bwana ulilowekewa ndani ya moyo wako tunalirudisha leo kwa jina la Yesu. “Daudi alisema eeh moyo wangu na vyote vilivyo ndani yangu mche Bwana”.
Shetani anajua issues zako zote za maisha yako zinatokea moyoni, kiu yako ya kuimba, kuhudhulia ibadani, kutoa fungu la kumi, kumtumikia Bwana vyote huanzia moyoni. Shetani ili abadilishe kusudi lako anaiba moyo, anabadilisha kusudi lililonakiriwa na Mungu moyoni mwako, anaweka maelekezo yake, unajikuta uliyokuwa unatenda hutendi tena, unaingiwa na kiu ya kutenda mambo mengine ambayo hujawahi hata kuyawaza. Lakini wewe ukikaa unaona upo sahihi sababu unachokifanya kinatoka moyoni, kumbe umebadilishiwa moyo ili uelekee upotevuni.
Kuna watu huwa wanajuta baada ya kutenda jambo, usiangalie kwamba hili jmbo linatoka moyoni mwangu, cha kufahamu ujue huo moyo ni wa kwako, unayoyatenda ni kusudi la Bwana tangu awali? Huu ni wakati wa kukana maelekezo ya moyoni mwako kama sio kusudi la Mungu. Shetani amepanda jambo ndani ya moyo wako umeanza kulitumikia, kumbe ni kusudi lililopandwa na shetani.
Shetani akitaka kukuandikia maelekezo yake, huwa lazima usumbufu utokee, ulikuwa unajiweza vizuri kifedha, ghafla unakosa hela ya kula, hata hela ya kwenda kanisani huna, kazi unafukuzwa kumbe ni shetani anakuandaa kukuchomoa kwenye lile kusudi la Mungu, ukishaona umechoka hueleweki shetani anakuambia hilo sio kusudi lako, anakubadilishia maelekezo yaliyondani mwako “mara unaalikwa kwenye semina ya “empowerment”, kumbe shetani ndio anakuwa anakutengeneza kwenye kusudi lake.
Leo ninamlazimisha shetani na watenda kazi wake wote kurudisha mioyo yenu ya asili irudi kwenu, na moyo wako unarudi kwa jina la Yesu. Unarudi kwenye kusudi lako la milele.
Ngo’a maelekezo ya kishetani yaliyopandwa ndani ya moyo wako ili yakuongoze kwenda mbali na kusudi lako la milele, nayaondoa maelekezo hayo kwa jina la Yesu. Ninakataa maelekezo yaliyowekwa ndani ya moyo wangu kugeuza kusudi la Mungu ndani yangu, kama niliandikiwa kuwa muombaji narudisha kusudi hilo kwangu kwa jina la Yesu, ninakataa kiu ya miziki ya kizazi kipya ndani yangu, kiu ya uzinzi, kiu zote za kishetani kunipindisha na kusudi langu la milele nakataa kwa jina la Yesu.
Leo namng’ang’aniza shetani na malaika zake na majini yake na vibwengo vyake warudishe moyo wako kwa jina la Yesu. Maelekezo ya kishetani yalioandikishwa ndani ya moyo wangu ili kunipeleka mbali na Mungu nayakataa kwa Jina la Yesu, maelekezo yaliyonipeleka mbali na baraka zangu naukataa moyo wenye maelekezo hayo kwa jina la Yesu, anza kudai moyo wako, moyo wa kumcha Bwana, moyo wa ubunifu, moyo wa mafanikio, moyo wa safari nautaka moyo wangu kwa jina la Yesu.
Moyo wa kiburi mlioniwekea naukataa kwa jina la Yesu, moyo wa mauti mlioniwekea naukataa kwa jina la yesu, nautaka moyo wangu kwa jina la Yesu. Nataka moyo wangu, moyo wa ushindi, moyo wa kushika fedha, moyo wenye msimamo, moyo unaompenda Yesu, naurudisha moyo wangu katika jina la Yesu Kristo.
Posted by Glory of Christ Tanzania Church: Nyumba ya Ufufuo na Uzima at 3:20 AM
Location: Kawe, Dar es Salaam, Tanzania
| 2017-09-26T14:44:08 |
http://ufufuonauzima.blogspot.com/2013/11/ibada-ya-jumapili-na-mchungaji-kiongozi.html
|
[
-1
] |
Mzee wa Mshitu: MKUTANO WA MILLIWARDBROWN NA WADAU WA MASOKO NA VYOMBO VYA HABARI
MKUTANO WA MILLIWARDBROWN NA WADAU WA MASOKO NA VYOMBO VYA HABARI
Mkurugenzi Mtendaji kanda ya Afrika na Kati kutoka Millard Brown Charles Foster akiwasilisha utafiti kuhusu teknolojia ya matangazo kwa bara la Afrika wakati wa semina na wadau wa vyombo vya habari,kampuni za matanganzo na vyombo vya habari leo jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Masuala ya Habari kutoka MillwardBrown Anderzej Suski akijibu baadhi ya masuali kutoka kwa wajumbe wakati wa mkutano wa masuala ya masoko ,matangazo na vyombo vya habari leo jijini Dar es Salaam.
Wadau na wataalamu wa masuala ya masoko na matangazo wakishiriki katika mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na watoa mada wakati wa mkutano uliowakutanisha wadau hao leo jijini Dar es Salaam.
Wadau na wataalamu wa masuala ya masoko na m atangazo wakifuatili mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa na watoa mada wakati wa mkutano uliowakutanisha wadau hao leo jijini Dar es Salaam.
| 2018-03-24T02:19:40 |
http://charaz.blogspot.com/2015/08/mkutano-wa-milliwardbrown-na-wadau-wa.html
|
[
-1
] |
KUISHINDANIA IMANI – …UTAIINUA MISINGI YA VIZAZI VINGI… (Isaya 58:12)
October 13, 2012 October 27, 2012 Sanga
KUISHINDANIA IMANI
Mwandishi wa kitabu cha Yuda ameanza kwa kusisitiza akisema, Wapenzi nilipokuwa nikifanya bidii sana, kuwaandikia kwa habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote, naliona imenilazimu kuwaandikia, ili niwaonye kwamba mwishindanie imani waliyokabidhiwa watakatifu mara moja tu (Yuda 1:3)
Imani ni nini? Biblia inasema ‘Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana’ (Webrania 11:1). Chanzo cha imani ni nini? Paulo kwa Warumi anafafanua akisema ‘Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo’ (Warumi 10:17). Hivyo imani ambayo tunapaswa kuishindani ni uhakika tulionao juu ya neno la Mungu, msingi ukiwa Yohana 3:16 inayosema ‘Kwa maana jinsi hii Mungu, aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele’.
Kwa nini tuishindanie imani?
Vita iliyopo kwenye ulimwengu wa roho kati ya Mungu na Shetani. Katika Waefeso 6:12 Biblia inasema ‘Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho’
Kuna watu wamejiingiza kwa siri ili kuivuruga imani yetu katika Kristo, Biblia inasema katika Yuda 1:4 ‘Kwa maana kuna watu waliojiingiza kwa siri, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, makafiri, wabadilio neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi, nao humkana yeye aliye peke yake Mola, na Bwana wetu Yesu Kristo’
Wapo walioangamizwa kwa sababu ya kushindwa kuishindania imani Biblia inasema katika Yuda 1:5 ‘…Bwana, akiisha kuwaokoa watu katika nchi ya Misri, aliwaangamiza baadaye wale wasioamini,
Bila imani hatuwezi kumependeza Mungu. Imeandikwa ‘Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao’ (Waebrania 11:6)
Kwa namna gani mtu unaweza kuishindania imani?
Kuendelea kuongeza imani yako (Rejea Luka 17:5, Warumi 10:17 na Mathayo 17:21) Kutokana na upungufu wa imani ambao wanafunzi walikuwa nao kwa mujibu wa Mathayo 17:21 ndipo katika Luka 17:5 wakamwomba Bwana awaongezee imani. Ili kuongeza imani sharti ujifunze ‘kusikia’ neno la Mungu kila siku. Naam ujenge nidhamu ya kusoma neno la Mungu, kujali ibada na pia kuwa na utaratibu wa kuwa na ibada hata nyumbani kwako.
Kwa kulinda nafasi uliyopewa/ulizopewa na Mungu (Rejea Yuda 1:6, Wimbo Ulio Bora 1:6, Mathayo 22:8). Maadam umeokoka wewe ni Mlinzi wa kusudi la Mungu katika ulimwengu wa roho kwenye eneo ulilopo. Zaidi kiroho, kiuchumi, kijamii, kifamilia, kiknisa nk kuna nafasi ambazo Mungu ametupa sit u katika ulimwengu wa mwili zaidi ni katika ule wa kiroho, hivyo ni jukumu letu kuzilinda. Je upo makini kiasi gani kulinda nafasi uliyopewa na Mungu katika ulimwengu wa roh na ule wa mwili.
Kwa kuwa na ufahamu wa nyakati unazoishi. Mungu ameziweka nyakati ili zituongoze kufanikisha kusudi lake kwa kufanya kile kinachotakiwa kufanyika kwa wakati husika. Naam ni jukumu lako kuwazanyakati ulizopo zinataka nini kutoka kwako. Naam jifunze kutoka kwa wana wa Isakari maandiko yanasema ‘Na wa wana wa Isakari, watu wenye akili za kujua nyakati, kuyajua yawapasayo Isareli wayatende; vichwa vyao walikuwa watu mia mbili na ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao’ 1Nyakati 12:32. Kwa ufahamu zaidi juu ya nyakati rejea maandiko yafuatayo (Muhubiri 3:1-8, Mwanzo 8:22, Waefeso 5:15-17, 1Wathesalonike 5:1-4, Luka 19:41).
Endelea kuwa mwaminifu hata kama huoni matokeo yake sasa. Uaminifu wako ndio utakaodhihirisha kwamba wewe unaishindania imani. Imeandikwa ‘Mtu mwaminifu atakuwa na Baraka tele (Mithali 28:20a). Mungu hawezi kukuacha uabike mpendwa wangu, usijiingize kufanya mambo yanayokuondolea uaminifu wako kwa Mungu, maana kwa kufanya hivyo utapelekea wokovu wetu katika Kristo kutukanwa.
Shetani anajua kwamba ameabikiwa na muda mchache wa kufanya kazi zake hapa duniani. Lengo lake ni kuhakikisha anadanganya watu wengi wa kwenda nao kwenye ziwa la moto ambalo kimsingi liliandaliwa kwa jili yake na Malaika walioasi. Usiruhusu hila yake, roho ya kuchoka na kukata tamaa vikumalize na kuharibu mahusaino yako na Mungu. Hakikisha unadumu katika kuishindania imani hata ajapo Mwana wa Adamu, maana pasipo Imani haiwezekani kumpendeza.
Mungu akubariki, na tuzidi kuombeana.
Previous KWA NAMNA GANI MTU ANAWEZA KUMZIMISHA ROHO MTAKATIFU?
Next NAMNA MWANAMKE ANAVYOWEZA KUTUMIA NAFASI ZAKE KUBADILISHA MAISHA YA NDOA YAKE (Sehemu ya 3)
Alphonce Michael says:
Tunamshukuru Mungu kwa huduma hii aliyo kupa kwakweli inatubariki, inatujenga na kutuimarisha pia. Mungu akubariki.
Glory to Jesus, Amen.
Asante saana, Mungu azid kukupa uweza, hakika umebarikiwa
Amina, glory to Jesus.
Ubarikiwe sana mtu wa Mungu, binafsi mafundisho yako yamenibariki sana na nitayatumia mafundisho haya kuwabariki wengine wasioweza kutembelea kwenye mitandao ya kijamii kama hii.
Utukufu kwa Mungu, uwe na amani, fanya kazi ya Mungu, uyatumie tu kadri BWANA akuongozavyo ili mwili wa Kristo uzidi kujengwa.
Baraka Kapele says:
Lukes osebe says:
Being blessed so mutch.Amen
| 2018-01-23T02:02:04 |
https://sanga.wordpress.com/2012/10/13/kuishindania-imani/
|
[
-1
] |
MTWARA KUMEKUCHA: MREJESHO WA KAMANDA WILFRED LWAKATARE
Na Wilfred Lwakatare,
“Kama raia!kama raia!kama raia!kama raia!
Kama raia…….”
Ni kweli kabisa na wala si hadithi kuwa ‘jela ni MBAYA, jela ni MATESO!’ Lakini zaidi ya hilo, kwangu mimi nimeyaona pia maisha ya gerezani ni mahala pa mafunzo ya kuijua jamii, kuyajua maisha, kuyaelewa mambo, kuifahamu nchi n.k.
Nimekubaliana mia kwa mia na maneno ya mwenyekiti wetu wa CHADEMA-Taifa Freeman Mbowe(MB) aliponitembelea gerezani Segerea na kuniambia; “hupaswi kulia na kujuta sana;now you are going to be a PRISON GRADUATE, uhitimu ambao kila mwanasiasa na mpigania haki mahiri duniani ameupitia.” Kipindi cha siku 92 nilichokaa ndani nikianzia polisi kituo cha kati, gereza la Keko na kisha kumalizia Segerea kimenipa uzoefu na ufahamu usio wa kawaida.
Lakini pia, nilitembelewa na viongozi wakuu wengi wa jeshi la magereza nchini akiwemo kamishena mkuu Minja.Wakuu hawa wana weledi mkubwa wa kumpa mtu somo la ‘ushauri nasaha’(counselling). Wanakufutia fikra zote za uraiani (nyumbani,mitaani na ofisini) na kukurejesha mahala pa maisha yako mapya ya gerezani na kukujuza taratibu na kanuni unazopaswa kuzifuata na kuzitii.
Kwanza tuhuma ya ugaidi niliiona kama kombora la mwisho la serikali ya CCM kukamilisha mkakati wao wa kuichimbia CHADEMA kaburi ambayo siku zote huwa ni ya pembe nne na katika kuichimba na kuifukia kawaida koleo lenye umbo la ‘U’ mbele na mpini wake hutumika.
“U” ya kwanza yenye kutubamkikizia tuhuma za ufamilia,Ukabila,Uchagga,Ukask azini alikuwa amebebeshwa mwenyekiti Mbowe zikashindwa. “U” ya pili yenye kuzoa tuhuma za Udini,Ukatoliki,Upadri alibebeshwa katibu mkuu Dr.Slaa nazo zikakwama CHADEMA ikapenya. “U” ya tatu yenye kulenga Uchonganishi,Umbea,Ufitinishaj i na Usongombingo, CCM wakalenga kumbebesha Naibu katibu mkuu kijana Zitto Kabwe lakini naye akawashtukia akawaumbua na kuwabwaga. Zitto ameendelea kuhimiza mshikamano mkubwa ndani ya chama na kuwaacha wapambe nuksi hoi. “U” ya mwisho yenye kubeba Ugaidi,Uuaji,Utekaji iliyolenga kukifuta kabisa chama vitabuni na kuwasweka viongozi gerezani, kabambikiziwa Wilfred Lwakatare Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama CHADEMA.Mungu mkubwa nayo hiyo mahakama kuu yenye baadhi ya majaji weledi wa sheria na wasiokubali mizengwe wameifutilia mbali.Hakika CHADEMA haizuiliki na kwa hakika lililobaki ni kulitumia koleo hilohilo na “U” hizo kuwafukia CCM humohumo kwenye kaburi walilojichimbia wenyewe. ‘Mchimba kaburi huingia yeye mwenyewe.’
Nashukuru CHADEMA hivi sasa imejipanga kama taasisi makini inayoongozwa na kusimamiwa kitaasisi na wala si kwa utashi wa mtu binafsi au kundi fulani la watu bali vikao vya kikatiba. Mshikamano wa pamoja na fikra zinazotuelekeza kulenga paala pamoja tulikodhamiria, hivi sasa ndiyo silaha kubwa na nusuru yetu kichama. Kama CHADEMA inavyoamini ; “TUNAANZA NA MUNGU, TUNAENDELEA NA MUNGU NA TUNAMALIZA NA MUNGU.”
Wakati nikihojiwa na jopo la maofisa wa makao makuu ya polisi la akina Mhigulu wakati huo akiwa Kaimu DCI na wenzake akina Obadia,Jonas,Simon Pasua,Beneth Kipasuka,Nyombi na wengineo baadhi yao niliwapa ujumbe wamfikishie ‘college mate’ wangu (IGP Said Mwema ) Chuo kikuu cha Dar es Salaam kuwa naziona jitihada na mbio zao za kuwatafuta hao watu wanaoitwa magaidi,wateka madaktari na waaandishi,wapiga risasi mapadri n.k mbio zao haziwezi kufaulu kutokana na namna wanavyoliendesha zoezi.
Wakili wangu Kichehere niliyekuwa naye katika mahojiano wakati nikihojiwa kituo cha kati alijaribu kuwapa changamoto japo chache za kupanua akili zao kuhusu huo unaoitwa ugaidi dhidi yangu na ‘ka-cd’ kao walikokachota kwenye mtandao wa “You Tube” (kama walivyotueleza) na kutuonyesha pale kwenye mahojiano. Hawakutaka kumsikiliza wala kumuelewa juu ya kasoro zilizojidhihirisha moja kwa moja . Hata pale alipowashauri kuwaita na kuwahoji baadhi ya watu muhimu walioonekana kuhitajika ili kuondoa walakini usio na sababu tangu mwanzo wa zoezi, hawakutaka kuuchukua ushauri huo. Wakaona waendelee kukimbia na hako ‘ka 109’ kao. Mimi naamini upo wakati ambapo mshtukiwa wa tukio linalochunguzwa aliye mzalendo na nchi yake anaweza kuwa msaada wa kuinusuru nchi yake anayoipenda endapo anapewa nafasi ya kutoa ushirikiano kwa njia za kuheshimiana kiutu .
Ukiacha kesi yangu hiyo ya kutuhumiwa ugaidi, lakini kukaa kwangu pale polisi central (kituo cha kati),gerezani,keko na Segerea kumenithibitishia vituko na mambo chungu nzima niliyokuwa nikiyasikia nikiwa uraiani na kufikiria ni ya uongo. Vitendo vya watu kubambikiwa kesi viko njenje na wenyewe kwa lugha zao wanaita; “kumpa mtu kichwa! kumpiga mtu armed robbery! kumpeleka mtu mapumziko!n.k” Nafikiri watu wanaofanya vitendo hivi wanahitaji kufanyiwa ‘concelling…’ ( kupewa ushauri nasaha) kwani sio vitendo vya kiutu.
Hivi huu ni utamaduni gani na taifa tunalipeleka wapi? Hivi kweli inaingia akilini wakati mchezo kama huo ukiendelea na watu kibao kubambikiziwa kesi kwa ‘kupewa vichwa’ wakati huohuo mh.JK yuko ‘busy’ kuwatunuku watu nishani za utumishi uliotukuka? ‘This is a typical shame!!’ Sijui kama usalama wa Taifa wapo. Hivi wanafanya kazi gani kama hawamsaidii mheshimiwa Rais kumjuza kinachoendelea? Au ni ugonjwa uleule mchanganyiko wa ‘sisiemhosis’. Naanza kukubaliana na usemi wa mtu mmoja niliyeongea naye gerezani Segerea aliyesema vyombo vya kulinda usalama huenda ni vya kulinda usalama wa viongozi walaji,wahujumi wa nchi,mafisadi na mfumo aliouita ; “chukua chako mapema.”
Na ni vyombo vyenye weledi mkubwa wa kuchora michoro ya fitina,uongo,wizi,hujuma,kusam baratisha vyama vya upinzani kuiba kura kutisha watu kutengeneza kesi bandia,kuandaa mashahidi feki n.k. Matokeo yake watu ambao leo hii wamejaa na kurundikwa magerezani na mahabusu za polisi,asilimia kubwa wanakuwa hawana hatia wahalifu wakubwa wako nje wakiendelea kula nchi! Asilimia kubwa ya kesi zinazopelekwa mahakamani ni feki na ni za kuwachosha mahakimu na majaji bila sababu kwani kesi hizo huishia kufutwa.
Mrundikano mkubwa magerezani wa wafungwa na mahabusu unasababisha hata huduma ziwe mbovu. Wapo wafungwa hawana sare za gereza wanavaa kitu kinachoitwa ‘nusu mlingoti’, kauka nikuvae, sare zilizochanika kiasi cha kutia aibu.Na kwa kuwa hata sera za uendeshaji magereza nyingi ni zilezile za ‘vichwa vya ki-CCM’ (chama dhaifu,wabunge dhaifu na serikali dhaifu) hakuna akili inayoweza kubuni namna ya kuitumia kiufanisi nguvu kazi kubwa iliyojaa magerezani. Ndani ya gereza kuna kila aina ya fani na vipaji lakini vimelala tu. Kama vile CCM, hawazai na hawana watoto nyumbani, huwezi kuamini watoto lukuki waliorundikwa Segerea bila utaratibu mzuri wa kimalezi na kimakuzi hata kama baadhi yao ni wakorofi na wahalifu. Tutake, tusitake hawa ni taifa la leo na la kesho.Hawa ni nguvu kazi yetu ya nchi ,hawa wanahitaji kukunjwa wangali wabichi.
Watoto hawa ambao wengine ni wa umri wa miaka kumi wenye kesi za kuiba embe tano,kuiba simu, kudokoa pochi zenye elfu 30,000/=n.k,wamo gerezani wakinyweshwa uji asubuhi,ugali wa dona na mchuzi mwingi wenye maharage thelathini kwenye bakuli na muda unaobaki kuutumia kufundishana ngumi,kupiga ‘vice’, na mengine mengi. Kuna kitu kipya ambacho kimebuniwa na uongozi wa jiji la Dar es Salaam ‘kuusafisha mji’ kwa kuwaondoa barabarani na mitaani watu wote mafukara na wasio na uwezo mkubwa wa kipato. Hawa wote wanakusanywa kwa mamia kila siku na kurundikwa Segerea kwa shtaka moja tu linaloitwa “kesi ya kubughudhi abiria.”
Uwe umekamatwa unakojoa kichochoroni, unauza maji ya Uhai barabarani,machinga wa bidhaa,mpiga debe,unayemsubiri jamaa yako pembeni mwa barabara au kituo cha mabasi Ubungo, uwe ni mama lishe, ni ‘dada poa’ n.k,ukishashindwa kuwakatia elfu kumi au elfu tano jamaa hao wanaoitwa askari wa jiji au walinzi shirikishi, ujue wewe tayari unakwenda Segerea kwa kesi ileile inayoitwa ya ‘kubugudhi abiria’. Wakati huohuo bidhaa zako zote zinakwenda,masufuria na wali wa akina mama lishe unapelekwa kunusuru familia za wasafisha jiji hao,simu na pesa yoyote uliyonayo mfukoni inakwenda;yaani ni kiama! Jamani, waheshimiwa wabunge na madiwani wa jiji la Dar es Salaam hususani wa CHADEMA chukueni hatua za haraka.
Mzee kikwete upo hapo? Unakumbuka ahadi zako za hotuba yako ya kwanza bungeni Dodoma na wakati ulipomaliza ziara yako ya magereza ya Keko na Segerea mwaka 2007? Achana na hayo yote,sasa njoo gerezani upate picha ‘live’.
Nikiwa kwenye selo yangu,kwa bahati nzuri niliruhusiwa kuletewa magazeti na kusikiliza redio . Siku moja wakati nasikiliza kipindi cha Bunge, Naibu waziri wa mambo ya ndani akijibu hoja za wabunge kuhusiana na hotuba ya bajeti yao iliyokuwa imewasilishwa na bosi wake Dr.Nchimbi, nikamsikia akizungumzia swala hilo la upekuzi wa wafungwa na mahabusu kwa utaratibu unaoonekana kumdhalilisha binadamu. Naibu waziri anasema tatizo hilo lipo lakini kutokana na ufinyu wa bajeti hawawezi kununua vifaa vya kisasa vya kufanyia upekuzi. Akasema kutokana na hali hiyo,wataendelea kutumia njia hizohizo za ‘ubunifu’ mpaka hapo serikali ya CCM itakapokusanya mapato yanayokidhi bajeti inayoweza kuvinunua vifaa hivyo.
Wafungwa, mahabusu, baadhi ya watumishi wa gerezani, mapolisi na wengineo wanatoa salamu nyingi sana. Wengi wanaipongeza kazi inayofanywa na CHADEMA ndani na nje ya bunge. Wanasema karibu wote ni CHADEMA japo wengi hawana kadi. Ili upokelewe vyema gerezani lazima uwe ‘vidole viwili’ ukijitia ‘ukada’ utalijua gereza. Wanasema kamwe wabunge wa CHADEMA msitiwe woga na tambo za wabunge wa CCM ndani ya bunge kwa kujiona wako wengi wakifikiria huo wingi upo hata nje ya mjengo. Wanasema katika hilo ‘wamebugi meen!!’. Nje ya Bunge CHADEMA mna mashabiki na wafuasi nyomi!! Yaonekana kwa hivi sasa Bunge ni uwanja wa nyumbani anaoutumia CCM kimchezo na ninyi CHADEMA uwanja wenu uko huku uraiani kwa umma.
Lipigwe jaramba na kuwekwa mpango mahususi utakaowezesha kila aitwaye mtanzania mwenye umri wa kupiga kura apate uhalali wa kupiga kura. Uwekwe mfumo wa kubanana kuhakikisha watu wanajipatia vitambulisho vya uraia wanatunza shahada zao au vitambulisho na wanakwenda kupiga kura. Wanaamini kwa hali ilivyo hivi sasa, ni binadamu ‘asiye majaliwa’ au wale wachache wasiojaa kiganjani waitwao ‘CCM maslahi’ watakaothubutu kuelekeza kura zao kwenye rangi ya kijani- mchicha, kisamvu!
Wamenituma niwaeleze, kwa kipindi kilichobaki, ‘chonde! Chonde! acheni kugombana, kurumbana na kufukuzana. Tumieni kipindi hiki kujenga mshikamano utakaowezesha kukisuka kikosi cha ‘Real Madrid’ au ‘Manchester United’ ya siasa za Tanzania ili uchaguzi ujao CCM walazwe chali-mwanguko wa kifo cha mende! Wanasema CCM ni wepesi kama nyama ya maini, wakibanwa kwenye kumi na nane hawana ujanja wataachia tu , tatu bila!!!
Pili alivyoweza kuwavuta na kuwashawishi waliokuwa mahasimu wake walio muhimu (kama vile Ruto) ambao bila ya kuwa nao asingeweza kufua dafu kwa Odinga. Tatu , namna Kenyatta alivyocheza mchezo wa kisiasa kwa kuzingatia na kutumia kanuni isemayo ‘siasa hazina rafiki wala adui wa kudumu’ bali ni kuangalia nani anawezesha kupenya vikwazo ili kuwezesha kufika salama ninakokwenda (kwa maana ya kuingia Ikulu). Ukishaingia ndani ya mjengo mambo mengine ni akili kichwani, utajua unachemsha vipi kichwa lakini muhimu kuliko yote si tayari umo ndani na unachezea ndani? Wanamuomba Mbowe azidi kuzamisha akilli na kuupanga mchezo kwa “formation” ileile ya Kenyatta, lakini kwa kuongezea na mbinu nyingine zinazozingatia mazingira yanayotunzunguka KICHADEMA.
Milima huwa haikutani lakini binadamu wanakutana. Ndivyo sakata la ugaidi lilivyonifikisha gereza la Segerea na huko nikajikuta nawekwa selo moja na ‘mjukuu wangu’ Issa Ponda mtoto kutoka Kigoma. Issa Ponda ni kiumbe wa mwenyezi Mungu wa aina ya pekee. Kwa nchi za wenzetu zilizoendelea mtu mithiri ya Ponda si mtu wa kuchukulia mzaa kama ninaouona ukichezwa hapa kwetu. Ni mtu ambaye fikra zake, ubunifu alionao kichwani na katika vitendo, hulka zake, nasaha zake, ushawishi wake, ujengaji hoja zake, uchaji wa Mungu wake, uswalihina wake na vingine vingi ni watu wachache sana unaoweza kukutana nao wakiwa navyo vyote kwa mpigo.
Tatizo wakubwa wanamuangalia kwa taswira ya upande mmoja ya kumuona ‘mkorofi, mchochezi’. Sijui na ndio maana nauliza, hivi ni mamlaka gani ya juu na yenye kauli ndani ya nchi hii imewahi kukaa na Ponda kwa karibu katika misingi ya kuheshimiana kwa dhati na kusikilizana ili kujua ana mawazo na mitizamo gani kwa masuala mbalimbali yaliyolalamikiwa na baadhi ya waislamu walio wengi?
Alinielewesha kuwa kwenye dini ya kiislamu mtu anapokuwa amefikia kiwango cha kuitwa U-Ustadhi kwa lugha ya haraka inayoeleweka na wengi ni sawa na U-profesa.Hakika Sheikh Ponda ni ‘profesa’.
Nilipata fursa ya kujadiliana naye pia mambo ya msingi yanayolikabili hivi sasa Taifa letu. Moja wapo ni nguvu nyingi zisizo na sababu zinazotumiwa na polisi kushughulika na watu kama sisi ambao hata rungu hatuna. Nguvu kubwa inayotumika ya kumpeleka Ponda au Lwakatare mahakamani ili kesi itajwe tu na kurudi Segerea kulala ni sawa na kumlipa daktari wa muhimbili mishahara mizuri ya miezi miwili. Magari nane na mapikipiki kujazwa mafuta,ving’ora barabarani,askari polisi zaidi ya hamsini kuvunja shughuli nyinginezo kwa siku nzima, barabara kufungwa na mengine kuzuiwa wakati wa kupita n.k Mikwara yote hiyo ya nini?
Mfungwa mmoja aliyesoma kwa kiwango fulani alipoletwa kulala kwenye selo yetu na kuikuta mada hiyo, alichangia hivi, “kawaida ya mtu yeyote anayelazimisha aonekane mbele ya wakubwa zake kwamba anafanya kazi ni lazima atengeneze mazingira yanayomfanya aonekane kweli anafanya kazi”. Kisha kasema hivi “nyie waheshimiwa ili wale waliowafungulia tuhuma za ugaidi na uchochezi lazima watoe taswira ya nje kwa umma kuonesha kuwa ninyi ni watu hatari sana na mkipewa upenyo wowote mnaweza kusababisha maafa makubwa sana wakati wowote kwa taifa. Kwa ufupi wanataka umma uwahukumu kinadharia kwamba mnahusika na tuhuma mlizoshtakiwa nazo hata kama mahakama haijazipitia tuhuma zenyewe kuona zina uzito gani.”
Jambo jingine lililoangukia katika mijadala yetu ni hii migogoro ya makundi ya kijamii na hata mauaji na maumizano yanayojitokeza mara kwa mara. Sheikh Ponda alitoa changamoto moja muhimu ambayo naona ina mashiko sana. Alisema hivi; huko uswazi (mitaani wanakoishi watu wengi kwa kubanana) ambako nyumba moja wanapanga na kuishi zaidi ya watu hamsini, mchanganyiko wa waislamu kwa wakristo, mbona hakuna ugomvi? Mbona akina mama humo ndani waislamu kwa wakristo wanaachiana watoto kwenda sokoni? Mbona wanaazimana vijiko na masufuria? Mbona wanapeana mboga bila kuulizana? Ponda akatumbukiza na utani pia kuwa “mbona humu selo ukileta chakula alichopika mama Frank siulizi na wala wewe chakula anachoniletea mama Mariam naona unabugia tu bila maswali yoyote?
Na mimi nikamwambia mbona ukiamka saa tisa usiku ukaanza swala zako za sunna mpaka alfajiri wakati wa ‘Azanna’ na kisha swala zote tano za ‘faradhi’ za siku nzima na lakhai zake mbilimbili humu humu ndani ya selo havijaingiliana na ibada zangu za ‘Tumwabudu Mungu wetu?’ Selo yetu ndio msikiti wetu na ndilo kanisa letu. Haya mambo chanzo na chimbuko lake ni nini? Hayawezi kuwa yanatengenezwa na kundi maalum la watu kwa malengo maalum?
Swali hili la mwisho likanikumbusha somo moja tulilowahi kufundishwa kipindi fulani nilipokwenda Ujerumani kwa mafunzo ya ‘Strategic Planning’. Katika kipengele kimojawapo cha mafunzo hayo nakumbuka kuna kitu mwalimu alikiita ‘Power Winning and Maintaining Strategy’, kwa tafsiri nyepesi ‘mkakati wa kuupata utawala na kuulinda’.
Njia nyingine ni ile iliyotumika tangu ukoloni ya ‘watawanye uwatawale’ (Divide and rule policy).
Nilimuuliza endapo hukumu itamuweka katika mazingira ya kumkata makali yake ya kazi ya utetezi anayoifanya na wakati huohuo upande wa pili wa ‘system’ ukamtaka aanze kutoa ‘Ushirikiano’ atafanyaje? Sheikh Ponda aliniambia kuwa haki huwa hainunuliwi wala kuombwa bali hudaiwa. Alisema atakuwa tayari kutoa ushirikiano kwa yeyote yule anayezungumzia utoaji na upatakanaji haki.Na akasema mdomo na nafsi vilivyodhamiria kuzungumzia na kuitafuta haki huwa havifungiki kwani vikifungika hata hiyo amani haiwezi kuwepo.
Lipo jambo moja muhimu ambalo tulikubaliana na Sheikh Ponda tulijadili na kulifanyia kazi kwa nia ya kuwanusuru watu wanaosota jela bila sababu endapo tungeliachiwa na kuwa huru uraiani. Namtafuta kwenye simu hayuko ‘reachable’. Nikishampata tukashauriana na likaonekana linatekelezeka, nitalitoa hadharani.
Mimi ni mtu mdogo sana na muumini wa kawaida ndani ya dhehebu la KKKT. Lakini natambua kanisa ni waumini na wajibu mkubwa wa kila muumini ni kuhakikisha anatimiza wajibu wake kama kanisa la Mungu linavyoelekezwa kupitia maandiko matakatifu ya Biblia. Wajibu mmojawapo sisi kama waumini ni kuonyana ( Ebr. 10:24 – 25).
Lazima mtambue hawa jamaa wakati mwingine huenda wanaitumia fursa hiyo kama chambo cha kuwanasia pindi wanapokua wana taarifa zenu zote za fursa ya misamaha iliyotumika vibaya. “Mnapaswa kushuhudiwa mema na watu walio nje…” (1 Tim 3:2-9)
Lakini zaidi ya yote ni imani yangu mimi binafsi kwamba madhehebu yenu ni makubwa na yana mtandao mkubwa na wenye nguvu ndani na hata nje ya nchi.Kama inawezekana tumieni mtandao wenu kuisaidia serikali ambayo vyombo vyake vinaelekea kushindwa kuwabaini wahalifu wachache wanaoelekea kuchafua na kuivuruga amani tuliyoizoea ndani ya nchi yetu. Kwa bahati nzuri nimesoma na kusikia kwenye vyombo vya habari kwamba IGP Mwema amezishauri taasisi za kidini kuanzisha ‘ulinzi shirikishi ndani ya misikiti na makanisa’. Kama mambo serikali ya CCM imeyafikisha hapo, tumieni fursa hiyo kuziomba taasisi makini mnazozifikia nje na ndani ya nchi.
Nikiwa gerezani Segerea nilimshangaa sana ‘bwana mdogo’ Julius Mtatiro-Naibu Katibu mkuu wa CUF alipozungumza kwenye vyombo vya habari kuwa ;”Lwakatare akiwa CUF hatukumfundisha ugaidi.” Sikumuelewa hayo maneno alikuwa na maana gani na alitumwa na nani. Kwanza sijui kipindi hicho nikiwa CUF yeye alikuwa wapi na sidhani kama kwa wakati huo alifikiria hata kujiunga na hiyo CUF.Awaulize CUF ‘Original’ kama wapo, Lwakatare alikuwa ni nani ndani ya CUF.
Hata siku moja haitatokea nibeze uzoefu na msingi wa kisiasa nilioujenga ndani ya akili zangu na nafsi yangu kutoka CUF. CUF iliniweka katika ramani ya kisiasa ninayoitumia kutamba hadi leo hii. CUF ilinijengea nguzo moja kubwa iliyonipaisha kisiasa na inayoendelea kunisaidia katika kazi niliyokabidhiwa CHADEMA ya ulinzi wa chama hadi leo ambayo ni UJASIRI WA KUJITOA KWA NAFSI YANGU NA KWA AKILI ZANGU ZOTE KUIPIGANIA NA KUITAFUTA HAKI BILA KUCHOKA NA KUTOKUBALI DHULUMA NA UONEVU. ‘HAKI HUWA HULETEWI KWENYE KISAHANI CHA KIKOMBE CHA CHAI, HAKI HUDAIWA NA KUTAFUTWA.’
Wachache wanaojaribu na kuthubutu kujitokeza wanapenda wafanye hivyo kwa kutokea mafichoni. Binafsi nawapongeza angalau hata kwa hilo maana najua ipo siku ambayo haiko mbali, ngoma itakapokolea watajitokeza hadharani kucheza. Kitendo hiki cha kuvishwa tuhuma za ugaidi na kikosi cha Mwigulu na CCM wenzake kilitukatisha sana ‘stimu’ ya kazi nyingi tulizokuwa bado tukizipanga. Kwa wahaya wanasema, “Bampeya ntakamazile…”kwa maana ya kukatishiwa safari kabla ya kufika mwisho wa safari. Makamanda tukaze buti, tushirikiane kwa dhati tusonge mbele mpaka kieleweke, neema inakuja.
“USHINDANI NDANI YA MFUMO KANDAMIZI (SAFARI YANGU KISIASA HADI KUTUHUMIWA KUWA GAIDI ASIYE GAIDI).
Nimeona ni wakati muafaka kwa baadhi ya watu wenye nia nzuri na hata mbaya wasionijua Wilfred Lwakatare ni nani wanijue maana nikiwa gerezani yuko mwandishi mmoja wa gazeti la TAZAMA aliandika makala yenye mtazamo wa kubeza akiuliza, “kwani Lwakatare ni nani?” Maneno yaleyale aliyoyatumia Waziri Steven Wassira kwa mwandishi Absalom Kibanda.
Naamini kazi na uzoefu nilioupitia wa uanafunzi hadi chuo kikuu, uafisa utawala na utumishi serikalini, ujasiliamali, ukulima, ufugaji, uenyekiti wa mtaa Omukituli Kibeta, uenyekiti wa CUF na CHADEMA mkoa, ubunge wa jimbo, ukuu wa upinzani Bungeni,uratibu mkuu wa ushirikiano wa vyama vya CHADEMA, NCCR-Mageuzi, TLP na CUF, unaibu katibu mkuu wa CUF, ukurugenzi wa ulinzi na usalama CHADEMA, ukuu wa familia ya mke na watoto wanne na HATIMAYE kujikuta mahabusu nikituhumiwa kuwa GAIDI ASIYE GAIDI – sio kazi za mchezo. YATAKA MOYO.
Waswahili husema ukishikwa, shikamana. Maana tunakoelekea sio siri CCM wameshashikwa pabaya . CCM hawana namna ya kuyakwepa mabadiliko ya nyakati. Kukunjwa ni kuzuri kuliko kuvunjwa. “If they can’t change, changes will change them.”
Wajiulize wataendelea kuishi maisha ya kila kitu ‘deal’ na uchakachuaji mpaka lini? Hawaoni kuwa ni utumwa wa kujitakia wenyewe? Naona hata baadhi ya hizi kesi zinazofunguliwa ni zenye msukumo wa ‘DEAL’. Wafanyakazi na watendaji ndani ya serikali na taasisi zake nawashauri anzeni kubadilika na kujipanga kifikra tayari kutumika chini ya utawala wa chama chochote. Anzeni kujiunga na chama chenu cha AGIP (Any Government In Power) ambacho sio lazima kisajiliwe wala kutoa kadi.
Kipekee nimshukuru sana Baba Mchungaji wa usharika wetu wa King’ong’o Kimara na mke wake. Mr & Mrs Rev Joseph Kyaka walionitembelea na kunijengea moyo wa imani, matumaini na faraja. Niwashukuru wote waliokuwa pamoja nami kifikra na kimaombi na ninasema kwa maombi yenu, yote yamewezekana. Mungu anasikiliza maombi na haachi kujibu.
Posted by Baraka Mfunguo at Friday, June 14, 2013
| 2018-05-20T21:24:48 |
http://mtwarakumekucha.blogspot.com/2013/06/mrejesho-wa-kamanda-wilfred-lwakatare.html
|
[
-1
] |
Anitha's Closet: My heart on my skirt...
My heart on my skirt...
Hello everyone! Two post in one week yeey! I do believe we are getting back to normal!! I can't whine enough about how hard it is to dress up now, I find myself looking for maxi everything because I just don't think anything else will look good, how terribly basic!!
But I strongly believe you can look good no matter what size you are or shape, you just have to find what works for you which is what am currently doing while I work on loosing this weight slowly and in a healthy. Maxis may be basic but they are comfortable, they don't hug you in any unflattering way and when worn and accessorized right, can be casual or dressy depending on the occasion. I found this beautiful kitenge at Mnazi mmoja last year while looking for my kitchen party sare, had it made into this free size maxi skirt with an elastic waist band so that even when I loose weight I can still wear it without having to alter it...I'm going to be making more of these for sale later on so watch this space!
Check out my receding hair line! all braiding I did while I was pregnant did a good of a job in growing out my hair, it's really long now, but the braids were done so tightly, each time and each repair was taking a little bit of the weaker hair on my hairline...it's time to get a weave on and grow it out before my next re-touch. I'm wearing: African print skirt ~ AnithasCloset, Black Tshirt ~ Bongoshopaholic, Black Blazer ~ Random brand, Box Clutch ~ Thrifted, Heels ~ Kelsi Dagger from Viatuzi, Earrings ~ kkoo
postmaternityfashion
Umependeza sana!nimependa hicho cha kichwan nakitaka Anitha
Anitha kwa kweli nimefurahi sana kurudi tena na umependeza sana. Mi ni mmoja wa wapenzi wa blog yako na nakupenda yaani una busara unavyojibu na kuelezea mambo unayopost. Kwa kweli ni mfano kwa blog zingine za wanawake . nakutakia afya na baraka tele ktk familia yako na lolote mnalololifanya na endelea kutuelimisha.
Napenda sketi yako sana. Yaani unawakalisha Uafrika wako kwenye hiyo sketi hadi raha.
rahaa zenji
Tatizo blog ya kuswahili sasa hizi English za nini jamani?
Asante...i will do a tutorial
Awwww asante sana...nakuwa encouraged nikisoma comments kama zako.
Asante Amor...
Dear rahaa zenji...blog yangu ni ya kuhusu fashion...na wasomaji wangu ni kutoka nchi mbali mbali na lugha mbali mbali...english inawaunganisha wote...
Hi Anitha, I just want to say that you are so so beautiful. Please dont be too hard on your body. You just had a baby-a freaking amazing miracle that grew inside of you.Cheers, congratulations and I hope you get back your pre-baby body or whatever weight goals you have are able to achieve.
brown-candy
Hie.. following your blog and loving it so far. It's quite tricky to find fellow Tanzanians that are blogging in English. I love your whole outfit and your make up so natural looking. Very beautiful. Do post more often :) congrats on the baby and kindly follow back www.brown-candy.blogspot.comxxx
u look insanely beautiful and i love ur hair ban ,hiyo make iz on pointwww.middysfashionsite.blogspot.com
love ur skirt dear and the make up is on point umejipaka mwenyewe?love ur hair toowww.middysfashionsite.blogspot.com
Hongera sana Anitha, nimefurahi kukuona umerudi na afya tele baby mzuri kafanana na baba yake,dada wa baby furaha tupu na Mr wako ndio furaha kabisa familia inazidi kukua,hongera sana mamy, mimi ni mdau wako mbeba box nilikua nakusubiri urudi kwa hamu zote, nina swali kuhusu zile nywele ulisukia siku ya harusi yako, zinasukwaje? naomba utuambie tumejaribu kuuliza wasusi wa huku wote hawaelewi pale chini mnaunga vipi? huyo mmoja alijaribu na rubber bend haikuwezekana nywele zinapatikana huku, nimeshatembea na picha yako kwenye simu yangu kila msusi namuonyesha sijapata mafanikio,please please naomba msaada wako May 16, 2014 at 12:26 AM
Thank you so much...i love ur blog!
Thanks Middy love...i do my own makeup love...thanks to youtube am learning some tricks
Thank you dear...omg rubber band hehehehe pole mwaya...zile nywele hazisukwi zinafungwa na some special elastic uzi nadhani saloon mbili tu zinasuka hivyo dar...mimi nilisuka Million hair saloon mikocheni kwa nyerere iko pembeni ya billionares club nimepoteza number yao ya simu ila huwezi kupotea wako barabarani kabisa wanasuka kuanzia laki moja kuendelea mbele inategemea na size unayotaka...
Anitha nashukuru kwa majibu ya nywele, huo uzi wa lastic ngoja nitautafute sijui nitaupata duka la uzi, natamani ungeujua huo lastic uzi,na jinsi unavyofungwa nitakupa update huku ughaibuni kusuka nywele ni tabu
Ohhh pole nilidhani uko tz...hiyo style inaitwa brazilian knots...angalia youtube kuna videos ya jinsi zinavyotengenezwa na uzi maybe inaweza order from ebay....pia labda ugoogle mtu anayeweza fanya brazilian knots in ur area...kama uko Uk then waportugese ndo wanafanya hiyo
Albaloving
Ulitumia extensions gani na ni bei gani?
Hello Alba...sijaweka extensions hapo kwenye post hiyo hapo juu ni nywele zangu nimezungushia tu hiyo braid ya rasta...ila if ur asking about hilo swali lililopita kuhusu brazilian knots nilitumia virgin peruvian hair kutoka kwa bongobeautyfix
You hair is gorgeous and the outfit is beautiful love your blogwww.fabulously-pink.blogspot.com
jamani anita huko wapi?????mimi nikomajuu.siwezagi kulala mpaka nikusome. napendaga sana blog yako. ARE YOU OKAY!!!!!HABARI YA BWANA NA WATOTO
| 2017-02-27T22:46:53 |
http://anithascloset.blogspot.com/2014/05/my-heart-on-my-skirt.html
|
[
-1
] |
Binafsi | Media Ownership Monitor
This is an automatically generated PDF version of the online resource tanzania.mom-rsf.org/en/ retrieved on 2019/11/15 at 13:25
Kanzi data ya Binafsi
Mambo mawili yanafurahisha sana unapoangalia wamiliki wa hisa mmoja mmoja, waasisi, mameneja wa vyombo vya habari; Wakati Watanzania matajiri wanawakilishwa zaidi, idadi ya wamiliki wanawake na mameneja wa vyombo vya habari ni takriban sifuri.
Wamiliki wa vyombo vya habari Tanzania wanabiashara nyingine nyingi
Hazinadata ya wamiliki inaonesha wamiliki watatu ambao pia wametokea kwenye orodha ya “The Forbes Top 5 of richest Tanzanians:
Rostam Aziz – bilionea wa kwanza kutoka Tanzania mwenye biashara za Kampuni za simu, Uchimbaji madini na usafirishaji kwa meli. Bado ana hisa Vodacom Tanzania na anahusika na New Habari (2006). Aliwahi kuchaguliwa mbunge mwaka 1993 na kuwa mbunge vipindi viwili. Aliacha siasa mwaka 2011 kuzingatia biashara.
Said Salim Bakhresa – ni milionea aliyejitengeneza kwa kuanzisha kampuni ya kutengeneza nafaka na utengenezaji vyakula, ameunda umaarufu wa Bakharesa Group. Alizindua Azam TV na huduma za kulipia TV, Afrika Mashariki. Hivi sasa Bakharesa Group ni miongoni mwa mkusanyiko mkubwa wa kampuni, Afrika Mashariki, anayeajiri zaidi ya wafanyakazi 5000 na uzalishaji wa vyakula na vinywaji baridi, ufungashaji, huduma za boti za usafiri na biashara ya mafuta.
Dr. Reginald Mengi – alikuwa mhasibu ambaye ameanzisha na sasa ni mwenyekiti wa IPP Group inaendesha magazeti 10 ya kitaifa na vituo 2 maarufi vya Televisheni Afrika Mashariki (EATV na ITV), na kiasi cha vituo 10 vya redio. Biashara zake pia zinajumuisha utiaji vinywaji kwenye chupa na uchimbaji dhahabu.
Utajiri unaohusiana na umiliki wa vyombo vya habari si lazima uwe ni tatizo. Hata hivyo kuna hatari kwamba wamiliki wa vyombo vya habari wenye ajenda za biashara wanaweza kutumia vibaya chaneli zao kwa lengo la kukuza na kuwezesha kampuni nyingine kwa kisingizio cha maudhui yanayofaa kwa jamii.
Jinsia na Vyombo vya Habari – a mada iliyopuuzwa kisiasa
Utafiti unaunga mkono jamii ya kiraia kile ambacho imekuwa ikilalamikia kwa muda mrefu: wamiliki hisa wanawake wa vyombo vya habari na mameneja hawawakilishwi vyakutosha:
Kwa mwanamke mmoja mwenye hisa nyingi – Dkt. Lilian Mtei mwenye hisa 75% kwenye Freeman Media. Anafanyakazi ya udaktari na mke wa Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe.
Kuna wamiliki sita wa hisa chache. Watano kati yao wanahusiana na JosephKusaga: Judith Violet Kusaga, Sheba Martha Kusaga, Joyce Alex Kusaga, Alex Justine Kusaga, Prisca Mkama Kusaga ambao wote wana hisa chache kwenye Clouds Entertainment. Justina Antoine Ciza ni mmiliki mwenza wa E-FM Company Limited.
Data zilizopo haziruhusu matamko yenye uhakika kuhusu uwiano wa mwanamke kwa mwanaume kwa wajumbe wa bodi au hata maripota wenye uwiano wa wanaume kwa mwanamke kwenye vyumba vya habari. Hii inahitaji utafiti zaidi na uwazi kwa vyombo vya habari kusaidia utafiti wa aina hiyo. Data zilizopo hata hivyo zinaonesha hatua inahitajika kuchukuliwa kubadili hali hiyo. Mpaka sasa, utashi wa kisiasa bado ni mdogo. MCT pamoja na wadau wengine wa vyombo vya habari wamependekeza hatua ya sera kuhusu usawa wa jinsia kwenye vyombo vya habari tangu 2001. Ilikuwa miongoni mwa mapendekezo 18 – na moja kati ya matatu tu, ambayo watayarisha sera hawakuyachukua. Inaelekea mpaka sasa kuna hali ya kutokuwa tayari kushughulikia suala hilo.
| 2019-11-15T12:25:23 |
http://tanzania.mom-rsf.org/sw/mmiliki/binafsi/
|
[
-1
] |
MARUFUKU KULIMA, KUINGIZA MIFUGO NDANI YA VYANZO VYA MAJI-MAJALIWA. | LIBENEKE LA KASKAZINI
Home / Habari / MATUKIO / MARUFUKU KULIMA, KUINGIZA MIFUGO NDANI YA VYANZO VYA MAJI-MAJALIWA.
MARUFUKU KULIMA, KUINGIZA MIFUGO NDANI YA VYANZO VYA MAJI-MAJALIWA.
Woinde Shizza Thursday, January 19, 2017 Habari , MATUKIO
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akisalimiana na Mkurugenzi wa Kampuni ia SAS, Bw. Salim Abri wakati alipokwenda kwenye shamba la ng'ombe la ASAS lililoko nje kidogo ya mji wa Iringa Januari 19, 2017. (Picha na Ofisi ua Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama ukamuaji ng'ombe wa maziwa katika shamba la Ng'ombe la ASAS nje kidogo ya mji wa Iringa Januari 19, 2017. Wapili kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wakurugenzi wa kampuni ya ASAS baada ya kutembelea shamba la ng'ombe la ASAS nje kidogo ya mji wa Iringa Januari 19, 2017. Kulia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wakuu wa mikoa ya Singida, Mbeya, Iringa na Dodoma wawasimamie wananchi wao na kuhakikisha hakuna shughuli za kibinadamu zinazofanyika ndani ya vyanzo vya maji.
Ametoa kauli hiyo leo (Alhamisi, Januari 19, 2017) alipozungumza na watumishi wa kituo cha kuzalisha umeme cha Mtera alipotembelea bwawa la Mtera akiwa njiani kwenda mkoani Njombe kwa ziara yake ya kikazi.
Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo baada ya Kaimu Meneja wa Kituo cha kuzalishia umeme cha Mtera, Mhandisi Edmund Seif kutaja baadhi ya changamoto zinazokikabili kituo hicho kuwa ni pamoja na kuongezeka kwa shughuli za kibinadamu ndani ya vyanzo vya maji.
Kufuatia hali hiyo Waziri Mkuu ameagiza vifanyike kwa vikao vya ujirani mwema ili wananchi waelimishwe umuhimu wa kutunza vyanzo vya maji na ni marufuku kuendesha shughuli za kibinadamu ndani ya kilomita 60 kutoka kwenye chanzo.
"Marufuku wafugaji kuingiza ng'ombe ndani ya vyanzo vya maji na badala yake utafutwe utaratibu wa kuwachimbia mabwawa pembeni. Pia wakulima nao wazuiwe kulima ndani ya vyanzo vya maji. Lazima tushirikiane kulinda vyanzo vyetu," amesema.
Awali, Mhandisi Seif alisema kituo hicho cha Mtera kinazalisha megawati 80 kwa siku ambazo zinaingizwa kwenye gridi ya Taifa. Alisema bwawa hili kwa sasa lina maji ya kutosha kuzalisha umeme hadi msimu ujao wa mvua.
Mhandisi hiyo alisema bwawa hilo linategemea kupata maji kutoka mto Ruaha Mkuu, mto Ruaha Mdogo na Vyanzo vyote hivyo vinaathiriwa na shughuli za kibidamu ambapo watu wanalima na kuingiza mifugo.
Baada ya kutoka kituoni hapo Waziri Mkuu alitembelea shamba la Igingilanyi ambalo ni moja kati ya mashamba matatu ya kufugia ng’ombe yanayomilikiwa na kiwanda cha kuzalisha bidhaa za maziwa ya Asas kilichoko mkoani Iringa.
Akiwa shambani hapo Waziri Mkuu aliwaagiza wakurugenzi wa halmashauri zote nchini kuhakikisha wanasimamia vizuri mgawanyo wa ardhi ndani ya halmashauri zao pamoja na kusimamia mipaka kati ya wilaya na wilaya.
“Wekeni mipango bora ya matumizi ya ardhi. Pimeni ardhi na mgawe hati ili kumaliza migogoro ya ardhi hata kwa waliopewa mashamba makubwa nao wapimiwe na ardhi yao na wapewe hati kwa mujibu wa muda uliowekwa kisheria,” amesema.
Pia aliwataka Maofisa Mifugo kuongeza kasi ya kutambua mifugo iliyoko kwenye maeneo yao na kuiwekea alama ili kuzuia uhamiaji holela wa mifugo kwa lengo la kuzuia migogoro kati ya wafugaji na wakulima.
Kwa upande wake mmoja wa Wakurugenzi wa kiwanda cha Asas, Bw. Fuad Abri alisema kiwanda hicho kina mashamba matatu yenye jumla ya ekari 2,000 na ng’ombe 1,010 kati ya hao 350 hukamuliwa maziwa na kutoa wastani wa lita 5,000 kwa siku.
Alisema katika mashamba hayo wameajiri wafanyakazi 175 na wamefanikiwa kutumia njia ya uhamilishaji (Artificial Insemination) katika mashamba yote na njia hiyo inawasaidia kuchagua jinsia ya ng’ombe wanayohitaji.
ALHAMIS, JANUARI 19, 2017.
| 2018-06-19T06:15:49 |
https://woindeshizza.blogspot.com/2017/01/marufuku-kulima-kuingiza-mifugo-ndani.html
|
[
-1
] |
dhana wanakabiliwa plywood - Uchina Weifang Joy Sea Trade
HPL / High taabu laminate karatasi
Melamine wanakabiliwa chipboard
High Gloss UV MDF Karatasi
dhana wanakabiliwa plywood
1. Samani: sahani samani, sebuleni samani, chumba cha kulala samani, utafiti samani, samani za watoto, samani jikoni
2. Meza na viti: dawati, meza ya mwanafunzi na viti, madawati, dawati, dawati, meza ya mkutano, kompyuta dawati
3. Mapambo makundi : mapambo ya ndani, mambo ya ndani murals, picha muafaka, sanaa picha, mazingira mapambo uchoraji
4. makundi ofisi: meza wafanyakazi, kabati za kompyuta, dawati mbele, kampuni ya ndani mabango
5. Movable milango: gorofa mlango, compartment bodi
6. makundi zingine: maonyesho samani, ununuzi counter samani, maduka makubwa partitions, kazi za mikono
utengenezaji Weifang Joysea Kimataifa Co, Ltd
bidhaa Fancy veneer plywood
unene 2-30mm
kuvumiliana +/- 0.3mm
nyenzo kuu poplar, WBP gundi
Formaldehyde kutolewa kiwango E0, E1, E2
Cheti ISO9001, ISO14001, Marekani CARB
malipo TT, L / C saa mbele, kwa mteja mara kwa mara, tuna suala bora ya malipo.
Plywood imekuwa moja ya kutambuliwa na kuaminiwa mbao za ujenzi kwa miaka mingi. Viwandani kutoka karatasi nyembamba ya veneer kuvuka laminated na Bonded chini ya joto na shinikizo na adhesives nguvu, plywood paneli na mkuu dimensional utulivu na bora nguvu-kwa-uzito uwiano na ni sugu sana kwa athari, kemikali, na mabadiliko katika hali ya joto ya mazingira na unyevu .
1.Your uchunguzi kuhusiana na bidhaa zetu na bei itakuwa alijibu ndani 24hours.
2. Free sampuli zinapatikana.
3. Naam mafunzo & uzoefu wafanyakazi ni kujibu inquires yako yote kwa Kiingereza bila shaka.
4.Detailed udhibiti wa ubora mfumo.
5. Kufanya cheti kibali desturi kwa mujibu wa mahitaji ya mteja.
6.Provide sekta bidhaa mwenendo kwa bure, kupendekeza bidhaa na ufumbuzi kulingana na hali ya wateja halisi.
7. Kutoa bure utangazaji vifaa kwa ajili ya biashara ya uchapishaji ya wateja na vyeo.
8 .. Biashara yako na uhusiano na sisi itakuwa siri kwa chama chochote cha tatu.
9. Habari za baada ya kuuza huduma zinazotolewa, tafadhali kupata nyuma ukienda swali.
10.We kutoa huduma bure katika China kwa wateja wa muda mrefu, kama vile hoteli booking, miongozo, msaada wa kununua, kuangalia habari zingine za kampuni, na kutafuta wauzaji ubora wa bidhaa nyingine.
1, MOQ yako ni ipi?
MOQ yetu ni kawaida 20ft chombo au chombo 40ft
2, ni wakati wa kujifungua wako?
Wakati wa kujifungua ni kawaida ndani ya 15days baada ya kupokea amana yako.
3, Wateja kubuni na alama ya inapatikana?
Ndiyo, mteja kubuni na alama ni kuwakaribisha na inapatikana.
4, ni bidhaa yako kuu ni nini?
Bidhaa zetu kuu ni Pine Plywood / Pine LVL / Melamine Bodi kwa vifaa msingi E0, E1, E2 / MDF / Chembe Board / Block Bodi / HPL Laminate Paneli / Veneer Paneli na High Glossy Paneli Acrylic / Waterproof Bodi / Anti-moto Bodi / Polyester resini wanakabiliwa bodi / karatasi akazifunika hizo mbao na kadhalika.
5, Je sampuli za kutosha?
Ndiyo, sampuli ni bure na mizigo malipo itakuwa zilizokusanywa katika upande wako. Na baada ya amri kuthibitishwa, chaja hii inaweza kuondolewa kwenye na malipo yote.
wasiliana nasi: Simu: 0086-536-5605673; mail: [email protected]; Simu: 0086-13395366556
Awali: plywood kibiashara
Next: HPL Laminated Plywood kwa Marekani / 1220x2440mm Formica HPL Laminate Sheets
Anti-kuingizwa filamu wanakabiliwa plywood
Black Film Wanakabiliwa plywood
Brown Film Wanakabiliwa plywood
Baraza la Mawaziri Daraja Plywood
bei nafuu Plywood
Zege Formwork Film Wanakabiliwa plywood
Ujenzi Marine Plywood
Exterior daraja la Plywood
Fancy Wanakabiliwa plywood
Film Wanakabiliwa plywood 18mm
Samani Plywood
Hpl Mapambo Laminates Plywood
Marine Daraja Plywood
Melamine Wanakabiliwa plywood
mchanganyiko Core Plywood
plastiki coated Plywood
Plywood Gharama
Plywood sakafu
Plywood Kwa Construction
Plywood Kwa Samani
Plywood Kwa Sale
Plywood daraja
Plywood Jopo
Plywood Bei
Plywood Karatasi ukubwa
Plywood Unene
Red Film Wanakabiliwa plywood
Aina ya Plywood
Asili Veneer
| 2020-05-28T16:18:59 |
http://www.joyseaplywood.com/sw/fancy-faced-plywood.html
|
[
-1
] |
Tuwaambie – Page 2 – News and Feeds
Tuwaambie Feeds PENSIONERS’ PAYMENT PROVOKED!
HILI NALO JIPU. Whether in monthly or other mode, Pensioners’ payment is of no sticky schedule, no specified paydate, thus not relied at … Continue reading PENSIONERS’ PAYMENT PROVOKED!
Feeds News and Views Continue reading Feeds HISIA ZA KISAIKOLOJIA KATIKA NDOA Wanandoa wengi hujikuta wameingia katika migogoro ya KIMAHUSIANO ambayo sababu kubwa kuliko zote ni MICHEPUKO, michepuko inayosababishwa na MIGOGORO ambayo … Continue reading HISIA ZA KISAIKOLOJIA KATIKA NDOA
Feeds MTENDAJI WA MTAA WA TAMBUKARELI-SHINYANGA ATUMIA VIBAYA AGIZO LA KUFANYA KAZI Katika hali isiyo kuwa ya kawaida Mtendaji wa Mtaa wa Tambukareli anaonekana kushindwa kutafsiri maagizo ya Serikali kuhusu Watanzania kufanya … Continue reading MTENDAJI WA MTAA WA TAMBUKARELI-SHINYANGA ATUMIA VIBAYA AGIZO LA KUFANYA KAZI
Feeds TUKIO LA NDOA NI KITU CHEMA Pichani ni ndugu wa familia ya Renatus Paul Wamba wa Nhelegani_SHY(M) na familia ya Late Stephen Nsolo ya Lubaga_SHY(M) katika … Continue reading TUKIO LA NDOA NI KITU CHEMA
Feeds KWA HILI LA TV LIVE WAKATI WA KAZI, … Kwa madhumuni ya TV kuonyesha live mjadala Bungeni, kauli "…. ni kuwanyima wananchi haki ya msingi …" imetumika kueleza kundi … Continue reading KWA HILI LA TV LIVE WAKATI WA KAZI, …
Feeds HOJA YA KIZUSHI Anaweza kuwa MKARIMU, MZURI kwa maana ya wazuri, MTENDAJI na mcheshi LAKINI akawa na TABIA MBAYA! “Tabia mbaya” hapa limetumikaje? … Continue reading HOJA YA KIZUSHI
Feeds HUMU HUMU SHINYANGA, HILI UNALIJUA? Hivi ndivyo ilivyo! Continue reading HUMU HUMU SHINYANGA, HILI UNALIJUA?
Feeds IT’S A RAINY DAY! After several draughty weeks in Shinyanga and neighbouring areas, rain resumed today dropping a fair charge from at least 2340hrs … Continue reading IT’S A RAINY DAY!
Feeds OCTOBER 28, 2015 KATIKA HISTORIA. http://goo.gl/0qFfkJ Tarehe 28-10-2015 itakumbukwa katika Siasa za Tanzania kuwa ni siku ya KITUKO na TUKIO la Kufutwa kwa Matokeo ya Hesabu … Continue reading OCTOBER 28, 2015 KATIKA HISTORIA. http://goo.gl/0qFfkJ
Feeds KUMBUKUMBU Leo ni mwaka mmoja tangu ututoke Mpendwa wetu Stephen Mateo Nsolo, Tulikupenda lakini Mungu alikupenda zaidi, Mapenzi yake yatimizwe. Mungu … Continue reading KUMBUKUMBU
Feeds KAULI HIZI, KWA WAKATI NA WATU TOFAUTI ZILITOLEWA NA NANI? Kauli hizi ni za KUKUMBUKWA na zina wenyewe, wataje! (1). “—, utapigwa tu”! (2). “Safari ya matumaini” (3). “— ushindi … Continue reading KAULI HIZI, KWA WAKATI NA WATU TOFAUTI ZILITOLEWA NA NANI?
Feeds UTUMBUAJI MAJIPU, KAULI MBIU HADI KWENYE NDOA! Katika Serikali ya Dr. J. P. Magufuli ie Serikali ya JMT Awamu ya Tano, Kauli KUTUMBUA MAJIPU imebeba Dhana ya … Continue reading UTUMBUAJI MAJIPU, KAULI MBIU
HADI KWENYE NDOA!
Feeds NILICHOJIFUNZA SAFARINI: MAWAKALA WA MABASI HUWAPANDISHIA NAULI ABIRIA! Kila kituo cha Mabasi kina Mawakala wa Mabasi ambao ndio wanaotoa tiketi za safari na kutafuta abiria, hawa ndio walioitwa … Continue reading NILICHOJIFUNZA SAFARINI: MAWAKALA WA MABASI HUWAPANDISHIA NAULI ABIRIA!
Feeds A DIALOGUE OF THE INNOCENT BOY! A boy got cramped by a thirsty prostitute: -Prost.: hey boy, come make use of me! -Boy: No thanks, I … Continue reading A DIALOGUE OF THE INNOCENT BOY!
Feeds MATAMKO@MATAMKO NI MATAKWA YA WANANCHI AU KIKUNDI TU? Sasa watu wataanza kuelewa cha KIELEWEKE kinachoendelea: -UKAWA walipiga kelele, kutangaza na kutoa TAMKO kuwa Edward Lowasa ni Fisadi, wakaeleweka. … Continue reading MATAMKO@MATAMKO NI MATAKWA YA WANANCHI AU KIKUNDI TU?
Feeds SIKU ZA KUELEKEA SIKUKUU, NI ….! Tukiwa katika msimu wa siku za kuelekea Siku kuu za Noeli na mwaka mpya 2016, kunakuwepo na changamoto kwa Wananchi … Continue reading SIKU ZA KUELEKEA SIKUKUU, NI ….!
Feeds YAHUSU KUPOTEA KWA VITAMBULISHO Mwalimu Venance Maziku Stephen wa Shule ya Msingi UJAMAA katika Manispaa ya Shinyanga, anatangaza kupoteza vitambulisho vyake vyote kama ifuatavyo: … Continue reading YAHUSU KUPOTEA KWA VITAMBULISHO
Feeds DHANA YA UPINZANI:
MH. ZITTO KABWE AWEZA KUWA MFANO MZURI! Katika hoja na dhana nzima ya Upinzani, Mh. Zitto Kabwe (MB), anaonesha mitazamo_jenzi ambayo ni endelevu kwa maslahi ya Wananchi: … Continue reading DHANA YA UPINZANI:
Feeds WAZO LANGU LEO Wazo langu liko katika |Wimbo ulio Bora 1:5-6| http://goo.gl/njFZA6 Continue reading WAZO LANGU LEO
Feeds UGOMBEA KWA MKOPO-UKAWA|CCM KUUNGANA TENA? Kuna kila dalili za UKAWA na CCM kuungana katika kuweka Mgombea wa Kiti cha Urais kwa tiketi ya UKAWA. Ukweli … Continue reading UGOMBEA KWA MKOPO-UKAWA|CCM KUUNGANA TENA?
Feeds R. I. P. PAUL MHOJA Leo ni miaka miwili kamili tangu ututoke Duniani, Mungu Baba Mwenyezi akupe pumziko la Amani, milele, AMINA! Continue reading R. I. P. PAUL MHOJA
Feeds UJUMBE WA LEO-JUMAPILI 14-06-2015 “Wapenzi, na mpendane; kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu”. goo.gl/puxMrG JUMAPILI … Continue reading UJUMBE WA LEO-JUMAPILI 14-06-2015
| 2017-06-23T08:42:56 |
https://nsolo14stif.wordpress.com/page/2/
|
[
-1
] |
MAKAMU WA RAIS AZINDUA URITHI FESTIVAL - Mwanaharakati Mzalendo | PressTZ - Your Number 1 Source of Aggregated Online Content
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikata utepe kama ishara ya kuzindua rasmi Tamasha la Urithi (Urithi Festival) katika uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma. Mtoto wa Shaaban Robert, Mzee Ikbali Robert akionyesha Tuzo ya Nguli wa Lugha ya Kiswahili katika Uandishi ya Urithi Festival ya mwaka 2018 aliyokabidhiwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ikiwa ishara ya kutambua mchango mkubwa wa Baba yake Mzee Shaaban Robert. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Tuzo ya Nguli wa Sanaa za Ngoma ya Urithi Festival mwaka 2018 Mjukuu wa Mzee Morris Nyunyusa kama ishara ya kutambua mchango wake mkubwa katika kutunza na kudumisha utamaduni. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais) Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiangalia moja ya bidhaa zilizotengenezwa kwa mikono na kikundi ch... Continue reading ->
| 2019-01-22T18:43:42 |
http://presstz.net/makamu-wa-rais-azindua-urithi-festival-41344333
|
[
-1
] |
WAFUASI WA CHADEMA WALIOKAMATWA MSIBANI WAFIKISHWA MAHAKAMANI | MALUNDE 1 BLOG
Home » siasa » WAFUASI WA CHADEMA WALIOKAMATWA MSIBANI WAFIKISHWA MAHAKAMANI
WAFUASI WA CHADEMA WALIOKAMATWA MSIBANI WAFIKISHWA MAHAKAMANI
Wafuasi zaidi ya 10 wa Chadema waliokamatwa wakiwa nyumbani kwa mwanachama mwenzao kuhani msiba wanatarajiwa kupandishwa kizimbani muda mfupi ujao.
Watu hao, leo Machi 14, 2018 tayari wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mwanza na kuwekwa katika mahabusu mahakamani hapo kusubiri kukamilika kwa taratibu za kimahakama ili wasomewe mashtaka dhidi yao.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi watu hao walikamatwa eneo la Mabatini Machi 13, 20018 baada ya kutokea kutoelewana kati yao na askari polisi.
Amesema askari hao walikuwa wakifuatilia nyendo za wafuasi hao tangu walipokuwa wakikusanyika kutoka sehemu mbalimbali za Jiji la Mwanza kwenda nyumbani kwa wanachama mwenzao kwa kile kinachodaiwa ni kuhani msiba.
Katika tukio hilo, polisi walilazimika kutumia mabomu ya kutoa machozi kutawanya kundi la watu zaidi ya 500 waliokuwa kwenye eneo hilo.
| 2020-02-17T03:04:52 |
https://www.malunde.com/2018/03/wafuasi-wa-chadema-waliokamatwa-msibani.html
|
[
-1
] |
HADITHI: RIWAYA: WASALIMIE KUZIMU========4
SEHEMU YA NNE Saadan akamtazama Nasra na kuyafikia majibu yake, zilikuwa hoja za uhakika ambazo zingemgharimu muda mwingi kuziweka sawa ili kuondoa mashaka kwa Nasra, akajikuta akishusha pumzi za kukata tamaa na kusema. “Sasa unataka kuniambia nini? Kwamba hunipendi na hutaki kuolewa na mimi?”
Ikawa zamu ya Nasra kumtazama Saadan kwa muda kabla hajayarudisha macho
chini, kwa ujumla Saadan alikuwa amekata tamaa. Akaachia tabasamu dogo na kumuonea huruma. “Sikiliza Saadan! Nikikwambia nakupenda, upendo kama huo ulionao wewe kwangu ninakuongopea! Baba wa watoto hawa ndiye haswa aliyeushika moyo wangu. Hata hivyo juhudi zako zimenifanya nigundue ni namna gani unavyonipenda. Na wanadiplomasia, wanasaikolojia na hata wanaaikolojia wote wanakubali kwamba ni vizuri zaidi ukaishi na mtu anayekupenda sana kuliko wewe unavyompenda! Kwa
kuzingatia usemi huu na sababu nilizokueleza hapo nyuma, sioni kwa nini
nikukatishe tamaa huenda nikakubali unioe, lakini kwanza unifanyie yafuatayo:- “Kwanza nataka kuja Oman kama mtalii ili wazazi na ndugu
zako wanione na pia unitambulishe kwao nione watanipokea vipi. Na labda
ikiwezekana niishi nao kwa muda fulani nione tabia zao, waone tabia zangu. Baadae nafikiri nitakuwa nimeshajua nifanye nini!” “That is good. Very good Nasra!” Saadan akishangilia. Nasra akamuonea huruma moyoni na kuendelea “Kwa sasa ningekushauri urudi Oman ukaendelee na shughuli zako. Acha umenikatia Pasport yangu na za wanangu pamoja na nauli sawa Saadan?” Furaha ya Saadan ikazimika. “kwa nini tusiondoke wote Nasra?”
“We nenda tu, watoto wangu bado wanahitaji matunzo na wangalizi wa karibu. Sio busara kuwaanzisha mikimiki ya safari kwa sasa!” Saadan akaelewa. “Sasa utakuja lini?” “Munkari wa nini? Mawasiliano yapo, hali itakapokuwa shwari nitakufahamisha tu. Muhimu shughulikia Passport kwanza!” “Nitashughulikia!” Saadan akasema akiwa ameridhika na kuongeza “Naomba uniruhusu nikuage kwa kukumbatia na kukubusu?” Nasra akatabasamu na kuinua uso. “Tuliza boli Saadan! Mambo yakiwa sawa, tutakuwa na karibuni robo karne
ya kuishi pamoja! Katika kipindi chote hicho utanikumbatia, kunibusu na
kukuruka nami tani yako!! Kwa sasa nione huruma, kumbuka mimi ni mzazi.
“Usijali Nasra!” Saadan akainuka na kuaga kabla hajaondoka, moyo na mwili ukiwa na furaha ambayo hakuwahi kuwa nayo kabla. Akamuaga pia mama
Nasra alieyekuwa akimalizia kufua na kuondoka. Mama Nasra akarudi wodini hima akiwa na mshawasha wa kutaka kujua kilichoongelewa. Akamuuliza Nasra juu juu hata kabla hajakaa chini. “Ah! Nimeamua kumtosa tu ili arudi kwao salama. Vinginevyo angerudi ndani ya sanduku!” Nasra akamwambia. “Una maana gani?” akauliza. Nasra akamsimulia kila kitu.
“Lakini hukufanya vizuri mwanagu kwa nini usimkatalie moja kwa moja ili
akatafute Mwarabu mwenzake huko kwao? Unajua kama ni dhambi kumpa mtu matumaini ambayo hayapo? “Dhamira mama! Ilinisuta. Alitaka kulia, tayari alishalengwa na machozi. Halafu vile alivyonisaidia pale ukumbini
na fedha anazolipa hapa hospitali vimenifanya nisifanye hivyo!” “Vizuri nilidhani utakaosa utu na kusahau fadhila. Sasa vipi utakwenda Oman? Manake ni lazima tu ataleta Passport kwani mie tayari ameniuliza juu ya cheti chako cha kuzaliwa!” “Nitakwenda mama! Hii itakuwa ni fursa nyingine nzuri ya kwenda kutalii. Sikuwahi kufikiria kama nitakuja
kufika Sultanate! Imetokea wacha niende, nitakwenda!” “Angalia isije ikawa ile hadithi ya mwonja aslali…” Akatania “Never mama!” Nasra akakataa kwa dhati “Haiwezi kutokea kwangu!” wakacheka kwa bashasha na kufurahi pamoja!
Jioni ya siku hiyo mama Nasra alikwenda kwake alikokutana na Alwatan Dafu. Akajua akianzisha madahalo hapo hawataelewana akajiandaa kwa mechi
na kumwita ndani. Dafu alipofika ndani, akakuta hali imebadilika mazingira yakamlazimisha afike kifuani kwa mkewe chezo la nguvu lakini la taratibu likaanza kuchezwa. Lilikuwa chezo la kiutu uzima! Hapo ndipo mama Nasra alipopata nafasi ya kumlaumu mumewe kwa kitendo kilichotokea mchana kule hospitalini, Dafu akakiri kosa na kuahidi kutorudia. Lakini alipoelezwa azma ya Nasra ya kutaka kumuwekea wakili Promota Halfan, hamu ya uroda ikamtoweka ghafla akawa mbogo mfano hakuna. Ilimlazimu mama Nasra kufanya kazi ya ziada kumrudisha tena kitandani, hali iliyopelekea mjadala wa Nasra kufungwa mara moja.
Hata hivyo tayari Alwatan Dafu alirudi akiwa na wazo moja na msimamo mmoja kwamba atadhibiti gari na akaunti ya Nasra isitolewe hata senti moja mbovu! Alipomueleza haya mkewe aliishia kutazamwa kwa mshangao kama anayemuhurumia. Ni kweli mama Nasra alimuonea huruma mumewe ambaye hasira zake zilikuwa sawa na zile za mbogo aliyejeruhiwa ambaye hupambana hata na mti!. Mama Nasra hakutia neno tena, alizidi kunyonga nyonga kwa hasira! Huku mawazo yakiwa mengi kichwani. Alimsapoti sana mwanae Nasra, lakini pia alikuwa akimuheshimu na kumuogopa sana mumwewe Alwatan D! Vitu hivi viwili vilimfanya ausubirie msuguano mwingine wa Nasra na baba yake kwa mshaka makubwa!
Ndivyo ilivyokuwa. Miezi mitatu baadae, watoto wa Nasra walikuwa na hali nzuri kiafya isipokuwa yule mdogo aliyeitwa Romota hali ya huyu haikuwa inaridhisha sana. Miezi miwili baadae aliruhusiwa na kurudi kwao. Ulinzi wake uliongezeka mara dufu, sasa aliajiriwa mtu mwingine kwa ajili ya kumlinda Nasra tu! Hili halikuwa geti kali tena. Bali geti chungu hasa. Bahati mbaya hali hii ambayo haikumfurahisha mama Nasra
wala Nasra iliondoa amani iliyokuwa imetawala katika nyuma hiyo na kukaribisha machafuko. Nasra akazidisha kiburi na lugha mbaya. Mara kwa mara Alwatan Dafu alikuwa akimpiga mwanae hasa pale Nasra alipomtamkia maneneo yasiyofaa.
Wakati huo Promota Halfan alishahukumiwa kifungo chake katika siku zote
za kesi, Nasra hakuwa amepata nafasi ya walu hata ya kutoka nje ya nyumba yao wachilia mbali kuhudhuria kesi ya Halfan kule Mahakamani.
Gari lake la ushindi ‘Caddilac’ lilidhibitiwa vilivyo na hata siku moja
hakuwahi kuiona funguo wala kadi yake. Mambo yote haya yalimuinamia Nasra na kumfanya aishi katika msongo mkuu wa mawazo pamoja na unyonge uliokithiri. Mama yake alimuonea huruma sana na pengine ili kumpumzisha na madhila haya, akamshawishi aende Oman kwa Sadaam akabadilishe walau hali ya hewa. Wazo ambalo Nasra aliliafiki. Lakini kabla wazo hilo halijafikishwa kwa Alwatan Dafu, Alwatan akaja na
wazo jingine la kumpeleka Tanga kwa mdogo wake Dafu. Wazo ambalo pamoja
na Nasra na mama yake kulipinga, bado Nasra alipelekwa Tanga kwa nguvu!
Mungu bariki mke na watoto wa baba yake mdogo walikuwa wakarimu hujaona, taabu ilikuja kwa huyo baba yake mdogo Mansoor! Alikuwa mkali na mkatili mara mbili ya Alwatan Dafu. Ulinzi aliopata Tanga ulichusha na kuudhi na vile Alwatan Dafu alikuwa amemueleza kila kitu, hali ikawa mbaya zaidi. Nasra alivumilia kwa muda lakini aliposhindwa kabisa akamtolea uvivu na kuanza kumfanyia kama vile anavyomfanyia Alwatan Dafu, kipigo kikachukua nafasi. Ni pale Nasra alipotishia kuingamiza familia nzima ya baba yake mdogo kwa sumu, ndipo Mansoor aliposalenda. Akainua mikono na kumrudisha Nasra Dar es Salaam. Nasra akafurahia kwani alijua endapo atakuwa anaongea na mama yake, basi
atapata mawazo na ushauri mzuri na hivyo kujipatia faraja ya pekee! Jioni Alwatan Dafu alirudi akiwa mbogo vibaya akitataka kujua ni kwa nini Nasra ametishia kuangamiza familia ya mdogo wake kwa sumu. “Ilinichosha baba. Na hata hapa naweza kufanya hivyo mkizidi kunifuatafuata!” Akajibu kijeuri.
“Eti?” Jibu la Nasra likaibua hasira kali iliyoamsha mvua ya kipigo kilichokuja kuamuliwa na mama Nasra. Usiku huo mama Nasra aliutumia muda
wake mwingi akimfariji Nasra pamwe na kumkumbusha ‘wazo la Oman’ kabla hajamshauri la kufanya. Nasra akapokea ushauri huo. Mpaka mama Nasra
anaondoka kwenda kulala kwa Alwatan Dafu; Nasra alikuwa bado anatabasamu kwa furaha ya ushauri wa mama yake. Unadhani walikosea walikosea walionena mtoto wa kike kwa mama yake? Hata kidogo! * * * “Baba naomba kuongea na wewe kabla hujaondoka!” Nasra alimfuata baba yake na kumueleza hayo muda mfupi kabla Alwatan Dafu hajaondoka kueleka katika shughuli zake. Dafu akamtazama bintiye ambaye sasa amekuwa sugu na mwenye tabia za ajabu ajabu toka alipozaa mapacha, akatikisa kwa
masikitiko. Hapo kabla, Nasra hakuwahi kutaka kuongea na mzazi wake, tena kwa upole na heshima kama alivyofanya leo. Ushauri wa mama yake aliyeamini dawa ya moto ni maji ndio ulimfanya Nasra awe hivi. “Hiyo ndiyo salaam Nasra?” Hasira zilificha nyuma ya swali hili. “I am so sorry father!” Nasra akatahayari “Shikamoo!” “Marhabaa! Enhe ulikuwa unataka kuongea na mimi kuhusu nini!”
“Mengi tu baba, mengi sana! Sidhani kama unaifurahia hii staili mpya ya
maisha yetu ya paka na panya. Kumbuka wewe ndio baba yangu, nisipoongea
na wewe juu ya shida zangu nani atafanya hivyo? Tafadhali nisikilize walau kwa dakika chache tu!” “Wakati mwingine unakuwa binti mwenye busara Nasra. Nipo kwa ajili yako Mama, ninakusikiliza mwanangu!” Nasra akatabasamu, tayari alishamtoa mzee wake kunako uadui na kumfanya rafiki
kitu ambacho kilikuwa kimeanza kuondoka katika kamusi za vichwa vyao. “Ni kuhusu hili swala langu la kuolewa na Saadan!” “Enhe, nakusikiliza endelea!” “Samahani baba kama nitakuudhi kwa swali hili. Hivi baba ni kweli mimi ni mwanao kabisa kabisa?” “Kwa nini unauliza hivyo mwanangu?!” Alwatan Dafu akamtazama vizuri. “Nijibu kwanza baba, nijibu tafadhali” “Of course! Wewe ni mwanangu wa kuzaa kabisa tena mtoto wangu wa pekee kwa nini unauliza swali kama hili Nasra?”
“Nina sababu baba! Nina sababu za kutosha. Kwanza mfumo wa maisha tunayokwenda nayo baada ya mimi kuzaa, ndio uliopelekea niulize swali hili. Kama mimi ni mwanao inaelekea hunipendi kabisa baba na uko tayari kunipoteza kama sitafanya kile ambacho unakitaka wewe. Kitu ambacho wazazi wenye upendo wa dhati kwa watoto wao huwa hawathubutu. I think now you know kwa nini nimeuliza swali la aina hiyo” “Sikiliza Nasra mwanangu, sio kwamba sikupendi la hasha! Nakupenda sana mwanangu tena nakupenda kuliko unavyoweza kufikiria! Unachojaribu kufanya wewe ni kupiga ngumi ukutani, kuuzia mkondo wa maji na wakati mwingine kujaribu
kuyapandisha mlima! Kwa hili,huwezi kufanikiwa mwanangu!” “Una maanisha nini baba?”
“Kwamba mimi ni baba yako mzazi niliyekuzaa, kukulea na kukusomesha. Mpaka sasa uko chini ya himaya yangu! Nimejaribu kukulea katika maadili mema kwa kadiri nilivyoweza, ili uje kuwa mke na mama mwema. Lakini yule
khabith Halfan amenizidi ujanja na kuharibu kila kitu! Mungu amlaani atumikie kifungo kwa mateso makuu. Tena inaonyesha amekujaza maneneo
ya ajabu ajabu kiasi kwamba umeshindwa kupokea hata shauri wangu, umenidharau, kunidhalilisha na kuniona sifai! Umediriki hata…..!” “Usiende mbali baba! Where are you going now?” Nasra akamuwahi alipoona ameanza kupandisha hasira ”Kwa hiyo endapo nitakubali kuolewa na Saadan amani itarejea baina yetu?” “Bila shaka. Huo ndio ugonvi wetu mkubwa, Halfan sio mtu ni mnyama.” “Oke, kukuonyesha ni kiasi gani ninakupenda baba yangu mimi nimekubali kuolewa na Saadan….” Nasra akatua kwa muda kuangalia Alwatan Dafu anaipokeaje kauli hiyo. Dafu aliruka na kupiga ngumi hewani, akarukaruka na furahi mno. Akamkumbatia na kumbusu mwanae kwa fujo mpaka alipotosheka, akamuachia.
Nasra akaendelea “Lakini naomba uniambie kitu kimoja Daddy! Hivi ni kwa
nini ukaamua kunitafutia mchumba toka mbali mbali hivi? Unataka kuniambia kuwa Tanzania nzima na nchi dada za Afrika mashariki amekosekana mtu wa kunioa hata uniletee Saadan toka Oman?” “Inawezekana wapo! Lakini kwa jinsi nilivyokulea, nilitarajia upate mume
mstaarabu kwa maana halisi ya neno hilo tena atakayekupenda kwa dhati. Oman ni nchi ya kiislam, nasi ni waislaam nilikuwa na yakini kabisa kule atapatikana kijana mstaarabu kama ninavyotaka. Na kweli, kama hutakuwa mnafiki utakubaliana na mimi kwamba Saadan ni mstaarabu! Wangelikuwa wachumba wa kibongo na pengine wa kiafrika, hadithi ingekuwa
nyingine pengine ningepigwa, ningetukanwa, ningedhalilishwa na kuwekwa katika daraja ambalo hata Matonya yule bingwa wa kuomba hastahili kwalo kuwako huko. Lakini ilikuwa tofauti. Ni Saadan aliyehisi tofauti
toka mwanzo, akakukimbilia na kukudaka toka ulipojifungua, akawa bega kwa bega na sisi pamoja na mama yako kukupeleka hospitali ili kuokoa maisha yako na ya wanao. Kumbuka anafanya hivi akiwa hahusiki kabisa na mimba yako. Hiyo tisa kumi ni pale alipokubali kukuoa hivyo hivyo ulivyo na watoto wako na kuahidi kuwalea na kuwatunza. Wachilia mbali kuwalipa gharama za matibabu na matunzo pale Agha Khan hospital! Tanzania ya leo nani anaweza kufanya kama yeye? Nani?!! Na ajitokeze tumuone. Kwa yakini hakuna, hakuna kwa maana ya watu wanaojua kupenda, natumai ushujua naongelea nini!” Akahitimisha. Nasra akatikisa kichwa kukubaliana nae. Akasema. “Ni kweli uyasemayo baba. Saadan ana moyo wa peke yake! Lakini mimi…..” Akasita na kumtupia jicho baba yake. Alitaka kusema ‘simpendi kabisa!’ macho ya Alwatan Dafu ndiyo yaliyombadilihia uelekeo wa maongezi. “Lakini mimi simjui fika! Nahitaji kumjua kwanza baba pengine inawezekana yeye akawa mbaya zaidi kuliko wote uliowataja. Inawezekana anajifanya Simba mwenda pole ili ale
“Good Nasra. Ndio sababu nakupenda Nasra. Wewe ni msichana wa ajabu. Ninajivunia hilo, I love you Nasra!” Baba Nasra akishangilia kwa vigelegele “Sasa umeamua jambo la busara kuliko yote ***NASRA anamuhadaa babake, naye ameingia mkenge..... Je akienda OMAN atatoka hivi hivi ama ndo penzi litachipukia huko?? ITAENDELEA KESHO
| 2017-01-18T10:11:57 |
http://menacotzhadithi.blogspot.com/2013/04/riwaya-wasalimie-kuzimu4.html
|
[
-1
] |
MAKONDA AFURAHISHWA NA MKAKATI WA TCRA KUWEKA MFUMO WA ANWANI ZA MAKAZI NA POSTIKODI DAR ES SALAAM. | Dar Mpya Online TV
August 17, 2018 John Marwa
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda leo amefungua semina ya kimkakati inayolenga kulifanya jiji la Dar es salaam kuwa katika mpangilio wa kisasa na kuhakikisha mitaa yote inawekwa katika mfumo wa anwani za makazi na Postikodi Kama ilivyo kwa majiji makubwa ulimwenguni.
Makonda amesema Mfumo huo ni ukombozi mkubwa kwa wananchi kwakuwa utarahisisha huduma kwa wananchi ikiwemo kuwezesha kila mwananchi kuwa na anwani, kuwasaidia wageni kujua maeneo,kudhibiti wezi na matapeli, ulinzi na usalama, kusaidia kampeni ya usafi pamoja na kusaidia Jeshi la zimamoto na uokoaji kufika haraka kwenye eneo lenye dharura Kama ajali ya Moto au nyinginezo na kuokoa maisha.
Baadhi ya viongozi wa mkoa wa Dar es salaam waliohudhuria semina hiyo
Aidha ameipongeza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA kwa kuzifikia Kata 45 Kati ya 102 za mkoa huo na kueleza kuwa atawapatia ushirikiano wa kutosha kuhakikisha Mfumo wa anwani za makazi na Postikodi unafikia jiji Zima.
Pamoja na hayo amewaomba TCRA kupeleka elimu hiyo kwa Madiwani na wenyeviti wa mitaa ili kuwajengea uelewa.
“Mfumo wa Anwani za Makazi na Postikodi unalenga kuhakikika kila Eneo, Kata na Mtaa vinapewa majina na kila nyumba inakuwa na namba ya utambuzi”Amesema
| 2018-12-17T17:57:53 |
https://www.darmpya.com/makonda-afurahishwa-na-mkakati-wa-tcra-kuweka-mfumo-wa-anwani-za-makazi-na-postikodi-dar-es-salaam/
|
[
-1
] |
CV ya January Makamba | JamiiForums | The Home of Great Thinkers
CV ya January Makamba
Discussion in 'Jukwaa la Siasa' started by NOT FOUND, Aug 4, 2011.
wakuu ningependa kufahamu maelezo (cv) ya mbunge januari makamba.
Kuanzia elimu yake, (na alama alizopata) na maisha yake kwa ujumla. Na ni sifa gani ya pekee ambayo ilimfanya apate nafasi ya kuwa msaidizi wa j.k (2005 -2010)
Inasemekana jamaa anaandaliwa kuja kuwa president wa Tanzania.
Bio - Click: January Makamba.com
Who Am I? - Click: January Makamba.comClick to expand...
Katika Interview akijibu mwenyewe:
Swali: Tungeanza na wewe kutupa historia yako (Elimu, Kazi, Maisha kwa ujumla):
J. Makamba:
Samahani hapa nime-digress kidogo kwa kukumbuka na kuelezea zaidi kipindi hiki. Lakini experience hii ni sehemu ya mimi. Siku hizi NGOs zinayaita haya "mazingira hatarishi", lakini watoto wengi vijijini ndio maisha yao ya kila siku. Some make it, through pure luck or strength of character, some don't.
Form one nilisoma Handeni Secondary School, hii ilikuwa ni shule mpya, sisi tulikuwa Form One ya pili – kulikuwa hakuna walimu, madawati, maabara, n.k. Form Two hadi Form Four nikasoma Galanos, Tanga Mjini. Wakati nikiwa Form Three nilichaguliwa Deputy Head Prefect pale Galanos. Form Five na Six nikawa Forest Hill Secondary School, Morogoro, ambapo siku ya graduation nilitunikiwa cheti cha Overall Best Student.
Anyway, wakati nasuburi kwenda university, nikaenda kutafuta kazi kwenye kambi za wakimbizi Kibondo na Kasulu mkoani Kigoma. Nikafanikiwa Kasulu. Ukiacha maisha ya kijijini na bibi, this was another rewarding experience kwenye maisha yangu. Nilipata responsibilities kubwa kadri muda ulivyoenda, hadi kufikia ngazi ya Assistant Camp Manager kwenye kambi ya Mtabila Extension au Mtabila II, ambayo literally niliianzisha mimi (baada ya kuwa Serikali imetoa eneo) from the scratch kwa maana ya kusimamia ujenzi wa infrastructure za kambi na kugawa plots kwa wakimbizi. Kwenye kazi hii ndipo kwa mara ya kwanza nilipokutana na kuanza ku-engage na kujenga urafiki na watu wa mataifa mbalimbali waliokuwa expatriates kwenye camps. Muda wa kwenda Chuo ulivyofika, sikwenda kwani nilinogewa na kazi, mwaka uliofuatia sikwenda tena kwani nilipata responsibilities kubwa zaidi kambini and I was making and saving good money.
Eventually nikapata Chuo Marekani. Nilianza Boston baadaye nikajiunga na St. John's University, Minnesota. Hiki ni Chuo cha Wakatoliki Wabenedicto kilichokuwa katikati ya pori na lakes, a very beautiful and quiet place, katikati ya Jimbo la Minnesota. Pale, degree niliyochukua ni BSc in Peace and Conflict Studies. Niliamua kusoma hii kozi kutokana na experience yangu kwenya makambi ya wakimbizi. Nilitaka kuelewa ni kwa namna gani tunaweza kuzuia watu wasikimbie kabisa nchi zao, kwani maisha ya ukimbizi, kwa nilivyoyaona, ni ya udhalilishaji mkubwa sana na yanaondoa dignity ya mtu.
Wakati nikiwa St. John's University, nilirudi tena kufanya research yangu na UNHCR kwenye makambi ya wakimbizi Kasulu na Kibondo lakini pia kwenye way stations ndani ya Burundi na DRC.
Baada ya kumaliza St. John's, nikapata research assistantship kwenye ofisi ya Rais wa zamani wa Marekani, Mzee Jimmy Carter, Carter Presidential Centre, kule Atlanta, Georgia. Kazi hiyo ilinipeleka hadi kufanya kazi Sierra Leone, ambako pia nilijifunza mengi. Pia Atlanta ndiko nilikofanikiwa kukutana na mke wangu mpendwa, Mona, ambaye mwakani itakuwa miaka kumi tangu tujuane, na ambaye, pamoja naye, tuna mtoto mmoja wa kike wa miaka mitatu na nusu.
Baada ya Carter Center, nikajiunga na George Mason University, iliyoko maeneo ya Fairax, Washington DC metro area, kusoma Masters kwenye fani ile ile ya diplomasia na usuluhishi wa migogoro. Nilikuwa a very active graduate student kwa maana ya kushiriki mijadala na professional and advocacy associations mbalimbali pale DC. I created a vast network of friendships in DC ambayo hadi leo nafaidika nayo. Nikiwa graduate school, nilipata fursa ya kufanya internship Wizara ya Mambo ya Nje.
Baada ya kumaliza graduate school nikaomba kazi Serikalini na kuajiriwa na Wizara ya Mambo ya Nje kama Afisa wa Mambo ya Nje Daraja la Pili (Foreign Service Officer II). Nikiwa Wizara ya Mambo ya Nje, nilipata fursa ya kufanya kazi kwa karibu na Waziri wetu wakati ule (Mhe. Kikwete), hasa kwenye harakati za kutafuta suluhu ya mambo ya Burundi na DRC. Kwahiyo, wakati alipoamua kugombea Urais, akaniomba nichukue likizo isiyo na malipo Serikalini nisaidie kuwa errand boy kwenye kampeni yake, ku-organise makaratasi na notes zake, na kuchangia hapa na pale kwenye tafakuri za kuendesha na ku-organise kampeni yake wakati ule. Tulifanikiwa kufanya mambo mengi mapya na ya kisasa kwenye kampeni ile (including TV campaign ads kwa mara ya kwanza). Nilishukuru sana kupata fursa ya kuzunguka Mikoa yote na Wilaya zote nchini, kwa kweli kila kona ya nchi, kwa njia ya barabara na kujua na kujuana na watu na kujua kwa kina changamoto na fursa za maendeleo katika maeneo yote. Mhe. Kikwete alipofanikiwa kuchaguliwa, akaniteua nije kumsaidia hapa Ikulu na hapa ndipo nilipo hadi leo.
Soma zaidi - From Mo's Blog: Exclusive Interview With January MakambaClick to expand...
Kuanzia elimu yake, (na alama alizopata) na maisha yake kwa ujumla.
Na ni sifa gani ya pekee ambayo ilimfanya apate nafasi ya kuwa msaidizi wa j.k (2005 -2010)
inasemekana jamaa anaandaliwa kuja kuwa president wa tanzania. Hmmm...! Urais at that age ?
ingia kwenye tovuti ya bunge..wait a minute..kakutuma uje kumpigia kampeni,..apate airtime a.k.a comments za wanajf..tuko bize na shimbo
Kwahiyo wewe umejiunga leo kuja kutafuta cv ya mtu-unadhani hili jukwaa la mipasho?
Mkuu maisha wa watu yaitaji moyo. maisha siyo CV ni soft-skills na siyo hard-copy.
999 Others said:
inasemekana jamaa anaandaliwa kuja kuwa president wa tanzania.Click to expand...
Hivi ma president wa Tanzania huwa wanaandaliwa na binaadam? mie nilifikiri huwa ni "chaguo la mungu"!
Hivi ma president wa Tanzania huwa wanaandaliwa na binaadam? mie nilifikiri huwa ni 'chaguo la mungu'!Click to expand...
faizaaaaaaaaaafoxy message sent n delivery...
Unataka kumzuia?
Watanzania wengine bwana. We alama na performance ya mtu inakuhusu nini, we angalia anaperform vp shughuli za maendeleo ya Taifa.
Hv huyu faizafoxy anaga shughuli nyngne kwnye kila thread lazma ukute comments zake za utata.
Who Am I? - Click: January Makamba.com
kwa cv yake fupi january ni mwanadiplomasia kitaaluma. alichukua mikoba ya jairo kama msaidizi wa jk baada ya jk kupata uraisi 2005 akaonelea asindelee na jairo aliekuwa msaidizi wake kwa miaka mingi. aliamua kumpa ukatibu mkuu kama asante ya kumsaidia kwa miakamingi. fununu ni kwamba january ambae amechaguliwa hivi karibuni kuwa mkurugenzi wa mambo ya nje wa ccm anateuliwa kuwa waziri wa mambo ya nje kuchukuwa nafasi ya membe ambae inasemekana na ni mmoja wa watu watatu ambao wanaweza kumrithi ngeleja. wengine ni magufuli na sitta. kwa taarifa tu ni hayo.
gwaigwa
jameni hebu nisaidieni kuna uhusiano wowote kati ya uwezo wa mtu darasani na uwezo na umakini wake kwenye uongozi? mana kumekuwa na watu wengi wengi ambao wamekuwa wakifanya harakati za chini chini za kuutaka Urais wa nchi yetu. wengine tunawafahamu namna ambavyo hawako makini toka utotoni mwao, hivi ikitokea kweli wakawa tutakuwa tunalipeleka wapi taifa letu? mfano ni hizi harakati za chini chini zinazofanywa na mbunge wa bumbuli, mh januari makamba ambaye anajipanga kugombea kwa kufanya mikutano ya hapa na pale na pia kujinadi ili kujitia umaarufu kwa wananchi na haswa kupitia ujana wake na kiu ya mabadiliko iliyopo nchini. hapa ofisini kwetu kuna mtu alisoma na huyu mheshimiwa. baada ya mimi kusoma post ya hawa wanafunzi wa vyuo vikuu hapa JF niliwashirikisha wenzangu nikiwaambia kuwa katika wabunge vijana huwa namfagilia sana Januari kwa namna anavyoonesha weledi kwenye kazi zake. ndipo jamaa akasema kuwa huyo hana kitu sababu alifeli kidato cha nne na cha sita na kutumia hela za usalama wa taifa kwenda kusoma nje kwa ushawishi wa baba yake mzee makamba. jamaa akathibitisha kuwa alisoma naye form six pale forest hill na kwamba januari makamba alipata division zero. kauli hii ilinishtua sana na kuniakatisha tamaa kabisa ndipo nikaamua kuwauliza hapa hivi akifanikiwa kuingia ikulu huyu itakuwaje?
mnhhhh no wonder
January he is just a puzzle....
Hebu tuambie alimaliza mwaka gani na alitumia jina gani ili twende tukafukunyue Baraza tukishathibitisha tutachangia. kale kaugonjwa ka kutoa habari zisizothibitishwa katika jamvi wengi mnako na sijui lini katakoma. Kuambiwa tu na mtu kuwa kasoma nae sio uthibitisho, mbona hata mimi naweza kusema nimesoma na wewe tukamaliza wote six na ukapata div. one wakati labda uhalisia ulimaliza 7 tena kwa shida na kwamba faida pekee uliyoipata ni kupiga picha na mwl. Mkuu.
gwaigwa said:
jameni hebu nisaidieni kuna uhusiano wowote kati ya uwezo wa mtu darasani na uwezo na umakini wake kwenye uongozi? mana kumekuwa na watu wengi wengi ambao wamekuwa wakifanya harakati za chini chini za kuutaka Urais wa nchi yetu. wengine tunawafahamu namna ambavyo hawako makini toka utotoni mwao, hivi ikitokea kweli wakawa tutakuwa tunalipeleka wapi taifa letu? mfano ni hizi harakati za chini chini zinazofanywa na mbunge wa bumbuli, mh januari makamba ambaye anajipanga kugombea kwa kufanya mikutano ya hapa na pale na pia kujinadi ili kujitia umaarufu kwa wananchi na haswa kupitia ujana wake na kiu ya mabadiliko iliyopo nchini. hapa ofisini kwetu kuna mtu alisoma na huyu mheshimiwa. baada ya mimi kusoma post ya hawa wanafunzi wa vyuo vikuu hapa JF niliwashirikisha wenzangu nikiwaambia kuwa katika wabunge vijana huwa namfagilia sana Januari kwa namna anavyoonesha weledi kwenye kazi zake. ndipo jamaa akasema kuwa huyo hana kitu sababu alifeli kidato cha nne na cha sita na kutumia hela za usalama wa taifa kwenda kusoma nje kwa ushawishi wa baba yake mzee makamba. jamaa akathibitisha kuwa alisoma naye form six pale forest hill na kwamba januari makamba alipata division zero. kauli hii ilinishtua sana na kuniakatisha tamaa kabisa ndipo nikaamua kuwauliza hapa hivi akifanikiwa kuingia ikulu huyu itakuwaje?Click to expand...
Mkuu wewe mwenyewe umekiri kuwa unamfagilia lakini kusikia ati kapata division zero unaonekana kuhoji tena uwezo wake! Usingepata hiyo habari basi ungeendelea kumkubali? Kama ni ufaulu wa darasani basi nchi zingekuwa zinaongozwa na maprofessor.
Kwa sasa ninaona uwezo wa makamba kama wa zitto. Haimaanishi kuwa naungana na hao uvccm bali yawezekana kweli alifeli lakini dakika za mwisho alijitambua
Hivi unaanzaje kumfagilia mtu ambaye ktk uongozi ht miaka 5 hajafika..kwa kifupi na muona wakawaida..sijui ni lipi kafanya la ajabu mpk ashawishi hao vijana hivyo..yale yale kumfagilia kikwete enzi hizo kumbe kazi hawezi
Siogopi Chochote!
January Makamba ajitokeze sasa kujibu tuhuma za kuiba mitihani Galanos Sekondari kidato cha nne.
Hatuwezi kuwa na naibu waziri wa sayansi na teknolojia mwenye tuhuma za wizi wa mitihani karne hii inayohitaji weledi bila kupata ufafanuzi wa kina.
Kuna wimbi la wanafunzi kukimbia masomo ya sayansi na wengine kutafuta mbinu za wizi.Tunazipinga ila katika kukabiliana nazo tunampa uwaziri mwenye tuhuma hizo.
Nahisi Mfalme **** atakua kwenye kiti cha enzi!
he can be president by english not by presidential traits
Mkuu wewe mwenyewe umekiri kuwa unamfagilia lakini kusikia ati kapata division zero unaonekana kuhoji tena uwezo wake! Usingepata hiyo habari basi ungeendelea kumkubali? Kama ni ufaulu wa darasani basi nchi zingekuwa zinaongozwa na maprofessor.Click to expand...
Mkuu Kimbunga sabah kheri!
Ukipata muda tembelea blogu ya January alivyojikanyaga kanyaga kuhusu kufutiwa matokeo ya kidato cha nne baada ya kuthibitika kuiba (kufanya udanganyifu) mitihani ya kidato cha nne Galanos Secondary School.
Pengine kama si kuwa mtoto wa Yusuph Makamba sashivi January angekuwa anachoma mahindi bumbuli pale Soni sokoni au kijijini kwekitui!
| 2016-10-23T01:27:36 |
http://www.jamiiforums.com/threads/cv-ya-january-makamba.161097/
|
[
-1
] |
HABARI ZA JAMII: Mashine za Kielektroniki Kuanza Kutumika Magogoni.
Mashine za Kielektroniki Kuanza Kutumika Magogoni.
Serikali inatarajia kutoa huduma za ukatishaji wa tiketi kwa njia ya mfumo wa kielekroniki katika kivuko cha Magogoni ili kudhibiti mapato yanayopotea kiholela.
Akiongea na Maelezo Jijini Dar es Salaam, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme Dkt. Musa Mgwatu alisema kukamilika kwa mfumo huo utakaogharimu bilioni 1.1 kutasaidia kuiongezea mapato serikali kwani mfumo huo utafanyakazi kwa njia za kielekroniki.
“Ujenzi wa mashine za kielektroniki umeshaanza na kukamilika kwa upande wa magogoni, Mkandarasi anatarajia kuanza ufungaji wa mashine hizo upande wa Kigamboni wiki hii,” alifafanua Dkt. Mgwatu.
Dkt. Mgwatu alisema Mkandarasi wa mradi huo anatarajia kukamilisha uwekaji wa mashine hizo julai 25 mwaka huu na utumiaji wa mashine hizo utaanza kutumika tu mara baada ya makabidhiano kutoka kwa mkandarasi.
Akizungumzia gharama za kuvuka Dkt. Mgwatu amesema, gharama za kuvuka zitabaki pale pale na hakutakuwa na ongezeko lolote mashine hizo zitakapoanza kutumika.
Bwana Ismail Juma, mkazi wa Kigamboni amesema kuanzishwa kwa mfumo huo kumekuja wakati muafaka na kutasaidia kuiongezea mapato serikali na kuepusha upotevu wa mapato katika vivuko hivyo.
Hivi karibuni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano aliwaagiza TEMESA kufunga mfumo kamili wa kupokea nauli wa elektroniki ambao utadhibiti ukwepaji wa kulipa nauli ili kuongeza mapato.
Posted by Dotto Mwaibale at 7:04 AM
| 2017-08-17T01:53:58 |
http://www.habarizajamii.com/2017/06/mashine-za-kielektroniki-kuanza.html
|
[
-1
] |
Mbunge wa Mtwara Hawa Ghasia afunika mchezo wa kuogelea
Posted on: December 31st, 2018
Mbunge wa Mtwara Vijijini Mhe. Hawa Ghasia ameonesha uwezo mkubwa wa kuogelea wakati wa tamasha la “Msangamkuu Beach Festival “lililofanyika Disemba 30,2018.
Ghasia ambaye anadai ana uzoefu wa kuogelea maji ya bahari tangu akiwa mtoto aliuacha hoi umati huo kwa jinsi alivyokuwa akibadili mitindo mbalimbali ya kuogelea hali ambayo ilizifanya meli za uokoaji kumzunguka mara kwa mara ili kujiridhsiha iwapo hayuko matatizoni.
Akizungumzia tamasha hilo Mhe. Ghasia amepongeza hatua hiyo na kuwataka wanachi na wawekezaji wa nje na ndani ya mkoa kujitokeza kwa wingi kuwekeza katika wilaya ya Mtwara, ambayo ina fukwe nyingi za kuvutia.
Amezitaja fukwe hizo kuwa ni pamoja na Msimbati ambayo ameitaja kama fukwe pekee hapa nchini ambayo binadamu anaweza kuendesha gari kama anavyoendesha kwenye barabara ya lami, fukwe ya Mnazi ambayo ina urefu zaidi ya kilometa ishirini, fukwe ya Naumbu pamoja na ile ya Mgao.
Aidha, Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Evod Mmanda amewapongeza wanaMtwara waliojitokeza katika tamasha hilo. Anasema Msangamkuu ni eneo moja katika maeneo mengi yanayohitaji kutangazwa hivyo atahakikisha dunia inatambua hilo.
Tamasha la “MsangaMkuu Beach festival” limefanyika kwa mara ya kwanza katika fukwe hiyo Disemba 30,2018 huku mwanzilishi wa tamasha hilo Mhe. Gelasius Byakanwa, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara akiwaomba wadhamini kujitokeza kudhamini tamasha hilo ambalo anakusudia liwe endelevu. Amesema hiyo ni fursa muhimu kwa kutangaza vivutio vya utalii vya mkoa wa Mtwara.
Video yake hii HAPA
Wanaowapa Mimba watoto wa shule waendelee kudhibitiwa- Waziri Waitara
Naibu Waziri Waitara afundisha HIsabati Masasi
Radi yaua mwanafunzi sekondari ya Mikindani
Byakanwa kuwaongoza wadau kujenga shule Mtwara
Kila Mtanzania kutibiwa kwa Bima
| 2019-03-19T09:45:28 |
http://www.mtwara.go.tz/new/mbunge-wa-mtwara-hawa-ghasia-afunika-mchezo-wa-kuogelea
|
[
-1
] |
swahilivilla: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
TAARIFA KWA UMMA KUKANUSHA HABARI YA "KASHFA MPYA MALIASILI"
Gazeti hilo linanukuu tangazo ambalo lilitolewa na Muungano wa Jumuiya Zilizoidhinishwa za Hifadhi za Maeneo ya Wanyamapori Tanzania (Authorized Associations AAs Consortium) kuhusu vitalu. Tangazo hilo ambalo lilitolewa kwa njia ya magazeti liliwataka wadau wapeleke maombi ya vitalu vya uwindaji wa kitalii vilivyoko katika Maeneo ya Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori (WMAs) kwa kipindi cha mwaka 2013 hadi 2018.
Tangazo lililotolewa na Muungano wa Jumuiya Zilizoidhinishwa za Hifadhi za Maeneo ya Wanyamapori Tanzania (Authorized Associations- AAs Consortium) siyo sahihi kwani Kifungu cha 31 (7) cha Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori Na. 5 ya mwaka 2009 kilichonukuliwa katika Tangazo hilo hakikuzingatiwa ipasavyo kwa misingi ifuatayo:- i. Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori hakushirikishwa na hakutoa ridhaa yake kabla ya tangazo hilo kutolewa; ii. Halmashauri za Wilaya viliko vitalu hivyo nazo hazikushirikishwa; na iii. Kifungu hicho [31(7)] hakitoi mamlaka kwa Muungano wa Jumuiya Zilizoidhishwa (Authorized Associations-AAs Consortium) kutoa tangazo la vitalu vya uwindaji wa kitalii katika Maeneo ya Jumuiya ya Hifadhi za Wanyamapori (WMAs). iv. Kanuni zinazotumika sasa hazitoi utaratibu utakaotumika kupata wawekezaji katika vitalu vya uwindaji wa kitalii vilivyoko katika WMAs. Kanuni za WMAs zinafanyiwa marakebisho na zitakapokamilika zitatoa utaratibu utakaotumika katika kutangaza vitalu vilivyopo kwenye WMAs.Kutokana na sababu hizo Wizara ya Maliasili na Utalii inatahadharisha kuwa tangazo hilo siyo sahihi kwa kuwa halikuzingatia sheria. Kwa hiyo wadau wa uwindaji wa kitalii wanatahadharishwa kutopeleka maombi ya vitalu hivyo.Wizara imewasiliana na Muungano wa Jumuiya Zilizoidhinishwa za Hifadhi ya Maeneo ya Wanyamapori Tanzania (Authorized Associations - AAs Consortium) kuwataka wasitishe mchakato huo wa kugawa vitalu katika maeneo ya WMA.
George Matiko:MSEMAJIWIZARA YA MALIASILI NA UTALII16 Mei 2012.. Simu 0784 468 047
| 2013-12-12T17:58:48 |
http://swahilivilla.blogspot.com/2012/05/taarifa-kwa-vyombo-vya-habari.html
|
[
-1
] |
Walei ni wakina nani? - AckySHINE MiniSites | Best of 2019
Watawa ni Waamini, Walei au Maklero waliowekwa wakfu kwa Mungu katika Kanisa kwa ajilli ya wokovu wao na wa dunia:-.. soma zaidi hapa
Maklero ni watu wote wenye daraja Takatifu yaani Maaskofu, Mapadri na Mashemasi… soma zaidi hapa
Taifa la Mungu limeundwa kwa Maklero yaani Maaskofu, Mapadri, Mashemasi, Watawa na Walei… soma zaidi hapa
Ushirika wa Watakatifu ni:-.. endelea kusoma zaidi
Mama wa Yesu Kristo ni Bikira Maria… endelea kusoma zaidi
Sala muhimu kwa Mkristo ni;.. endelea kusoma zaidi
Sakramenti inayokamilisha ubatizo na kipaimara ni ekaristi, iliyo kuu kuliko sakramenti zote kwa sababu ndiyo Yesu mzima, Mungu-mtu, katika maumbo ya mkate na divai… endelea kusoma zaidi
| 2019-09-20T05:42:25 |
http://www.ackyshine.com/katekisimu:walei-ni-wakina-nani
|
[
-1
] |
PHP Scripts / MiscellaneousFunny Jokes— Add-On kwa WorldWideScripts.netKujiunga na kulisha wetu kukaa hadi tarehe!Mpya! Kufuata yetu kama unataka!★★★★★Sehemu hii inapatikana katika 37 lugha nyingine!ArabicBengaliCatalan/ValencianDanishDutchEnglishEsperantoFinnishFrenchGermanGreekGujaratiHindiIndonesianItalianJapaneseKannadaKoreanMalayNorwegianPersianPolishPortugueseRomanian/Moldavian/MoldovanRussianSimplified ChineseSpanish/CastilianSwedishTagalogTamilTeluguThaiTraditional ChineseTurkishUkrainianUrduVietnameseKuishi PreviewViwamboAds
"Mapenzi Jokes" ni tayari alifanya utani tovuti ambalo lina zaidi ya 40,000 utani ambayo ni kusambazwa miongoni mwa makundi 65, zaidi ya 40,000 utani pia inaruhusu watumiaji na wageni kuwasilisha utani yao wenyewe ambayo admin unaweza kupitisha. Ni inaruhusu wageni kwa kiwango utani, ili, utani bora kusimama mbali. Makala 40,000 utani Makundi 65 Msaada Adsense Google Vifungo mtandao jamii jumuishi User rating Maoni ya utani kuwasilisha Wageni utani kuwasilisha Kurasa ukomo viumbe kupitia CMS SEO URL kirafiki Kwa urahisi customizable Mandhari msaada Jopo admin Kusimamia utani Juu ya kutafuta Kusimamia kurasa Kusimamia Matangazo ya Google Export orodha user Dashboard na stats / grafu Admin http://www.madlogics.com/jokes-app/index.php/admin
jina la mtumiaji / password admin / 123456
Mahitaji PHP 5.1.0 au zaidi inahitajika. MySQL 5.x PDO MySQL ugani PHP GD http://madlogics.com/jokes-app/requirements DownloadVipengele vingine katika jamii hiiKila sehemu ya mwandishi huyuMaoniMara kwa mara kuulizwa maswali na majibuMaliKuundwa:19 Agosti 12Badiliko:9 Agosti 13Sambamba Browsers:IE7, IE8, IE9, Firefox, Safari, Opera, ChromeFiles Pamoja:JS JavaScript, HTML, CSS, PHP, SQLMfumo wa Programu:YiiProgramu Version:PHP 5.0-5.2KeywordseCommerce, eCommerce, Vitu zote, furaha, utani funny, ucheshi, muda kupita
| 2017-06-22T11:58:41 |
https://sw.worldwidescripts.net/funny-jokes-41074
|
[
-1
] |
MATONDO: WASUKUMA HIVI NDIVYO TUNAVYOHESABU - SOLO, BILI, YATU...
WASUKUMA HIVI NDIVYO TUNAVYOHESABU - SOLO, BILI, YATU...
Kikwenu mnahesabuje? Picha imetoka kwa dada Florah Lauwo
Chacha WamburaSeptember 4, 2009 at 3:13 PMkamwe, kabhere, katato, kane, katano, kasansabha, muhungate, monane, kenda, ikominadhani upo hapo ng'wanawane. kuna raha yake ukifika vila ukakuta wanatwanga malugha hayo, yee!!ReplyDeletemumyherySeptember 5, 2009 at 7:32 AMkwa wenyeji wangu wao huhesabu hiviichi, ni, san, yon/shi, go, roku, nana, hachi,kyu, ju.ahsanteReplyDeleteMasangu Matondo NzuzullimaSeptember 5, 2009 at 6:19 PMMumyhery, ni lugha gani hii? Kwa hakiki si Kibantu. AsanteReplyDeleteChacha WamburaSeptember 8, 2009 at 2:51 PMlabda ni kijepu cha kyotoReplyDeletemumyherySeptember 10, 2009 at 2:02 PMmami hao ni wenyeji wangu wajapani ambao wao huesabu kwa makumi, ikifika kumi atakwambi kumi moja na ishirinir ni makumi mawiliReplyDeleteAdd commentLoad more...
| 2016-12-11T13:41:55 |
http://matondo.blogspot.com/2009/09/wasukuma-hivi-ndivyo-tunavyohesabu-solo.html
|
[
-1
] |
Azuay Markapi PJ llankaypi chapakkunami shuyakun ayllullaktakuna riksichun antawakuna kutincharishkata | Policia Nacional del Ecuador
Azuay Markapi PJ llankaypi chapakkunami shuyakun ayllullaktakuna riksichun antawakuna kutincharishkata
2 de abril de 2014 - 4:21 pm
Tiempo de lectura: | No. de palabras: | 1711 visitas
Cuenca Kitypimi, chapakkuna rikurayay ruraykunapi, tukuri hunkaypa punchakuna, tukuripika hapishkami 17 antawakunata, shinallatak 25 kuyukta chikan chikan llaktakuna kay markapi, Policia Judicial llankay kamakpi antawakuna wakichinapi shuyakunmi riksichun shinallatak ña apachun
Capitán Ricardo Valdiviezo, Policía Judicial llankaypak kipa pushaka willarkami, kutin charshka antawakunaka ña willashkami shuwashkamanta chikan chikan markakuna mamallaktapi, yupaykuna, antawa kuyuchik yupaykuna wawanchishkami
Kay antawakunataka hapishkami rikurayay ruraykunap llakta ñankunapi, antawa allichinapi, antawakuna hatuna, rantinapi, ashtawankarin ayllukuna ña randishkami wantawakuna hatunapi shuktak markapi, ña kay markapi rikukpika shuwashka antawakunami kan, Valdiviezo chapak pushak rikuchirka
Kuyukkuna
Chapakkunata Pushak rikuchirkami kuyukkunamanta, runakunaka kuyuta purichikukpika kay uchilla antawakunaka, mana charirkachu paypak killka pankata, chaymantami charirayashka kuyukkunata
Valdiviezo pushakka yuyachishkami, ayllullaktakunata manarak kay kuyuk antawakunata rantishpa shamupaychik, chapakkunapak llankay wasiman tapunki, mana kashpa killachi killkapi rikuytukunkimi kay antawakuna ima llakita charikta
Chapakkunaka mañashkami ayllullaktakunata, ña shuwashka huchachishka killa pankata charishpaka, shamupaychik chapakkunapak llankay wasiman, riksinkichik antawakunata, kikinpak chaypi kakpika killka pankatami kuna kanki tikrachichun
| 2020-01-22T08:58:44 |
https://www.policiaecuador.gob.ec/azuay-markapi-pj-llankaypi-chapakkunami-shuyakun-ayllullaktakuna-riksichun-antawakuna-kutincharishkata/
|
[
-1
] |
MICHUZI BLOG: Introducing Nyimbo MPYA ya Jay Maiko Ft. Come Dash – "Sio Mbali" '; if(img.length>=1) { imgtag = '
Introducing Nyimbo MPYA ya Jay Maiko Ft. Come Dash – "Sio Mbali"
| 2018-07-21T01:51:08 |
https://issamichuzi.blogspot.com/2017/09/introducing-nyimbo-mpya-ya-jay-maiko-ft.html
|
[
-1
] |
ITV yaigwaya Policcm | JamiiForums | The Home of Great Thinkers
ITV yaigwaya Policcm
Discussion in 'Habari na Hoja mchanganyiko' started by Mpanzi, Nov 10, 2011.
Televission ya ITV imeshindwa kutoa majibu ya kipimajoto cha jana juu ya udhaifu wa jeshi la polisi, inaonekana wamechimbwa biti na policcm!
Anayetoa hizo amri ni nani!!!! ndiye anayelipaka hilo Geshi la Polisi matope!!
materu74
duh! Kweli uonevu unaongezeka,mimi nangoja tu NTCL WA TZ,mbona tutawachomoa kwenye makalvati tu
magamba tu hao! hawana lolote....
Itv ni mammbwa hakika hii imekaa vibaya lakini Namshukuru Mungu sana kujua haya yote.Itv wamekuwa Wasaliti kwa watanzania,Naomba wawekwe kwenye kundi la Kikwete na Mafisadi watakaoondoka baada ya siku 100.
Wafungue kituo cha polisi pale Itv ili wajiakikishie usalama laa sivyo hatutakuwa tayari kuvumilia upuuzi wa vyombo vya habari Wasaliti wa haki za Watanzania kamwe.
imekaa vibaya hata nyinyi ninaye waamini kwa kunipa habari basi Tanzania Imekwisha
Mengi kuna time ni mnafiki sana!
Wakuu mimi nilidhani mawazo yangu yamenielekeza huko kumbe watu wengine wameliona hilo?kweli wakuu hata mimi niliona wamjaribu kuficha ili watu wengi wasione jinsi maoni ya watu wanavyoliona jeshi la polisi,pamoja na yote ukweli utabaki pale pale kwamba POLICCM wanaonea sana siku hizi kwa kufuata maagizo ya CCM.hawa ITV nao wameshakuwa kambi moja na magamba
Wakuu mimi nilidhani mawazo yangu yamenielekeza huko kumbe watu wengine wameliona hilo?kweli wakuu hata mimi niliona wamjaribu kuficha ili watu wengi wasione jinsi maoni ya watu wanavyoliona jeshi la polisi,pamoja na yote ukweli utabaki pale pale kwamba POLICCM wanaonea sana siku hizi kwa kufuata maagizo ya CCM.hawa ITV nao wameshakuwa kambi moja na magambaClick to expand...
Mengi ni gamba loong time ago!
Wasaliti, wamejiunga na wenzao TBC. Who is next?
Televission ya ITV imeshindwa kutoa majibu ya kipimajoto cha jana juu ya udhaifu wa jeshi la polisi, inaonekana wamechimbwa biti na policcm!Click to expand...
Results zilikuwa very high kwa waliopinga udhalimu wa polisi. Uwt wakaamuru wasitangaze. Sasa hivi itv ni ITVCCM. Period
Magamba ya CCM yanatumia kila njia kuwakandamiza watu,yamejaza vibaraka JF.
Mi siku hizi taarifa ya habari napata star tv na kidogo chanel ten. Itv imeboa kuliko hata tbc1. Siku ukiiona itv inapambana na baazi ya mafisadi, ujue kwamba kuna tonge la kifisadi linagombaniwa kati ya Mengi na mafisadi wenzie.
Wakitangaza au wasitangaze ukweli utabakia vifuani mwa waliodhulumiwa. If you are out to describe the truth, leave elegance to the tailor.
vibaraka kila kona
kipindi cha uchaguzi itv wanaonyeshaga vita vy rwanda na wakimbiza,huu mradi alianza tokea 95,hivi analipa kodi huyu?
| 2017-01-19T17:24:02 |
https://www.jamiiforums.com/threads/itv-yaigwaya-policcm.191417/
|
[
-1
] |
Siku ya wapendanao ya Siku ya wapendanao ya Siku ya Wapendanao - Ushawishi wa Fitness
nyumbani » Misfit » Siku ya Siku ya Wapendanao ya Misri ya Misfit
Kwa Siku ya Wapendanao 2018, unaweza kuokoa kwenye watumiaji wa shughuli za Misfit.
Uuzaji huu unajumuisha 40% kwenye Awamu ya Misfit, Ray, Shine 2, na Flare Plus. Pia unaweza kuchukua 75% kutoka Crystal Shughuli ya Crystal.
Uuzaji huu unafanyika hadi Februari 14th, 2018
Februari 6, 2018 FitnessRebates Misfit Hakuna maoni
| 2018-08-18T10:54:48 |
http://sw.fitnessrebates.com/misfit-2018-valentines-day-sale/
|
[
-1
] |
Huduma za afya Marekani kujadiliwa - BBC Swahili
Huduma za afya Marekani kujadiliwa
http://www.bbc.com/swahili/habari-40723745
Image caption Huduma za afya kujadiliwa nchini Marekani
Bunge la Marekani limepiga kura kuendelea na mjadala wa ama isalie sera ya afya iliyo anzishwa na kumpa heshima kubwa aliyekuwa raisi wa taifa hilo Barrack Obama iondolewe.
Hatua hii inaonekana kama ushindi kwa rais Trump aliye ahidi wakati wa kampeni zake kuiondosha sera hiyo iliyo anzishwa kwa mujibu wa sheria ya huduma kwa gharama rafiki.
Siku za nyuma majaribio kadhaa ya chama cha Republican kuibadilisha sera hii maarufu kwa jina la Obamacare yaligonga mwamba, mara hii kauli ya kuanzisha mjadala ilioibuliwa na kiongozi wa kundi la walio wengi bungeni kabla ya kubainika iwapo ingeungwa mkono vya kutosha na chama cha Republican
Sambamba na hilo la Obamacare, huko Capitol Hill, nyumba ya wawakilishi pia inajiandaa kupiga kura kuiwekea vikwazo vipya Urusi, hatua ambayo tayari imeidhinishwa na baraza la mawaziri ikiwa ni kama kujibu mapigo kwa Urusi kutuhumiwa kuingilia uchaguzi wa Taifa hilo.
Ikulu ya Marekani inasema maamuzi yatafanyika hivi karibuni juu ya hatma ya mwanasheria mkuu wa nchi hiyo Jeff Sessions kwa kushindwa kumchunguza mpinzani wa rais Donald Trump, Bi Hillary Clinton
Aliye kuwa meneja wa kampeni wa Rais Trump,Paul Manfort amekutana na jopo la wapelelezi kujibu maswali juu ya uhusiano na Urusi, na wakati haya yakiendelea msaidizi wa msemaji wa Ikulu Michael Short amejiuzulu.
| 2017-08-17T14:37:40 |
http://www.bbc.com/swahili/habari-40723745
|
[
-1
] |
R. Kelly akimbizwa hospitalini baada ya kuanguka, wakati akitazama makala ya namna alivyowafanyia vitendo vibaya mabinti wadogo - Bongo5.com
Contributor January 12, 2019 - 11:21 am
| 2019-06-19T13:36:36 |
http://bongo5.com/r-kelly-akimbizwa-hospitalini-baada-ya-kuanguka-wakati-akitazama-makala-ya-namna-alivyowafanyia-vitendo-vibaya-mabinti-wadogo-01-2019/
|
[
-1
] |
UJIJI RAHAA: NAIBU SPIKA WA BUNGE AKUTANA NA UGENI KUTOKA JHPIEGO
NAIBU SPIKA WA BUNGE AKUTANA NA UGENI KUTOKA JHPIEGO
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson (kulia) akisalimiana na Mkurugenzi Mkazi wa JHPIEGO nchini Tanzania Ndg. Jeremie Zoungana, aliyekuja kuzungumza nae na kubadilishana uzoefu wa kazi, kabla ya kuanza kikao kilichofanyika jana Mei 3, 2017 Ofisini kwake Mjini Dodoma
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson (kulia) akizungumza na ugeni uliomtembelea jana Mei 3, 2017 Ofisini kwake Mjini Dodoma, ukiongozwa na Mkurugenzi Mkazi wa JHPIEGO nchini Tanzania Ndg. Jeremie Zoungana (wa pili kulia).
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson (kulia) akimsikiliza Mkurugenzi wa Mradi wa USAID wa Boresha Afya, Ndg. Dustan Bishanga (wa pili kushoto) akizungumza katika kikao kilichofanyika Ofisini kwake Mjini Dodoma. (PICHA NA OFISI YA BUNGE).
| 2017-05-27T21:24:48 |
http://ujijirahaa.blogspot.com/2017/05/naibu-spika-wa-bunge-akutana-na-ugeni.html
|
[
-1
] |
Mshukuru Sana Yeyote Ambaye Amewahi Kukunyanyasa, Bila Yeye Huenda Usingepiga Hatua. – AMKA MTANZANIA
Mshukuru Sana Yeyote Ambaye Amewahi Kukunyanyasa, Bila Yeye Huenda Usingepiga Hatua.
Habari za leo rafiki yangu?
Hongera kwa siku hii nyingine nzuri sana ya leo. Kila unapopata nafasi ya kuiona siku mpya, ni jambo kubwa la kushukuru na kutumia nafasi hiyo vizuri kwa sababu wapo wengi walipanga kuitumia lakini hawajaiona.
Karibu kwenye makala hii ya leo ambapo nakwenda kukukumbusha jambo moja muhimu sana kuhusu maisha yetu ya mafanikio.
Wapo watu ambao wamepitia magumu sana mpaka kuweza kufikia mafanikio. Na kwa hakika, kila mtu kuna ugumu lazima aupitie kabla hajafanikiwa. Mafanikio siyo rahisi, na huwa hayaji kwa wale walioridhika na maisha waliyonayo. Lazima ufike mahali useme imetosha na kuamua kuchukua hatua, ndipo unafanikiwa.
Katika kupitia changamoto hizi za mafanikio, wengi wamenyanyaswa sana. Wapo watu ambao wamepitia mateso na manyanyaso makubwa kutoka kwa watu ambao waliwategemea sana. Manyanyaso hayo yaliwapa hasira kubwa ya kuchukua hatua na kushika hatamu ya maisha yao. Wakapambana kweli mpaka wakafanikiwa.
Lakini sasa wanakuwa wanaendelea kufanya kosa moja kubwa sana kwenye maisha yao, ambalo linawazuia kufurahia mafanikio yao.
Kosa hilo ni kuendelea kuwa na vinyongo kwa wale ambao waliwanyanyasa na kuwatesa. Hivyo hufanya mambo kuwaonesha kwamba na wao sasa wana nafasi, au wakati mwingine hata kutaka kulipa kisasi. Pale inapotokea mtu aliyewanyanyasa anahitaji msaada, wanamkumbusha kwamba waliwanyanyasa na hivyo hawawapi msaada kwa moyo mmoja.
Hili ni kosa kubwa sana rafiki yangu, kama umewahi kulifanya basi leo ni siku ya kuachana nalo mara moja.
Mtu yeyote ambaye aliwahi kukunyanyasa au kukutesa huko nyuma, ukapata hasira na kuamua kupambana kwenye maisha yako ili ufanikiwe, ni mtu ambaye unapaswa kumshukuru sana. Tena kama yupo ambaye unamkumbuka chukua hata simu sasa na mpigie kumwambia asante.
Najua hili linaweza kuwa gumu kwako, hasa kama maumivu aliyokusababishia ni makubwa, lakini ni jambo jema sana kwako unaloweza kufanya kwenye maisha yako.
Huenda ni mzazi alikufukuza nyumbani na kukuambia hataki kukuona tena kwa sababu amekuvumilia na kashindwa. Ukalazimika kwenda kuomba kukaa kwa watu kwa muda na kuanza maisha yako mwenyewe.
Huenda ni mwajiri ambaye alikuwa anakunyanyasa kwenye kazi, au walikuwa hakulipi kwa muda na huenda alikufukuza kazi bila sababu, na hapo ukapata hasira na kuamua kwenda kujiajiri.
Au ni ndugu ambaye ulikuwa unamtegemea wakati huna kazi wala biashara, mwishowe akakuambia hawezi kukusaidia tena na utafute utaratibu mwingine. Huenda mtu alikufukuza kama mbwa na kukudhalilisha sana, hayo yote yakakupa hasira kubwa, huu ni wakati wa kuwashukuru wote hao.
SOMA; Huu Ndiyo Wakati Sahihi Wa Kutua Mizigo Tuliyobeba Kwenye Mioyo Yetu.
Kwa nini nakuambia hili?
Iko hivi rafiki, sisi binadamu ni viumbe wa tabia na mazoea, huwa tuna tabia ya kuzoea mambo haraka halafu kujenga tabia kwenye mazoea hayo. Baada ya kujenga tabia, huwa ni vigumu sana kubadilika kwa kuanzia ndani yetu wenyewe. Unaendelea kufanya kile ulichozoea, na ni vigumu kujaribu vitu vipya, kwa sababu huna uhakika wa matokeo, na kile ulichozoea kufanya tayari kinakupa matokeo fulani.
Hivyo ili kubadilika kutoka kwenye mazoea, kunahitajika nguvu kubwa mbili;
Nguvu ya kwanza ni kutoka ndani yako, kuwa na hamasa kubwa ya kutoka pale ulipo sasa na kufanya makubwa zaidi.
Nguvu ya pili ni kutoka nje, ambapo mazingira yanakulazimisha ubadilike.
Sasa nguvu ya ndani huwa siyo kubwa sana kwa wengi, na hivyo kitu pekee kinachoweza kuwasukuma watu kuchukua hatua ni nguvu ya nje, tena nguvu hiyo iwe kubwa sana, ambayo inaweza kuchochea nguvu ya ndani nayo kukazana kupata mabadiliko.
Na hapo ndipo manyanyaso na mateso yanapofanya kazi. Yanakusukuma kubadilika kwa nje, kufukuzwa nyumbani, kufukuzwa kazi, kunyimwa chakula, yote hayo yanakulazimisha uangalie njia mbadala. Lakini pia yanachochea nguvu ya ndani ya kutaka kubadilika, hapo unapata hasira, kudhalilika na kuamua kwamba umechoka na aina hiyo ya maisha ya mateso na manyanyaso.
Hali hii inakufanya uone huna namna nyingine zaidi ya kuchukua hatua, na unapochukua hatua, hutakuwa na hofu ya kushindwa, kwa sababu unajua ni bora ujaribu ushindwe kuliko usijaribu kabisa.
Unapokuwa huna pa kula wala kulala, ukiitiwa kazi yoyote utafanya, wala hutasema kwamba hiyo siyo hadhi yako. Lakini kama upo nyumbani, au kwa ndugu, ambapo unakula na kulala vizuri, iwe unafanya kazi au la, utakuwa mtu wa kuchagua sana kazi, kwa sababu huna cha kukusukuma kuchukua hatua. Sijui unaanza kuipata picha rafiki?
Hivyo kaa chini na tafakari kwa kina, angalia watu wote ambao wamewahi kukunyanyasa, kukutesa au hata kukunyima kitu ambacho ulikitaka sana. Angalia hamasa uliyoipata baada ya tukio lile, na hatua kubwa ulizoweza kuchukua kwenye maisha yako. Ona kama huna sababu ya kushukuru kwenye hilo.
Unaweza kufikiria lakini asingeninyanyasa au kunitesa, ningefanikiwa zaidi ya nilivyofanikiwa sasa. Huo ni uongo. Na ukitaka kudhibitisha mwenyewe, angalia wale waliokuwa kwenye hali kama zako lakini hawakunyanyaswa wala kuteswa.
Kama ulifukuzwa kazi kwa uonevu na kuamua kwenda kujiajiri, angalia wale wenzako ambao uliwaacha kazini, utashangaa wanaokuonea wivu kabisa. Yaani wewe unakuwa umepiga hatua kuliko wao.
Kama ulifukuzwa nyumbani, angalia wenzako ambao waliendelea kukaa nyumbani, utakuta wewe umepiga hatua kubwa kuliko wao. Tena wengine wanaweza kuwa wazembe zaidi kuliko wewe.
Hii ndiyo sababu nakutaka leo rafiki yangu, kama yupo yeyote ambaye amewahi kukunyanyasa au kukutesa kwenye maisha yako, mshukuru sana. Huyu amekusaidia wewe kuchukua hatua muhimu kwenye maisha yako, ambapo bila yeye huenda usingepata hamasa ya kutosha ya kuchukua hatua hizo.
Na kama una kinyongo chochote na watu wa aina hiyo, wasamehe mara moja.
Maisha yangu binafsi nimekuwa napiga hatua kutokana na manyanyaso na hata kukataliwa. Nimeweza kufanya mambo mengi makubwa baada ya kukosa namna au kukataliwa kitu ambacho nilikuwa nahitaji sana.
Kila jambo ambalo nimeweza kufanya kwenye maisha yangu, kuna mchango wa wengine katika kuninyima kitu au kuninyanyasa kwenye kitu fulani. Hivyo mara zote huwa nawashukuru sana watu hao.
Kama nisingefukuzwa chuo kikuu mwaka 2011, leo hii wewe usingenijua, ningekuwa ni daktari sehemu fulani huko ambaye anatibu wagonjwa wake na kusubiri mshahara uingie na maisha yaendelee. Lakini baada ya kufukuzwa, nililazimika kuchukua hatua ambazo huenda nisingekuja kuzichukua iwapo mambo yangeenda bila ya msukosuko. Na mara zote huwa nashukuru sana tukio lile la kufukuzwa, kwa sababu limeniwezesha kuingia ndani zaidi na kujua kumbe ndani yangu kuna mengi na makubwa kuliko niliyokuwa nimefundishwa miaka yote ambayo nimekuwa kwenye mfumo wa elimu.
Hivyo rafiki, shukuru kila mtu na kila tukio ambalo limewahi kutokea kwenye maisha yako. Lina mchango mkubwa kwa hapo ulipo sasa.
SOMA; Chanzo Kikuu Cha Maumivu Ya Ndani Tunayopitia Kwenye Maisha Yetu.
Kwa upande wa pili, kama baada ya kunyanyaswa au kuteswa ulikata tamaa na maisha yako yakawa mabovu zaidi, amka sasa na chukua hatua ya maisha yako. Usiendelee kuwalaumu na kulalamika kwamba wengine wamekuharibia maisha, hakuna wa kukuharibia maisha yako ila wewe mwenyewe.
Pia kama kuna mtu anakunyanyasa au kukutesa sasa, usikubali kuwa mwenye hatia, badala yake chagua kuchukua hatua, chagua kushika hatamu ya maisha yako, kutokuruhusu mtu aweze kukufanyia vile atakavyo. Fanya hivyo siyo kwa hasira juu yake au kutaka kumwonesha kwamba na wewe unaweza, bali kama njia ya kujenga maisha yako kuwa imara zaidi.
Mambo yakienda vizuri, sisi binadamu tuna tabia ya kuzoea na kujisahau, tunahitaji manyanyaso, mateso na kukataliwa mara kwa mara ili tukumbuke kuchukua hatua na kuwa huru zaidi.
Kama umejifunza kupitia makala hii karibu tujifunze zaidi kupitia KISIMA CHA MAARIFA, ambapo utaingia kwenye kundi la wasap na kupata mafunzo kila siku. Bonyeza maandishi haya kujiunga na KISIMA CHA MAARIFA.
Kwa kupata vitabu vya biashara na mafanikio tembelea www.kisimachamaarifa.co.tz/vitabu
Yafahamu Mambo Muhimu Ya Kuzingatia Kabla Hujauza Nyumba Yako.
USHAURI; Mambo Ya Kuzingatia Kama Unataka Kurudi Shuleni Ili Kukamilisha Ndoto Zako.
One thought on “Mshukuru Sana Yeyote Ambaye Amewahi Kukunyanyasa, Bila Yeye Huenda Usingepiga Hatua.”
Pingback: Maneno Manne (04) Unayopaswa Kutumia Ili Kutengeneza Mahusiano Bora Na Kufikia Mafanikio Makubwa. – AMKA MTANZANIA
Hawa Ndiyo Walengwa Wakuu Wa SEMINA YA KISIMA CHA MAARIFA 2018, Kama Ni Mmoja Wao Chukua Hatua Sasa. September 20, 2018
Huu Ndiyo Uwekezaji Unaolipa Kwa Riba Kubwa Duniani September 20, 2018
Maswali Sita Ya Kujiuliza Kila Siku Kuhusu Biashara Yako Ili Kuepuka Kupotea Kibiashara. September 19, 2018
Maeneo Manne Muhimu Ya Kufanyia Kazi Kwenye Maisha Yako Ili Uweze Kufikia Ndoto Zako Kubwa. September 18, 2018
USHAURI; Jinsi Ya Kuzuia Changamoto Za Kifedha Zisizuie Mipango Yako Na Uwekezaji Wa Kufanya Unapokuwa Mbali Na Nyumbani. September 17, 2018
Maeneo Manne Muhimu Ya Kufanyia Kazi Kwenye Maisha Yako Ili Uweze Kufikia Ndoto Zako Kubwa.
Huu Ndiyo Uwekezaji Unaolipa Kwa Riba Kubwa Duniani
Maswali Sita Ya Kujiuliza Kila Siku Kuhusu Biashara Yako Ili Kuepuka Kupotea Kibiashara.
#TANO ZA JUMA #37 2018; Jinsi Ya Kununua Wateja Kwenye Biashara Yako, Hatua Nane Za Kutoka Chini Mpaka Mafanikio Makubwa, Jinsi Ya Kuongeza Kipato Chako Kila Mwezi Na Kama Hujisikii Vizuri Ni Tatizo Lako.
Hawa Ndiyo Walengwa Wakuu Wa SEMINA YA KISIMA CHA MAARIFA 2018, Kama Ni Mmoja Wao Chukua Hatua Sasa.
Uchambuzi Wa Kitabu; The Most Successful Small Business In The World (Kanuni Kumi Za Kuwa Na Biashara Ndogo Yenye Mafanikio Makubwa.)
BIASHARA LEO; Kuuza Vitu Vya Kawaida Kwa Watu Wa Kawaida…
UKURASA WA 1359; Ni Jukumu Lako, Lipokee Na Songa Mbele…
#TAFAKARI YA LEO; MAISHA NA KIFO…
BIASHARA LEO; Kujenga Imani Ya Wateja Kwenye Bei…
UKURASA WA 1358; Kuwasiliana Na Kupiga Kelele…
BIASHARA NA UJASIRIAMALI (204)
FEDHA NA UWEKEZAJI (95)
KUTOKA KWA KOCHA MAKIRITA (121)
MAFANIKIO NA HAMASA (1,206)
TANO ZA JUMA (34)
USHAURI (145)
Makala Za Zamani Select Month September 2018 (26) August 2018 (40) July 2018 (39) June 2018 (35) May 2018 (23) April 2018 (23) March 2018 (21) February 2018 (22) January 2018 (25) December 2017 (23) November 2017 (28) October 2017 (29) September 2017 (30) August 2017 (31) July 2017 (36) June 2017 (32) May 2017 (32) April 2017 (27) March 2017 (20) February 2017 (20) January 2017 (22) December 2016 (19) November 2016 (22) October 2016 (31) September 2016 (26) August 2016 (20) July 2016 (21) June 2016 (21) May 2016 (19) April 2016 (17) March 2016 (14) February 2016 (19) January 2016 (19) December 2015 (20) November 2015 (28) October 2015 (32) September 2015 (34) August 2015 (32) July 2015 (38) June 2015 (42) May 2015 (46) April 2015 (53) March 2015 (44) February 2015 (30) January 2015 (52) December 2014 (45) November 2014 (50) October 2014 (87) September 2014 (67) August 2014 (25) July 2014 (25) June 2014 (30) May 2014 (22) April 2014 (30) March 2014 (23) February 2014 (13) January 2014 (23) December 2013 (16) November 2013 (13) October 2013 (19) September 2013 (25) August 2013 (41) July 2013 (61) June 2013 (7) May 2013 (2) April 2013 (1) March 2013 (1)
| 2018-09-20T22:08:48 |
https://amkamtanzania.com/2017/09/17/mshukuru-sana-yeyote-ambaye-amewahi-kukunyanyasa-bila-yeye-huenda-usingepiga-hatua/
|
[
-1
] |
MATUKIO @ MICHUZI BLOG: KAMPENI YA BINTI WA KITAA YAZINDULIWA RASMI ENEO LA PAKACHA KATA YA TANDALE JIJINI DAR
KAMPENI YA BINTI WA KITAA YAZINDULIWA RASMI ENEO LA PAKACHA KATA YA TANDALE JIJINI DAR
Mkurugenzi Mtendaji wa (CVF) Ndg. George David maarufu kwa Ambassador Angelo akizindua rasmi kampeni ya Binti wa Kitaa
Zawadi Mansende akizungumzia anayesoma Shule ya Sekondari ya Manzese Kidato cha Tatu akizungumzia changamoto mbalimbali wanazokutana nazo kama wasichana wa mtaani ikiwa ni pamoja na kurubuniwa na Vijana jambo linalowapelekea kukumbia majumbani mwao na wengine kupata Mimba za utotoni, wakati wa uzinduzi Rasmi wa Kampeni ya Binti wa Kitaa.
ya Mabinti waliokati ya umri wa miaka 14 na kuendelea wakiwa wanafuatilia kwa makini uzinduzi wa Kampeni ya Binti wa Kitaa iliyofanyikia Tandale Baadhi ya waliofanikisha uzinduzi wa Kampeni ya Binti wa Kitaa wakiwa wanaonesha #tag Binti ya Kitaa.
Baadhi ya wadau na Mabinti wa Kitaa wakiwa katika uzinduzi huo
Bwana Godfrey Nteminyanda ambaye ni Mkurugenzi wa Applemackbooks_tz akielezea
namna alivyo ipokea kampeni hiyo na wao kuahidi kuisapoti kwa hali na mali Baadhi ya akina mama wa Tandale pamoja na waendeshaji wa Kampeni ya Binti wa kitaa wakiwa katika uzinduzi
Mama Consalva Genes Samba ambaye ni Mkazi wa mda mrefu wa Tandale akielezea namna mabinti wamekuwa wakirubuniwa na kudanganywa .
Baadhi ya wawezeshaji, na wakazi wa Tandale wakionesha Mabango ya Binti wa Kitaa
Madam Sophia Mbeyela akizungumza jambo wakati wa Uzinduzi huo Ulifika Muda wa kupata mambo ya Kitaa yaani Bagia, Vitumbua Chachandu na Ujii ilikuwa ni safi sana
Hawa ni Baadhi ya Timu ya waandaaji wa Kampeni ya Binti wa Kitaa
Hii ni timu nzima ya kitengo cha habari cha Kampeni ya Binti wa Kitaa wakiwa katika picha ya pamoja baada ya uzinduzi kuisha
Tukio likiwa linaendelea
na kuwa ni Kampeni ya Binti wa kitaa wanaume nao wamehamasika kuisapoti
mwanzo mwisho hapa wakiwa pamoja na Mabinti wengine wanaosapoti.
Picha ya pamoja .Picha zote na Fredy Njeje/Story na Mwana Libeneke wa Funguka Live Dickson Mulashani
isiyo ya kiserikali ya Community Voices In Focus (CVF) imezindua kampeni kwa jina BINTI WA KITAA eneo la Pakacha kata ya Tandale wilaya ya Kinondoni itakayodumu kwa mwaka mmoja yenye lengo la kuelimisha jamii
ili kupunguza na kuondoa tatizo la mimba pamoja na ndoa za utotoni nchini Tanzania.Akizungumza wakati wa uzinduzi huo mwanzilishi na mkurugenzi mtendaji wa (CVF) Ndg. George David amesema kama mtanzania
ameguswa na tatizo hili ambalo limedumu kwa muda mrefu katika jamii hata katika kipindi hiki cha utandawazi hivyo anaamini kupitia kampeni hii, elimu itawafikia walengwa kwa namna ya tofauti na licha ya kupunguza tatizo hili itasaidia kulimaliza kabisa."Inauma sana kuona nchi yetu inatajwa kati ya nchi 5 duniani zinazotambulika kwa janga la mimba pamoja na ndoa za utotoni, hivyo ni dhahiri kuwa huu ni wakati wa kuunganisha nguvu na kuhakikisha mabinti kwenye jamii yetu wanafikia malengo yao kwa wakati husika na sii vinginevyo" alisema George.BINTI WA KITAA imelenga mabinti kuanzia umri wa miaka 12
hadi 17 sio tu kwa wale waliopo shuleni bali hata wale waliopo mitaani na inatarajiwa kuzuru mikoa zaidi ya 10 nchini huku ikiwa na agenda ya kuwafikia mabinti katika mitaa wanayoishi ili kuwapa fursa hata wazazi kuweza kushiriki katika kuwa sehemu ya ukombozi wa binti wa Kitanzania.
kuwa kwa kiasi kikubwa changamoto zinazowapelekea mabinti kupata mimba na kuolewa zipo katika jamii hasa mitaani,hii ndio iliyosababisha kampeni hii kuzinduliwa mtaa wa Pakacha Tandale kwani.Kadhalika mmoja kati ya mabinti waliohudhuria katika uzinduzi huo Zawadi Isihaka ameomba wazazi kufuatilia maendeleo na kuwa karibu na watoto wao ili kuweza kuyagundua mapema mabadiliko ya tabia pamoja na kuwapa elimu ya makuzi sambamba na kutokuwa wakali kupitiliza kwa lengo la kujenga mahusiano mazuri.Uzinduzi huo ulihudhuriwa na wadau mbalimbali ikiwemo waratibu wa eneo ambao ni Tandale Youths, Applemacbooks Company,wakazi wa eneo la Pakacha ,Tandale, waandishi wa habari pamoja.Sambamba
na uzinduzi huo katika kata ya Tandale,Ndg. George David ametoa wito kwa Watanzania wote kuunga mkono kampeni hii ili kuweza kuwasaidia mabinti kwani ni wazi kuwa hili limekuwa sehemu kubwa ya kuzalisha wimbi
kubwa la watoto wa mitaani, vifo wakati wa kujifungua, athari za kisaikolojia na kiuwanyima mabinti nafasi ya kupata haki yao ya msingi ya elimu. Posted by
| 2017-04-23T21:36:38 |
https://michuzi-matukio.blogspot.com/2016/10/kampeni-ya-binti-wa-kitaa-yazinduliwa.html
|
[
-1
] |
Zilivyo balozi mbalimbali za Tanzania huko ng'ambo - Aibu tupu! | JamiiForums | The Home of Great Thinkers
Zilivyo balozi mbalimbali za Tanzania huko ng'ambo - Aibu tupu!
Discussion in 'Jukwaa la Siasa' started by Tungaraza Jr, Aug 24, 2012.
*Baadhi hawajalipwa mishahara miezi sita, zimeajiri Wakenya*Ufaransa pango Sh milioni 720, wanatumia anwani ya Uganda*Ofisi zinaporomoka, Kikwete asema Richmond imeiponza nchi*Membe alia Serikali kukata bajeti yake ikabaki asilimia 44 tu
Mishahara ya mabalozi
Taarifa ya Kamati inaonyesha kuwa baadhi ya balozi za Tanzania nje ya nchi, watumishi na mabalozi wanaishi kwa kudra za Mwenyezi Mungu. "Hadi wajumbe wanafanya ziara katika Ubalozi huu [Stockholm, Sweden], watumishi wa Serikali walikuwa wamepata mishahara yao hadi kufikia Machi na hawakuwa wamepata mishahara ya miezi mitatu wakati wajumbe wa Kamati wanaondoka Stockholm tarehe 29 Juni, 2012," inasema sehemu ya taarifa hiyo.
"Hakuna jengo la Serikali kwa ajili ya ofisi na nyumba za watumishi, hivyo umepangishwa (ubalozi) na Uganda pamoja na kutumia sanduku la posta la Uganda. Hata mkalimani anayetumika ni Mkenya," inasema taarifa hiyo iliyosainiwa na Makamu Mwenyekiti, Mussa Zungu.
Baada ya kuona shida wanayopata watumishi wa Ubalozi wa Tanzania, New Zealand iliamua kuiuzia Tanzania jengo inalolimiliki nchini Ufaransa kwa bei nafuu, lakini Serikali ya Tanzania haijatoa jibu iwapo italinunua jengo hilo au la na ifikapo mwezi ujao wa Septemba, ofa hiyo itafutika. "Ubalozi umekuwa ukiathirika na gharama kubwa unayotumia kwa ajili ya kodi ya kupanga ofisi na nyumba sita za watumishi. Hali hii huugharimu ubalozi kiasi cha euro 31,435.40 (Tshs 59,727,260) kwa mwezi ambazo ni sawa na Th 716,727,120 kwa mwaka na ni asilimia 34 ya bajeti ya ubalozi," inasema sehemu ya taarifa hiyo.
Hapa kuna tatizo la uwakilishi mpana, Kamati imependekeza kuwa ufunguliwe ubalozi nchini Cuba badala ya kutegemea Ubalozi wa Canada. Pia kuna tatizo la Watanzania wanaofanya kazi ubalozini kulipishwa kodi, ila hii imetokana na Tanzania kuwalipisha kodi watumishi wa Ubalozi wa Canada waliko Tanzania, hivyo nchi hiyo inasema mabalozi wao nao wakiacha kulipishwa kodi nao wataacha kuwalipisha kodi watumishi wa Ubalozi wa Tanzania.
Jengo Na 2139 R Street, NW Washington DC, linalomilikiwa na Serikali jijini Washington, limeendelea kuchakaa kwa Serikali kutotoa ruhusa likarabatiwe. Hadi sasa wamejitokeza wapangaji wenye nia ya kupanga katika jengo hilo ambao wangelipa wastani wa kodi ya dola 400,000 kwa mwaka, karibu Sh milioni 600 za Tanzania, lakini kwa mwaka mzima sasa Serikali imeshindwa kutoa uamuzi wa kuwakubalia wapange jengo hili linaloendelea kuoza. Pia ubalozi huu una kashfa ya kuajiri Watanzania ‘waliojilipua' nchini Marekani kama watumishi wenyeji. "Kuna watumishi wenyeji (local based) ambao ni Watanzania waliozamia nchini humo [Marekani] kitu ambacho ni kinyume cha sheria," inasema taarifa hiyo.
Kwenye ubalozi huu kuna tatizo la kukosa ruhusa ya kutumia maduhuli wanayokusanya. Nyumba ya Balozi wa Tanzania UN 30 Overhill Road, Mount Venon, ina hali mbaya kiasi kwamba haikaliki. Kamati imeshauri ikarabatiwe haraka. Kamati imeishauri Serikali kununua nyumba ambayo kwa sasa Ubalozi wa Tanzania unapanga inayouzwa Na. 86 Judson Avenue, Dobbs Ferry, New York. Kwa kuwa katika Umoja wa Mataifa kuna masuala mengi, Kamati imependekeza kila wizara hapa nchini iwe na dawati la Umoja wa Mataifa litakalosaidia kuratibu shughuli za umoja huo.
Katika ubalozi huu kuna tatizo sawa na balozi nyingine wakati jengo la ubalozi limechakaa sehemu kubwa inavuja na lina nyufa. Pia sheria ya China inataka gari liendeshwe si zaidi ya miaka 10, lakini ubalozi unatumia gari lililonunuliwa mwaka 2001 hivyo Tanzania inavunja sheria kwa balozi kuendesha gari chakavu. Pamoja na umuhimu wa pekee ilionao China katika uchumi wa dunia ya sasa, hadi leo hakuna Mtanzania mtaalamu wa masuala ya uchumi anayefanya kazi katika ubalozi huu. Kamati inapendekeza mtu huyu ateuliwe haraka. Kamati pia inashauri kutokana na China kuwa na fursa nyingi za kiuchumi, Balozi wa Tanzania nchini China awe na wasaidizi wawili huku ikipendekeza uanzishwe Ubalozi Mdogo katika mji wa viwanda wa Guang-zhou. China pia imeipa Tanzania fursa ya kulipia ada wanafunzi 100 ikiwa Tanzania itaamua kusomesha idadi kama hiyo. Kamati imeishauri Bodi ya Mikopo kutumia fursa hiyo kwa kupeleka Watanzania masomoni China (scholarships).
Ubalozi huu una uhaba wa magari na watumishi. Lakini pia wana tatizo la msingi: "Ubalozi unapoomba taarifa na ufafanuzi wa masuala muhimu kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa hukosa taarifa hizo au kupata kwa kuchelewa," inasema taarifa ya kamati. Hili ni tatizo sugu kwa balozi karibu zote. Pia kuna tatizo kuwa asasi za kiraia za Japan zilitoa msaada wa kompyuta 1,000 kwa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) na magari ya wagonjwa kwa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, isipokuwa Serikali hadi sasa haijarudisha ‘export certificate' kuonyesha kuwa msaada huo uliwafikia walengwa, hali inayowatia shaka Wajapani kudhani kuwa labda uliyeyukia njiani. Kamati imeona fursa na inapendekeza Tanzania ianze mara moja mkakati wa biashara na nchi hii.
Ubalozi umeshindwa kulipa ankara za umeme, maji, gesi, simu na matibabu hadi kufikia hatua ya kukatiwa huduma hizo. Maafisa wa ubalozi wameanza kujilipia ankara hizo bila kurejeshewa. Pia katika kile kinachoonyesha kuwa aibu kwa taifa, ubalozi umeshindwa kulipa deni la kampuni ya ulinzi hadi ukaandikiwa barua na wakili wa kampuni hiyo inayotaka kuushitaki ubalozi mahakamani kwa kulimbikiza deni.
Mbali na hati za utambulisho kwa nchi ambazo Balozi wa Tanzania nchini India analiwakilisha taifa, kuna tatizo la mawasiliano duni kati ya Ubalozi na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Majengo ya kisasa ya ubalozi yaliyoanza kutumika mwaka 2007 hadi sasa hayajatengewa fedha kwa ajili ya kuyafanyia ukarabati kwa miaka mitatu mfulululizo. Kamati imependekeza ubalozi uwezeshwe kifedha.
Mbali na kucheleweshwa kwa kibali cha kutumia fedha zinazotokana na mauzo ya viza, ubalozi una kiwanja Na. 19 Denewood Road, N64AQ kilichotelekezwa katikati ya Jiji la London. "Sasa hivi Serikali ya Uingereza inaweza kukichukua kiwanja hicho, kwani kinahatarisha usalama wa wananchi wa eneo husika kwa jumla," inasema taarifa hiyo. Pia Serikali imetakiwa kufanyia matengenezo nyumba Na. 6 Colindeep Gardens, NW4 4RU ambayo nayo imetelekezwa kwa sasa haitumiki kabisa.
Mwakani meli ya mv Liemba inayofanya kazi katika Ziwa Tanganyika inatimiza miaka 100. Ujerumani imejitolea kuikarabati, lakini haipati mwitikio wowote kutoka Tanzania, hali inayowakatisha tamaa kuwa huenda Tanzania haihitaji msaada huo. La kushangaza hata kiwanda cha saruji cha Wazo Hill kimejitolea kutoa msaada wa euro milioni 2.5 kwa ajili ya ukarabati wa meli hiyo, lakini Serikali imeukataa msaada huu.
Ofisi na nyumba ya Balozi wa Tanzania vipo katika jengo la Serikali ya Urusi lililojengwa mwaka 1886. Tanzania ilianza kutumia jengo hili mwaka 1964 na hadi leo halijawahi kufanyiwa ukarabati. Ubalozi unadaiwa deni kubwa la pango katika jengo hili. "Kwa sababu hiyo hali ya jengo ni mbaya sana kiasi kwamba ilitokea katika Ofisi ya Ubalozi, udongo wa dari (concrete) wenye uzito wa nusu tani ulianguka ofisini kwa balozi na kuacha nondo zote zikiwa wazi," inasema taarifa hii. Pendekezo la ubalozi ni kununua jengo lililopo jirani na ubalozi lenye ghorofa sita kwa wastani wa dola milioni 10 (sh bilioni 16), ambalo wao watatumia ghorofa mbili na nyingine kupangishwa.
Nukuu kutoka kwenye gazeti la JAMHURI
Tungaraza Jr, ulichoandika ni "facts"; baada ya wewe kuzipitia nini maoni yako? Tuache kujenga barabara tuboreshe hadhi za balozi zetu au tuendelee kuwakopa walimu na madaktari ili wafanyakazi wa balozi waishi kifahari? Mimi kwa maone yangu kuna haja ya kupunguza balozi zetu. Badala ya kuwa na balozi kwa kila nchi inayotumia sarafu ya Euro, tunaweza kuwa na ofisi moja katika makao makuu EU; Canada na USA tunaweza kuwa na ofisi moja; Bara la Amerika ya kusini tukawa na ofisi moja. Nchi za Afrika ya Mashariki hakuna haja ya kuwa na ubalozi kwani masuala yote ya Kidiplomasia yanaweza fanyika kupitia East Africa Community.
Kuhusumu kumiliki majengo, umesema kiasi kinacholipwa lakini hukusema gharama (running costs) za kumiliki majengo + gharama ya kununua jengo
Ni aibu sana kwa Tanzania.
Nilipata pale Ottawa kwenye ubalozi wetu kwa nje yaani utafikiri nyumba ambayo imetelekezwa miaka mingi iliyopita.
Halafu cha kufadhaisha zaidi ni kwamba sehemu hiyo ina balozi nyingi za Afrika zimekaa sehemu moja ukisogea mbele kidogo kuna ubalozi wa kenya ambao unamiliki jengo kubwa zuri. Mimi naona hizi balozi nyingine tuzifunge tu.
Halafu cha kufadhaisha zaidi ni kwamba sehemu hiyo ina balozi nyingi za Afrika zimekaa sehemu moja ukisogea mbele kidogo kuna ubalozi wa kenya ambao unamiliki jengo kubwa zuri. Mimi naona hizi balozi nyingine tuzifunge tu.Click to expand...
Mkuu Maundumula nenda pale wizara ya uchukuzi ukaone jinsi ofisi ilivyominywa na Vi "partition"; kama wanaoteuliwa wanatoka kwenye viofisi vya aina hiyo watapata wapi mawazo ya kuboresha ofisi huko ughaibuni?
Kuhusumu kumiliki majengo, umesema kiasi kinacholipwa lakini hukusema gharama (running costs) za kumiliki majengo + gharama ya kununua jengoClick to expand...
We need to understand the concepts of Costs sir! Kwa maoni uliotoa ni haki kabisa kua na ubalozi katika nchi ambazo ni very potential to us kwa kuweka wazi kua Botwana, namibia, Swaz zote ubalozi husika ni ule utakakua na makao makuu SA. Huu ni mfano tu bro.
Ila wale ndugu na jamaa zao, wanajeshi waliostaafu, marafiki wa shule na wabunge alioshindwa katika chaguzi (James Msekela-Italy). Hii NDIO HOFU KWAO kama kweli cost is on the tips of their fingures.
Hebu fananisha na ule wa BANGLADESH ulioko Tanzania, that is the image of Tanzania abroad rit?
Hebu fananisha na ule wa BANGLADESH ulioko Tanzania, that is the image of Tanzania abroad rit?Click to expand...
Imagine Mzungu ambaye yupo huko nje anafikiria between kuitembelea Tanzania au Kenya ameambiwa nchi zote mbili ukiwepo unaweza kufika Serengeti au Kilimanjaro. Anaenda kwenye ofisi za ubalozi zote mbili kuomba maelezo ya Visa. Obviously hawezi kuja bongo.
Imagine Mzungu ambaye yupo huko nje anafikiria between kuitembelea Tanzania au Kenya ameambiwa nchi zote mbili ukiwepo unaweza kufika Serengeti au Kilimanjaro. Anaenda kwenye ofisi za ubalozi zote mbili kuomba maelezo ya Visa. Obviously hawezi kuja bongo.Click to expand...
Na ndio maana wengi hutua Kenya ili kuupanda Mlima Kilimanjaro. Sasa napata picha na kwa nini budget ni 70% reccurent expenditure. Inaelekea wapi sasa?
wanasubiri watoto wao wamalize shule za kuunga unga huku ughaibuni ndio wakashike nafasi hizo........halafu ndio pesa zitumwe kikamilifu....damn!
nani alaumiwe?????
wizara ya mambo ya nje iko wapi???
Eti...mishahara yao huko 'balozini' ni kama ya kwetu huku?
Atakua mpuuzi mzungu huyo,maana info zote zipo online na pia kuna mawakala mbali mbali wanao toa recomm.. kwa watalii,So hiyo sio issue, serekali inavitu vya muhimu ambavyo inahitaji kuvikamilisha kwa sasa kabla hata ya kukimbilia huku na kuja kuwapa wala fedha za umma mapango ya kujificha.
Atakua mpuuzi mzungu huyo,maana info zote zipo online na pia kuna mawakala mbali mbali wanao toa recomm.. kwa watalii,So hiyo sio issue, serekali inavitu vya muhimu ambavyo inahitaji kuvikamilisha kwa sasa kabla hata ya kukimbilia huku na kuja kuwapa wala fedha za umma mapango ya kujificha.Click to expand...
Seeing is believing, mtu anaishi Ottawa down town 10 minutes walk aanze kuhangaika wakati ubalozi upo hapo hapo mjini. Sidhani kama Tanzania inatoa Visa online.
Hizo balozi zina kazi gani hasa zaidi ya kuendeleza uwizi wa wakubwa?
zifungwe tu hazina tofauti na wakuu wa wilaya na mikoa
kazi kweli kweli jamani,balozi ambazo hazina tija na maslahi kwa taifa hili zifungwe kwani ni hasara kuziendesha ukilinganisha na faida tunayopata kutoka mataifa hayo.
| 2017-01-19T21:51:03 |
https://www.jamiiforums.com/threads/zilivyo-balozi-mbalimbali-za-tanzania-huko-ngambo-aibu-tupu.312552/
|
[
-1
] |
Mkutano wa Kampeni wa CCM Waandaliwa na Halmashauri (W) Serengeti! | JamiiForums | The Home of Great Thinkers
Mkutano wa Kampeni wa CCM Waandaliwa na Halmashauri (W) Serengeti!
Discussion in 'Uchaguzi Tanzania' started by Buchanan, Sep 29, 2010.
Bado kuna watumishi wa uma wasiojua wanawajibika kwa nani, hawajui tofauti ya serikali na chama, hawawezi kutofautisha mali za uma na mali za chama.
Wengine wanafanya vitendo hivyo kujipendekeza tu.
Tatizo hili lipo kuanzia ngazi za chini kabisa za serikali hadi juu kabisa na wanahitaji kukemewa na kuwajibishwa ili kuendeleza na kudumisha demokrasia hapa nchini.
Matumizi ya rasilimali za uma kwa upendeleo wa kikundi chochote kile kiwe cha kisiasa au cha kijamii ni kosa kubwa na ni muendelezo wa ufisadi ambao madhara yake tunayaona na makali yake yatazidi kuonekana na kuwatesa watoto wetu na vizazi vijavyo.
Tunahitaji kuliangalia jambo hili kwa mtazamo wa mbali zaidi ya uchaguzi wa mwaka huu!
Kila mtanzania kwa nafasi yake anatakiwa achukue hatua za makusudi kabisa kuhakikisha vitendo vya kuturudisha nyuma kidemokrasia havipati tena nafasi na badala yake tunajenga jamii ya watu walio sawa kwa uhuru wa kisiasa na kiuchumi kwa kupewa fursa sawa na wale waliopewa dhamana ya kusimamia taasisi za uma.
Chadema iishitaki ccm kwa nec na tuone nec inafanya nini..............................
Kila mtanzania kwa nafasi yake anatakiwa achukue hatua za makusudi kabisa kuhakikisha vitendo vya kuturudisha nyuma kidemokrasia havipati tena nafasi na badala yake tunajenga jamii ya watu walio sawa kwa uhuru wa kisiasa na kiuchumi kwa kupewa fursa sawa na wale waliopewa dhamana ya kusimamia taasisi za uma.Click to expand...
Mkuu you have nailed it, unajua kuna watu hata wakisoma habarik hii kwenye gazeti wataanza kulishangaa gazerti na hata kufika hatua ya kuona gazeti linamsakama JK. It is true this is beyond uchaguzi huu, na kama unakumbuka Mtikila aliwahi kutoa ufafanuzi wa mambo haya kwa kirefu in 1995 wakati ule kasi ya Mrema imepamba moto. Very few did pay attention and see mpaka leo we are still haunted!
| 2016-12-08T22:16:19 |
http://www.jamiiforums.com/threads/mkutano-wa-kampeni-wa-ccm-waandaliwa-na-halmashauri-w-serengeti.75828/
|
[
-1
] |
Swahili na Waswahili: EXTRA BONGO NEXT LEVEL YAWAAGA WAPENZI NA WASHABIKI WAKE KWA SHOW KALI ILIYOSINDIKIZWA NA MATONYA, Q CHIF NA CHID BENZ NDANI YA UKUMBI WAO MPYA NEW WHITE HOUSE - KIMARA KOROGWE JIJINI DAR ES SALAAM
EXTRA BONGO NEXT LEVEL YAWAAGA WAPENZI NA WASHABIKI WAKE KWA SHOW KALI ILIYOSINDIKIZWA NA MATONYA, Q CHIF NA CHID BENZ NDANI YA UKUMBI WAO MPYA NEW WHITE HOUSE - KIMARA KOROGWE JIJINI DAR ES SALAAM
| 2017-09-24T13:51:41 |
http://swahilinawaswahili.blogspot.com/2012/07/extra-bongo-next-level-yawaaga-wapenzi.html
|
[
-1
] |
Viwanja vya ndege kutozwa faini - BBC Swahili
Viwanja vya ndege kutozwa faini
http://www.bbc.com/swahili/habari/2010/12/101220_viwanja_faini
Serikali ya Uingereza inafikiria kuyatoza faini makampuni yanayomiliki viwanja vya ndege, ikiwa safari za ndege zitasimamishwa kwa sababu hayakujiandaa vya kutosha kukabiliana na hali mbaya ya hewa.
Image caption Baadhi ya wasafiri waliokwama Heathrow
Waziri wa uchukuzi wa Uingereza Philip Hammond, alisema hayo, alipohojiwa na gazeti la Sunday Times, baada ya theluji na barafu, kufunga uwanja mkubwa kabisa wa ndege wa London, Heathrow, ambapo safari za ndege zilisimamishwa na wasafiri walilazimika kulala sakafuni katika jumba la uwanja huo.
Naye Waziri wa safari za anga, Theresa Villiers, amesema viwanja vya ndege vinahitajika kufanya kazi zake inavyotakiwa na kujiandaa ipasavyo.
Heathrow, moja ya viwanja vya ndege vikubwa duniani vyenye kupokea abiria wengi kila siku, kiliathirika zaidi wiki iliyopita kutokana na theluji nyingi kuanguka nchini Uingereza na kampuni inayoendesha uwanja huo, BAA, ilituhumiwa kushindwa kuwekeza vya kutosha katika zana za kuondoa theluji.
BAA, yenyewe inayofanya uchunguzi kubaini wapi palikwenda mrama, imesema inaafiki sheria hiyo mpya ili kuwapatia abiria huduma nzuri.
| 2017-12-15T18:26:47 |
http://www.bbc.com/swahili/habari/2010/12/101220_viwanja_faini
|
[
-1
] |
Gökçek Inatoa Marejeleo ya Vijito vya Güvenpark Minibus | RayHaber | raillynews
NyumbaniTURKEYMkoa wa Anatolia wa KatiAnkara ya 06Mapendekezo ya kura ya maoni ya Güvenpark Minibus inakoma kutoka Gökçek
Mapendekezo ya kura ya maoni ya Güvenpark Minibus inakoma kutoka Gökçek
24 / 02 / 2017 Ankara ya 06, RAILWAY, GENERAL, KENTİÇİ Reli Systems, Mifumo ya Magurudumu ya Tiro, Metro, TURKEY
Mapendekezo ya kura ya maoni ya Guvenpark Minibus Anashuka kutoka Gokcek: Meya Mjini Melih Gokcek, Manispaa ya Mjini Metropolitan, Meih Gokcek, Guvenpark mabasi ya kusimama chini ya ardhi, juu ya shamba la kijani kwenye shamba la kijani la mradi aliulizwa kujenga kituo cha kupigia kura.
Meya Gökçek alisema, gelince Wakati Subway Keçiören inakuja Crescent Red, je, mahali hapa watafutiwa? Hiki kiliondolewa. Je, ni tukio mbaya la kuchukua basi ya mabasi chini na kuifanya upande wa juu eneo kubwa la kijani na kuongezea kwenye kijani baada ya kuchimba? Ikiwa kazi ya Subway inachukua miezi 3, basi tutaingia. Nadhani tunaweza kumaliza katika miezi 6. Tutaisha hapa kwa sauti, "alisema.
Meya Gökçek, kwenye Radio Trafik, iliyopangwa na Elvan Palaşoğlu na Mwandishi wa habari Deniz Gürel, waliunganishwa kwenye mjadala wa ına Güvenpark katika kila kipengele "mpango uliohudhuriwa na Emre Sevim, Rais wa Tawi la Ankara la Chama cha Wafanyakazi wa Jiji.
Katika mpango huo, Wizara ya Usafiri imepangwa kufanyika chini ya basi ya mabasi katika Subway ya Güvenpark Kecioren ya hatua ya pili ya ujenzi wa kituo hicho wakati huo huo basi ya mabasi ya kusimama mradi chini ya ardhi Rais Emre Sevim kinyume na mradi utaenda kwa mahakama ili kuizuia.
Kisha, Rais Gökçek akasema, "Rafiki, kwa nini unapinga hili? Hapa, magari haya yamekuja, 40 imekwisha kuja kwa miaka. Hivyo magari haya yanaonekana mbaya hapa? Hivyo ndio mahali pa kupasuliwa kabisa, ambapo kuna mabasi ya inapanda, ndiyo. Kwa nini unakabiliana nayo? Ikiwa unapingana na sisi, unapendekeza jinsi gani kutatua trafiki ya dolmuş katika Red Crescent, napenda kujibu kwanza?
- CHAIRMAN: FINDA KUFUTA MAJIBU "
Sevim juu ya swali la Rais Gokcek, Guvenpark Minibus Stop haina haja ya kuwa chini ya ardhi, watapinga mradi huu wa kufanywa, wakidai kwamba basi basi si usafiri wa umma kwa sababu hii, alisema kuwa trafiki ya Ankara inapaswa kuondolewa kabisa.
Rais Gökçek, Chama cha Wafanyakaziji wa Jiji la Rais wa Ankara wa TMMOB Emre Sevim walisema kuwa basi hiyo itapaswa kubadilishwa kabisa, alisema:
"Sasa hutaki subway chini, unafanya. Subway inakuja, inakuja. Je, Metro ya Keçiören inakuja Kızılay, ndiyo. Iwapo inakuja, je, mahali hapa vitafunuliwa au la? Baada ya kuchimba, kutakuwa na mapungufu yoyote juu ya mita za 30? Je! Ni tukio mbaya la kuongeza eneo kubwa la kijani kwenye bustani na kuongeza eneo kubwa la kijani kwenye bustani? No. Kwa nini unakabiliana nayo? Je! Hiyo inaweza kuwa isiyo na maana? Je, si aibu kwa watu hawa ambao hutumikia hapa, ambao hutumikia hapa?
Mheshimiwa, kazi nzuri ilikuwa kuondoa mabasi ... Hebu nenda, hebu tujadili hili mbele ya mabasi. Naam, sijui wanafanya nini. Je! Hiyo ni kweli? Kuna mabasi ya 2 ya 700 katika Ankara, itaendelea kutumika. Huna nafasi ya kuondoa hiyo hivi sasa. Je, unapoinua wakati gani? Tunauondoa mara kwa mara. Wakati barabara kuu inapoanza kufanya kazi kwenye mistari fulani, mistari hutoka moja kwa moja. Hii labda tukio ambalo litatokea baada ya miaka 30-40. Bila kuinuka na kufanya barabara kuu na kutoa usafiri muhimu, utasema kwa watu wa Dikmen, kaldır Tumeinua mabasi, kuja, kwenda kwa kutembea, kuja gelin kutembea
- "TUNAFANYA KATIKA KUTEMA KATIKA MAFUNZO YAKE
Meya Gökçek alisisitiza kuwa wanasisitiza kwamba watatambua mradi na kuendelea:
"Maoni yangu; Hebu tufanye sanduku la kura pale, fanye kura ya kura. Je, watu wanataka dolmus kuacha hapa au wanataka? Hebu tuweke sahani za 3. Unamleta mtu. Hebu tuone utambulisho wa kila mtu. Hebu tupiga kura kulingana na yeye baada ya kuona. Hebu angalia kile kinatoka ndani yake. Mimi nitashika kura ya maoni juu yako. Mwezi huu tutachukua uamuzi kutoka bunge. "
Rais Gökçek, mwandishi wa habari Deniz Gurel, wakati kura ya maoni itafanyika na mradi huo utakamilika juu ya swali la muda gani, alisema:
"Kazi hii ya ujenzi iliyopo itaenda pamoja na ujenzi wa kituo cha subway. Tutaanza kazi yetu baada ya kuanza barabara. Ikiwa kazi ya Subway inachukua miezi 3, basi tutaingia. Tunataka kuanza mwaka huu. Natumaini sisi kuanza na kumaliza. Pengine sisi kumaliza katika miezi 6. Tutaweza kutumia njia ya Kumrular kwa kuacha kama kuacha.
Tuliamua kushikilia kura ya maoni ili kufundisha vyumba vya kitaaluma na marafiki zetu. Kama neno la mwisho; Tutaisha hapa kwa sauti. "
Güvenpark Dolmuş ataacha, kuchukuliwa chini ya ardhi
Minibus huacha Mpya
Udhibiti mkali wa Minibus na Bus unasimama huko Van
Kama matokeo ya kura ya maoni, gari la cable litajengwa huko Hamburg
Rejea ya Kufanywa kwa Uwekezaji wa Reli ya Antalya Leo
Uhamisho wa minibus umekamilika Istanbul!
Minibus huondoka Istanbul, watu wa 20 'havaray' huja
Wasiliana na Meli moja kwa moja
basi ya mabasi
Usafi wa Hifadhi ya Usafiri, Mafunzo ya Kusafisha
Leo katika Historia: 25 Februari 1909 Chester Project iliyowasilishwa kwa serikali
| 2020-01-22T11:19:49 |
https://sw.rayhaber.com/2017/02/kura-ya-kura-ya-gokcekten-guvenpark-minibus-ataacha/
|
[
-1
] |
MATUKIO @ MICHUZI BLOG: WASIOENDELEZA MASHAMBA ARUMERU KUNYANG’ANYWA-MAJALIWA
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akipiga ngoma ya msanja iliyokuwa ikichezwa na wnanwake wa Arusha baada ya kuwasili kwenye kijiji cha Ondenderet wilayani Arusha Desemba 27, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifurahia burudani ya wanawake wa kimasai baada ya kuzindua mradi wa maji wa kijiji cha Ondenderet wilayani Arusha Desemba 27, 2016. kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wananchi wa eneo la Kwamrombo wilayani Arusha ambao walijipanga kwa wingi barabarani na kumshawishi kusimama ili kuzungumza nao. Alikuwa katika ziara ya mkoa wa Arusha Desemba 27, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa kizungumza na wananchi wa kijiji cha Ormapinu wilayani Arusha ambao wlijipanga kwa wingi barabarani na kumshawishi kusismama ili kuwasikiliza. Alikuwa katika ziara ya mkoa wa Arusha Desemba 27, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizundua mradi wa maji wa kijiji cha Ondenderet wilayani Arusha Desemba 27, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majliwa akimtwisha ndoo ya maji bibi Agness Silima ikiwa ni ishara ya kuzindua mradi wa maji wa kijiji cha Onderet wilayani Arusha Desemba 17, 2016.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu.
WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema Serikali itawanyang’anya ardhi wamiliki wote wa mashamba makubwa wilayani Arumeru ambao hawajayaendeleza kwa sababu wamekiuka mkataba wa umiliki.
Amesema Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mheshimiwa William Lukuvi atakuja mkoani Arusha kwa ajili ya kufanya mapitio ya mashamba yote makubwa ambayo hayajaendelezwa na kuyarudishwa Serikalini.
Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumamosi, Desemba 17, 2016) wakati akizungumza kwa nyakati tofauti na watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Arumeru na wananchi wa kijiji Bwawani na kitongoji cha Mapinu katika kata ya Nduruma akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Arusha.
“Tufanya mapitio ya kila shamba ili kujua linamilikiwa na nani na alipewa lini na tangu alipokabidhiwa amefanya nini. Shamba lisiloendelezwa litarudisha kwa wananchi. Kama mtu ameshindwa kupata mtaji kwa muda wa miaka 10 atapata leo,” amesema.
Amesema Serikali haiko tayari kuona wananchi wakinyanyaswa kwa kukosa ardhi ya kilimo kwa sababu ya watu wachache kumiliki maeneo makubwa bila ya kuyaendeleza..
"Ninataarifa kwamba hapa Arumeru kuna baadhi ya wawekezaji wanamiliki mashamba makubwa na hawajayaendeleza. Wengine wanakodisha kwa wananchi ili kujipatia fedha kinyume na mikataba yao ya umiliki. Hatutawavumilia,” amesema.
Amesema wilaya ya Arumeru inaongoza kwa migogoro ya ardhi na maeneo mengi yametwaliwa na mtu mmoja mmoja na baadhi yao wamekuwa wakilitumia vibaya Jeshi la Polisi kwa kuwanyanyasa wananchi wanaokatiza au kulima kwenye maeneo hayo.
“Kuanzia leo marufuku Jeshi la Polisi kutumiwa na mtu binafsi kuwanyanyasa wananchi. Mtafanya hivyo kama kuna uvunjifu wa amani na si vinginevyo,” amesema.
Awali, akisoma taarifa ya wilaya mkuu wa wilaya ya Arumeru Bw. Alexander Mnyeti alimweleza Waziri Mkuu kwamba wilaya hiyo ina mashamba makubwa yanayomilikiwa na wawekezaji ambayo hayajaendelezwa.
Mkuu huyo wa wilaya amesema kitendo cha kutoyaendeleza mashamba hanayo kisababisha wananchi kuyavamia hali inayochangia kushamiri kwa migogoro ya ardhi katika wilaya hiyo.
Amesema tayari ofisi yake imefanya uhakiki wa mashamba hayo na kumuomba Mheshimiwa Rais, Dk. John Magufuli kufuta hati za mashamba 12 ambayo hayajaendelezwa kwa muda mrefu.
Katika hatua nyingine Waziri Mkuu amesema Serikali imepeleka sh. bilioni 800 katika halmashauri mbalimbali nchini kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu.
Waziri Mkuu alitoa kauli hiyo wakati akizindua nyumba ya walimu na vyumba vinne vya madarasa katika shule ya sekondari ya Orjolo, hatua ambayo inalenga kuboresha mazingira ya kufanyiakazi na kupunguza changamoto ya makazi kwa walimu.
Amesema changamoto ya makazi imekuwa ikiwakabili walimu kwa mrefu hivyo Serikali imeamua kujenga nyumba za gharama nafuu ambazo zinawezesha familia sita kuishi pamoja.
Pia amewataka wazazi kuunga mkono jitihada za Serikali kwa kuboresha miundombinu ya shule na kuhakikisha wanafuatilia miendendo ya elimu kwa watoto wao.
“Tumeondoa ada na michango yote iliyokuwa inawakera na kusababisha mshindwe kuwapeleka watoto shule. Jukumu lenu kwa sasa ni kufuatilia mienendo ya watoto wenu hadi kwa walimu ili kuhakikisha wanaingia darasani na wanasoma,” amesema.
Awali, Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Dk, Wilson Mahera alisema mpango wa maendeleo ya elimu ya sekondari ya awamu ya pili (SARPCCO II) umewezesha ujenzi wa vyumba vya madarasa 4,vyoo 20 pamoja na vyumba vya madarasa 6 vyenye jumla la Sh. milioni 289.52.
| 2018-03-20T19:20:36 |
https://michuzi-matukio.blogspot.com/2016/12/wasioendeleza-mashamba-arumeru.html
|
[
-1
] |
MAMLUKI BIN ZUBEIRY YANGA SHAKEEL INVESTMENT
MAMLUKI BIN ZUBEIRY YANGA Uongozi wa Young Africans unawaomba wapenzi, wanachama na wadau wa soka kuacha kusoma habari za blog ya Bin Zubeiry kutokana na kuandika taarifa zisizokuwa na ukweli huku lengo lake kubwa likiwa ni kuhakikisha
timu ya Young Africans inafanya vibaya kwenye michezo yake na kuwavunja
moyo viongozi wake pamoja na wachezaji.
Akiongea na mtandao rasmi wa klabu Mwenyekiti
wa Kamati ya Mashindano Abdallah Binkleb amesema uongozi wao umemvumilia kwa muda mrefu juu ya habari zake za kutaka kuwavunja nguvu na kuisusa timu ili ibakie katika hali mbaya zaidi lakini kwa saaa umechoka na hatua za kisheria zinafuata.
"Kuelekea mchezo wa jumapili Waziri wa mambo ya nje anasisitiza timu ikafanye vizuri kwani inabeba bendera ya nchi, balozi anashiriki maandalizi ya kupokea timu mara itakapofika Misri lakini muandiishi huyu kazi yake imebakia kuandika uongo juu ya Yanga lengo lake ni kuondoa morali kwa wachezaji alisema" Bin Kleb
Hakuna asiyetambua kwamba Al Ahly walipokua jijini Dar es salaam alikuwa nao bega kwa bega Uwanja wa Taifa siku moja
kabla ya mchezo wakati wakifanya mazoezi, wakati waandishi wenzake wakionysesha uzalendo na kuandika habari zenye mlengo wa kuisaidia timu ya Yanga kufanya vizuri. Inafahamika
kilichomuondoa Habari Cooperation na kuamua kuendesha blog ambayo halipii chochote kwa mwezi wala kwa mwaka zaidi ya kupata pesa za matangazo kutoka wadhamini wanaomdhamini kwa kulipia matangazo yao kwake
na kupata idadi kubwa ya wasomaji kwa kuandika habari za Yanga.
Tunaomba
aachane na habari za Yanga kwenye blog yake vinginevyo taratibu zinafanyika kuweza kuushtaki mtandao huo ambao umekosa weledi kwa kuandika taarifa za kupotosha muda wote, huku klabu ya Yanga ikiambulia kuchafuliwa na yeye kujipatia pesa kwa habari hizo.
Ni jambo la kushangaza katika dunia ya sasa ya karne ya Sayansi na Teknlojia mwandishi wa habari kuandika habari zisizokua na ukweli jambo ambalo linapelekea wapenzi, wadau na wachama kushindwa kuelewa ukweli ni upi na
kuwapa kazi uongozi kujibu hoja zao.
Taarifa kwamba Uongozi ulitoa posho ya laki moja sio kweli, hiyo ni pesa iliyotolewa mfukoni na
mmoja wa viongozi wa Young Africans kufuatia furaha ya ushindi mara tu baada ya kumalizika kwa mchezo, Kamati ya mashindano ilikua na zawadi nyingine ya ushindi huo ambayo wachezaji wameshakabidhiwa.
Tumewekeza
kwa zaidi ya miaka miwili sasa, tumesajili wachezaji wazuri, wanapata huduma nzuri ikiwemo timu kuweka kambi nchini Uturuki mara mbili na mazingira ya michezo ya ligi kuu ikiboreshwa kwa asilimia 100, mishahara
wachezaji wanapata kila mwisho wa mwezi hayo ni mabadiliko kiungozi na kuelekea kwenye mafanikio katika mchezo wa mpira wa miguu.
Suala la Ahadi/Zawadi ni nje ya mkataba kati ya wachezai na viongozi, klabu imekua na utamaduni wa kutoa Bonus kulingana na ushindi unaopatikana, au
mara timu inapotoka sare hivyo ni vyema angeweza kuuliza uongozi kabla ya kuandika vitu asivyovijua. Aliandika kuhusu uwezo wa Kocha Hans takribani kwa mwezi mzima pasipo kujua taaluma yake, Hans ni miongoni mwa makocha wachache wenye Cheti cha Ualimu wa Mpira Miguu barani Afrika CAF chenye Daraja A ambacho hutolewa kwa kocha aliyepata mafanikio tu na si kwa kusomea darasani kama ilvyo kwa madaraja mengine.
Mkataba wa SGM ulikuwa ni wa dolla 55,000 ambapo walitoa Advance ya dolla 20,000 kisha ikabakia dolla 35,000 ambazo walipaswa kuilipa Yangakabla ya kuanza kwa mchezo wenyewe, lakini SGM walitoa sababu kuwa ofisa wao aliyekua anakuja na pesa hizo amezuiliwa Cairo Airport na kuomba wapewe link waonyeshe mpira na watamalizia malipo hayo
baada ya mechi, Uongozi wa Yanga ulikuwa makini na kuwakatalia kuwapa link mpaka wamalizie pesa iliyobakia kwani endapo wangepata hiyo link basi ingekuwa vigumu kumalizia malipo baada ya mchezo kumalizika.
hizo zote na nyingine amekua akiandika bila kuwauliza viongozi wa Yanga
kupata uhakika jambo linalopelekea kuamini kuwa anatumika na baadhi ya taasisi kuisakama Yanga ionekana haipo makini na kuonekana viongozi wake
hawapo makini jambo ambalo sio kweli.
Tunatambua ana masilahi na upande gani, na timu gani ila kwa sasa tunaomba aachane na klabu ya Yanga aandike taarifa za upande unaotumia kuhakisha anaiharibia Yanga, akumbuke Yanga ilikuwepo na itaendelea kuwepo, wengine wanakuja na kuondoka kama upepo.
Mwisho tunaomba aachane na taarifa za Yanga aendelee kuandika habari za wafadhili wake wanaomsadia kwani hata wao habari ni nzuri, habari za Yanga ziwe nzuri au mbaya zitaendelea kuandikwa na waandishi wenye weledi na wanaoheshimu taasisi zinawapowaptia habari.
Mungu Ibariki Young Africans Mungu Ibariki Tanzania. imewekwa saa
| 2016-12-05T20:37:28 |
http://shabanishakeel.blogspot.com/2014/03/mamluki-bin-zubeiry-yanga.html
|
[
-1
] |
MICHUZI BLOG: KONGAMANO MAALUM LA UWEKEZAJI KUFANYIKA NCHINI ISRAEL
KONGAMANO MAALUM LA UWEKEZAJI KUFANYIKA NCHINI ISRAEL
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji ,Clifford Tandari akizungumza na baadhi ya Watumishi wa Kituo hicho pamoja na Waandishi wa Habari wakati walipotembelewa na balozi wa Israel kuzungumzia Kongamano la Biashara na Uwekezaji litakalofanyika Tel Aviv Israel. Balozi wa Israel Nchini Tanzania,Yahel Vilan akizungumzia Kongamano hilo ambalo kwa mara ya kwanza litafanyika nchini Israel baada ya kufanyika Tanzania kwa mara ya Tatu mfululizo.
| 2017-07-24T08:36:07 |
https://issamichuzi.blogspot.com/2016/11/kongamano-maalum-la-uwekezaji-kufanyika.html
|
[
-1
] |
DEE-7-EVEN®: RAMA DEE-SI WAOAJI HAO...
RAMA DEE-SI WAOAJI HAO...
NIMEKUSIKIA KTK SINGLE YAKO MPYA YA "SI WAOAJI HAO"...UKISEMA MABINTI WASIWAPE MAPENZI WASHUSHA SURUALI KWA NYUMA(KATA KUNDU)....HALAFU WASIWAPE MAPENZI WABANA PUA KWA TRACK ZA NJAA....HEBU NAOMBA UFAFANUZI HARAKA....WAKATI BADO UNAJIPANGA TUELEKEE HUKU>>>>>>>
kama vipi download the track hapa:-
RAMA DEE-SI WAOAJI HAO.mp3
Posted by Dee Seven at 1:03 AM
hii ni kwa yeyote anae husika kama nimuowaji hauwezi msumali kukuchoma ila kama sio mmmmmmmm alafu unakuta watu wanafanya mziki si kama ofisi wanafaya ili wapate mababy wengi wao wabana pua!! ninapo sema track zanjaa niwale wanao fata mkumbo nakuwa naimani potofu kuwa rnb haiuzi!! kiukwali hata mimi hii ngoma inani dc kimtindo kikubwa ninacho kifanya sasahv ni kuja na kila ki2 kipya idia mpya namambo mengi..sasahv nakuja na vdio zakufa m2
rrrrrrraaaaaaa,nimekusoma RAMA DEE...ila bado sijaridhika,umesema inakudis pia hii track,fafanua kiaje?
| 2018-07-15T22:41:55 |
http://ujazo.blogspot.com/2010/05/rama-dee.html
|
[
-1
] |
Masomo » Emmaus Shule ya Biblia
Emmaus Kenya
KLB Publishers
Kuchunguza Maandiko Matakatifu
Kozi hii inaeleza kifupi sehemu za Biblia na kusudi lake.
Somo la kwanza Download PDF
Mtihani Download PDF 0/-
Mungu Mmoja Njia Moja
Kwa mifano ya Agano la Kale na Agano Jipya kozi hii inaeleza jinsi Mungu alivyo na makusudi yake kwa watu wa dunia yetu. 1500/-
Mtumishi wa Mungu
Somo hili linafafanua sehemu ya kitabu cha Injili ya Marko. 1500/-
Kozi hii inachunguza maswali yafuatayo:
Mungu ana tabia gani?
Kuna miungu mingapi? Je, Mungu anajulikana? 1500/-
Somo linahusu Injili ya Yohana, yaani kitabu cha nne cha Agano Jipya. Kinachoonesha habari ya Bwana Yesu na maisha yake duniani. Kinatueleza kuwa Yesu ni neno la Mungu na matendo yake aliyotenda. Somo hili likusaidie kumjua Mungu mwenyewe. 1500/-
Njia ya Wokovu
Jinsi ya kuupata wokovu wa Mungu ni jambo gumu linalowasumbua watu wengi sana leo. Kitabu hiki kinaeleza mambo muhimu yanayohusu jambo hili.
Ndani yake kuna mistari iliyonukuliwa kutoka katika Neno la Mungu, yaani Biblia. 1500/-
Chupa12
Mtume Petro aliwaambia Wakristo kuwa lazima wawe kama watoto wachanga na siku zote wawe na kiu ya maziwa safi ya kiroho,
1 Petro 2:2. Maziwa haya ni Neno la Mungu ambalo hutusaidia kukua kama Wakristo.
Kunywa kwa wingi, Mpendwa.
Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema, (Zaburi 34:8). 1500/-
Majuma mawili katika Shule ya Maombi
Kwa mfano wa mtu na mchungaji wake tunajifunza jinsi ya kuzungumza na kumsikiliza Mungu.
Kusudi la somo hili ni kwamba upate kujiendeleza katika mambo ya maombi. Unaposoma habari za watu hawa utajifunza siri chache zilizo muhimu kuhusu maombi yanayojibiwa. Mungu anadhihirisha siri hizi katika Biblia. 1500/-
Masomo ya kitabu hiki yanatufundisha baadhi ya mambo yaliyo muhimu sana katika maisha ya Mkristo. Lakini tutafakari maana ya maneno hayo Mkristo na Maisha. Biblia husema kwamba wanaomwamini Yesu Kristo wana “uzima wa milele,” milele maana yake daima. Mkristo akifa ataendelea kufurahia aina hii ya maisha katika nyumba ya Mungu, mbinguni. 1500/-
Biblia Ifunzavyo
Mafundisho ya msingi kuhusu Biblia, Mungu, dhambi, Wokovu n.k. 1500/-
Mwokozi wa Ulimwengu
Maelezo ya Injili ya Luka.
Somo linahusu maisha ya Bwana Yesu Kristo. Mwandishi Luka aliyekuwa daktari, aliwauliza watu wamwambie yale waliyoyaona na kuyasikia kuhusu Yesu. Kisha akayakusanya yote aliyokuwa na uhakika nayo akiongozwa na Roho Mtakatifu. 1500/-
Mwenendo wa mwamini
Matokeo ya kuzaliwa mara ya pili, uhakika wa wokovu, kushinda majaribu n.k. 1500/-
Waraka kwa Warumi
Waraka huu unaonesha jinsi Mungu anavyokutana na nia mbalimbali ambazo akili za mwanadamu huzifuata katika kuhusiana naye mwenyewe na kweli zake.
Njia rahisi ya kuelewa kitabu hiki ni kukiona kama mfululizo wa maswali na majibu. 1500/-
Je, Twaweza Kumjua Mungu?
Watu wengi hawamwamini Mungu. Wengine huishi tu kana kwamba hakuna Mungu. Wengine husema, labda Mungu yupo lakini hakujionesha kwa wanadamu. Kwanza tutajibu swali lisemalo, “Je, kuna Mungu?” Pia maswali yafuatayo yatachunguzwa: Mungu yukoje? Mwanadamu ni nani? N.k. 1500/-
Wanaume Waliokutana na Bwana
Katika somo hili tumechagua wanaume sita waliokutana na Bwana Yesu katika matukio yaliyohusiana na kifo chake. Walifanya nini watu hao katika wakati huo muhimu? Ndiyo, baadhi yao walitenda kinyume naye; na wengine walimwunga mkono kwa ujasiri. Na sehemu ya yale waliyoyatenda na kuyasema, yameandikwa kwa ajili yetu kwamba tuweke moyoni mafunzo tunayopata humo. 1500/-
Petro na Kanisa
Mafundisho kufuatano na maisha ya Petro uhusiano wake na kanisa. 1500/-
Kukua katika Imani
Hatua zinazosaidia kukua katika Imani na umuhimu wake, k.m. kutubu, kukariri mistari ya Biblia, matendo mema n.k. 1500/-
Roho Mtakatifu na Kazi Yake
Roho Mtakatifu ni nani? Mifano ya kazi za Roho Mtakatifu na nguvu yake. 1500/-
Umoja wa Biblia, Biblia ilitokeaje, Kanuni ya Biblia, kuenezwa kwa Biblia duniani. Biblia ni pumzi ya Mungu. 2000/-
Nyaraka za Yohana
Nyaraka za Yohana ni za kiutendaji. Pia zinaweza kushtua, kwa sababu Yohana anazungumzia mambo yote kwa uwazi bila kuficha jambo lolote katika maisha yetu. Mambo hayo yote ama ni meupe au meusi, ni ya kweli au uongo, mema au maovu ameyataja. “Mungu ni nuru, na ndani yake hakuna giza hata kidogo”.
Kwa hiyo nyaraka hizi zinafaa sana kwetu siku hizi. 2000/-
Safari katika Biblia
Somo linaanza na mpango wa Mungu kwa uumbaji. Mpango wa Mungu kwa mwanamume na mwanamke wa kwanza hadi mpango wa Mungu kwa kanisa na hata kwa siku zijazo zinaelezwa na mengine mengi pia. 2000/-
Mambo Yajayo
Bwana Yesu aliwaambia marafiki zake mambo mengi yatakayotokea baadaye. Jambo moja zuri limeandikwa katika Yohana 14:3, “Nitakuja tena”. Yeye alikuwa anaondoka ili awatayarishie mahali na kuahidi kuja tena. Alitaka wawe pamoja naye huko mbinguni. Je, Bwana Yesu yuko wapi leo? Yuko mbinguni, anataka tuwe pamoja naye mbinguni. Sisi hatuwezi kuona njia inayoelekea mbinguni au kufika wenyewe pale, kwa hiyo aliahidi kurudi tena. Huu ni ukweli mkuu wa kwanza ambao inabidi tuufahamu: Bwana Yesu aliahidi kuja tena. Somo linachunguza mambo mengi zaidi kwenye Biblia kuhusu muda ujao. 2000/-
Chakula cha Bwana
Somo linafundisha kuhusu Ushirika wa Chakula cha Bwana na Pasaka, mifano na maana yake, kutimiza agizo, na jinsi ya kujiandaa kwa Ushirika 1000/-
Je, kuwako kwa madhehebu kunaungwa mkono na Maandiko? Kwa sababu ya dhambi gani Mkristo anaweza kutengwa na kanisa lake? Je, ni haki kwa mwamini kumshtaki mwamini mwenzake mahakamani? Ndoa inapewa nafasi gani katika Agano Jipya? Kipawa cha kunena kwa lugha ni nini? Mwili wa ufufuo utakuwaje?
Haya ni baadhi ya maswali makubwa ambayo Paulo anayajibu katika waraka wake wa kwanza kwa Wakorintho. 3000/-
Kuzikwa kwa njia ya Ubatizo
Uchunguzi wa ubatizo katika Agano Jipya na uhusiano wake na imani katika Kristo. 1000/-
Timotheo na Tito
Nyaraka hizi za uchungaji zinafundisha maana ya kanisa la kibiblia, wajibu wa Wakristo, na jinsi inavyopasa kanisa litawaliwe. 3000/-
Kristo alilipenda Kanisa
Kozi hii itakusaidia kwa kuiruhusu Biblia izungumze yenyewe kuhusu swala hilo la Kanisa.
Je, maana ya Kanisa iliyoelezwa katika Agano Jipya ikoje? Ni nini mawazo ya Mungu kuhusu Kanisa? Je, mwanzoni Kanisa lilikuwaje? Na leo Kanisa linapaswa liweje? 2000/-
Uvuvi wa Watu
Mojawapo ya faida kuu za mwamini, yaani mfuasi wa Kristo, ni kuhusishwa na Mungu katika kazi muhimu ya kuwavua watu, yaani kuwavuta kwa Bwana Yesu Kristo waokolewe (Mithali 11:30). Kati ya mambo yatendwayo na wanadamu ni machache tu ambayo matunda yake yatadumu milele. Hakika mtu anayefanya kazi hiyo anajiingiza kwenye mambo ya milele, na thawabu yake itadumu milele (Danieli 12:3).
Kozi hii inachunguza huduma hii kwa upana wake. 2000/-
Tunaishi katika siku za maana sana.
Je, Biblia inasema nini kuhusu nyakati kama hizi? Je, tunaishi wakati wa siku za mwisho? Je, Biblia inazungumza kwa uhakika na kwa mamlaka juu ya mambo hayo na matatizo ya siku hizi? Je, inaweza kutufunulia mambo yanayopaswa kutokea? Kitabu cha Ufunuo hufunua mambo yatakayotokea. 3000/-
Kwa moyo mkunjufu tunakukaribisha kwa kozi hii ya Biblia.
Mwislamu mashuhuri mtunzi wa mashairi katika karne ya kumi na tatu B.K. (Baada ya Kristo), aliyeitwa Jalul’l-Din huko Rumi alisimulia hadithi ya tembo aliyekuwa katika chumba chenye giza.Baadhi ya watu fulani walimleta tembo huyo Arabuni na wengi wakaenda kumwona. Kwa bahati mbaya chumba alichowekwa kilikuwa na giza sana hata wageni waliofika „walimwona“ kwa kumgusa tu. Mmoja wao aligusa mkonga wa tembo na aliamini kuwa tembo ni kama mwanzi. Mwingine aligusa sikio na alisema amefanana na kipepeo. Wengine walibishana kuwa amefanana na ukuta, maana waligusa ubavu, wengine shina la mti, maana waligusa mguu, wengine kamba, maana waligusa mkia, na kadhalika. Kila mmoja wao alikuwa na sehemu ndogo ya ukweli lakini hakuna hata mmoja aliyejua kwa hakika tembo amefanana na nini.
Kozi hii ya Biblia imetayarishwa ili kuwasaidia Waislamu kumjua „tembo“ wa Biblia kama tunavyoona katika hali yake ya mwanzo katika Al-Kitab ama kwa ukweli Al-Kutubul-Muqaddas, „Maandiko Matakatifu“, yaani Biblia. Na kozi hii inaweza kusaidia kuzungumza kuhusu habari ya Biblia. 3000/-
Kitabu cha Matendo kinatusimulia jinsi kanisa la kwanza lilivyolikabili Agizo Kuu la Bwana. Kinatuambia jinsi Injili ilivyoenea magharibi na hatimaye kuingia katika jiji la Rumi. Kitabu hiki kinasimulia juu ya watu na pia sehemu mbalimbali. Kinadhihirisha kanuni za mipango makini ya kupeleka injili katika pande zote za ulimwengu.
Masomo ya kitabu hiki kwa ujumla ni rahisi, hata hivyo yanaleta changamoto kubwa. Lengo la masomo haya ni kutazama matukio yanayosisimua, ambayo yalibadili kabisa historia ya nyakati zote zilizofuata. Tunatumaini kwamba yatakupa changamoto na pia baraka kwako. 3000/-
Jifunze Biblia Nzima
Mafunzo haya yanaeleza kwa muhtasari vitabu vyote vilivyomo katika Biblia. Mambo hayo yote yameoneshwa katika nyakati zake, mahali pake pamoja na maelezo mafupi. 3000/-
Kitabu cha Mwanzo
Kitabu cha Mwanzo ni msingi na mahali pa kuanzia ujumbe wa Neno la Mungu zima. Ukitaka kuelewa vitabu vyote vya Biblia inakupasa ujue kitabu cha Mwanzo. 3000/-
Injili ya Marko
Marko aliandika Injili hii kwa ajili ya mtu wa kawaida.
Katika Injili hii tunapata habari njema kuhusu Mtumishi Mkamilifu wa Mungu, Bwana wetu Yesu Kristo. Hizi ni habari za yule aliyeweka kando utukufu wake wa mbinguni na kuvaa hali ya utumishi wa hapa duniani (Wafilipi 2:7).
Tunapochunguza Injili hii tutazingatia maswali matatu yafuatayo:
1. Je, inasema nini?
2. Je, inamaanisha nini?
3. Je, mimi ninapata fundisho gani?
Kwa watu wote walio na nia ya kuwa watumishi waaminifu wa Bwana, Injili hii itakuwa msaada kabisa. 3000/-
Njia ya Kutoka na Kuingia
Kitabu cha Mwanzo kinaishia na habari ya kufa kwa Yakobo katika nchi ya Misri.
Kitabu cha Kutoka kinaendelea na historia ya watu waliochaguliwa. Mfalme mpya wa Misri aliwafanya kuwa watumwa. Kitabu cha Kutoka kinaeleza jinsi Mungu alivyowaongoza watu wake kutoka Misri na kuingia jangwani. Neno “Kutoka” maana yake “Njia ya Kutoka”. Tutachunguza kitabu cha Kutoka kwa makini na pia kitabu cha Mambo ya Walawi ambacho ni vigumu sana kuelewa bila maelezo. Pia somo hili linalinganisha mistari ya Biblia sehemu ya Agano la Kale na Agano Jipya zenye maana moja. 3000/-
Safari Jangwani
Vitabu vya Hesabu na Kumbukumbu la Torati ni sehemu muhimu za Neno la Mungu. Kama ukielewa kitabu cha Hesabu na cha Kumbukumbu la Torati, utaweza kuelewa vizuri zaidi sehemu nyingi za Biblia. Pia utaelewa zaidi kuhusu Mungu pekee wa kweli. Pia somo hili linalinganisha mistari ya vitabu hivi na Agano Jipya na kueleza zinatokea wapi katika Agano Jipya na kwa tukio gani. 3000/-
Emmaus Shule Ya Biblia
kwa Njia ya Posta
P.O.Box 1424, Dodoma, Tanzania
Mobile: +255 765 442 452
(Jumatatu hadi Ijumaa siku za kazi
saa 2 hadi saa 10 tu.)
Email: [email protected]
Location: Dodoma, Ipagala,
Eneo la Emmaus, off Dar Road
Washiriki wetu
Kozi za Kiingereza
Kozi zinapatikana pia kwa lugha ya Kiingereza. Ukipenda kujiunga kwa kozi hizi wasiliana nasi.
© 2017 Emmaus Shule ya Biblia.
KLB Plublishers
| 2017-09-20T05:45:49 |
http://emmaus-tz.org/masomo/
|
[
-1
] |
Thu Dec 07 10:09:55 EAT 2017
Zaidi ya miaka miaka 10, mikopo elimu ya juu kwa rufaa
By Julius Mnganga
Desemba 5, bodi hiyo ilitangaza orodha ya wanafunzi 2,679 wa shahada za kwanza ambao wameshinda rufaa hivyo kutengewa Sh9.6 bilioni. Licha ya hao, kuna wahadhiri 45 ambao watapata Sh441.4 milioni.
Inapendeza kuona Bodi ya elimu ya Juu (Heslb) imeongeza wanafunzi wanaonufaika na mikopo baada ya kutokidhi vigezo kwenye awamu ya kwanza licha ya hatua hiyo kufikirisha.
Kusoma si anasa. Kwanza ni haki, pili uvumilivu. Wapo wanafunzi wengi wanaoshindwa kuendelea kutokana na kukosa uvumilivu licha ya kuwa na sifa za kuendelea.
Takwimu zinaonyesha wanaohitimu elimu ya msingi ni wengi kuliko wanaojiunga kidato cha kwanza. Vivyo hivyo, wanaojiunga kidato cha tano, shahada ya kwanza mpaka uzamivu.
Ingawa kuna wanaokosa vigezo vya kuendelea kutoka hatua moja kwenda nyingine, wapo ambao mfumo unawakataa. Hapa bodi ya mikopo nayo inaingia. Inawaacha baadhi ya wanafunzi wenye sifa lakini hawana fedha kugharamia masomo yao ya juu.
Si kuwaacha leo kisha kuandaa utaratibu wa kuwapa fursa hiyo siku zijazo, bila juhudi binafsi wanafunzi hao wanapoteza kabisa nafasi ya kuendelea na masomo. Hapa panahitaji tafakuri.
Hali hii imedumu kwa muda mrefu. Bodi inahitaji kutafakali. Wanaenda wapi wanafunzi hawa wanaoachwa kila mwaka? Wanafanya nini? Kuna mpango gani wa kuhakikisha wanapata nafasi waliyoikosa?
Wakato bodi inaanzishwa mwaka 2005, wapo wanafunzi waliokosa mkopo. Kwa kutumia njia nyingine, wapo waliofanikiwa kujiendeleza na kutimiza ndoto zao. Wengine waliishia hapo hata baada ya kuomba tena na tena.
Kwenye taarifa yake ya rufaa, bodi imebainisha idadi ya walioshinda rufaa na jumla ya wanafunzi wanaonufaika mwaka huu wa masomo. Haisemi iliowaacha. Inawezekana walioachwa ni wengi zaidi ya waliopata, lakini haisemi kama ina mpango wa kuhakikisha wanapata walichokikosa.
Kuwa na taifa lenye wasomi wengi hata kama hawana ajira rasmi kuna faida kwa taifa lolote duniani. Hili linaweza kufanikiwa kwa kuweka mikakati endelevu.
Waliopewa dhamana waumize vichwa kuhakikisha hakuna mwanafunzi mwenye sifa anayekosa mkopo.
Kwa waliosoma wanafahamu changamoto zilizopo mpaka anahitimu na kupata sifa za kujiunga na chuo kikuu. Ni vijana wenye malengo pekee wanaofanikisha hili, haioendezi bodi kukatisha mipango yao.
Zaidi ya muongo mmoja wa uzoefu wa kutoa huduma hiyo, si wakati wa Watanzania kuendelea kukosa mikopo hii.
Kuna kila sababu kwa bodi kujiimarisha kwa kutafuta vyanzo mbadala vya mapato ili isikatishe ndoto za wananchi kupata elimu ya juu.
Wenye sifa na wanaohitaji kuendelea na shahada za juu nao wakopeshwe tafauti na utaratibu uliopo sasa hivi wa kuwakopesha wahadhiri pekee.
Kwa fursa zilizopo kwenye mfumo wa elimu uliopo hivi sasa, wapo vijana wanaostahili kujiunga elimu ya juu wakiwa na chini ya miaka 18, umri mdogo kwa elimu waliyonayo kutimiza ndoto zao.
Ikilazimu, pawepo na udahili zaidi ya mara moja ili wanaokosa mkopo Novemba, kwa mfano, waombe tena kwenye udahili wa Machi, Juni au Septemba.
Julius ni mwandishi wa gazeti hili. Kwa maoni, anapatikana kwa 0717 298 276.
8 Minutes Ago Bajeti Maliasili na Utalii yapita, mradi wa Stigle’s Gorge watikisa
Ndugai aunga mkono usitishwaji wa kuweka mipaka
| 2018-05-22T19:23:45 |
http://mobile.mwananchi.co.tz/Zaidi-ya-miaka-miaka-10--mikopo-elimu-ya-juu-kwa-rufaa/1597608-4218118-format-xhtml-n3fhyyz/index.html
|
[
-1
] |
Hofu ya CCM ni kwa CHADEMA kuwa na pesa? | JamiiForums | The Home of Great Thinkers
Hofu ya CCM ni kwa CHADEMA kuwa na pesa?
Discussion in 'Jukwaa la Siasa' started by Zak Malang, Mar 15, 2011.
CCM imekuwa chama chenye nguvu kwa sababu ya pesa walizo nazo au wanazo-control, kuiba (kama vile EPA) na michango ya mabilioni kupitia wafanyabiashara ambao baadhi yao hupata mwanya ya kufanya wizi na ufisadi mwingine bila hofu kubwa ya kuchukuliwa hatua.
Sasa ukiondoa pesa basi CCM hakuna kitu. Baada ya uchaguzi, mgao wa CCM wa ruzuku kutoka serikalini umepungua kwa zaidi ya Sh milioni 200 kila mwezi na tayari tumeona hilo limeanza kuwawewesesha.
CCM wanazo taarifa kwamba CDM wanapata fedha nyingine nyingi ukiachilia mbali ruzuku ya serikali. Hili linawatia wasiwasi mkubwa. Taarifa hizo ni kwamba kuna baadhi ya wafanyabiashara wakubwa wameanza kukichangia CDM kama kinga kwamba kutokana na dalili zinazoonekana waziwazi wa kupungua umaarufu wa CCM, huenda CDM ikachukua nchi 2015.
Hawa wafanyabiashara (Waesia na Waafrika) wajanja sana, wanachangia CDM kimya kimya, (ukiuachia huyo Sabodo) tena mabilioni mengi. Wameona upepo jinsi unavyovuma.
Sasa hilo ndilo linaipa CCM kiwewe kikubwa na ndiyo maana wanatoa kauli kwamba CDM inapata hela kutoka nje "kufanya machafuko". Wanajua kwamba wakisema wanapata kutoka ndani, haitakuwa na element ya "crime" ndani yake kwani nao CCM si wanapata pesa kutoka ndani?
Lakini hizi ndizo siasa -- na ninasema hivi -- CCM iko tayari kutumia kila mbinu katika uwezo wake, za halali na haramu, iko hata tayari kumwagika damu kuliko kuachia madaraka kwa chama kingine kwa njia halali za kidemokrasia. Dalili hizo ziko na baadhi yake na kama hili la kuwasingizia CDM wanapata hela kutoka nje.
Lakini hizi ndizo siasa -- na ninasema hivi -- CCM iko tayari kutumia kila mbinu katika uwezo wake, za halali na haramu, iko hata tayari kumwagika damu kuliko kuachia madaraka kwa chama kingine kwa njia halali za kidemokrasia. Dalili hizo ziko na baadhi yake na kama hili la kuwasingizia CDM wanapata hela kutoka nje.Click to expand...
Na hasa CCM wakitafakari hali walionayo wenzi wao wa zamani -- yaani UNIP ya Zambia! UNIP sasa hivi iko nyikani -- haina mapesa tena kama ilivyokuwa enzi zake za mikutano ya kifahari ya Mulungushi! Ewe Mola wangu, naomba CCM nayo itokomee huko huko nyikani!!
Lakini hata hivyo naisifu UNIP na Kaunda wake kwa kuachia madaraka bila mizengwe kabisa.
jamani hizo siasa zenu mnakotupeleka siko sasa,kama chadema wanapata pesa kutoka nje mnataka serikali ikae kimyaaaa?hata nao wakibahaatika wakaingia madarakani mchezo utakuwa ni huo huo...ila penye ukweli inatakiwa serikali iingilie kati na kusema...nawasilisha
Nasikia UNIP walikuja Dom mwaka fulani (baada ya kuwa nje ya madaraka) kwenye mkutano mkuu wa CCM kutokana na mwaliko. Wajumbe wake walifikia hoteli za uchochoroni hadi CCM waliposikia wakaenda kuwaondoa na kuwaweka katika hoteli nzuri.
Nakubaliana nawe Bwana -- kwa chama kutokuwa na pesa ni balaa. CCM inaanza kuona jeuri ya CDM -- PESA!! Ingependelea jeuri hiyo wawe nayo wenyewe tu.
jamani hizo siasa zenu mnakotupeleka siko sasa,kama chadema wanapata pesa kutoka nje mnataka serikali ikae kimyaaaa?hata nao wakibahaatika wakaingia madarakani mchezo utakuwa ni huo huo...ila penye ukweli inatakiwa serikali iingilie kati na kusema...nawasilishaClick to expand...
Sawa - kama wanapata kutoka nje serikali ya CCM iache kubwabwaja - itoe ushahidi, iwakamate wahusika na kuwapeleka mahakamani. CCN hawana lolooooote! kazi yao kuu siku hizi ni kusemasema hovyo.
Mfano maneno ya 'uhaini" au ya 'matusi' ya viongozi wa Chadema majukwaani hayajawekwa bayana, CCM hawasemi ni maneno gani hayo ya uhaini au ya matusi au kuwapeleka wahusika mahakamani.
Ni kweli -- CCM imekuwa inaringia pesa walizonazo. sasa wanaone CDM nayo inaanza kuwa nazo - basi all hell has broken loose. Hawana hata aibu.
CCM wana siasa za kipesa. Ile CCM ya zamani na TANU yake ilikuwa na siasa ya kiutu zaidi.
CCM wameijenga Chadema, na wanaendelea kuijenga. Kabla ya Uchaguzi wa 2010 ni watu wachache sana waliona tishio lolote la maana kwa CCM na watu humu ndani walikuwa na kauli maarufu kuwa CCM iaendelea kutawala hadi 2050. Kwa nini mambo yamebadirika sana ghafla tu?? Sababu ni mapambano na minyukano ya ndani ya CCM ambayo walioko madarkani wamethibitisha kuwa hawana chembe ya uwezo wa kupambana na minyukano hiyo. Sasa kuja kwa "dimension" ya pili ya pesa, kunazidi kuongeza kasi ya uwezekano wa CCM kung'oka madarakani haraka zaidi kuliko hata wao wenyewe CCM walivyofikiria. Muundo wa CCM kuwa chama dola, chama ambacho kimuundo na kiutendaji ni sehemu ya serikali ulikifanya CCM kishindwe kuwa na miradi ya maana ya kukiwezesha kupata fedha. Chama ambacho kimekaa madarakani kwa zaidi ya miongo mitatu, utashangaa kikiondoka madarakani hakina mradi wowote wa maana. Sasa hivi watu tulitarajia CCM iwe mojawapo ya taasisi zenye ukwasi wa nguvu kama ilivyo mifuko kama PPF na NSSF, kwa sababu ya uwezekano kilio kuwa nao wa kujikusanyia mali bila kushughulikiwa na watoza ushuru. Lakini muundo uliokifanya chama hicho kiwe sehemu ya dola umekifanya kiwe chama cha kudokoa na kuchota mifedha kutoka serikalini kila kinapotaka. Bonanza hiyo ya wizi na uporaji umekifanya chama kilewe ulevi wa madaraka na kushindwa kusimamia miradi yake!
Kutokea kwa Chadema na uwezo wake wa kuvutia fedha za wanaotaka mabadiriko (au wale wanohisi kuwa mabadiriko lazima yanakuja), ni tishio kubwa kwa CCM. CCM sasa inaona kuwa kuna chama chenye uwezo wa kufika kule ambako ilikuwa ni CCM pekee wenye uwezo wa kufika huko, hasa maeneo ya vijijini. Lakini tishio kubwa zaidi kwa CCM ni uwezo mdogo wa ku "manage" rasilmali fedha. Udhaifu huu umejikita sana ndani ya CCM kiasi kuwa kikinyang'anywa dola ndo mwisho wake. CCM ni taasisi ya kutumia tu na mara nyingi hutumia bila ukaguzi. Ni nani wa kuikagua CCM? Pengine wao walikuwa wanaona huo ubabe kama faida, lakini ukweli hiyo ni hasara kubwa mno. Ili CCM wafanye kitu chenye "magnitude" ile ile, wanahitaji fedha mara kumi zaidi ya chama kama Chadema. Kwa hiyo utaona kuwa Chadema wakiwa na uwezo wa kutumia asilimia kumi tu ya ile wanayotumia CCM, watapata matokeo sawa na yale wanayoyapata CCM. Hili kusema ukweli ndo tishio kubwa zaidi kwa CCM kuliko matishio mengine yote!
Suala ni je CCM wanaweza kupambana na hali hii ya udahaifu katika matumizi ya fedha? Ukweli ni kuwa haiwezekani na hii ni mojawapo ya mambo yanayoifanya CCM iwe chama kisichoweza kurekebishwa. Ni kuwa 2015, madaraka yapo wazi kwa Chadema. Wakikosa watakuwa wamepoteza, ila si kushindwa!
Si utoe ushaidi acha kubwabwaja.
Vyama vya Siasa na NGOs zina tofauti gani? Vyama vya siasa haviruhusiwi kufanya "Fund Raising" nje ya wanachama wake wa ndani ya nchi?
Kuwa na pesa si dhambi tatizo ni kwamba watuambie ccm nao pesa zao wanapata wapi?.
Hofu inakuja kwa kuwa siasa siku hizi ni pesa na bila pesa hakuna siasa. Je ambaye amegeuza mchezo huu ni ccm ambao wanamiliki serikali au chadema wasio na serikali???.
Ccm ina pesa, ina dora na ina wafadhiri na wanachama wengi kuliko cdm hofu ya nini sasa, na inatoka wapi???.
Tatizo la Serikali ya JK ni kulalamika tu, utafikiri hawana meno yoyote! Kama wanaona kuwa fedha zinazoingizwa nchini kwa ajili ya kuipatia CDM kinyume na Sheria, kwa nini wasichukue hatua ya kuwakamata? Yaani CCM kwa sasa haina tofauti na chama cha UPINZANI!
Hivi woga wa CCM zidi ya CDM unatoka wapi? Kupata pesa kutoka nje ya nchi ama mahara popote kwa Chama chochote cha siasa si kosa ili mradi pesa hizo zimelenga kujenga demokrasia ya kweli miongoni mwa wananchi na kukijenga Chama chenyewe. Na hii ndiyo kazi inayofanywa na Chadema. Kwa kweli inasikitisha kuona viongozi wa chama tawala na serikali yao kila kukicha wanalalama kwenye vyombo vya habari na kikubwa zaidi wanachokiongelea ni CDM wakati yapo matatizo rukuki yanalikabili taifa, hawaoni kama wananchi tunaumia na huduma mbovu za umeme, miundombinu, maji, elimu duni, afya na mfumuko wa bei na kuporomoka kwa shilingi, CCM na serikali yake hawaoni kama haya ni matatizo bali tatizo ni CDM. Jamani M/Kiti wa CCM aliwahi kusema vyama vya upinzani ni vyama vya msimu, inakuwaje macho yenu na masikio yenu mnayaelekeza kwa CDM? Kumbuka CCM ni chama tawala na wajibu wako mkubwa ni kutatua matatizo yanayolikabili taifa kupitia ilani ya uchaguzi na kazi ya Chadema ni kukukosoa na kukuponda ilivyo pale unapokosea na kuuelimisha umma juu ya madhaifu yako na hii yote huitaji pesa. Ikumbukwe kabisa kuwa serikali ya ccm imejengwa katika misingi ya ombaomba wakati nchi ina rasilimali za kutosha na hii haiwafurahishi wafadhiri wa kweli maana nao wangependa kuiona Tanzania ikitoa misaada kwinginepo afrika, kwa hiyo inapotokea Chama makini kama CDM chenye uwezo wa kuzitumia rasilmali zilizopo wafadhiri hao lazima wakisupport ili baadaye waondokane na mzigo wa serikali ya ccm ya ombaomba! Hakuna namna yoyote ya kuweza kuidhibiti CDM isipate pesa toka kwa wafadhiri wake wakati serikali na chama tawala ni ombaomba wa kutupwa na ndomaana Membe hawezi kuitaja hata nchi moja inayotoa pesa kwa CDM na CDM wakikomaa na membe na Sophia Simba outcome yake mtaiona kwenye budget ya 2011/2012! Ushauri wangu wa bure kwa CCM ni ku concentrate kuondoa kero za maji, miundombinu, umeme, afya, elimu, n.k maana wananchi tumechoka na propaganda zenu!
tatizo ndugu zako(CCM &co),wanabwabwaja tu bila kuthibitisha madai yao.....wameshapoteza dira!
Hapana. CCM wanaogopa mapambano dhidi ya ufisadi. Kwa nini? Kwa sababu CCM na serikali yake chini ya mawakala wa mafisadi, ndiyo ufisadi. Mtu yeyote anayepambana kutomeza ufisadi ni mhaini kwa mujibu wa CCM. Alafu, kama hamjui CCM iko sahihi ktk hili. KWANI serikali ya CCM ndiyo ufisadi. Ukiangusha au ukipindua ufisadi umepindua serikali ya Tanzania. KATIKA TANZANIA ya CCM, mtu hawezi kutomeza ufisadi halafu asitokomeze serikali ya CCM.
Rushwa ya Tanzania haina aibu. Rushwa ina baraka zote za CCM. BILA RUSHWA CCM haiwezi kutawala. Mtu yeyote apambanae na rushwa anapambana na CCM ya leo chini ya mawakala wa mafisadi. Wananchi tukilijua hili hatupata shida na vitisho vya CCM dhidi ya wapambanaji wa ufisadi. Tunapaswa pia kujua vyombo vya habari ya mafisadi: magazeti ya RAI, MTANZANIA, THE AFRICAN, UHURU, MZALENDO, TBC ...
kwan mazuri kuona mpinzani wakoanakukaribia?lzm mchecheto lzm uwpo. goo go go go go chadema
Chanzo cha pesa za CDM ishapoteza uzito labda waje tena na singo ingine
Kulalamika ovyo ni dalili za kushindwa, huna jinsi unaishia kulalama. Hta katka soka ukimwona mchezaji mlalamishi mno, jua kiwango kinaelekea mwisho kama c kuisha kbs. Mfano wote twamkumbuka Jimmy flloyd Hesellbaink aliyekuwa Chelsea, Diouf na sasa Gattuso. Ccm kwisha baba, usiumize kichwa kuwaza sana. Labda jiulize, ungekuwa mgombea wa ccm na huu ni mda wa kampeni ungewambia nn wa Tanzania wakuelewe?
Sasa ukiondoa pesa basi CCM hakuna kitu. Click to expand...
Kweli kabisa. Lakini pia kuna kitu kingine ambacho kinaitisha CCM kuhusu CHADEMA. CHADEMA kina tendency ya kuwavutia members ambao wengi wao ni vijana wenye above average intelligence na pia wenye fikra huru linapokuja suala la politics za Tanzania. Kwa upande mwingine, chama kichovu kifkra na kiuongozi kama CCM, kinachofanya blunders kila kukicha katika masuala muhimu na nyeti kwa uchumi wa nchi, hakiwezi kuvutia watu makini zama hizi. Hivyo, wengi wa mashabiki wa CCM zama hizi ni maopportunists wanaojiunga na CCM kwa lengo la kupata favor fulani fulani hivi (si unajua ukiwa na kadi ya CCM most likely things will go smooth on you -- or so they think?), au wenye udini na ukabila uliokithiri. Sasa suala linakuja kuwa overtime CHADEMA ina accumulate finest people of the country wakati CCM inaaccumulate majambazi (Rostam), wapuuzi (Sophia Simba), vilaza (the so called president) na maopportunists wengineo wengi. Na hiki kinaitisha sana CCM.
Matokeo yake nini? CCM hawana jinsi bali kubakia kutapatapa kwa vitisho na visingizio. Na hapo ndo linapokuja visingizio vya huyu mama mpuuzi kweli kuwa mabalozi wanaifinance CHADEMA. It's just so pathetic to have these people being leaders of our country. God forbid it come 2015!
| 2016-12-04T02:16:18 |
http://www.jamiiforums.com/threads/hofu-ya-ccm-ni-kwa-chadema-kuwa-na-pesa.118084/
|
[
-1
] |
Jiajiri kupitia Dudumizi Reseller Web Hosting Plan
Moja kati ya maombi ambayo tumekuwa tukiyapokea sana kutoka kwa wateja wetu ilikuwa ni huduma ya Reseller plan. Wateja wengi walikuwa wanataka nao wajiajiri kuitia Web Hosting. Ili kuanza kutoa huuma ya Reseller plan, kunahitajika kuweka sawa mambo mengi, ikiwemo ya kimfumo na kiutendaji kazi ili kuweza kuwahudumia wateja wa moja kwa moja, na wale wanaokuja kupitia kwa resellers.
Reseller plan ni moja ya huduma ya Website Hoting ambapo muhusika ananunua plan kwa bei nzuri na yeye kwenda kuwauzia wengine kwa gharama anazoziweka yeye. Kwa lugha ya haraka tunaweza kusema, reseller ni kama kununua kwa bei ya jumla na wewe ukaenda kuuza kwa bei ya rejareja.
Reseller plan, ni mahususi sana kwa wale wanaohitaji kuanza kufanya biashara ya Web Hosting ila hawana uwezo wa kumiliki server zao wenyewe, au hawana timu ya kutosha kuchunga server zao.
Tofauti na shared hosting, reseller hosting inakupa uwezo wa kuhost unlimited domains kwenye account moja, na wewe ukaanza kuziuza kwa wengine kwa ghara nafuu au ya juu kulingana na mfumo wako wa kibiashara.
Kwa sasa, kuna aina tatu za reseller plan ambazo tunazo, nazo ni Mama Nyoni Plan, Kinjeketile Plan na Mkwawa Plan, tumezipa majina haya ili kuwaenzi ama viongozi ama watu muhimu kwenye maisha yetu. Hii inaendana na umuhimu wa Reseller Plan.
Makundi ya Reseller Plan, unaweza kulipia kwa mwezi na kwa mwaka. Unapolipia kwa mwaka, gharama huwa za chini zaidi.
Features za kwenye reseller
Je reseller ni kwa ajili ya makampuni pekee?
Hapana, reseller ni kwa ajili ya mtu yoyote mwenye utayari wa kuanza kufanya biashara ya Website hosting
Je ninaweza kulipa Hosting ya Reseller kwa mwezi?
Niyo, kwa kifurushi cha reseller, unaweza kulipia kwa mwezi au kwa mwaka, ingawa kama utalipia kwa mwezi gharama zitakuwa pungufu zaidi.
Je ninaweza kuhost akaunti zaidi ya moja kwenye Reseller Plan?
Ndiyo, todauti kati ya reseller na shared account ni kuwa, kwenye reseller, hakuna ukomo wa akaunti unazoweza kuhost. Ingawa tutachunga kiwango cha matumizi ya hazina za server kulingana na matumizi. Hivyo, inashauriwa usijaze akaunti nyingi kwenye plan moja.
| 2020-02-20T05:26:42 |
https://dudumizi.com/blog/258-jiajiri-kupitia-dudumizi-reseller-web-hosting-plan.html?tmpl=component&print=1&layout=default&page=
|
[
-1
] |
Boku Pay kwa njia ya simu Casino Bill Amana | Kushinda £££ kwenye Simu ya Mkononi |
nyumbani » Boku Pay kwa njia ya simu Casino Bill Amana | Kushinda £££ kwenye Simu ya Mkononi
Boku Bill Casino – Amana Simu SMS:
Kutoka £ 3 Minimum…Real Money Mafanikio: Priceless!
A Boku Phone Casino 2015 Tathmini na Randy Hall & Thor Thunderstruck kwa MobileCasinoFreeBonus.com
'Kulipa kwa njia ya simu Bill Amana’ ni kwa Slots, Roulette, au Enthusiasts Blackjack, nini hali ya hewa nzuri ni ice-cream Parlor: si 100% muhimu, lakini rahisi sana kupata wateja kwa njia ya mlango! Ambayo ni kwa nini yote ya juu kampuni ya simu casino, kama vile LadyLucks £ 20 Free Bonus Casino kuwa akaruka juu ya Boku Casino bandwagon.
Ziara LadyLucks Casino kwa simu za £ 20 Bonus – Hakuna Amana Inahitajika!
Simu Casino Choice – Simu na Online Kulipa kwa njia ya simu Bill Michezo!
Kuna mizigo ya faida kali kwa Boku Online Casino Billing. moja dhahiri zaidi kuwa kuwa wachezaji wanaweza haraka juu juu akaunti zao kwa michezo ya kubahatisha uninterrupted. Kutumika na kupendwa na maelfu ya online casino mashabiki nchini Uingereza, Boku Billing kuhakikisha kwamba amana casino si tu haraka - wao ni kweli salama pia!
Boku Online Casino Faida kwa Everyday Gamer
Hebu uso yake, wengi wetu simu ya mkononi casino mashabiki si kweli 'High-Rollers': sisi Gamble kuwajibika, na wanapendelea wager kiasi kidogo wakati, hivyo betting £ 480K juu ya spin moja ya Roulette Wheel si jinsi sisi roll. Kama hii pia inaonekana kama michezo ya kubahatisha yako wasifu online, kisha Boku Casino ni dhahiri haki ya kuchagua kwa ajili yenu! Kwa kuzingatia kwamba spin moja juu ya Progressive Jackpot inafaa Machine katika CoinFalls Casino Unaweza kuanza kutoka tu 2p-10P, hakuna haja ya kwenda kubwa ni pale?
Angalia-Kati Coinfalls Casino £ 5 Free Bonus – ziara Sasa
Boku Casino Simu Amana ni zaidi inafaa kuelekea:
Watu ambao hawana akaunti ya benki: Mtu yeyote na simu ya mkononi anaweza kuitumia kama wao amana kupitia SMS Casino
On--Go-Gamblers: Kuna kitu tedious zaidi ya kuwa na kujaza maeneo isitoshe juu ya habari online tu kufanya malipo…Boku Casino inazuia yote ya kwamba. Wakati Mfukoni Fruity Bure Simu Slots Casino Simu, kuweka £ 10 kiwango cha chini kupitia Boku Pay na Mkono simu SMS inachukua chini ya 60 sekunde!
Ziara Pocket Fruity – Kupata £ 10 za simu za
Usalama Conscious Gamers: shughuli zote ni mamlaka ya moja kwa moja kutoka kwa wachezaji’ simu ya mkononi ili habari nyeti benki kamwe mahitaji ya kuwa pamoja na anakaa 100% kupata
Meja Networks Uingereza: Boku Simu Casino imeshirikiana na zote watoa huduma ya simu Uingereza (k.m. O2, Vodafone, bikira Simu) hivyo inaweza kutumika kwa idadi yoyote ya Uingereza mkononi
Gamers kuwajibika: Boku Simu Casino Amana ni capped katika £ 30, hivyo wachezaji wanaweza kamwe kwenda juu ya fedha nyingi kuendesha wapate majuto!
Kuna yoyote Boku Billing Casino Bonus faida?
upande wa chini tu kwa Boku Casino Amana ni kwamba wachezaji mara nyingi hawezi kufaidika na amana mafao ya mechi, mikataba pesa au mafao ya juu-up. Wakati kasinon kama vile mFortune Amana kwa njia ya simu Bill Simu Casino and with PocketWin Casino Maalum Inatoa, hii inaweza kufanya kabisa tofauti kubwa kwa sababu wagering mahitaji yao juu ya mafao bure ni kweli mazuri: Wachezaji haja ya tu kucheza mafao yao bure kwa njia ya mara moja, na kisha waweze kuendelea wanayo kushinda!
ZIARA PocketWin Casino, PLAY £ 5 Free, KEEP What You Win
Wakati kasinon nyingine ambapo wachezaji haja ya kucheza ingawa mafao yao 30 - 50x kabla wanaweza kujiondoa winnings yao, 'Kukosa nje’ si kama mpango kubwa. Licha, kuna mafao mengine kama vile Titanbet ya rejea-rafiki ziada £ 25 kuwa wachezaji wanaweza kunufaika na bila ya kuwa na maelewano yao Boku Online Casino Faida hivyo ni kweli kushinda na kushinda hali!
Ziara Titanbet Casino & Kupata ajabu Amana-Match Bonus
Kwa kweli, kuna sababu kwa nini wote wa karata mkononi kinatumia Uwezekano Michezo, kama vile LadyLucks Casino, simu Michezo, na Wasomi Simu ya Casino wote ni Boku Billing Casino kuwezeshwa: Boku’s innovative 1-Tap PaymentTM mfumo ina maana kwamba wachezaji ambao wanataka kupata haraka na rahisi kwa Slots yao favorite, Roulette, Blackjack au Poker michezo unaweza kupata wakati wanataka hivyo.
Tuangalie OFA mengine FABULOUS kutoka meza ya ziada chini & KUMBUKA kwa kufurahia hakuna mafao amana ya kwanza!
| 2017-08-23T10:10:40 |
http://www.mobilecasinofreebonus.com/sw/boku-amana-casino/
|
[
-1
] |
Kim Jong-un amefanya ziara ya kushtukiza China? - BBC News Swahili
https://www.bbc.com/swahili/habari-43552307
Image caption Babake Kim Jong-Un, Kim Jong-il, hakupenda kutumia ndege kusafiri
Image caption Afisa wa ngazi ya juu mno wa Korea Kaskazini kwa sasa yumo ziarani Beijing
Image caption Polisi wa China wakiwa wamefunga barabara kuruhusu msafara wa magari yanayodaiwa kuwa na maafisa wa Korea Kaskazini kupita karibu na ikulu ndogo ya rais ya Diaoyutai, Beijing
Hakimiliki ya Picha @martyn_williams @martyn_williams
Msimamizi wa duka moja nje ya kituo cha treni Beijing amesema ameshuhudia "shughuli zisizo za kawaida" kituoni.
"Kulikuwa na maafisa wengi wa polisi nje na kwenye barabara upande wa mbele wa kituo. Kituo hicho kilikuwa kimefungwa ndani," ameambia AFP.
Image caption Rais wa Korea Kusini Moon Jae-in
Mikutano mingi
| 2018-11-13T01:38:25 |
https://www.bbc.com/swahili/habari-43552307
|
[
-1
] |
"The Way You See The Problem Is The Problem": Da Mina apumzishwa
Da Mina apumzishwa
Maisha ya Dada yetu Mina Said Omar hapa duniani yaitimilika Septemba 21 hapa Maryland. Maisha mapya yameanza. Na kati ya maisha ya kale na mapya, kuna hatua za kupumzisha mwili. Na ndilo lililofanyika jana katika makaburi ya Al firdaus Memorial Gardens yaliyopo bara bara ya New Design, Frederick, Maryland nchini Marekani.
Baadhi ya wapendwa waliweza kutuwakilisha katika tukio hilo na TUNAWATHAMINI KWA HILO. Kaka yetu Ebou Sharty wa blogu hii ya Swahili Villa alihudhuria na kuweza kushirikiana nasi baadhi ya kumbukumbu
Waumini wakitoka msikitini baada ya sala ya ijumaa pamoja na sala ya maiti tayari kuelekea makaburi ya Al firdaus Memorial Gardens yaliyopo bara bara ya New Design, Frederick, Maryland.
Kwa picha zaidi toka BLOGU YA SWAHILI VILLA, BOFYA HAPA
PUMZIKA KWA AMANI Da MINA
Posted by Mzee wa Changamoto at 10:45 AM
| 2017-10-22T17:23:56 |
http://changamotoyetu.blogspot.com/2011/09/da-mina-apumzishwa.html
|
[
-1
] |
chromoselector rangi picker ni Plugin jQuery ambayo inatumia canvas API kama injini utoaji. Ni hutoa njia rahisi ya kuongeza rangi wakusanyaji na aina katika kurasa yako, hivyo kuruhusu watumiaji kuchagua rangi katika muundo wengi kwa mtindo user-kirafiki. Sasa kwa mkono rangi miundo ni RGB, HEX, HSL na CMYK (plus alpha, kama ni lazima).
Nini watu wanasema
Mufti nyaraka na kwa kweli ni nzuri na rahisi kutumia widget.
Shukrani kwa ajili ya chromoselector ajabu, rahisi kufunga, kutumia na nyaraka kubwa na thamani.
Si tu kuwa hii unono rangi picker kwamba I / tuna kutekelezwa, msaada / huduma ambayo roccivic hutoa ni kiwango kabisa kwanza. mapatano Ajabu kwa sehemu nyingi bei.
Sana utekelezaji mzuri, na mwandishi pia alifanya kazi haraka kutatua mdudu kwamba alionekana na toleo la karibuni la Chrome. rahisi sana kutekeleza, na tovuti ina mengi ya mifano ya vitendo na manufaa.
API Chromoselector ni wazi kwa umma, unaweza basi tazama ni nini chromoselector rangi picker ni uwezo wa kabla ya kununua leseni.
Chromoselector pia ni pamoja na " kupata kuanza " mwongozo wa kukusaidia kwa ushirikiano wa rangi wakusanyaji mara moja.
Kuna mambo kadhaa demos kuishi inapatikana katika http://chromoselector.com/demos/. Na karibu kila demo kuja na sandbox (jsFiddle), kwamba utapata kucheza na mazingira yake na kanuni, tena, kuruhusu wewe kupata kujua Chromoselector API bila kununua leseni.
Android Browser 2.2 +
17 Januari 13
24 Aprili 15
eCommerce, eCommerce, All Items, turubai, turubai rangi picker, turubai rangi picker, rangi, rangi picker, colorpicker, rangi, rangi picker, colourpicker, HTML5, jQuery, jQuery rangi picker, jQuery rangi picker, picker, Chomeka
| 2017-12-18T05:13:42 |
https://sw.worldwidescripts.net/chromoselector-a-jquery-color-picker-plugin-42131
|
[
-1
] |
Read Online Bible - Swahili New Testament Bible online on Jesus Work Ministry John Chapter 17:1-26.
JN 17:1 Yesu alipokwisha sema hayo, alitazama juu mbinguni, akasema, "Baba, saa imefika! Mtukuze Mwanao ili naye Mwana apate kukutukuza.
JN 17:2 Maana ulimpa Mwanao mamlaka juu ya watu wote ili awape uzima wa milele wote hao uliompa.
JN 17:3 Na uzima wa milele ndio huu: kukujua wewe uliye peke yako Mungu wa kweli, na kumjua Yesu Kristo uliyemtuma.
JN 17:4 Mimi nimekutukuza hapa duniani; nimeikamilisha ile kazi uliyonipa nifanye.
JN 17:5 Sasa, Baba, nitukuze mbele yako kwa ule utukufu niliokuwa nao kabla ya kuumbwa ulimwengu.
JN 17:6 "Nimekufanya ujulikane kwa watu wale ulionipa kutoka duniani. Walikuwa watu wako, nawe ukanipa wawe wangu; nao wamelishika neno lako.
JN 17:7 Sasa wanajua kwamba kila ulichonipa kimetoka kwako.
JN 17:8 Mimi nimewapa ule ujumbe ulionipa nao wameupokea; wanajua kwamba kweli nimetoka kwako, na wanaamini kwamba wewe ulinituma.
JN 17:9 "Nawaombea hao; siuombei ulimwengu, ila nawaombea hao ulionipa, maana ni wako.
JN 17:10 Yote niliyo nayo ni yako, na yako ni yangu; na utukufu wangu umeonekana ndani yao.
JN 17:11 Na sasa naja kwako; simo tena ulimwenguni, lakini wao wamo ulimwenguni. Baba Mtakatifu! Kwa nguvu ya jina lako ulilonipa, tafadhali uwaweke salama ili wawe kitu kimoja kama sisi tulivyo mmoja.
JN 17:12 Nilipokuwa nao, mimi niliwaweka salama kwa nguvu ya jina lako ulilonipa. Mimi nimewalinda, wala hakuna hata mmoja wao aliyepotea, isipokuwa yule aliyelazimika kupotea ili Maandiko Matakatifu yapate kutimia.
JN 17:13 Basi, sasa naja kwako, na nimesema mambo haya ulimwenguni, ili waweze kushiriki kikamilifu furaha yangu.
JN 17:14 Mimi nimewapa neno lako, nao ulimwengu ukawachukia, kwa sababu wao si wa ulimwengu kama vile nami nisivyo wa ulimwengu.
JN 17:15 Siombi uwatoe ulimwenguni, bali naomba uwakinge na yule Mwovu.
JN 17:16 Wao si wa ulimwengu, kama vile nami nisivyo wa ulimwengu.
JN 17:17 Waweke wakfu kwa ukweli; neno lako ni ukweli.
JN 17:18 Kama vile ulivyonituma ulimwenguni, nami pia nimewatuma wao ulimwenguni;
JN 17:19 na kwa ajili yao mimi mwenyewe najiweka wakfu ili nao pia wafanywe wakfu katika ukweli.
JN 17:20 "Siwaombei hao tu, bali nawaombea pia wote watakaoamini kutokana na ujumbe wao.
JN 17:21 Naomba ili wote wawe kitu kimoja. Baba! Naomba wawe ndani yetu kama vile wewe ulivyo ndani yangu nami ndani yako. Naomba wawe kitu kimoja kusudi ulimwengu upate kuamini kwamba wewe ulinituma.
JN 17:22 Mimi nimewapa utukufu uleule ulionipa mimi, ili wawe kitu kimoja kama nasi tulivyo mmoja;
JN 17:23 mimi niwe ndani yao, nawe uwe ndani yangu; naomba wakamilishwe na kuwa kitu kimoja, ili ulimwengu upate kujua kwamba wewe ulinituma, na kwamba unawapenda wao kama unavyonipenda mimi.
JN 17:24 "Baba! Nataka wao ulionipa wawe pamoja nami pale nilipo, ili wauone utukufu wangu ulionipa; kwa kuwa ulinipenda kabla ya kuumbwa ulimwengu.
JN 17:25 Baba Mwema! Ulimwengu haukujui, lakini mimi nakujua. Hawa nao wanajua kwamba wewe ulinituma.
JN 17:26 Nimekufanya ujulikane kwao na nitaendelea kufanya hivyo, ili upendo ulio nao kwangu uwe ndani yao, nami niwe ndani yao."
| 2018-01-18T00:16:00 |
http://spiritualwarfare.jesuswork.org/online-bible-swahili-newt/john_17.html
|
[
-1
] |
11 nights cruise in Hawaii - SR11H028
Vancouver (British Columbia),Kauai (Nawiliwili) (Hawaii),Hilo (Hawai) (USA),Kaiula Kona (Hawai, USA),Lahaina (Maui) (Hawai),Lahaina (Maui) (Hawai),Honolulu (Oahu) (Hawai, U.S.A)
7 Kauai (Nawiliwili), Hawaii 08:00 17:00
8 Hilo (Hawai), USA 09:00 18:00
9 Kaiula Kona, Hawai, USA 08:00 18:00
12 Honolulu (Oahu), Hawai, U.S.A 06:00 00:00
| 2020-01-23T18:29:02 |
https://www.navigator.gr/en/cruise/SR11H028
|
[
-1
] |
Pitio la 13:42, 14 Mei 2015
61 bytes added , miaka 5 iliyopita
→Uhuru
Pitio la 13:40, 14 Mei 2015 (hariri)
Pitio la 13:42, 14 Mei 2015 (hariri) (tengua)
(→Uhuru)
=== Uhuru ===
Mwaka 1moja kabla ya uhuru kulikuwa na uchaguzi wa kwanza chini ya usimamizi ya [[UM]] na chama mshindi ilikuwakilikuwa UPRONA iliyoongozwakilichoongozwa na mwanamfalme Mtutsi [[Louis Rwagasore]] aliyemwoa mke[[mwanamke]] wa Kihutu na chama kiliunganisha pande zote mbili. Lakini miezi michache Rwgasorebaadaye Rwagasore aliuawa na chama chake kilitengana kufuatana na ukabila.
Mwaka [[1962]] Umoja wa Mataifa uliamua kuipa Ruanda-Urubdi uhuru kamili, lakini kila nchi pekee.
Baada ya uchaguzi wa [[1965]] mapigano yalitokea kwa [[silaha]], na kikundi cha Watutsi wakali kilichukua serikali. 1966 mwami alipinduliwa na mwanasiasa Michel Micombero aliyejitangaza kuwa rais na nchi kuwa jamhuri. Kuanzia sasa wanasiasa na watumishi wakubwa walio wahutu walifukuzwa, kukamatwa au kuuawa.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/wiki/Maalum:MobileDiff/949701"
| 2020-08-11T10:58:49 |
https://sw.m.wikipedia.org/wiki/Maalum:MobileDiff/949701
|
[
-1
] |
Mwakilishi wa Marjaa dini mkuu Ulaya, apongeza mafanikio ya Atabatu Abbasiyya tukufu na aisifu harakati ya Qur’an..
Mheshimiwa Sayyid Murtadha Kashmiri
Mwakilishi wa Marjaa dini mkuu katika nchi za Ulaya Mheshimiwa Sayyid Murtadha Kashmiri amepongeza mafanikio ya Atabatu Abbasiyya tukufu katika nyanja ya majengo na elimu, pia amesifu harakati za kiqur’an zinazo fanywa na Ataba hiyo ndani na nje ya Iraq, kinacho fanywa na Maahadi ya Qur’an tukufu katika mji mkuu wa Uingereza Landan ni ushahidi wa wazi wa utendaji bora unaofuata misingi ya Qur’an tukufu.
Aliyasema hayo katika hafla ya kufunga semina ya masomo ya Qur’an iliyo endeshwa na Maahadi ya Qur’an tukufu tawi la Landan, iliyo fanyika jioni ya siku ya Ijumaa (18 Dhulqa’adah 1438h) sawa na (11 Agosti 2017m) katika taasisi ya Imamu Khui (q.s), akaongeza kusema kua: “Hakika viongozi wa Maahadi ya Qur’an tukufu wanafanya juhudi kubwa sana wanastahiki pongezi, wanafuata mwenendo bora na madhubuti ambao ni mwenendo wa Qur’an tukufu na kizazi cha mtume kitoharifu, amebarikiwa kila atakae shikamana na lulu hizi tukufu, nawasisitiza wazazi wawahimize watoto wao kuja kushiriki katika semina hizi za Qur’an tukufu”.
Naye mwakilishi wa Atabatu Abbasiyya tukufu Shekh Dhiyaau-dini Almajidi Zubaidiy mkuu wa kituo cha maarifa ya Qur’an kuifasiri na kuichapicha alipata nafasi ya kuzungumza katika hafla hiyo, alitoa shukrani kwa wasimamizi wa semina, akaelezea mambo muhimu yanayo fanywa na tawi la Maahadi ya Qur’an katika mji wa Landan au katika miji mingine, namna wanavyo endesha semina mbalimbali na nadwa kuhusu Qur’an na mengineyo, pia akaelezea mafanikio mbalimbali yaliyo patikana katika Atabatu Abbasiyya tukufu hususan yanayo husiana na Qur’an, kwa kufundisha maelfu ya wanafunzi katika semina za Qur’an tukufu, zinazo endeshwa na Maahadi ya Qur’an pamoja na matawi yake yote, likiwemo tawi la Landan ambalo limesha toa wahitimu karibu (150) wakiume na wakike, walio fundishwa mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na namna ya kuamiliana na riwaya za Ahlulbait (a.s), hukumu za usomaji wa Qur’an, Tajwidi na Hifdhu, zilizo fanyika katika miji ya Glasgow, Scotland, Brigham, Livapul na Landan”.
Hafla ikahitimishwa kwa mashairi ya kumsifu mtume (s.a.w.w) na kugawa vyeti kwa washiriki wa semina pamoja na kupandisha bendera ya kubba la Abulfadhil Abbasi (a.s) iliyo letwa kutoka Karbala kama sehemu ya kutabaruku nayo wahudhuriaji walio kuwepo.
| 2020-04-01T02:53:19 |
https://alkafeel.net/news/index?id=5768&lang=sw
|
[
-1
] |
MICHUZI BLOG: fancy nkuhi aibuka kidedea kura za maoni UVCCM mkoa wa singida
fancy nkuhi aibuka kidedea kura za maoni UVCCM mkoa wa singida
Msimamizi mkuu wa uchaguzi huo ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Singida,Mh. Pascal Mabiti akimpokngeza Fancy Nkuhi kwa kupata nafasi hiyo.Fancy Nkuhi akiwa na mpinzani wake wa karibu Jamila Hasani mara baada ya matokeo. Picha ya pamoja ya wajumbe wa mkutano huo mara baada ya uchaguzi kwisha.Na Hillary Shoo,Singida.KATIBU wa asasi isiyokuwa ya kiserikali ya (UNA) United Nation Asociation iliyopo kwenye jengo la umoja wa mataifa jijini Dare s salaam Fancy Nkuhi (25) amechaguliwa kuwa mmoja wa wagombe Ubunge kundi la vijana kutoka mkoani Singida.Fancy aliibuka kidedea kwa kupata kura 16 kati ya kura 29 zilizopigwa jana na wajumbe wa mkutano mkuu wa UVCCM mkoani hapa.Katika uchaguzi huo mshindi alipata upinzani mkali kutoka kwa msindi wa pili Jamila Hasan aliyepata kura 10 huku Vailet Eliasi ambaye ni mfanyakazi wa ofisi ya UVCCM makao makuu akiambulia kura 3.Mjasiriamali kutoka Kinondoni Mosi Ntandu aliambulia patupu baada ya kupata kura sifuri.Akizungumza mara baada ya kupata ushindi huo Fancy mwenye shahada ya sheria kutoka chuo kikuu huria,alisema matarajio yake ni kuhakikisha fursa wanazopata vijana katika nyanja mbalimbali zinafanikiwa.Alisema atahakikisha kuwa fursa hizo zinapata msimamizi mwenye uwezo wa kuzitetea katika bunge pindi atakapochaguliwa kushika nafasi hiyo.Hata hivyo msimamizi mkuu wa uchaguzi huo ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Singida Pascal Mabiti aliwataka vijana hao kuunganisha nguvu ya pamoja na kuvunja makundi ili kuhakikisha mwakilishi huyo kutoka mkoani hapa anaibuka mshindi katika awamu ya pili Mkoani dodoma Agosti 3 mwaka huu.
is she Fancy or Zaitun of Mnazi Mmoja Dar?
Ankal naomba namba ya Nancy...
She is so Cute na pia anaelimu hao ndio watu wanaofaa kutuwakilisha Vijana wenzao,sio mnatuwekea mtu ambaye ni mbumbumbu mzungu wa reli dada wa watu kasoma anaelimu yake...big up Fancy tuko pamoja
Kampeni za uchaguzi na kura za maoni zimetawaliwa na vitendo vya rushwa. Kwa mara ya kwanza naona TAKUKURU wanafanya kazi yao, lakini cha ajabu watuhumiwa wanaachiwa na ndivyo itakavyokuwa hawatafikishwa mbele ya sheria au kufunguliwa mashtaka. Wabunge waliupitisha mswada huu bungeni kwa kauli moja na Mhe. Rais akausaini kwa mbwembwe. Sasa sheria hii inawageukia na wanaiona TAKUKURU kuwa adui. Kweli hatuwezi kupata viongozi bora wenye mtizamo wa Utawala Bora, utetezi wa maslahi ya wanyonge na usawa mbele ya sheria. Nia yao kubwa ya kuchaguliwa ni kujinufaisha na siyo uwakilishi wa wananchi.
bila ufisadi maisha bora kwa wote yanawezekana, lakini ubinafsi wa viongozi, hembu tujiulize bongo kuna wabunge wangapi?
maskini kalivyo kazuri lazima katashinda afu ile mibaba ya vijicent inamsubiria kwa hamu wammege, Fancy pliz be yourself umesoma na mzuri, i see bright future without rushwa ya ngono.
Annon unayezungumzia uzuri wa Fancy umenigusa sana, maana hata mimi nimeguswa sana na uzuri wake! Ila ndio hivyo, inategemea na yeye mwenyewe ana mtazamo gani katika maisha na anataka nini toka kwa waheshimiwa sana wa mjengoni.All in all, mimi siipendi kabisa CCM, ila Fancy angeweza kunihadaa kwa sura yake na nikajikuta napigia kura CCM kama anagekuwa mgombea kwenye jimbo langu la Kawe!
| 2016-09-26T22:26:26 |
https://issamichuzi.blogspot.com/2010/07/fancy-nkuhi-aibuka-kidedea-kura-za.html
|
[
-1
] |
theNkoromo Blog: AMINA MOHAMED ALIVYOMEREMETA KATIKA USIKU WAKE WA KITCHEN MADA, SINZA, JANA
AMINA MOHAMED ALIVYOMEREMETA KATIKA USIKU WAKE WA KITCHEN MADA, SINZA, JANA
Bi harusi mtarajiwa, Amina Mohamed akiwa katika pozi
Bi harusi mtarajiwa, Amina Mohammed akimwaga tabasamu la furaha wakati wa shughuli yake ya kuagwa (kitchen mada) iliyofanyika Sinza Mapambano, Dar es Salaam jana, tayari kwa leo Ijumaa, Desemba 23, 2016 akijaaliwa atafunga ndoa na mwandani wake. Inshaallah tumtakie kila la Kheri.
hivi punde Bi harusi mtarajiwa, Amina Mohamed (wa tano kulia) atafunga Ndoa yake na mpendwa wake Ashrafu Issa, hapa akiwa katika picha ya pamoja wanafamilia Bi harusi mtarajiwa, Amina Mohamed akiingizwa katika ukumbini wakati wa
shughuli yake ya kuagwa (kitchen mada) eneo la Sinza Mapambano Dar es Salaam
cha kinamama wakitumbuiza kwa dufu wakati wa hafla ya kumuaga Bi Harusi mtarajiwa, Amina Mohamed iliyofanyika nyumbani kwao
Sinza Mapambano, Dar es Salaam
Mmoja wa mwanafamilia akimtuza zuria la kufutia miguu Bi Harusi mtarajiwa, Amina Mohamed katika pozi na Muuguzi wa Hospitali ya Taifa Muhumbili ambaye ni wifi yake mtarajiwa, Subira Mheta.
Amina Mohamed (kushoto) akiondoka ukumbini tayari kwa kujiandaa na hafla ya Harusi yake itakayo fanyika leo baada ya Swala ya Ijumaa nyumbani kwao Sinza Mapambano Dar es Salaam
Wana kikundi cha Upendo Group wakimtunza Amina Mohamed (wanne kushoto) ambapo ni wanakikundi wenzake na Wifi yake, Subira Mheta ambaye ni Muuguzi Hospitali ya Taifa Muhimbili. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA wa Kampuni ya K M Express Photo Studio na Mmiliki wa ujijirahaa blog
| 2017-04-30T18:43:34 |
http://bashir-nkoromo.blogspot.com/2016/12/ni-usiku-wa-kitchen-mada-ya-amina.html
|
[
-1
] |
HABARI PICHA-UZINDUZI WA KAMPENI YA SHAMIRI YA KUSOMESHA WATOTO 112 | Politiksi Kurunzini
Home HABARI HABARI PICHA-UZINDUZI WA KAMPENI YA SHAMIRI YA KUSOMESHA WATOTO 112
HABARI PICHA-UZINDUZI WA KAMPENI YA SHAMIRI YA KUSOMESHA WATOTO 112
SeriaJr TW Thursday, July 16, 2015 HABARI Edit
Meneja Mahusiano shirika la The Foundation For Tommorow , Anton Asukile akifafanua jambo juu ya Kampeni ya SHAMIRI inayolenga
kuchangisha milioni 50 kwa ajili ya kusaidia watoto wanaoishi kwenye mazingira hatarishi ,kulia ni Meneja Programu wa masuala ya kijamii na
afya Hedwiga na kushoto ni Hilda Lema (Mfanyakazi).
Picha na Ferdinand
| 2018-02-25T02:02:45 |
https://arusha255.blogspot.com/2015/07/habari-picha-uzinduzi-wa-kampeni-ya.html
|
[
-1
] |
Yanga hawana tatizo na Ibrahim Ajib kurejea Simba
13 October 2018 Saturday 12:00
Siku chache tangu meneja wa mchezaji wa Yanga, Ibrahim Ajib kutamka kuwa kuna baadhi ya timu zimeonyesha kumhitaji mshambuliaji huyo, uongozi wa Klabu ya Yanga umeibuka na kusema hakuna kitu cha bure na yeyote anayemhitaji staa huyo aende mezani wakazungumze ikiwemo Simba.
Ajibu ambaye alisajiliwa na Yanga msimu uliopita akitokea Simba, amekuwa na kiwango bora msimu huu kwani mpaka sasa amehusika katika mabao nane na kutoa asisti sita huku akifunga mabao mawili.
Katibu wa Yanga, Omary Kaya alisema kuwa kiwango cha Ajibu kuongezeka ni jambo zuri na wao kama uongozi wanamuomba azidi kuongeza juhudi zaidi lakini hakuna taarifa ambayo ipo mezani kwake inayohusu timu kumtaka Ajibu hivyo kama wanamtaka waende kukaa mezani na siyo kuongea maneno pembeni kwani hakuna kitu cha bure.
“Taarifa hizo ndiyo kwanza nazisikia kwako wewe ila kwenye meza yangu hakuna barua ya timu ambayo inasema kuwa inamhitaji Ajibu lakini pia hakuna kitu cha burebure duniani, kwani hata ukimtaka mwanamke lazima umtongoze, hivyo kama wanamtaka Ajibu waje mezani tukae tuongee na siyo kuongea pembeni tu, wakija na pesa za kutosha sisi tunamuachia.
“Huwezi ukaanza ligi bila kujipanga, hivyo sisi kama uongozi wa Yanga tumejipanga kuhakikisha tunaendelea kufanya vizuri katika mechi zetu za ligi kuu na kurudisha heshima yetu,” alisema Kaaya.
Alipotafutwa Ajibu kuzungumzia ishu ya kutakiwa na timu kadhaa za Uarabuni, Afrika Kusini pamoja na Simba, simu yake iliita bila kupokelewa.
Ibrahim Ajib kuondoka Jangwani?
Yanga yaichapa Mbao FC 2-0
Ibrahim Ajib 'ashikwa uchawi' taifa
Meddie Kagere, Haritier Makambo wapewa mikoba ya Emmanuel Okwi, Ibrahim Ajib
Updated: 13.10.2018 12:18
YangaIbrahim AjibOmary KayaSimba
| 2018-10-15T21:59:02 |
http://www.azaniapost.com/michezo/yanga-hawana-tatizo-na-ibrahim-ajib-kurejea-simba-h23503.html
|
[
-1
] |
BLOG RASMI YA OFISI YA MKUU WA MKOA WA SINGIDA.: WAFANYABIASHARA MKOANI SINGIDA WAJIPATIA BILIONI 1.8 KWA MAUZO YA KUKU.
Posted by RAS SINGIDA at 05:11
| 2018-05-21T20:57:54 |
http://singidars.blogspot.com/2016/11/wafanyabiashara-mkoani-singida.html
|
[
-1
] |
Retrechment ya ndoa;kuwe na mafao yake!!! | JamiiForums | The Home of Great Thinkers
Retrechment ya ndoa;kuwe na mafao yake!!!
Discussion in 'Habari na Hoja mchanganyiko' started by Pdidy, Oct 4, 2009.
Jamani kuna ndoa za ajabu ajabu watu wanaoana siku mbili wanaachana wengine miezi miwili wanaachana kwa ujumla hakuna tofauti na retrechment ya makazini.....
sasa basi nikaona vyema kama retreachment za makazini zinatolewa mafao vivyo hivyo inabidi yule anaemwacha mwenzake kuwepo na makubaliano ya mafao kwa yule anaeachwa...vinginevyo kutakuwa na kuachana kama mbwa kila siku...je mafao yanaweza kupunguza ongezeko la kuvunjika kwa NDOA??
najua SA ipo sheria ya aina hiyo TZ sinauhakia
Kwa Tanzania sheria inasema kile mlicho chuma mkiwa pamoja ndo kinagawanywa sawa kwa sawa kama hamna watoto, lakini kama mna watoto yule anayekaa/kutunza watoto ndo anapewa robo tatu ya mali. Hii inamaanisha watoto nusu ya mali, baba robo na mama robo.
Na hii haiangalii nani anazalisha zaidi ilimradi tu mali hizo mmezipata mkiwa pamoja. Nadhani wanaoachana baada ya miezi hawastahili hata kuwa na kesi yoyote kwa sababu kila mtu anaweza kuondoka na alichokuja nacho. Ikiwa mmoja atamkataa mwenziwe basi asidai chochote, na yule anayekataliwa ana haki ya kushitaki ili alipwe fidia na yule anaye mkataa, na sheria zipo (za madai)
Nadhani kuachana huku kunasababishwa na kukosa subra. Maana katika process za group (couple) formation inachukua hadi a year sometime kwa watu kuelewana na kuamua kuwa pamoja. Vijana wanashindwa kuvumilia kipindi cha mwanzo ambacho wakati katika baadhi ya ndoa huwa rahisi na nyingine huwa ni kipindi kigumu.
Hata hivyo, cha msingi kisiwe namna watakavyogawana bora wafikirie namna watakavyoimarisha ndoa yao. Ikitokea basi ni sheria ti zinazowasimamia zifuatwe ila kuita retranchment benefits, Mh!!!
| 2017-01-21T04:22:53 |
https://www.jamiiforums.com/threads/retrechment-ya-ndoa-kuwe-na-mafao-yake.40291/
|
[
-1
] |
Wits Shule ya Sheria na Taasisi ya Kimataifa ya Mafunzo ya Jamii (ISS) (programu ya PhD ya Erasmus Chuo Kikuu) 2018 - Tuzo ya Tuzo ya Tuzo. |. | Fursa Kwa Waafrika
nyumbani Scholarships udaktari Wits Shule ya Sheria na Taasisi ya Kimataifa ya Mafunzo ya Jamii (ISS) (Erasmus ...
Wits Shule ya Sheria na Taasisi ya Kimataifa ya Mafunzo ya Jamii (ISS) (programu ya PhD ya Erasmus Chuo Kikuu) 2018 - Tuzo ya Tuzo ya Tuzo.
Mwisho wa Maombi: 8 Juni 2018.
The Wits Shule ya Sheria na Taasisi ya Kimataifa ya Mafunzo ya Jamii (ISS) (Chuo Kikuu cha Erasmus Rotterdam) inalika maombi kutoka kwa waombaji wa PhD wanaotarajiwa kwenye mada mbalimbali katika sheria ya kimataifa, jamii na maendeleo kama vile:
Waombaji wanapaswa kuwa katika ngazi ya kuingia kwa PhD na wastani wa angalau 70% katika shahada ya Mwalimu ndani ya eneo husika. Waombaji wanapaswa kuwa na historia ya kisheria na lazima wamepata shahada ya LLB.
Mishahara ya gharama na gharama
Waombaji ambao wamefanikiwa kukiri kwenye programu watakuwa imetolewa Ada ya masomo kutoka ISS mbili na Wits. Kizuizi, utaalamu wa miezi ya 6 inapatikana, lakini wagombea wanajibika kwa kufunika gharama zao za maisha na utafiti.
Waombaji wanaovutiwa wanaweza kuomba kuingia kwenye Mpango wa PhD wa WSI-Wits kwa kuwasilisha zifuatazo:
Maneno ya riba, na kichwa cha kazi, ambacho kinaelezea kiini cha utafiti wa PhD unayotaka kufanya (takribani kurasa tano bila ukiondoa maelezo yako ya awali);
Maombi lazima Emailed na [email protected] na 8 Juni 2018. Ikiwa hukujisikia nyuma ndani ya mwezi mmoja tafadhali angalia maombi yako yamefanikiwa.
Kwa maelezo zaidi tembelea: www.iss.nl/jointwitsphd
Maswali ya jumla yaani muundo wa shahada, admissions, muda, na ada: [email protected]
Masomo kuhusiana na Masomo: (Wits) [email protected], (ISS) [email protected]
Wito wa Maombi kwa Maombi
Tembelea Tovuti rasmi ya programu ya Wits-ISS PhD
Makala zilizotanguliaWito kwa Mawasilisho: Tume ya Umoja wa Afrika 2018 Elimu Innovating katika Afrika EXPO huko Dakar - Senegal
Makala inayofuataMpango wa Mafunzo ya Wanafunzi wa Nigerian (GTP) 2018 kwa vijana wa Nigeria
cosmas ndani munyao Mei 11, 2018 katika 8: 22 am
PhD AGE LIMIT - Ninatafuta msaada juu ya jinsi ya kupata [Scholarship] kwenye programu hii.
Profaili yangu ya umri wa sasa imesimama kwa miaka 60. Je, tuna chaguo ambalo umri hauwezi kupunguzwa?
| 2018-07-21T07:39:48 |
https://sw.opportunitiesforafricans.com/wits-iss-phd-programme-2018/
|
[
-1
] |
TANZANIAN GAYS NETWORK (TGN): SHINYANGA REGION
SHINYANGA POST HERE
Posted by TANZANIAN GAYS NETWORK (T.G.N) at 2:52 PM
Anonymous December 15, 2015 at 4:46 AM
Nipo mkoa wa shinyanga ninatafuta versatiles bottom na tops waliopo shinyanga,kahama,nzega na tinde.acha mawasiliano yako hapa ni kutafuta. Nipo kahama mjini. Asante
Anonymous December 18, 2015 at 11:35 PM
Nipo kahama 0768432968
Anonymous December 18, 2015 at 11:39 PM
0768432968 kahama
Nipo Kahama. Nitafute kupitia : [email protected]
nahitaji top mi nipo mwanza kama upo shy gharama za usafiri zangu nipe email au namba ya simu tuwasiliane
Anonymous March 13, 2015 at 11:31 PM
Top nipo mwanza, [email protected]
Anonymous March 18, 2015 at 9:27 AM
lukavala unazingua tu wewe wala email yako haipo tukituma msg zinafail
Kahama 0768432968 yes
Musa Habibu January 9, 2016 at 12:40 AM
Elias Shija January 15, 2016 at 1:26 PM
0682375557 nitumie msg...ujitambulishe
57 wewe top au bottom mimi top niko nzega
nipe email nikutafute tupeane raha
top wa nzega nipe email yako tuwasiliane
Anonymous April 13, 2015 at 5:33 AM
nipo mwanza natafuta top wa shinyanga
Anonymous May 1, 2015 at 2:29 AM
[email protected], mimi ni top
Anonymous July 5, 2015 at 12:14 AM
wasap only 0689920371
Jovin Sevan July 27, 2016 at 1:44 AM
Top shinyanga apa nipo shinyanga 0786633052
any bottom from shy
Anonymous June 11, 2015 at 7:46 AM
am in mwanza if we can arrange for you to come i will pay for the cost if so give me your email number for more communication
Upo wapi best??
nna miaka 22 tall black handsome natafuta versatile kuanzia miaka 45 na kuendelea tutafutane kwa email [email protected]
kelvin martin September 26, 2015 at 3:15 AM
Anonymous September 28, 2015 at 7:50 AM
mi nipo mwanza natafuta top aliye nje ya mwanza gharama zote kwangu
Hassani Jumanne November 21, 2015 at 11:29 AM
Anonymous November 23, 2015 at 12:01 AM
nitaitumaje nauli nipe email tupeane namba huko
jembe mpini May 15, 2017 at 3:08 PM
[email protected] top hpa
Kahama 0768432968
nipe makusudio ya hizi aina tatu " top na bottom na versatile ".....
Any btm or ves in shinyanga weka namba nikutafute
cute boy January 15, 2016 at 1:34 PM
Acha yako
cute boy January 16, 2016 at 1:36 AM
cute boy January 16, 2016 at 1:38 AM
Niko shinyanga natafuta top mkweli na anaejari
Anonymous February 14, 2016 at 8:27 AM
NIko Mwanza ila kesho nakuja Shy ni top mimi nakuomba nikifika tuonane ili unipe mgongo.
Namba yangu ni 0654 343135
Karibu naitwa Adam
Anonymous January 22, 2016 at 9:47 AM
Nakupataje nipo shy
cute boy January 26, 2016 at 12:29 PM
Nipe namba mkuu
cute boy January 26, 2016 at 12:28 PM
Ingia fb Jack James utanipata nipo shy
Jmn Kwa mtu aliye serious, natamani kuingiziwa mboo taratiibu kwani sijawahi bado na pia uwe tayari nawe kuingiziwa mboo. Nipo Kahama namba ya msg hii hapa 0776624471. Plz andika msg ntaipata. Nahitaji wanaoweza kuwa Wa siri.
Minaingiza tu siingiziwi VP nikutafute..
Anonymous February 10, 2016 at 10:18 PM
unayeingiza tu nipe mawasiliano nikutafute
Kido Pee February 11, 2016 at 8:10 AM
0768432968 naingiza tu, nafira
Mimi niko Mwanza ni TOP ila nakuja kesho Shinyanga nakuomba bottom tuonane ili unipe nikufire hadi ujisikie kama uko ulaya vile.
mwanza warudi lini nikutafute
Anonymous February 18, 2016 at 12:38 AM
Tarehe 27/2
mbona nikikutumia msg hujibu best au hupendi mawasiliano
cute boy February 22, 2016 at 9:50 PM
Top Niko shy
Anonymous March 1, 2016 at 3:19 AM
top wa shy karibu mwanza kwa gharama zangu kama vipi nipe namba tuwasiliane
Anonymous March 2, 2016 at 2:43 AM
mavin February 13, 2018 at 4:51 PM
[email protected]
Nitafute mimi bottom
cute boy March 4, 2016 at 4:56 AM
Habari niko mkoni shinyanga ninahamu yakuingizia mboo yenye afya
Tutafutane nije Shy
Nope number
Anonymous March 30, 2016 at 12:49 AM
A man above 30 is needed am only 23 yrs old here in tabora. Yeah i prefer elders not young boys below 30 plz dont. [email protected]
riqo brown April 3, 2016 at 9:46 AM
I'm in shy 24 years can we meat??
mavin February 13, 2018 at 4:47 PM
Meet me. Im intetested
erick July 18, 2016 at 4:33 PM
Vipi wadau
erick July 18, 2016 at 4:35 PM
Dah mwanza hakuna top 0782035117
AK July 25, 2016 at 10:03 PM
Top niko Kahama for 3 days from 25th July kama wewe ni bottom au versatile nipe namba nikutafute au ni email kwa [email protected]
idrian mashaka March 24, 2017 at 1:36 PM
AK August 25, 2016 at 6:28 AM
Dah!Kahama hamna ma bottom ama ni vipi?
Anonymous August 30, 2016 at 11:57 PM
Nipe email nikutafute.
Anonymous September 18, 2016 at 1:57 AM
Mtu mzma top anyejiheshkmu na msiri sana age kuanzia 30 nicheki niko kahama kwa siku tatu.nipe email yako nikutafute.
0693228990
Anonymous September 30, 2016 at 2:22 AM
Top aliye kahama nitext hapa 0764659434
Verse au Bottom Shinyanga nitumie message kwa e-mail hii:- [email protected]
Top aliye kahama nitext 0764659434
Hata ukipigiwa simu hupokei,sms nazo hujibu kwa wakati.....sasa hiyo number uliweka ili iweje sasa!?
Nipo shy naitaji btm acha co
Any, verse or bottom boy in kahama nichek
Terry November 11, 2016 at 4:12 AM
mavin February 13, 2018 at 4:45 PM
Mimi Bottom shy nicheck
Bottom aliye tayari kwa mahusiano serious weka number yako au e-mail ili iwe rahisi kuwasiliana na kupanga mipango na uhusiano,
bottom awe maeneo ya Shinyanga,Kahama,Tabora,Geita au Simiyu.
0693228990 txt me through my no.
text me....nipo shinyanga
0782492249
Top guys mlio dar plz follow me on instagram @lexer mckasie tupange yetu so horny...Hi mm ni cute bottom nina tako kubwa , laini na sijioneshi . Nina miaka 20 i speak 3 laguages fluently.. natafuta top age miaka 19_25 awe handsome, muscular, smart na asiwe mchovu kitandani.. kwa top yeyote aliyepo dar,shyinyanga,tabora,moshi au mwanza aje kwa inbox tuendelee... always playin saf
Anonymous December 26, 2016 at 6:59 AM
hot top in shy
Njoo kahama, andika namba kwenye email: [email protected]
mavin February 13, 2018 at 4:43 PM
We hot top im bottom nearly checking in @ shy. Nicheck
Nasikia Shinyanga kuna dawa za kukuza uume, mwenyewe taarifa zaidi anijuze kuna bbm hariziki na saiz ya sasa
Bottom alie pande za Kahama tutafutane
idrian mashaka March 24, 2017 at 1:34 PM
Anonymous January 8, 2017 at 1:02 PM
Me bottom nipo kahama 0769663878
Any verse or top in shinyanga (town)nicheck 0756605816
people March 9, 2017 at 1:11 PM
Any big btm in geiita
NAHITAJI MWANAUME MWENZANGU WA KUFANYA NAE MAPENZI YA JINSIA MOJA MIMI NI BOTTOM NATAFUTA TOP MWELEWA 0753888100
Waukwelisana April 17, 2017 at 2:57 AM
Mwanza only call for men to men sex 0782518161
0769663878 am bottom npo Kahama.
nicheki [email protected]
Kimson August 30, 2017 at 8:43 AM
Bottom alie Shinyanga na yuko tayari usiku huu text me 0784836505
Anonymous November 6, 2017 at 5:38 AM
Helloo..naitwa felix from kahama am bottom 24 yrs am looking for top ambaye anageto lake call 0758057404
Anonymous January 5, 2018 at 10:30 AM
Hello shytown nahitaji top anaejielewa nipo shy kwa muda wa wiki tatu yeyote anaejielewa aweke namba yake nitamtafuta Nina nafasi muda wote
[email protected]
Nimeskucheck kwa gmail yako so ujibu
mavin February 13, 2018 at 4:37 PM
Habari natafuta top aliye shinyanga. Anayejielewa,mstaarabu na anayejiamini.Mimi ni mgeni hapa mkoani
Nina miaka 21 naishi miti mirefu karibu na hospitali
Kama unagettoh lako, Safi na unaweza game vizuri fresh. Sijioneshi ila utafurahi na show.
Kama upo interested check me through
Gettoh,Usafi,kinga,vilainishi muhimu. Usinisumbue kama huna na hujiamini. Mvuto muhimu pia unahusika
| 2018-02-19T01:54:13 |
http://tzgays.blogspot.com/2014/03/shinyanga-region.html
|
[
-1
] |
DJCHOKAblog: Tanzania's Entertainment Blog: (News) JAMBO SQUARDS NA LADY FIRE WATISHIWA KUUAWA NA MTU ANAYEJIITA KAKA KIBO WA ARUSHA
(News) JAMBO SQUARDS NA LADY FIRE WATISHIWA KUUAWA NA MTU ANAYEJIITA KAKA KIBO WA ARUSHA
Kuanzia kushoto ni Nigger C, Ordinally na Lady Fire
Exclussive akiongea na DjHaazu wa MJ FM Arusha mmoja kati ya member wanaounda kundi la Jambo
Squard NIGGER C a.k.a Chaalii Mtoto wa bibi amefunguka kuhusu wao kutishiwa Kuuwawa na mtu ambaye anajihisi kuwa yeye ndiye Wamemuimbia wimbo unaokwenda kwa jina la KAKA KIBO ambapo ngoma hiyo ilitungwa na Vijana hao na kupewa nafasi ya kuiimba Mdogo wao anayejulikana kwa jina la Lady Fire Manzi ya Ara.
Nigger C amesema baada ya wimbo huo kuanza kufanya poa kwenye Vituo kadhaa vya radio Nchini hatimaye ametokea Mtu ambaye anadai kuwa wao wamemuimbia yeye na vitu vyote vilivyoimbwa vinamlenga yeye Direct na jina lake ni Kibo na huyo mtu alishawahi kujiita yeye ni manager wa Jambo kitu ambacho wao kiliwaudhi na hatimaye kumkataa na kukaa mbali naye ambapo kilichofuatia ni uhasama
uliosababishwa na mtu huyo kuwashikia fedha zao million 3 akidai kuwa anawatengenezea future kibiashara huku akijitapa kuwa na mkwanja wa kutosha na mwishowe wasanii hao walipogundua ni mbabaishaji hatimaye walimbwaga na walipoulizia fedha zao jamaa aliwapa laki 8 tu kitu ambacho kiliwakera wasanii hao.
ameendelea kumiminika zaidi na kusema kuwa wamemrecord mtu huyo wakati akiongea na moja kati ya Viongozi wa GrandMaster record Studio ambayo wanafanyia kazi wasanii hao na sauti hiyo wanayo ya Kaka Kibo huyo akisema kuwa amewatafutia Majambazi vijana hao na amewalipa advance kwa ajili ya kuwalima risasi vijana wa Jambo Squard ambao ni Nigger C na Ordinally a.k.a Kisu kikali a.k.a Jogoo Kichaa na pia kumkata miguu na mikono Mwanadada Lady Fire.
Hata Hivyo wamewaahidi wananchi Kufikisha Sauti hiyo Radioni Leo Jumatatu Na watu watamsikia Mtu huyo akitiririka akiamini kiongozi huyo atakuwa upande wake bila kujua kwamba
anarecordiwa na Kiongozi huyo hayuko tayari kuwasaliti vijana wake kisa
fedha za mtu huyo.
Jambo Squard wanasema kinachowauma zaidi
ni kwamba mtu huyo anasema atasambaza fedha kwa MaDJ na Mapresenter ili
ngoma za jambo Squard zisipigwe na kwamba kuna kituo kimoja cha Radio arusha ambacho kimeandika Tangazo kabisa ukutani ukiingia studio kwao kwamba wimbo wa jambo squard usipigwe....
Nigger C amesema hadi sasa wao wanafuatilia RB Kumkamata mtu huyo ambaye inasemekana ana Mabov ya kutosha kumwaga ila wao wanaamini kama YAHAYA aliimbwa na JD na hakumshtaki JD inamaanisha kuwa walikuwa wengi na wao wanawajua Kibo wengi.
MSIKILIZE NIGGER C AKIONGEA NA DJHAAZU HAPA CHINI
KUSIKILIZA CLICK LINK HII >> http://old.hulkshare.com/ow4wkucz81ds
Ndani ya wimbo huo ameimbwa au wamefikishiwa ujumbe watu ambao wanapenda
kujioshea au kujibandika vyeo wasivyostahili mfano kuna line inasema " Eti anasema ni Maneger wa Jambo"
SIKILIZA WIMBO HUO KAKA KIBO WA LADY FIRE AKIWASHIRIKISHA JAMBO SQUARDS NA RAMA B HAPA CHINI
CLICK HAPA >>> http://www.reverbnation.com/grandmastertz/song/18838396-kaka-kibo-lady-firejambo-squad9grandmaster
FUATILIA HAPA HAPA KITAKACHOENDELEA
Jambo Squad,
| 2017-01-24T15:13:19 |
http://djchoka.blogspot.com/2013/11/news-jambo-squards-na-lady-fire.html
|
[
-1
] |
KANDAMIZA: MDAU TOKA PANDE ZA BELIJIAMUUUUUUU
MDAU TOKA PANDE ZA BELIJIAMUUUUUUU
HEBU NICHEKIIIIIII,NINAVYONG'AAAAA... SHOST TOKA PANDE ZA BRUSSELS BELGIUM
kifaa cha ukweeeeeh
kiburudisho cha ukweeeeh
Mwe!!Mkongo au?
hahaha sio Mkonho na bila shaka hiyo comment imetoka kwa kakake wa kuleee...Lily
| 2017-09-22T06:25:07 |
http://mkandamizaji.blogspot.com/2011/03/mdau-toka-pande-za-belijiamuuuuuuu.html
|
[
-1
] |
Swahili na Waswahili: Siku kama ya Leo da'Sandra-Neema Alizaliwa....!!!
Shukrani kwa ndugu/jamaa na Marafiki wote kwa kushirikiana nasi katika Maombi,Sala/Dua na malezi kwa ujumla..Tunaamini mtoto halelewi na wazazi tuu..
Happy bdy..mungu akulinde na akujalie ufikie malengo yako..na uwe mlezi wetu..amin
NADHANI SIJACHELEWA...HONGERA SANA KWA SIKU YAKO YA KUZALIWA
| 2016-12-10T01:04:14 |
http://swahilinawaswahili.blogspot.com/2015/07/siku-kama-ya-leo-dasandra-neema.html
|
[
-1
] |
Tetemeko la Ardhi la Ukubwa wa 8 laikumba Mexico, watu kadhaa wahofiwa kupoteza maisha. Tahadhari ya Tsunami yatolewa | JamiiForums
Tetemeko la Ardhi la Ukubwa wa 8 laikumba Mexico, watu kadhaa wahofiwa kupoteza maisha. Tahadhari ya Tsunami yatolewa
Tetemeko la ardhi lenye nguvu ya ukubwa wa 8.0 kipimo cha tetemeko, limeikumba nchi ya Mexico kwenye pwani ya Kusini ya nchi hiyo katika bahari ya Pacific
Kitovu cha tetemeko hilo kilikuwa kinakaribia umbali wa kilometa 100 (62 miles) Kusini-Magharibi mwa mji wa Pijijiapan na lenye kina cha kilometa 35, Mtafiti wa Kijiolojia wa Marekani ameripoti.
Tahadhari ya Tsunami imetolewa kwa nchi za Mexico, Guatemala, EL Salvador, Costa Rica, Nicaragua, Panama and Honduras.
Tetemeko hilo la ardhi limesikika katika mji wa Mexico City, kusababisha majengo kutikisika na kupelekea watu kukimbilia mtaani.
Karibia watu 29 wamefariki dunia baada ya tetemeko hilo la ardhi kuipata Mexico ambalo ni kubwa kuipata kwa kipindi cha karne nzima.
Rais wa Mexico Enrique Peña Nieto amesema tetemeko hilo ni kubwa kwa nchi hiyo kulipata kwa kipindi cha miaka 100.
Tsunami imethibitishwa katika nchi ya Mexico, ambalo lilikuwa na mawimbi yenye urefu wa futi 3 (mita 1), hili limesemwa na National Weather Service's Pacific Tsunami Warning Center kupitia ukurasa wao wa mtandao wa kijamii wa titwa.
National Weather Service's Pacific Tsunami Warning Center kupia ukurasa huo huo wa titwa imesema kuwa tsunami ambayo inaweza kuwa na mawimbi yenye kubwa wa zaidi ya futi 10 (mita3) yana weza kuipata Mexico, wakati tsunami yenye mawimbi ya urefu wa futi 3 yanaweza kuzifikia hadi nchi za Ecuador, New Zealand and Vanuatu.
Mwenyezi Mungu awanusuru
kyaibumba
View attachment 583919
Matetemeko, vimbunga, maporomoko ya udongo, mamilioni ya samaki kufa kwa kukosa oksijen huko kwenye mito, ukame, joto kali, n.k. n.k. Naam, ule mwisho u karibu enyi watu wa Mungu!
Majaribio ya Kinyuklia hudisturb tectonic plates za dunia, na athari zake huweza kutokea maelfu ya kilometa mbali na yalipojaribiwa!
Noel Mobeto
Poleni watu wa Mexico, Mungu awe nanyi hasa familia zilizo athiriwa.
Takribani watu 90 wameuwa kufuatia tetemeko la ardhi la uzito wa 8.1 katika vipimo vya richa nchini Mexico kwa mujibu wa maafisa.Msemaji wa serikali alisema kuwa watu 71 walikuwa wameuawa katika jimbo lililo kusini magharibi la Oaxaca.Mamia ya familia zimeripotiwa kushinda katika mitaa, zikihofia hatari za mitetemeko midogo.Wanajiolojia nchini Mexico wanasema kuwa mitetemeko midogo 721 imerekodiwa tangu tetemeo kubwa la Alhamisi.Tetemeko hilo lilikuwa la nguvu nyingi zaid kuwai kushuhudiwa nchini humo kwa karne moja.Siku ya Ijumaa, pwani ya mashariki mwa Mexico ilikumbwa na dhoruba inayojulikana kama Katia.Watu wawili walifariki kwenye maporoko ya udongo baada ya mvua kubwa. Pia Nguvu ya upepo mkali unaondamana na kimbunga, kimeanza kugonga visiwa kadhaa kusini mwa jimbo la Florida nchini Marekani, huku kimbunga kikiacha uharibifu mkubwa katika visiwa vilivyoko kwenye bahari ya Atlantic huko Caribbean, kuelekea Marekani.Kimbunga Irma, kinatarajiwa kugonga maeneo hayo, baadaye leo Jumapili.Viwango vya maji tayari vimeanza kuogezeka katika maeneo ya pwani ya Florida, eneo ambalo linatarajia kimbunga kikubwa kuwasili.Taharuki na hatma ya baadaye ya mji wa Tampa, ambao unakabiliana ana kwa ana na njia inakopitia kimbunga hicho, haijulikani.Zaidi ya watu milioni 6 huko Florida wanaondolewa majumbani mwao- robo tatu ya idadi nzima ya watu wa jimbo hilo.
Mungu tunusuru
Yaliyotabiriwa yanaendelea kuonekana.
Dunia ishafika jioni ndugu...
Tukio kubwa linalosubiriwa ni Kuja kwa yesu hakuna kipya tutake tusitake.
haya uyaonayo usitegemee nafuu tegemea zaidi ya hayo.
Kila lenye mwanzo halikosi mwisho. na dunia ndio mwisho huo
Reactions: Elli Mshana, Domhome, lokomu and 3 others
MKUU USISAHAU KUNA WATU WASIOJULIKANA WANALIAMSHA DUDE KILA MARA,HAWA NI HATARI ZAIDI MAANA HAWANA UTABIRI KAMA WA HALI YA HEWA.POPOTE WANAZUKA HAWA
Reactions: lokomu, gemmanuel265 and mbauba11
Hayana budi kutokea ..! (Mathayo 24)
Mungu atusaidie tu.
Mungu atusaidie pole zao nyingi
Nipe tarehe.....
Reactions: Online Pastor
hapa tunajadili dunia inakoelekea vs matukio yanayoiandama.
Tarehe mimi Sio kalenda mkuu.
Hata kama yatatokea mafuriko,kamwe hayawezi kuwa makubwa kushinda yale ya Nuhu!
Upinde wa mvua ndiyo alama ya agano kati yetu na Mungu juu ya kuiharibu dunia!
Tetemeko ni zao la sahani za mabara kugongana,kusagana au kuachana!
Zinapogongana,kuachana au kusagana mtikisiko wake ndiyo uleta tetemeko!
Ni majanga ya asili ila ni kumwomba Mungu madhara yasiwe makubwa!
nataman hilo tetemeko lingepita na pale magogon lifunike kila kiumbe kilichopo mule. harafu likate kona liingie mitaa ya lumumba likwangue kila kitu cha pale.
Reactions: Nalendwa and ze kokuyo
Mkuu hio avatar yako ni wapi? Basically inatuambia kuna vitu visivyo vya msingi tunavifanya kama hao wajenzi!
Hii dunia hii.!!
Tetemeko la ardhi la ukubwa wa 6.7 Elazığ Uturuki International Forum 7 Jan 25, 2020
Mindanao, Ufilipino: Tetemeko la ardhi yenye ukubwa wa kipimo cha 6.5 laua watatu International Forum 0 Oct 31, 2019
Tetemeko la Ardhi la ukubwa wa 7.1 laikumba nchi ya Peru! Hakuna vifo vilivyoripotiwa International Forum 2 Mar 1, 2019
MEXICO: Tetemeko la Ardhi lenye ukubwa wa kipimo cha 5.9 limeukumba Mji wa Oaxaca International Forum 1 Feb 19, 2018
Tetemeko la Ardhi lenye ukubwa wa kipimo cha 7.3 latikisa Pwani ya Peru International Forum 0 Jan 14, 2018
Tetemeko la ardhi la ukubwa wa 6.7 Elazığ Uturuki
Mindanao, Ufilipino: Tetemeko la ardhi yenye ukubwa wa kipimo cha 6.5 laua watatu
Tetemeko la Ardhi la ukubwa wa 7.1 laikumba nchi ya Peru! Hakuna vifo vilivyoripotiwa
MEXICO: Tetemeko la Ardhi lenye ukubwa wa kipimo cha 5.9 limeukumba Mji wa Oaxaca
Tetemeko la Ardhi lenye ukubwa wa kipimo cha 7.3 latikisa Pwani ya Peru
| 2020-06-05T22:53:01 |
https://www.jamiiforums.com/threads/tetemeko-la-ardhi-la-ukubwa-wa-8-laikumba-mexico-watu-kadhaa-wahofiwa-kupoteza-maisha-tahadhari-ya-tsunami-yatolewa.1314955/
|
[
-1
] |
Barua Kwa Kizazi cha P.O.Box – Niwezeshe.com
May 26, 2018 May 26, 2018 Madenge1 Comment on Barua Kwa Kizazi cha P.O.Box
Salam Kwenu (Shikamooni)
Binafsi naendelea Vizuri na afya, nalisukuma gurudumu la maendeleo kwa kuifanya leo yetu mlio iita “KESHO YA WATOTO WETU” iwe njema ili kesho ya wajukuu zenu ikawe na matumaini. Si mlisema “WATOTO NI TAIFA LA KESHO?” Kesho yetu imewadia na ni ngumu haswa na nihapa ndipo nimkumbukapo “Sijui Mhenga gani aliye sema (Kuwa Uyaone)” ila kikubwa ni kushukuru kwa malezi yenu mliyo tupa na sasa tunajivuna kuitwa #Wantanzania.
Neno langu Watanzania nimeliwekea alama # na yawezekana hujafahamu maana yake ingawa wengi huita alama ya reli. Si lengo langu kukupa somo juu ya alama hii ila lengo langu haswa ni kukupa Shule ambayo pengine Mtoto wako umuitaye kizazi cha Dot (.) Com hajakufahamisha. Mambo muhimu ambayo leo nimeona nivyema niyazungumze japo kwa uchache wake. Najua huwezi choka kusoma kwasababu kizazi chenu ni tofauti na chetu. Enzi zenu mlikuwa mnapenda kuandika” Barua ndefu kama hii”, Natena mlikuwa mnapenda kusoma haswa, ubaya ni kwamba hamkupandikiza mbegu mwanana kwa sisi vijana wenu na ndio maana tunapuuzia maandiko kama haya.
Niende kwenye lengo la Barua Hii.
Mpendwa Baba, Mama, Mjomba, Shangazi na kadharika. Tupo kwenye ulimwengu ambao kwa namna moja ama nyingine mmetuandalia, bahati mbaya ni kwamba “Teknolojia” na maarifa haya hamkuyapata na zaidi miaka ya 2000 mliita kipindi cha Y2K, wengi wenu mliona ni kupoteza muda kujishughurisha na Mambo ya barua pepe kipindi hicho mlitumia Hotmail na Yahoo na mitandao ya kijamii ilikuwepo kwa uchache wake hapa nazungumzia miaka ya 2005 na kadharika.
Huwa ninapitia pitia kurasa zenu za Mitandao ya kijamii na muyawekayo humo hunifanya nitabasamu. Somo langu kwenu ni hili, KILA UKIWEKACHO KATIKA INTERNET WATU WOTE WANAONA, zaidi kitadumu kwa miaka mingi. Hapa simaanishi picha za utupu na kadharika ambazo vijana na watoto wetu wanaweka kila kukicha.
Hapa ninamaanisha Maandiko, Comments, Likes na kila picha uiwekayo katika Facebook Page yako itakuwepo tu. Yani miaka Kumi ijayo Kitukuu chako kikitaka kutizama Swagga za babu yake miaka kadhaa nyuma ataona.
Kwanini Nimeandika?? Nifananishe zama hizi na zama za ALBAMU na picha mlizo kuwa mnapiga kwa kila aina ya POZI, na miaka kadhaa baadaye mmekuwa mkituonesha namna mlivyo ishi nasi hufurahia hayo yote huku tukisema wazee walikuwa “MAJEMBE” hapa ninamaanisha walikuwa watu makini na kila picha ina maelezo yenye ujumbe mwanana ndani yake.
Miaka kadhaa ijayo hatuto tumia albam tena, badala yake tutatumia Kurasa zenu za mitandao ya kijamii kushare na wanetu na wajukuu Habari zinazo kuhusu. Wakitaka kukufahamu, namna ulivyo kuwa unaongea, una-reason na kadharika watatumia Maandiko yako, post zako na kila kitakacho onekana waki-Google au Ku-Facebook jina lako.
Wengi wetu hatufahamu haya, sasa imagine kipindi kile ulipo kuwa unapiga picha na kuzihifadhi kwenye Albamu, ndio ungekuwa unapiga picha za sisimizi, au unajaza picha za kwenye magazeti cha Nyerere na Mwinyi kama rasi, Natena wa wakristu albamu nzima ungekuwa umejaza Picha za Yesu na mama maria, Kwa waislam na madhehebu mengine mkafanya hivyo hivyo, sidhani kama albamu zingetazamika.
Ninacho maanisha ni hiki, Hizo kurasa zenu ni sehemu za kuandika au kushare mambo ambayo utapenda ukumbukwe nayo kwasababu hakuna namna dunia tuishiyo ndivyo itakavyo. Kwa uwepo wa smart phone mtu unajikuta nilazima uwe na Barua pepe ambapo hapo mwanzo zilionekana hazina Maana, ili uweke CV zako za kazi mahala Fulani wanakutaka uwe ni ukurasa wa Linked In na kurasa nyingine za kijamii.
Basi ni muda muafaka wa Kujifunza namna Sahihi ya Kuandika katika kurasa zako za kijamii. Masomo yatakayo fuata yataelezea kwa kina namna ya kuyafanya haya.
| 2019-04-20T12:52:28 |
http://www.niwezeshe.com/2018/05/26/salaam/
|
[
-1
] |
Kashfa nzito zaibuliwa dhidi ya Ubadhirifu Bodi ya Mikopo | JamiiForums | The Home of Great Thinkers
Kashfa nzito zaibuliwa dhidi ya Ubadhirifu Bodi ya Mikopo
Discussion in 'Jukwaa la Siasa' started by ASSASSIN, Aug 26, 2012.
Vigogo wajilipa mishahara minono, ajira kinyemela
Mikopo inayopaswa kurudishwa ni Sh. bil.300/-
Hadi sasa fedha zilizokusanywa ni Sh. bil. 9/- tu
Vigogo Bodi ya Mikopo (HESLB), wanakabiliwa na tuhuma nzito za ubadhilifu wa fedha kwa kujilipa mishahara minono na matumizi mabaya ya madaraka huku mmoja wao akidaiwa kuajiri ndugu zake 11 wasiokuwa na sifa.
Nusu ya vigogo walioajiriwa katika bodi hiyo wanadaiwa kutokuwa na sifa wala vyeti stahiki kama kibali na tangazo la kazi lilivyotangazwa gazetini.
Vigogo hao pia wanadaiwa kulipwa mishahara minono ya mamilioni ya fedha huku Bodi hiyo ikiwa haizalishi chochote.
Chanzo chetu cha habari ndani ya bodi hiyo kimedai kuwa kigogo wa ngazi ya juu analipwa Sh. 13,875,000 yakiwemo marupurupu na posho.
Anayefuatia analipwa Sh. 12,950,000 kwa mwezi ikiwemo posho wakati mwingine mshahara wake pamoja na posho ni Sh. 12,025,000.
Watumishi wanaofuata baada ya menejimenti mishahara yao inaanza Sh. 3,000,000 kwenda chini bila posho yoyote, kilisema chanzo hicho.
Tangu Bodi hiyo ianzishwe mwaka 2005 mikopo iliyotolewa na kupaswa kurudishwa ni Sh. bilioni 300 lakini hadi sasa fedha zilizokusanywa ni Sh. bilioni 9 tu (sawa na asilimia 3).
Kwa mujibu wa chanzo hicho, licha ya utaratibu wa sasa wa serikali wa kutaka ajira zote zitangazwe kwenye vyombo vya habari ili kutoa fursa kwa Watanzania kushindania, lakini kigogo mmoja ametoa ajira za kudumu kwa watumishi kumi (majina tunayo) bila kutangaza wala wahusika kufanyiwa usaili.
Chanzo hicho kimesema kuwa, miezi michache iliyopita bodi hiyo ilitangaza ajira za watumishi 21 wakati kibali cha ajira kilikuwa ni nafasi 24.
Cha kushangaza nafasi 11 zimejazwa na ndugu wa mmoja wa vigogo hao akiwemo mtoto wake (jina tunalo) ambaye alipewa nafasi ya mwanamke (jina tunalo) aliyekuwa amefaulu nafasi hiyo, nafasi nyingine tatu (majina tunayo) wamepewa wajomba zake, kimesema chanzo hicho.
Chanzo hicho kimedai watumishi wamekuwa wakipandishwa vyeo kiholela bila kufuata sifa na sheria zilizopo.
Kwa mfano zipo nafasi kadhaa (majina tunayo) ambazo wale waliopewa hawana sifa, moja inamtaka mtu aliye na sifa na uzoefu wa usiopungua miaka mitatu na nyingine ilikuwa inahitaji mtu mwenye Uzamili (masters), yupo aliyepandishwa cheo bila ya kuwa na CPA (T) kama miongozo inavyosema, kimebainisha.
Aidha, chanzo kimeendelea kufichua kuwa nusu ya wakurugenzi walioajiriwa hawana sifa wala vyeti stahiki na wanaajiriwa kiudugu.
Baadhi ya vigogo walioajiriwa wanadaiwa kupewa ajira, wakiwa hawana kiwango cha elimu kilichokuwa imetangazwa na kwamba wengine walikuwa bado wanafunzi na wengine hawakuwa na taaluma ya kazi aliyoajiriwa.
Pia chanzo hicho kimedai kigogo wa ngazi ya juu amekuwa na matumizi mabaya ya madaraka ambapo mwaka 2010 alitumia zaidi ya Sh. milioni 50 kwa ajili ya safari nchini Zambia akiambatana na vigogo wengine wawili.
Chanzo hicho kimesema ubadhilifu mwingine ni posho za vikao vya bodi na safari.
Kimebainisha kuwa, malipo ya fedha za wanafunzi vyuoni hutolewa kwa mfumo wa bajeti na kwamba katika mwaka mmoja wa masomo idadi ya vikao vya bajeti HESLB huwa ni 30 au 32.
Chanzo hicho kimesema kwa mwaka posho za vikao hivyo kutengwa kiasi cha Sh. milioni 600 na wanaopitisha bajeti hizo huwa ni wajumbe wa bodi wa kamati ya utoaji wa urejeshwaji mikopo (LARC) na menejimenti ya bodi.
Kamati hii ina wajumbe wasiopungua watano na wakurugenzi kumi wa bodi yaani menejimenti, kwa kila kikao mjumbe wa bodi hulipwa posho Sh. 500,000 huku wakurugenzi kumi kila mmoja hulipwa Sh. 400,000, kimesema chanzo na kuongeza:
Ukijumuisha gharama zilizosalia za posho za kujikimu kwa wajumbe wanaotoka nje ya Dar es Salaam, chai na gharama nyingine kikao kimoja hugharimu Sh. milioni 20, hivyo kwa vikao 30 ni Sh. milioni 600, kimebainisha.
Aidha, chanzo hicho kimesema kuwa, kiwango hicho kinachotumika kwa mwaka kwa ajili ya vikao hivyo ikizidishwa mara miaka saba ya bodi hiyo kukaa madarakani ni sawa na Sh. bilioni 4.2 kwa kamati moja ya bodi.
Hii ni sawa na kusomesha wanafunzi wa Shahada za Sayansi ya Jamii 1,400, ila kwa makusudi menejimenti imekuwa ikiagizwa iweke vikao vingi vya LARC wakati akijua kuwa wanafunzi wanateseka vyuoni na njaa kwa urasimu huu usio na tija, kimefafanua chanzo hicho na kuongeza:
Bajeti ya mwaka kwa vikao vya bodi na menejimenti ni Sh. bilioni 3 ambapo fedha hizi kama utawakopesha wanafunzi kwa mwaka jumla yao ni 1000, kimesema.
Aidha, chanzo hicho kimesema kuwa, katika mwaka wa masomo 2011/12 Baraza la Mawaziri kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi, chini ya Waziri Shukuru Kawambwa, lilitangaza kwenye vyombo vya habari vigezo vya utoaji mikopo.
Chanzo hicho kimesema licha ya vigezo vya utoaji mikopo kutangazwa lakini ilikiuka kwa kutoa mikopo kwa wanafunzi 600 wasiostahili.
Kimefafanua nafasi hizo zilizotolewa ni wanafunzi 45 wa mwaka wa kwanza wanaosoma shahada ya Law Enforcement Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambao ni waajiriwa wa Jeshi la Polisi nchini.
Tangazo lilitoa kipaumbele kwa kozi zote za afya ya binadamu na mifugo, ualimu wa Sayansi na Hesabu. Pia uhandisi, ualimu wa Art, na kozi za Sayansi ambazo zitazingatia uwezo wa muombaji kiuchumi na asiye na sifa linganishi yaani cheti na diploma, kimesema na kuongeza:
Kozi ya sayansi ya jamii, hizi si kozi za kipaumbele kwa taifa hivyo watapata fedha itakayokuwa imesalia kwa uhitaji kwa kupima mtu hali yake ya kifedha na shule ya sekondari aliyosoma na kuchukua ile gharama ya juu zaidi , ufaulu haukuwa na kigezo, mikopo isitolewe kwa mtu mwenye sifa linganishi yaani cheti/diploma au aliyeajiriwa, sehemu ya tangazo hilo imesema.
Chanzo hicho kimesema, wanafunzi hao ambao wengi wao wakiwa na sifa linganishi za cheti/ diploma kinyume cha mwongozo kwa mwaka huo wa masomo awali walikosa wote mikopo.
Aidha, kimesema kuwa baadaye wanafunzi hao kupitia uongozi waliwapatia mikopo kwa njia zisizoeleweka na suala hilo lilifikishwa kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu ambaye hakuchukua hatua zozote.
Wapo wanafunzi zaidi ya 100 watoto wa vigogo wenye sifa linganishi cheti/diploma wanaosoma kozi zisizo za kipaumbele vyuo mbalimbali ambao mwanzoni walinyimwa mikopo na sasa wamepata kinyume cha taratibu, kimebainisha chanzo hicho.
Chanzo hicho kimesema kuwa, wanafunzi hao wa vigogo walisoma shule za sekondari zenye ada kubwa kati ya Shilingi milioni tatu hadi saba na kwamba huko vyuoni hawasomi kozi za vipaumbele kama tangazo lilivyoainisha.
Waliosoma shule za Sekondari Fedha Boys na Girls ni wanafunzi 29, Marian Girls Bagamoyo wanafunzi 41, St. Marys wanafunzi 200, Laurentine International wanafunzi 20, Baobao Sekondari wanafunzi 40, St. Francis Mbeya wanafunzi 28, Loyola high school wanafunzi 60 na waliosoma nje ya nchi wanafunzi 10, kimebainisha chanzo hicho.
Chanzo hicho kimetoa ubadhilifu mwingine uliofanywa na vigogo hao kuwa ni matumizi ya Sh. milioni 300 kwa ajili ya kuhonga ili kuzima zoezi la kuiwajibisha Bodi hiyo baada ya kuundwa Tume ya Rais kuichunguza.
Katika hatua nyingine, chanzo hicho kimesema kuwa katika mwaka wa masomo 2010/11, bodi ilitangaza tenda ya 'scan' fomu za wanafunzi na kampuni iliyokuwa imeshinda ni Digital Scap na kupewa barua ya kufanya tenda hiyo lakini uongozi ulitengua maamuzi hayo na kuipa kampuni ya Koseke.
Hili linafahamika mpaka PPRA lakini hadi sasa hakuna hatua zilizochukuliwa, kimesema.
Pia chanzo hicho kimesema ubadhilifu mwingine ni bodi hiyo kujilipa mishahara na mikopo mikubwa ya aina mbili yenye riba ya asilimia mbili tu isiyo na uwiano na watumishi wengine.
Jumla ya mikopo iliyotolewa kwa watu hawa 16 ni Sh. 2,560,000,000, kiukweli fedha hizi ni sawa na kutoa mikopo kwa Watanzania 853, kimebainisha.
Pia chanzo hicho kimesema unyanyasaji wa wafanyakazi HESLB umesababisha wafanyakazi watatu waliofukuzwa na kushinda kesi hiyo iliyokuwa mahakamani Bodi kulazimika kuwalipa fidia ya Sh milioni 300.
Katika hali isiyo ya kawaida, chanzo hicho kimesema, toka mwaka 2005 Bodi hiyo ianzishwe mikopo iliyotolewa na inapaswa kurudishwa ni Sh. Bilioni 300 lakini hadi sasa fedha zilizokusanywa ni Sh. Bilioni 9 tu sawa na asilimia 3.
NIPASHE ilimtafuta Mkurugenzi Mkuu wa Bodi hiyo ili kupata ufafanuzi wa madai hayo lakini ilijibiwa na mtu wa mapokezi kuwa yuko nje ya mkoa kikazi.
Licha ya kupigiwa simu yake ya mkononi na kutumiwa ujumbe mfupi, hakupokea wala kujibu ujumbe.
Chanzo: Nipashe - Agosti 26, 2012
JK mpe Mwakyembe wizara mama ya bodi ya mikopo
Duh iyo hatari na ndio maana wanatupa asilimia 20 za mkopo
ruhi JF-Expert Member
kwa sasa tufaneje? na hali inazidi kua mbaya?
Hii li serikali libovu mpaka linatia hasira. ningekuwa na uwezo ningepindua hili liserikali. haya yote yanatokea na mengine mengi tuu, mabilioni kule uswisi, pesa zinaliwa kwenye halimashauri, walimu hawalipwi vizuri, madaktari shida tupu, dawa hospitali za kubabaisha, vitabu mashuleni hakuna, hapo hapo tunasamehe kodi kwenye migodi, misaada kibao kutoka nje, pesa hazionekani zinafanya nini, viongozi hawajali, wabunge wanajiongezea mishahara utadhani wao ndo wafanyakazi bora kuliko daktari au mwalimu na wengineo, aaaaaaaaarrrrrrrrrrrrrrrggggggggggggggghhhhhhhhhhhh!!!!!!!!!!!!!!!!!!!. hii ni SERIKALI AU KUNDI LA MAJAMBAZI?????
p_prezdaa JF-Expert Member
Kiliooooooooooooo, kiliooooooooooooooooooo, kiloooooooooooooo, kilio cha samaki machozi kwenda na majiiiii
dah!! watu watateketea sana kwa moto...hawana hata huruma mtoto wa masikini unampa asilimia sifuri wakati pesa za kujilipa mishahara mikubwa ipo..
Kingo JF-Expert Member
Kila mbuzi hula kulingana na urefu wa kamba yake, akiwa karibu na majani atakula majani kama ni marando/matembele yeye atakula tu! Na siku hizi mbuzi wa mjini wanakula hata maembe na ugali wa watoto, halafu sisi tunashangilia ... ooh ona mbuzi wa mjini.. wa kisasa hawa... hata ugali na maembe wanakula...!!!
Kula na mimi nile
Mimi nina swali moja tu,
First Year wa 2012 mkopo upo au haupo??
ole wao watunyime mkopo wakati siri yao imefichuka....
Messages: 24,955
Likes Received: 37,495
Lakini tujiulize waziri mhusika nini atafanya baada ya kashifa hii kuibuliwa leo. Si ajabu kashifa hii ikapita hivi hivi kwasababu mawaziri wengi hawana ujasiri wa kuchukua maamuzi mazito. Kuna mawaziri kila baraza linapovunjwa na kuundwa upya wao wamo lakini utendaji wao hauridhishi kabisa.Kweli kupeana vyeo kama sadaka ni jambo baya sana na la kuisikitisha na kuathiri taifa kwa kiasi kikubwa.
Ufisadi huu ni wa kutisha na wanaoteseka ni wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu ambao kila wakati hupigwa mabomu.Wanafunzi wakiandama wanaambiwa wanatumika kisiasa kumbe ni kwasababu ya wazembe wachache tu.
Uozo nchii umekuwa kama wimbo kwasababu raisi na mawaziri wake wamekuwa ni wazito kuchukua maamuzi magumu na kubaki kuwa watu wa maneno zaidi kuliko vitendo. Hivi kweli kama raisi na baraza lake la mawaziri wangekuwa wanachukua maamuzi magumu kama haya ya mh. Mwakyembe na mh. Kagasheki uozo huu kweli ungeendelea? Nani angekubali kuvuliwa madaraka na kufikishwa kwenye vyombo vyo dola? Rais asipotimuwa mawaziri wazembe na wasiowajibika nani tumlaumu?
Tangu baraza jipya liundwe ni mawaziri wawili tu ndio wanaoonekana kuchukua hatua lakini wengine utadhani wizara zao hazina madudu haya au wako likizo. Hizi tuhuma za ufisadi zilizoibuka bodi ya mikopo zinatosha kabisa kuwaamsha hawa mawaziri wengine nao waanze kuchukua hatua vinginevyo maendeleo katika taifa hili itakuwa ni ndoto.
Raisi kikwete ukiwa mkali kwa mawaziri wako utendaji wao utaonekana lakini mkienda kwa kubembelezana wewe ndio umma utakuja kukulaumu kwani wewe ndio mteuzi na mwenye mamlaka juu yao.
Taarifa hii ya gazeti labda itawaamusha wa-TZ. Bodi hii ni kama tulivyosikia ajira za BoT. Kuna baadhi ya watu pale unamkuta baba yuko kwenye bodi, dada ni muajiliwa na kaka ni muajiliwa hapo hapo, siyo kwa sifa bali ni kwa sababu kuna pesa ya kuchezea.
Bodi haijawahi kupata kiongozi. Mkurugenzi mkuu anayelipwa zaidi ya mil 13 siamini kama ni mtu mwenye akili timamu. Ukimuona si mtu wa kuhangaika kufikiri ili kuboresha hali ya utendaji.
Hata ukiangalia background yake siyo mtu anayestahili kushika nafasi hiyo. Amekulia NBC enzi za ukiritimba na kama kawaida ya NBC yetu kazi muhimu ilikuwa ni kuchota pesa tu! Hajawahi kuwa kwenye taaisis ya elimu ya juu yoyote.
Bodi haina sera! Kila mwka inaunda upya na ukiangalia sera zenyewe zinategemea matatizo ya mtu Fulani au mkubwa Fulani.
Kuna mwaka walilipia wanafunzi kusoma Masters kwa sababu tu kulikuwa na ndugu yake na mwaka uliofuata wakaachana na sera hiyo.
Sasa juu ya kuwanyoosha, hiyo tushau! Hakuna mtu ikulu! Rais wetu kila kitu ni majaliwa ya mwenyezi. Nimekuwa nikidhani labda mkuu wetu anafanya kwa makusudi lakini sasa naamini kabisa kwamba kuna tatizo la maumbile. Baada ya kuwapa miradi wanawe, kiongozi wetu anaamini nchi imeendelea!
Majungu tupu
Majungu matupu ,nasikia kuna kigogo mmoja (jina tunalo) amepigwa chini kwa ku "foji"vyeti ndio anawachafua wenzake kuandika makala hii ya uchochezi....tunasubiri majibu ya bodi maana hata ile tume iliyoundwa mwaka jana chini ya Prof Maboko ilibaini Bodi iko sawa,na inajitahidi sana kwa kasma waliokuwa wanapata kwa mbinde toka Wizara ya Elimu na si Wizara ya Fedha!!
Acha tusubiri majibu toka kwa Bodi husika ila wanasikitika sana maana huyo kigogo alietolewa bila kufikishwa mahakamani,yatampata asiyoyatarajia maana sheria ni msumeno!
Dah hi kasheshe.EWE MUNGU TUJALIE TUSINYIMWE MIKOPO.ameen.
usungilo JF-Expert Member
king roja said: ↑
hivi hakunaga member wa jf bodi ya mikopo? Haya mambo ya jina tunalo tumechoka nayo. Tunahitaji mtu atajwe tumzomee mtaani na kumpiga mawe. Au kwa sababu wanalipwa vizuri ndo maana hawaleti uozo wao huku?
tunataka majina ya wanaohujumu bodi tuwafuatilie zero distance
Hii ndio Tanzania!!!!!!!!
I miss MWANAHALISI....Hii mambo ya "Jina Tunalo" "Majina Tunayo" huwa hakuna... wangeweka hapo majina na hata jina la kigogo Mwenyewe+ Namba za simu .....Kuhusu kujua kuwa bodi ya mikopo ina ubadhirifu kila mtu anajua issue ilikua nani anafanya ubadhirifu ambapo hata "chanzo cha hii makala" hakijamtaja....Same Old story za kulindana na kutengeneza mianya ya Rushwa katika tasnia ya Habari.... hapa ni huyo Kigogo au vigogo kusoma hii story na kumtafuta muandishi wampoze ili aipotezee hii issue......
| 2018-01-17T13:44:09 |
https://www.jamiiforums.com/threads/kashfa-nzito-zaibuliwa-dhidi-ya-ubadhirifu-bodi-ya-mikopo.313857/
|
[
-1
] |
Mchezo Kuwasili Plane Parking
You alikuwa utume ngumu - Hifadhi ya ndege. Ili kufanya hivyo ni lazima kutumia funguo arrow kwa hoja ndege kuwekwa katika uteuzi kwa nafasi hii.
Online michezo Kuwasili Plane Parking - kucheza kwa bure bila usajili katika mchezo michezo flash Kuwasili Plane Parking online zxgame9.com.. Kama wewe kama mchezo online Kuwasili Plane Parking - kushiriki kwa rafiki yako.
Jinsi ya kucheza mchezo online Kuwasili Plane Parking. Udhibiti wa mchezo Kuwasili Plane Parking. You alikuwa utume ngumu - Hifadhi ya ndege. Ili kufanya hivyo ni lazima kutumia funguo arrow kwa hoja ndege kuwekwa katika uteuzi kwa nafasi hii. Wewe ni juu ya kazi si muda mwingi na kwa hiyo ni muhimu kwa haraka.
Kiwango cha mchezo huu: Alicheza: 249
Kuwasili Plane Parking ( Kura1, middlecover binafsi: 5/5)
Gravitation zone
Operation Tupa zawadi
Bombay teksi - 2
Nishati ya jua surfer
Kuwaokoa Tatu Sayari
Global Uokoaji
Anga Drakojan
Mgeni uvamizi 2
Metal hasira
Mars kukutana
| 2018-10-16T22:38:55 |
http://tz.zxgame9.com/2080/
|
[
-1
] |
Infobox music genre with invalid colour combination All articles with unsourced statements Articles with unsourced statements from February All stub articles. For a better experience, please enable JavaScript in your browser before proceeding. Streams Videos All Posts. Ya bure yenu mayowe, huyu sasa siye wenu. Zanzibar Tanzanian music Kenyan styles of music Music genre stubs Tanzania stubs.
Mtajirusha wenyewe, roho na akili zenu x2 Na mseme, x2 msizuweee kilicho mtowa kwenu. Cholo anasema taarabu asilia imeweza kuendelea kuheshimika hasa katika Visiwa vya Zanzibar ambapo ndipo palipoasisiwa muziki huo. Namshauri asikate tamaa kujifunza ni kwa nini wakongwe kama Maulid Taarab asilia, Chimbeni Kheri na wengineo bado wanavuma? Joined Jan 20, Messages 2 Likes 0 Points 0.
Infobox music genre with invalid colour combination All articles with unsourced statements Articles with unsourced taarrab from February All stub articles. Ya bure yenu mayowe, huyu sasa siye wenu. Streams Videos All Posts. Log in Aslia Up.
Anasema mziki huo wa taarabu asilia umeweza kukubalika pia katika nchi nyingi za Ulaya hali ambayo inachangia wao kufanya maonyesho katika nchi za mbalimbali za Bara hilo. Said57 New Member Jun 26, Mambo ya mod kina bwabwa na welawela vijiwe vyao basi tabu tupu kama si karaha kabisa. He subsequently decided to send to Egypt Mohamed Ibrahim to learn music and he also learned to play the Kanun.
While the usual harmonium is missing, there is a more standard organ to taarab asilia its position in the taara. InZanzibar’s second music society, Ikwhani Safaa Musical Clubwas established and continues to thrive today. Joined Aug 3, Messages Likes 4 Points For anyone wishing yaarab look into the many, many facets of taarab, taarab asilia is one necessary stop along the tour.
The word Taarab is a loanword from Arabic.
Yaani raha hizi tunazikosa siku hizi kwa hizi vurugu mechi na matusi wanayoita “modern taarab’. Forums New posts Search forums.
taarab asilia Katibu huyo alisema kundi hilo limefanikiwa kutawanyika katika maeneo mengi ya Ulaya na Asia lengo likiwa ni kutoa burudani ambayo imekuwa ikikubalika zaidi. Alisema katika miaka ya hivi karibuni kumeibuka taarabu ambazo zinadai kuwa zinaenda na wakati jambo ambalo alilipinga kwa kusema taarab asilia mziki wa taarabu unaharibiwa na watu ambao amewataja kuwa wenye tamaa.
By using this site, you agree to the Terms of Use and Privacy Policy. Wacha pupa na vishindo, Mapenzi siyo papara.
Qucosa – Leipzig: Women’s Taarab lyrics in contemporary Zanzibar
taarab asilia Rainy Day Relaxation Road Trip. Drinking Hanging Out In Love. Others would surely include the taarab of other taarzb, including the strong Mombassa tradition. Ikhwani Safaa Music Club feat: Kundi hili lenye maskani yake katika visiwa vya Zanzibar lilianzishwa katika mwaka huo likijulikana kama Nadi ikwaan Safaa.
Zuhura Taarab (Tamasha Records) Music – Free MP3 Download or Listen |
Upon his return, he formed the Zanzibar Taarab Orchestra. Hapo sijakupa kipande kimoja kitamu cha shairi kilichowahi kuimbwa na kundi hilo na Al marhum ,gwiji, ustadh, Seif Salim katika wimbo wa “kheri Pendo la NdoNdoNdo” Kheri pendo la Ndo! Joined Mar 11, Messages 3, Likes 22 Points This article about a music genre is a stub.
The club is a musical institution on the small island, founded by the sultan of Zanzibar taarab asilia Pendo la Wasikitisha Love Regrets Them.
NYUSHA VYSHE FREE DOWNLOAD
| 2020-03-29T11:37:13 |
https://leperroquetbasque.info/taarab-asilia-83/
|
[
-1
] |
Baba ya mwanafunzi aliyetaka kuingia Ikulu asema mwanawe anaugua maradhi ya akili ▷ Tuko.co.ke
Baba ya mwanafunzi aliyetaka kuingia Ikulu asema mwanawe anaugua maradhi ya akili
Maoni: 1319
- Mwanafunzi huyo alipigwa risasi kwenye bega lake la kushoto akijaribu kuingia Ikulu
- Babake anasema mwanawe ana maradhi ya akili na kwamba alianza kuonyesha dalili hizo Februari 2018 baada ya kukamatwa katika mbuga ya wanyama ya Mlima Kenya
- Alilazwa hospitalini kwa muda wa wiki mbili na amekuwa akipata msaada kutoka kwa msaikolojia katika chuo kikuu cha JKUAT
Baba ya mwanafunzi anayesomea uhandisi katika Chuo Kikuu cha Kilimo na Teknolojia cha Jomo Kenyatta (JKUAT), ambaye alipigwa risasi akijaribu kuingia Ikulu, anasema mwanawe ana matatizo ya kiakili.
Brian Kibet Bera alipigwa risasi kwenye bega lake la kushoto, baada ya kuchomoa kisu alipoagizwa asimame na walinzi wa Ikulu munamo Jumatatu, Juni 10 alfajiri.
Brian Bera ambaye baba yake anasema anaugua maradhi ya akili. Picha: Facebook
Habari Nyingine: Sintofahamu yaibuka baada ya mwanafunzi wa JKUAT kupigwa risasi akijaribu kuingia Ikulu
Babake, David Bera, anasema mwanawe amekuwa akilazwa hospitalini mara kadhaa baada ya kuanza kuonyesha dalili za maradhi ya akili na hii ni kwa mujibu wa gazeti la Standard.
"Munamo Juni mwaka jana, Brian alilazwa katika hospitali ya Reale mjini Eldoret kwa kipindi cha miezi miwili. Baada ya kutambuliwa kuwa anaugua maradhi ya akili," Bera alisema huku akithibitisha kwa kuonyesha stakabadhi za hospitalini.
Kulingana na ripoti kutoka hospitalini, Brian alitambuliwa kuwa na matatizo ya kuzungumza na mpenda vita na ikabainika alihitaji msaada kutoka kwa mtaalamu wa masuala ya kisaikolojia.
"Baada ya kuondoka hospitalini mwaka jana, hali yake iliimarika na hata kuomba kurejea shuleni kumalizia masimo yake na alihudumiwa na kupewa matibabu ilivyofaa," alisema.
Habari Nyingine: Magazeti ya Kenya Jumatano, Juni 12: Babake mwanafunzi aliyejaribu kuingia Ikulu amtetea mwanawe
Baada ya kisa cha kupigwa risasi, Brian alipelekwa katika Kituo cha Polisi cha Kileleshwa na kusajiliwa kabla ya kupelekwa katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta kwa matibabu ambapo madaktari walibaini risasi hiyo ilitoka kupitia kwa mgongo wake.
Ilivyoripotiwa awali na TUKO.co.ke, mwanafunzi huyo aliandika katika ukurasa wake wa Facebook kuwa angeingia Ikulu kumuua mwizi asiyejulikana pamoja na wenzake na atakuwa anatekeleza kazi ya Mungu aliyomtuma kufanya.
"Mwizi ni Rais Uhuru Kenyatta na wenzake. Kesho nitaingia Ikulu. Mungu amenituma kutoa hukumu kwa kila mwizi na mwenzake. Kutoka kwa aliyekuwa mkuu wa Ethiopia aliyeitwa Brian Kibet Bera," ujumbe wa Kibera katika Facebook ulisema.
Marafiki walijaribu kumzuia kutekeleza azimio lake lakini alikataa na ni kupitia taarifa ya Iliku ndipo walipofahamu hali alimokuwa mwenzao.
Dada ya mshukiwa, Vivian Bera ambaye ni mwanafunzi katika Chuo Kikuu cha Eldoret ni miongoni mwa waliojaribu kumtafuta kwa simu lakini hawakumpata.
Babake Brian Bera, David Bera asema mwanawe anaugua maradhi ya kiakili. Picha: Standard
Habari Nyingine: 3 wachomeka kiasi cha kutotambulika katika gesti jijini Nairobi
"Baada ya kunizua alikataa kuchukua simu zangu baada ya kumuuliza kuhusu ujumbe huo aliokuwa ameandika...anaitaji matibabu ya akili," alisema Vivian, na kusisitiza kuwa kakake si muhalifu
Bera alimsifu mwanawe ambaye ni kifungua mimba katika familia ya watu sita kwa kudokeza kuwa alikuwa miongoni mwa wanafunzi waliopita mtihani yao katika shule ya Kitale kwa kupata maksi 401 katika KCPE kisha Nairobi School alipoibuka na alama ya A.
"Katika mwaka wa 2016 tulianza kuona mabadiliko akiwa nyumbani. Alianza kujitenga na kujifanyia mambo yake. Pia alikuwa na uhasi kuhusu maisha na kila kitu," Bera ambaye ni mwalimu katika taasi ya kiufundi ya Ol’lessos alisema.
Bera alisema aligundua tatizo la mwanawe lilikuwa limeongezeka wakati alipokea simu kutoka kwa afisa wa polisi wa Naromoru na kufahamishwa kuwa Brian alikuwa amekamatwa baada ya kupatikana ndani ya Mbuga ya Wanyama ya Mlima Kenya.
Habari Nyingine: Jamaa afichua walivyowawinda makahaba Nairobi na kuwaua kisha kuuza viungo vya miili yao
Alifika na kumchukua mwanawe na kumpeleka nyumbani na ghafla kuanza kuatafuta msaada katika hospitali mbalimbali na pia katika madaktari wa kiasili.
Tabia yake ilianza kubadilika alipoanza kujitenga na familia yake kwa kujifingia katika chumba chake ama wakati mwingine kuenda kutembea katika msitu wa Mlima Elgon ulio karibu na boma lao mjini Kitale.
Bera anasema munamo Juni mwaka jana mwanawe alipotea kwa muda na kisha kupatikana kwa binamuye Athi River.
Jamaa yao huyo alimweleza kuwa Brian alikuwa mbishi sana.
"Mwanangu hajawai patikana katika visa vyovyote vya uhalifu tangu utotoni. Kwanza miongoni mwa watoto wenye nidhamu,mwaminifu na tena mwerevu bila kisa chochote cha kutumia mihadarati. Ni mwanachama wa kanisa la SDA.
" mbi langu kwa serikali ni kutomshitaki mwanangu kwa sababu alichokifanya ni kisa cha kiakili. Brian ni mgonjwa na anacho kihitaji ni huduma ya magonjwa ya akili.Kumpeleka mahakamani ni kumuathiri zaidi," baba aliirai serikali.
Msemaji wa chuoni anakosomea Hindzano Ngonyo, amethibitisha kuwa chuo hicho kilikuwa na ufahamu wa tatizo la mwanafunzi huyo na alikuwa akipokea msaada wa kisaikolojia.
"Alikuwa miongono mwa wanfunzi ambao walikuwa wakihudumiwa na idara yetu ya ushauri," alidokza Ngonyo.
Real Madrid watua Ufaransa kumnasa nyota wa PSG, Neymar
| 2019-08-24T05:38:43 |
https://kiswahili.tuko.co.ke/307831-baba-ya-mwanafunzi-aliyetaka-kuingia-ikulu-asema-mwanawe-anaugua-maradhi-ya-akili.html
|
[
-1
] |
IGP Mwema heshima uliyoijenga inapotea | Gazeti la Jamhuri
Miezi ya Desemba 2012 na Januari, 2013 imenitia hofu. Imenitia hofu baada ya kuwapo matukio mengi ya wizi, ujambazi na ukatiri dhidi ya binadamu. Wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha wamelazimia kuandamana baada ya majambazi kuwa wanawavamia kwenye mabweni yao na kuwapora kompyuta za mkononi, fedha na vitu vya thamani. Imeelezwa kuwa hadi wanafikia uamuzi huo tayari walikwishaporwa laptop zipatazo 300.
Kwa mkoa wa Kagera ndani ya miezi hiyo miwili, polisi wanne wameuawa na wananchi. Mkoani Arusha na Mara, polisi wanne wamekamatwa wakisafirisha meno ya tembo na wengine bangi. Mirungi imeelezwa kushamiri Arusha na Kilimanjaro. Wimbi la ujambazi limeibuka na kuongezeka kwa kasi ya kutisha.
Kabla ya Rais Jakaya Kikwete kuchaguliwa kushika wadhifa huo, majambazi yalikuwa yanatamba hapa nchini. Kikwete akakuteua wewe Said Mwema kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini. Mwema ukatekeleza kwa vitendo ahadi ya Kikwete kwa wananchi kuwa angedhibiti ujambazi.
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Hili nimewahi kulisema na wala sioni aibu kulirudia kuwa Kikwete amefanikiwa kwa kiasi kikubwa kudhibiti ujambazi walau kwa miaka karibu nane sasa aliyokaa madarakani. Ila kwa bahati mbaya, hali imeanza kuharibika.
Huko Tabata risasi zimeanza kusikika tena. Kigamboni majamabazi wamejihalalishia kila mali aliyochuma kwa tabu Mtanzania. Mwanza nako tumesikia mivumo mwishoni mwa mwaka. Taarifa mbaya za polisi kurejea katika mchezo wa kushirikiana na majambazi na kisha kubambikia kesi wananchi zimeanza kufika tena kwenye vyumbo vyetu vya habari.
Mwema ulivyoingia madarakani, posho za polisi zilikuwa zinatolewa kwa wakati. Kwa sasa taarifa zilizonifikia ni kwamba kasma ama nyingi zimefutwa au zinatolewa kama hisani. Ulivyoingia taarifa za magari ya polisi kukosa mafuta ilikuwa zimepotea, lakini hawa askari wako sasa wanalalamika.
Wanasema polisi anakwenda kwenye lindo kuzunguka mji kama Dar es Salaam usiku mzima anapewa mafuta lita 10. Hivi huyu unatarajia apambane na jambazi aliyejaza tenki zima na tena wakati mwingine amekwishalifanyia mbinu gari lake linajaza hadi lita 200 kwa wakati mmoja?
Yapo maneno yanasemwa na mimi sitaki kuyakubali. Wapo wanaosema kuwa Mwema sasa umeona muda wako wa kustaafu umekaribia hivyo umeamua kupumzika kazi. Wengine wanasema kwa uzoefu wakuu wa polisi wengi wanapokaribika kustaafu uhalifu uongezeka.
Wanasema uhalifu uongezeka kwa sababu mabosi wengi wanakuwa wakichuma fedha za kustaafia. Nieleweke vyema, sisemi Mwema naye anachuma kwa sasa, lakini aibu hii ya polisi kukamatwa na meno ya tembo, kuuawa na wananchi wakiwa ‘kazini’ inatia shaka.
Mwema jiulize, ni wapi umelegeza kamba ubane. Utastaafu kwa heshima kubwa ikiwa utaondoka madarakani Watanzania wanaacha milango wazi. Imani uliyoijenga kwa wananchi juu ya polisi, sasa inaanza kupotea kwa kasi, hasa zinaposikika taarifa kuwa polisi wanasindikiza magogo ya mbao, meno ya tembo na kuwajulisha majambazi wapi wakaibe kisha wao wanafika baada ya tukio.
Nasema haya uliyakuta na ukayadhibiti, nguvu uliyokuwa nayo imepotelea wapi? Mwema linda heshima yao. Wabane polisi, lakini wapatie haki zao wachape kazi kwa nguvu na kuijenga Tanzania iliyosalama, kiasi kwamba historia ikukumbuke. Mungu ibariki Tanzania.
Previous: TCRA kuvifungia vituo vya runinga
Next: Ufisadi washamiri TTCL
| 2019-06-16T18:53:18 |
http://www.jamhurimedia.co.tz/igp-mwema-heshima-uliyoijenga-inapotea/
|
[
-1
] |
Ulanguzi katika soka :BBC imegundua - BBC News Swahili
Ulanguzi katika soka :BBC imegundua
https://www.bbc.com/swahili/habari/2015/07/150720_fifa_bbc
Image caption klabu ya Champasak matatani kwa ulanguzi wa wachezaji
Wachezaji wa Afrika,miaka 14 wanasafirishwa kiharamu barani Asia, BBC yagundua.
Wanalazimishwa kusaini mikataba kinyume cha sheria.
Wachezaji 6 bado wako katika klabu ya Champasak United baada ya klabu hiyo mjini Laos kuwachukua watoto 23 kutoka Afrika magharibi kuwapeleka chuo bandia cha soka mwezi Februari.
Kanuni za FIFA zimeharamisha kuwasafirisha watoto chini ya miaka 18 kwa klabu za kigeni au chuo cha soka.
"FIFA inawasiliana na mashirikisho kadhaa kukusanya maelezo na kuchunguza suala hilo ili ihifadhi maslahi ya watoto,'' amesema afisa wa FIFA.
Image caption wachezaji wajikuta katika dhiki Laos
Inadaiwa kuwa klabu ya Champasak United inatarajia kufaidi kwa kuwauza wachezaji hao baadae.
Ikiwa na makao yake mji wa kusini wa Pakse, klabu hiyo imekanusha madai yote.
Kinyume kabisa na sheria za shirikisho la soka duniani, kalbu hiyo imewashirikisha wachezaji wadogo kati ya miaka 14 na 15 katika ligi za msimu huu.
Mchezajiwa miala 14 wa Liberia,Kesselly Kamara, hata amewahi kufunga bao.
Kabla ya kuchezea timu hiyo ya wakubwa, anasema kuwa alilazimishwa kusaini mkataba wa miaka 6.
Licha ya kusaiani mkataba huo, na kuahidiwa mshaharana makao, Kamara anasema kuwa hajawahi kulipwa na amelazimika kulala sakafuni katika uwanja - kama walivyofanya pia vijana wengine waliosafiri naye.
"ilikuwa mbaya sana, kwasababu huwezi kuweka watu 30 kulala katika chumba kimoja,'' Kamara, ambaye sasa anachezea klabu moja nyumbani Liberia, ameambia BBC.
Wote walisafiri kujiunga na chuo cha mafunzo ya soka cha Asia 'IDSEA Champasak' baada ya kupata mualikko kutoka kwa mchezaji wa zamani wa kimataifa kutoka Liberia Alex Karmo, ambaye kisha alikuwa kapteni wa klabu hiyo.
Mualiko huo ulipokewa kwa hamu kwa kuwa Liberia haina chuo chake cha mafunzo ya soka, licha ya kuwa nchi ya pekee Afrika kuwahi kutoa mchezaji bora wa FIFA duniani- George Weah (1995).
Image caption Alex Kamara anadai kuwa kocha wa watoto
"Ni chuo tapeli ambacho hakijawahi sajiliwa kisheria ,'' amesema mwandishi wa michezo nchini Liberia na mhamasishaji wa soka Wleh Bedell, ambaye alisafiri na kundi hilo mjini Laos mwezi Februari kisha akarejea nyumbani.
"Ni chuo ambacho hakina mkufunzi, wala daktari. Karno ndiye aliyekuwa kocha, meneja biashara, kila kitu ni yeye. Ni ajabu kweli.''
Image caption watoto wa Afrika magharibi waliohadaiwa
Kufuatia shinikizo kutoka kwa FIFA, na Umoja wa wachezaji duniani FIFPro, Champasak ililazimika kuwarudisha watoto 17 kutoka kundi lililosafirishwa na akiwemo Kamara miongoni mwao, miezi 3 iliyopita.
Lakini wachezaji 6 walikataa kurudi.
FIFPro inasema kuwa hao 6 wamesaini mikataba waliyoletewa na Karmo, anayejidai kuwa 'meneja wa wachezaji kutoka Afrika wa klabu ya Champasak' na rais wa klabu Phonesavanh Khieulavong.
Image caption mkataba waliosaini
Hii imesababisha Champasak kutowalipa vijana hao chochote huku ikiitisha matakwa yasiyowezekana iwapo vijana hao watataka kuondoka klabu hiyo.
Hata hivyo Karmo amesisitiza kuwa wachezaji hao wamalishwa milo mitatu kwa siku na wanalipwa kila mwezi.
"Hatuwezi kuwapa watoto hao mikataba ya kitaalamu,ila ni mikataba inayoruhusu kuwapa marupurupu,'' Khieulavong ameambia BBC.
Khieulavong wala Karmo hawakukanusha kuwepo watoto wadogo katika vyuo hivyo japo raia huyo wa Liberia anadai kuwa ni kijana mmoja wa miaka 16 - kutoka Guinea.
BBC imegundua kuwa kuna watoto 5 zaidi kutoka Liberia katika klabu hiyo.
Pamoja na wachezaji wakubwa 8 (6 kati yao wa Liberia, mmoja wa Ghana na mmoja wa Sierra Leone) wote wanaishi katika ''mazingira ya kutamausha'' kama anavyoeleza Bedell.
Kwa miezi 5 wamekuwa wakilalia magodoro membamba katika chumba kimoja ambachi hakina hata madirisha wala konji katika mlango wake.
"ni vigumu sana kuishi katika chumba ambacho hakina madirisha. Ilifanya kualal kuwa vigumu sana kwakuwa saa zote unafikiria maisha yako,'' amesema Kamara.
"Wachezaji wamewekwa katika mazingira sawa na yale ya wakati wa vita vya ndani vya Liberia ambapo watu walilazimika kukimbia makwao n akutafuta hifadhi katika majengo tupu na ukumbi,'' Bedell, ambaye alishuhudia vita vya ndani nchini mwake mwaka wa 1989-96 na 1999-2003, ameambia BBC
Uhuru wa wachezaji hao ulibanwa zaidi baada ya visa zao kumalizika mnamo mwezi Machi na kulazimika kuishi kama wahamiaji haramu.
Image caption watoto hawana visa wala vibali vya kufanya kazi
Sasa wana matumaini ya kupata vibali vya kufanya kazi, japo hili ni vigumu kwa kuwa wote hawajafika umri.
Karmo, ambaye anasisitiza kuwa alimlipa Kamara, amekiri kuwa wachezaji 14 wa Afrika kweli hawana vibali vya kuajiriwa, lakini amehakikisha kuwa wanazo stakabadhi za kuishi mjini Laos.
"Hakuna anayeishi knyume cha sheria. Kila mmoja anacho kibali,'' ameambia BBC.
Huku klabu hiyo ikishikilia pasi zao za usafiri tangu kuwasili kwao, ni nadra sana kwa vijana hao kutoka nje ya uwanja huo ambako wanaishi na kufanya mazoezi mara mbili kwa siku.
Lakini licha ya masaibu yao, sio kila mtu anawataka watoke Laos.
"Mimi sitaki arudi nchini Liberia hadi afaulu ndoto yake,'' amesema Bella Tapeh, zazi wa mmoja wa vijana wa miaka 17 ambaye bado yupo Pakse.
Baadhi ya vijana waliorudi nchini Liberia wameambia BBC kuwa hawakulishwa vizuri, walilipwa kwa nadra sana na hawakupokea matibabu kutoka kwa klabu hiyo licha ya kuambukizwa malaria na homa ya tumbo kwasababu ya hali ilivyo.
Mmoja hata ameelezea kuwepo katika klabu hiyo ya Champasak, iliyozinduliwa mapema mwaka huu kuwa 'sawa na utumwa'.
"Hii ni hali ya dharura sana,'' Stephane Burchkalter,afisa wa FIFPro ameambia BBC.
"Inashtusha kwa FIFPro kuwa klabu kutoka Laos, ambayo - bila kuikosea heshima - ni nchi ndogo sana ya soka imewavutia wachezaji (ISHIRINI) walio chini ya umri kutoka Liberia bila FIFA kujua.''
Katika taarifa, FIFPro imesema kuwa wanashuku hiki ni kionjo tu ya hali ilivyo.
Shirika moja lisilo la kiserikali (<http://www.footsolidaire.org/>), linakisia kuwa takriba vijana wachezaji wa soka 15,000 wa umri mdogo wanasafirishwa kutoka Afrika Magharibi kila mwaka - wengi wao kinyume cha sheria.
FIFPro pia imetoa wito kwa FIFA ichukua hatua dhidi ya shirikisho la soka la Laos ambalo kufikia ssa limesindwa kuiadhibu klabu ya Champasak kwa kukiuka kanuni zake.
Ushahidi wa vilabu vinavyovunja sheria za kuwasajili wachezaji chini ya umri wa miaka 18 ni nadra sana japo klabu ya Barcelona imekutikana na hatia hii na imepewa marufuku ya miezi 14 ya kuwanunua wachezaji.
Wakati uo huo wazazi wa watoto 12 wamejikuta katika matatizo ya kifedha baada yakuchukua mikopo kugharamia $550 kuwasafirisha wanao mjini Laos. Mojawepo ya kesi hizo iko mikononi mwa polisi.
Kuna nafasi tatu pekee ambapo sheria hii ya FIFA ya kuwasafirisha wachezaji chini yamiaka 18 inaweza kutumika na zote hazitumika hapa.
| 2018-08-20T15:38:09 |
https://www.bbc.com/swahili/habari/2015/07/150720_fifa_bbc
|
[
-1
] |
UNBOUNDARIES NEWS: Wakulima, Wafugaji wajadili Katiba Morogoro
Wakulima, Wafugaji wajadili Katiba Morogoro
Wakulima wadogo na wafugaji kutoka mikoa yote nchini wanakutana mkoani Morogoro kujadili Katiba iliyopendekezwa, iwapo imezingatia maslahi ya wazalishaji wadogo.
Mkurugenzi wa mtandao wa vikundi vya wakulima Tanzania, MVIWATA Stephen Ruvuga, akizungumza mjini Morogoro, amesema pamoja na Katiba hiyo iliyopendekezwa kuangalia suala la haki za ardhi kwa wakulima bado wanaona haki zilizopo hazitoshelezi.
Naye Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania Deus Kibamba, akiwaasa wananchi kuepuka maneno ya kuonesha kuiomba serikali kufanya jambo kupitia katiba, hali inayoweza kuzua mtafaruku kama uliotaka kujitokeza bungeni pale kamati ya bunge ilipozozana na serikali ikitaka baadhi ya mikataba.
Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Eliya Ntandu amewaasa wakulima na wafugaji kuwa na ushirikiano usio wa kisiasa ili kuweza kusaidiana sambamba na makundi hayo kuwa na umoja wenye nguvu ili kuongeza uzalishaji na kuboresha soko la ndani, huku wakulima na wafugaji wakilalamikia mifugo kufa nyakati za kiangazi kwa kukosa mvua kutokana na uharibifu wa mazingira hususani ukataji wa miti ovyo.
Posted by santos chuwa at 9:31 AM
| 2018-12-13T19:54:27 |
http://santoschuwa.blogspot.com/2014/12/wakulima-wafugaji-wajadili-katiba.html
|
[
-1
] |
WordPress / UtilitiesEasy Upload Renamer for WordPress— Add-On kwa WorldWideScripts.netKujiunga na kulisha wetu kukaa hadi tarehe!Mpya! Kufuata yetu kama unataka!★★★★★Sehemu hii inapatikana katika 37 lugha nyingine!ArabicBengaliCatalan/ValencianDanishDutchEnglishEsperantoFinnishFrenchGermanGreekGujaratiHindiIndonesianItalianJapaneseKannadaKoreanMalayNorwegianPersianPolishPortugueseRomanian/Moldavian/MoldovanRussianSimplified ChineseSpanish/CastilianSwedishTagalogTamilTeluguThaiTraditional ChineseTurkishUkrainianUrduVietnameseKuishi PreviewViwamboAds
Easy Pakia Renamer Plugin kwa WordPress Kujenga moja kwa moja pretty, binadamu-someka SEO filenames kama wewe upload files yako vyombo vya habari kwa WordPress! Plugin hii itakuwa kubadili jina picha yako na attachments kama wewe upload yao kwa mechi cheo post yako au ukurasa. Kuongeza blog yako jina kwa uploads yako yote! Watumiaji ambao kushusha photos yako au kuwaona kwenye Google Image Search, na blog yako jina moja kwa moja ni pamoja na katika jina la faili. Hivyo kama mtu hotlinks, downloads au akiiba maudhui yako, jina la faili vyenye maandishi yako mteule, isipokuwa mtumiaji wa mwisho huenda kwa njia ya shida ya kutaja tena. Ni wazo kubwa ya kuwa na pretty, binadamu-someka, filenames ya maana. Badala ya DSC1234.jpg au image0001.jpg utapata filenames kama gulliverstravelblog.com-london-safari-01.jpg au thebestrecipes-ladha-apple-pie-02.jpg. Search injini upendo majina ya faili ya maana. Kupata PageRanks ya juu na Tafuta-injini yako Optimized uploads WordPress! Ila bado hatua nyingine: Unaweza kuchagua moja kwa moja kuweka WordPress attachment cheo kwa mechi post yako. Kwa urahisi Locate files yako baadaye katika WordPress Media Library: mafaili yote yako sasa maana, majina ya kueleweka, na wewe utakuwa kujua katika ambayo baada ya wewe kutumika yao. Kwa mujibu wa makubaliano katika SEO (Search Engine) jamii, filenames wote ni moja kwa moja sanitized na alifanya lowercase kufanya URL yako friendlier kwa injini za utafutaji. chaguzi rename na tabia Plugin ni configurable kwa ladha yako. Unaweza kuchagua kubadili jina attachments wote au picha tu. Kabisa Automatic! 1. Kujenga posta au ukurasa na kuwapa cheo 2. Pakia faili... 3... kusubiri kwa upload yako ili kukamilisha... 4 ya faili yako jina na cheo sasa mechi post! Customize Plugin kwa mahitaji yako Unaweza kuchagua kubadili jina tu picha uploads yako au Plugin kubadili jina uploads yako yote. Ni pamoja na aina na kuwatenga baada ya kutoka upload renaming Ingiza maandishi kwamba unataka kuweka katika mwanzo wa upload yako filenames, kwa mfano jina la blog yako. Unaweza kuchagua kutumia aidha '-' (dash) au '_' (underscore) kama separator ishara kati ya sehemu ya jina la faili. Kama wewe hawataki rename files yako kwa kutumia cheo, unaweza afya yake na kutumia kamba tu prepend utendaji. Unaweza kuchagua kuwa na sifa Title la faili uploaded kuwa sawa kwa kila attachment (kwa mfano "Post Title") au kwa pamoja na idadi vinavyolingana attachment (kwa mfano "Post Title 1", "Post Title 2" na kadhalika), au kuchagua si kwa kuweka Title sifa wakati wote. Jinsi ya Kufunga Unaweza kufunga Plugin hii manually na FTP upload (kuweka Plugin folder moja kwa moja kwenye server yako) na inleda Plugin WordPress Plugin katika screen, au unaweza kutumia nusu moja kwa moja WordPress admin jopo upload mbinu. Rahisi hatua kwa hatua ufungaji maelekezo ni katika readme.txt faili ni pamoja na katika download yako. Changelog 2.1.1 = = * Bugfix: Upload directory si kuweka kwa usahihi wakati kuweka kwa Media Library. * Ingia habari troubleshooting wakati upload directory data ni kukosa 2.1.0 = = * Aliongeza baada ya aina ya kuchuja 2.0.0 = = * Matumizi ya maktaba ya nje propietary kwa renaming na kamba usindikaji: Mchakato wa UTF-8 na masharti ISO-8859-15 kwa kutumia desturi maktaba hata katika kesi ambapo PHP Multibyte kamba ugani na PCRE UTF8 ugani hazipatikani. * Filenames wote daima Herufi za chini. * Aliongeza kuchuja kubadili wahusika accented na kuwateka punctuation. * Fallback ya awali `baada slug` (Permalink) wakati baada ya cheo renaming inashindwa. * Fallback ya awali filename wakati kichwa cha habari na Permalink renaming kushindwa. * Ujumbe Hitilafu wakati akijaribu kupakia faili kwamba itakuwa kusababisha attachment kuvunjwa juu ya mitambo Windows-msingi. * Hesabu wote wawili Byte na tabia urefu wa masharti wakati kuzingatia maximums kuruhusiwa. * Mpya chaguzi: `wahusika cheo use`,` kutumia picha ya awali metadata wakati possible`. 1.1.5 = = * Corrected mdudu kwa uppercase utunzaji ugani. * Aliongeza chaguo kubadili filenames kwa lowercase. * Truncate njia muda mrefu sana na filenames (zaidi ya 200 wahusika). 1.1.1 = = * Plugin sasa seti slug ya ukurasa attachment kwa yanahusiana na yake "title" sifa. 1.1.0 = = * Aliongeza utendaji kuandika upya "title" sifa ya attachment. 1.0.0 = = * Kwanza kutolewa. DownloadVipengele vingine katika jamii hiiKila sehemu ya mwandishi huyuMaoniMara kwa mara kuulizwa maswali na majibuMaliCreated:15 Februari 13, Badiliko la MwishoProgramu Version:WordPress 3.9, WordPress 3.8, WordPress 3.7, WordPress 3.6, WordPress 3.5Files Pamoja:PHPKeywordseCommerce, All Items, picha, vyombo vya habari, kubadili jina, seo, upload, shirika, workflow
| 2017-06-25T15:47:29 |
https://sw.worldwidescripts.net/easy-upload-renamer-for-wordpress-42404
|
[
-1
] |
Viingilio vya mchezo wa Simba na Yanga J2 hivi hapa… – Millardayo.com
Viingilio vya mchezo wa Simba na Yanga J2 hivi hapa…
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetangaza viingilio vya mchezo wa siku ya jumapili kati ya Simba SC na Young African utakaofanyika kwenye dimba la Uwanja wa Taifa kuanzia majira ya saa 10 kamili za jioni.
Tiketi zitaanza kuuzwa kesho (jumamosi) saa 2 kamili asubuhi katika vituo vya, Karume (Ofisi za TFF), Mgahawa wa Steers (Posta Mpya), Oilcom (Buguruni), BigBon (Kariakoo), Olicom (Ubungo), Dar Live (Mbagala), Uwanja wa Uhuru, Kivukoni (Ferry) na Makumbusho (kituo cha mabasi).
Magari yenye vibali maalum ndiyo yatakayoruhusiwa kuingia ndani ya uwanja siku ya jumapili kwa kupitia barabara ya Mandela na Uwanja wa Uhuru, barabara ya Chang’ombe itafungwa kuanzia saa 12 kamili asubuhi.
Aidha, katika mchezo huo TFF itatoa ujumbe maalum kupitia kwa wachezaji kuhamasisha juhudi za Taifa za kuzuia mauaji dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino).
← Previous Story List ya mastaa 10 wa soka matajiri zaidi kwa sasa…
Next Story → Adhabu ya FA dhidi ya wachezaji hawa waliotemeana mate uwanjani…
| 2019-10-17T18:57:45 |
http://millardayo.com/simbayanga-march6/
|
[
-1
] |
Kwa takribani siku nane ambazo mvua za masika zimenyesha mfululizo katika Jiji la Dar es Salaam, athari zilitokea, vikiwamo vifo vya watoto wawili, hivyo funzo tunalolipata ni kuwa mwarobaini ni kuboreshwa kwa miundombinu.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa, tukio la kwanza lilitokea Mei 8, mwaka huu, saa 9:00 alasiri maeneo ya Goba wilayani Kinondoni, ambapo mtoto mmoja alifariki dunia, baada ya kutumbukia kwenye kisima cha futi 30 kilichokuwa wazi nyumbani kwao.
Kamanda Mambosasa alisema mtoto mwingine ambaye anakadiriwa kuwa na umri wa miaka (4-5), alifariki dunia Mei 12, maeneo ya Mongo la Ndege, kwamba mwili wake ulikutwa ukielea katika Mto Msimbazi bila kuwa na jeraha lolote.
Mbali na vifo hivyo, wakazi wa maeneo kadha ya Jiji la Dar es Salaam wameathirika kutokana na nyumba zao kuzingirwa na maji.
Kadhalika, mvua hizo zimesababisha usumbufu mkubwa kwa wakazi wa Jiji kutokana na maji kuathiri miundombinu hususan baadhi ya barabara, hivyo baadhi kufungwa kwa muda, huku baadhi wakikwama kupita kwenye baadhi ya maoeneo kwenda kwenye shughuli zao za ofisi, biashara na za kijamii.
Baadhi ya miundombini ya taasisi iliathirika. Kwa mfano, Kamanda Mambosasa alisema, mvua hizo zimesababisha uharibifu wa baadhi ya majengo ya Shule ya Msingi Mwale iliyopo Kiwalani, Majani ya Chai Kiwalani na Shule ya Sekondari Kibasila iliyopo Manispaa ya Temeke ambayo imejaa maji na kusababisha kushindwa kuendelea na masomo.
Kutokana na hali hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, ametoa tahadhari kwa wakazi wa jiji hilo waishio mabondeni kuhama maeneo yao.
Aliyataja maeneo yaliyofurika ni Jangwani, Magogoni Kigamboni, Ilala Kata ya Mchikichini, Kipunguni, Viwege, Majohe, Kata ya Tabata Madona na Temeke Shule ya Sekondari Kibasila.
Mengine ni Kinondoni Kata ya Kigogo, Tandale, Bunju eneo la Basihaya, Mwananyamala Mitaa ya Bwawani, Kambangwa, Msisiri ‘A’, Mbezi darajani na katikati ya Jiji.
Alisema Serikali inaendelea kuchukua hatua kurekebisha athari zilizojitokeza ili kuwaondolea adha wananchi kwa kuhakikisha mifereji iliyoziba inazibuliwa, kuweka madaraja ya muda pale madaraja yalipoharibiwa na maji, na kurekebisha barabara ili wananchi waendelee na shughuli zao.
Suala la kuboresha miundombimu lina umuhimu wa pekee katika kukabiliana na athari za mara kwa mara pale mvua zinapokuwa zinanyesha.
Hatua hizo zonaweza kuwa ujenzi wa madaraja ya muda katika maeneo ambayo yanakumbwa na mafuriko kama akivyosema Makonda, lakini pia ipo haja ya kujenga madaraja katika maeneo sugu kwa kuathiriwa na mafuriko kama Jangwani ili kurahisishia wananchi usafiri wakati wa mvua.
Tukio la Jumatatu lililowasababishia usumbufu wakazi kadhaa wa jiji na kulazimisha kulipa nauli ya Sh. 1,000 hadi 2,000 kutoka Jangwani hadi Posta na Kariakoo baada ya barabara kujaa maji na kufungwa kwa muda, linapaswa kuchukuliwa kama somo, ili kujengwa miundombimu ya uhakika.
Ushauri wetu ni kuwa pamoja na mamlaka zetu kuwataka wananchi kuondoka katika maeneo ya mabondeni, pia zijishughulishe na kujenga mitaro ya maji katika maeneo mengi yanayoathirika kwa maji na barabara kutokupitika wakati wa mvua, ingawa sio ya mabondeni.
Ni matumaini yetu kuwa hatua za dharura zinaweza kuchukuliwa sasa kutokana na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), kueleza kuwa mvua kubwa za masika zitaendelea kwa siku kadhaa.
Hatua ya kuwafuatilia tembo ina lengo zuri
| 2020-05-28T07:01:19 |
https://www.ippmedia.com/sw/maoni-ya-mhariri/miundombinu-iboreshwe-kuepusha-mafuriko-dar
|
[
-1
] |
PMORALG - Information Centre - News ORODHA YA WALIMU WAPYA NA WALIOKUWA WANAJIENDELEZA ... wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Mhe.Dk.Shukuru Kawambwa ametangaza majina ya walimu ...
Free Download Watch of Wizara Ya Elimu Ma Mafunzo Ya Ufundi ... ... Coloridos Para Amigos A Depoimentos Para Amigas, Hammarton Mudlarks, Comunicare Le Emozioni Un Tempo Per Farlo Si Scriveva Una Lettera, Applehack T35 Com/FBHACKV3, ...
2012-1-19!2!47-17_ajira Mpya Ya Walimu Wa Sekondari - Shahada 2011 ... AJIRA MPYA YA WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI WENYE ELIMU YA SHAHADA MWAKA 2011/12 ... tovuti za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Ofisi ya Waziri Mkuu- TAMISEMI ...
Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Uchaguzi wa nyongeza wa ... Uchaguzi wa nyongeza wa Kidato cha tano 2010 Wizara imeendelea kupanga wanafunzi wa ... 583 S0770/060 AUGUSTINE RAPHAEL SUMVE TARIME PCB 46 S0655/048 AUGUSTINO R MGAYA ...
Kitabu Cha Wasichana 2012 Shule Atokayo jamhuri ya muungano wa. tanzania wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi wanafunzi waliochaguliwa kuingia kidato cha tano, vyuo vya ufundi na chuo cha usimamizi wa maji ...
Kidato, free PDF download NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA. NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF ... Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi. uchaguzi wa nyongeza wa kidato cha tano 2010. s/nexam no ...
Jamii:Dar es Salaam - Wikipedia, kamusi elezo huru Kijitonyama; Kimara; Kimbiji; Kinyerezi; Kipawa; Kisarawe II; Kisutu; Kitunda (Ilala) Kivukoni ... Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii; Wizara ya Ardhi; Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Matokeo ya Ualimu na Ufundi - May 2010 - The National Examinations ... national examinations council of tanzania matokeo ya ualimu na ufundi may 2010. dsee: dte: gatce: gatscce: muka
Website Meta Keywords Wizara Ya Ajira Na Kazi
| 2014-10-02T04:34:16 |
http://www.pulsitemeter.com/WIZARA/WIZARA-YA-ELIMU-NA-MAFUNZO-YA-UFUNDI-AJIRA-MPYA.html
|
[
-1
] |
You are at:Home»Teknolojia»Ndege»Boeing wasimamisha utengenezaji wa ndege za 737 Max
By Mhariri Mkuu December 17, 2019 No Comments
Kampuni ya Boeing imesimamisha utengenezaji wa ndege za 737 Max. Kampuni hiyo imesema kuanzia Januari mwaka 2020 itaacha shughuli zote za utengenezaji wa ndege hiyo ilipigwa marufuku kufanya kazi duniani kote baada ya ajali mbili zilizotokana na matatizo ya kiufundi.
Ndege ya familia ya Boeing 737 Max ilikuwa tayari ndio ndege inayouza sana kwa sasa kutoka kampuni hiyo. Ajali ya kwanza ilikuwa ya ndege ya kampuni ya Lion Air iliyodondoka baharini – Java Sea Oktoba mwaka 2018, wakati bado uchunguzi ukiwa unaendelea ndege ya Ethiopian Airlines nayo ikadondoka ghafla Addis Ababa mwezi Machi mwaka 2019.
Watafiti wanaona Boeing walifanya haraka katika utengenezaji wa ndege hizi bila utafiti wa kutosha kiusalama. Walikuwa na haraka ili waweze kuleta ndege ya kushindana na ndege isiyotumia mafuta mengi kutoka Airbus, A320 Neo.
Ndege hizo mbili zimeua watu 346. Baada ya ajali hizi mbili vyombo vya usimamizi wa safari za anga duniani kote zilipata wasiwasi wa kuendelea kuacha ndege hizo kuendelea kufanya kazi kabla ya uchunguzi mkubwa. Hadi sasa uchunguzi unaonesha kampuni hiyo ilifanya utengenezaji wa haraka ambao haukuzingatia baadhi ya mambo ya kiusalama. Pia hakukuwa na mafunzo mazuri kwa marubani juu ya teknolojia mpya za kwenye ndege hizo zilizokuwa na uwezo wa kumpokonya rubani uwezo wa kufanya mabadiliko ya kiundeshaji dhidi ya progamu ya kompyuta.
INAYOHUSIANA Huawei Mate 20X ya 5G yaingia sokoni
Kwa muda mrefu kampuni ya Boeing imeamini baada ya kufanya mabadiliko na maboresho (yaliyohusisha mabadiliko katika programu ya kompyuta ya kwenye ndege hizo – na hivyo rubani kupewa kipaumbele katika maamuzi ambayo mwanzo programu ya kompyuta ndio ilikuwa juu) basi wangewahi kuruhusiwa kuendelea na mauzo na wateja wao kuendelea kutumia ndege hiyo.
Chombo cha usalama wa anga cha Marekani, tayari kimesema bado hakijaridhisha kuhuruhusu ndege hizo kurudi kazini hivi karibuni.
Ndege za 737 Max zikiwa zimechukua nafasi ya eneo la maegesho ya magari ya wafanyakazi wa Boeing. Bila uwezo wa kuzipeleka kwa wateja wake ndege hizo zimekwama kuondoka kiwandani.
Hadi sasa kampuni ya Boeing ina takribani ndege mia 400 za Max 737 zilizokaa kwenye viwanda vyake tayari kwa kupelekwa kwa wateja. Kama ndege hiyo ikakataliwa moja kwa moja basi itakuwa ni moja ya hasara kubwa zaidi kuwahi kupatikana katika sekta hiyo.
INAYOHUSIANA Windows 10 inatumika katika Vifaa Milioni 300, Kuipata BURE mwisho Julai
Kwa kampuni ya inayoshindana na Boeing, Airbus hiki kimekuwa kipindi ambacho ndege yao inayoshindana moja kwa moja na Max 737, ndege ya 320 neo kuendelea kuangaliwa kama chaguo bora kwa mashirika ya ndege yanayotaka kununua ndege mpya.
Vyanzo: CNN na tovuti mbalimbali
Previous ArticleRCS, Google waanza kusambaza teknolojia mpya ya SMS
Next Article iPhone Hizi Ndio Zinazokubali Teknolojia Ya “Wireless Charging”!
| 2020-04-03T11:43:09 |
https://teknolojia.co.tz/boeing-wasimamisha-utengenezaji-wa-ndege-za-737-max/
|
[
-1
] |
THE SUPERSTARS TZ: AGNESS MASOGANGE AKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA AFRIKA KUSINI Pages
AGNESS MASOGANGE AKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA AFRIKA KUSINI HATIMAYE wale Wanawake wawili walionaswa na madawa ya kulevya Afrika kusini
| 2016-12-06T16:13:13 |
http://thesuperstarstz.blogspot.com/2013/07/agness-masogange-akamatwa-na-madawa-ya.html
|
[
-1
] |
Sintah.Com: IAM BACK LIKE NEVER WENT,ALAMA YA X MOVIE IKO MITAANI GRAB YOUR COPY
IAM BACK LIKE NEVER WENT,ALAMA YA X MOVIE IKO MITAANI GRAB YOUR COPY
nikiwa katika pose na mdau
jlo in the mix
camera man akifuatilia pose za jlo
tino &jlo
jlo nikiwa katika simanzi
alama ya X ni movie ambayo nimeicheza na Tino,nilikaa takribani miaka saba sijacheza movie sasa nimerudi,nilishoot hii movie katika kipindi cha ramadhani ilinipa shida sana coz nilikuwa natoka kazini then naenda location huuu it was a tough week for me
thanks God i managed Behind the scene
screen test sikutaka kula chips nililazimishwa
tukiendelea ku shoot
kama kawa palipo ma celeb lazima tupige picha na wadau wetu
jlo& tino namshukuru Mungu sana kwa kuwa nimemaliza hii kazi,sasa napumua jamani heee,stay tuned for Sintah Europe tour ya movie nyingine hii ni kwa hisani ya watu wa Sweeden thanks and stay blessed
Vp tena swahiba!ulisema hutocheza tena filamu shurti watu wakakubembeleza humuhumu bloguni ukasema never imekuwaje umaarufu umegoma bishoga
jaman thnx for caming back to the move mamy wel came back mdada hope ful utafanya vizur
HATA KM MOVE NZURI MI CTAKUPONGEZA, ULISEMA KUWA HUTAINGIA TENA KWENYE HII MAMBO YA KUACT NINI IMETOKEA?? USIONGEE VITU NA KUAPA HUKU HUWEZI KUTIMIZA HUKO UNAPOFANYA KAZI HULIPWI VIZURI???? MAISHA YAKO YALIKUWA KIMYAAAA KILA M2 ANAKUADMIRE JUU UMEBADULIKA UNARUDI KULE KULE KWENYE KASHFA AM SURE UMEMISSS KUPAMBA MAGAZETI YETU.
OOH MIE SIRUDII KUIGIZA OOOH MIE CJUI NINI KIKO WAPO?????? ACHA PASHAU
SIKUSHAURI HATA KDG UNLESS KM HUKO UNAPOFANYA KAZI HAWAKULIPI VIZURI AND USIJIDAI KM WATU WAMEKUOMBA SN CJUI WAMEKUBEMBELEZA HAKUNA UMETEKA MWENYEWE AFU UMESEMA JUZI UMEPETA KAZI KWA TV HURIDHIKI??? KWANINI UNARUDI KWENYE VITU VITAKAVO KUSHUSHA HADHI???
NAISAPOTI MNO MNO SANAA YA BONGO NA NAPENDA KUANGALIA JUU YA KWAMBA NYINGI HAZINOGI ILA NAANGALIAGA BAADHI. WADADA WA FILAMU BONGO WEEEEENGI WANADHARAULIKA HATA WALIOLEWA WANAJIANIKA MNO MPK HESHIMA INASHUKA. TATIZO NIIII HATA SEHEMU ZA KUJISTIRI WAO WANAJIANIKA NDO ZARAU INAKUJA MPK WATU WANAISI KM WANAJIUZA FILAMUNI SINTA UNARUDI HUKU KULIKOCHAFUAGA MAISHA YAKO???KWELI WATU HAWABADILIKI AND SOON UTAPATA JUMA NATURE MWINGINE
MI NILIZANI BLOG NA IYO KAZI YA TV ULOPATA UMAARUFU UTAPANDA KM ULIKUWA UMEPUNGUA KUMBE BADO UNAONGEZEA???? HAYA NENDA KWENYE MAJUNGU UKO UPAMBE MAGAZETI YETU. HONESTLY SPEAKING KM UMEENDA SHULE KM YAKO NA KAZI NZURI SHUTI UNAMINGO NA WATU WAKUBWA HUWEZI KUFANYA FILAMU HADHI ITASHUKA MIMI NAWAHESHIMU WANAUME TU TENA C WOTE JB,KANUMBA,RAY,CLOUD NA WALE WAZEE WANAWAKE WANAFANYA KAZI NZURI CKATAI HATA KDG ILA MUONEKANO WAO NI MBAYA UNAWAFANYA WAHISIWE MAMBO MABAYA
SEHEMU SIYO YA KICHUPI M2 KAVAA KICHUPI, SEHEMU YA HESHIMA M2 KAVAA HOVYO WAKIACT KIJIJINI WALAI UTAWAPENDA WANAFANYA VIZURO MNOOOOOOOOOOO ILA MJINI YANI CJUI NI KUPANIA HATA SIELEWI LAZIMA WACHEMSHE WANANIUZIIIIIIII NATAMANI KUWAAMBIA JUU MI NAJUA WANAWEZA SASA KUIGA KWA NINI??? WENGINIE MIBONGEEEEEEE MINYAMA KILA MAHALI AFU ANAJIANIKA UNAONA MPK MICHIRIZI ILE SINTA JIANDAE KUZARAULIKA 4 THE 2ND TYM
Hongera sintalicious , unafanya vizuri mama. kwangu mimi napenda sana mtu akihangaikia maisha yake. Jane wa L
uyo aliyeandika comment kwa herefi kubwa ni m2 m1 wala usivunjike moyo kwani maneno yako ni msahafu hayawezi kubadilika jamen tuweni wajasiliamali maisha ni kkt cha muhimu ni kumshauri ushauri mzr na aachane na skendo pindi atakapoingia kwny game
Hii foundation uliyopakwa hapa ndio color yako,uwe unapakaa hii hii,usije paka white zaidi ya hii unaonekana kituko
Hii make up kweli ni nzuri kama mdau alivyoshauri, tunaomba usipake nyingine tumia hii, usije ukakosea kama ile ya kwenye harusi. Hongera sana bi dada na endelea kukamua kama kawaida.
Sintah wewe ni mzuri na ni mzuri kweli nimekuangalia kwenye pics nimekukubali. Nakuomba tu dada kama utapenda kukubali ushauri wangu wa bure na si chuki kama unavyofikiria ila ni kwa ajili ya maendeleo yako baadae, nakuomba ukuze jina lako mwenyewe usipende kuwa second_hand nadhani umenielewa. Jipende mwenyewe na penda watu wakujue kama wewe na utafika mbali.George USA
Asante sana George kwa kuliona hilo hata mimi kwa kweli sijapenda Sinta unavyojiita JLO WA BONGO, jivunie jina na utanzania wako mi nashangaa Wabongo wengi wanajiita majina ya macelebrity wakubwa wa nje kwanini mtu usikuze jina lako lijulikane kote? mfano Judith au LADY JD mbona anajulikana kila mahali. utakuta mtu eti mare KIMORA, KIM KENDRA jamani hayo ni majina walopewa na wazazi wao na wanajivuna nayo hayo yakwenu kwanini mwayadharau? ni hayo tu
| 2017-07-28T02:35:29 |
http://prettysintah.blogspot.com/2011/10/iam-back-like-never-wentalama-ya-x.html
|
[
-1
] |
The CEO Culinary Artist Tanzanian Executive chef Issa Kapande: JIFUNZE KUTENGENEZA MKATE HUU AINA YA PUTO
MKATE HUU NI MWEPESI SANA NA UNAVIMBA UNAKUA KAMA PUTO KIASI FLANI UNAPENDEZA KWANI UNAKUA KAMA MKATE WA MAAJABU KAA TAYARI KWA RECIPE SOON.
1/4 chumvi kijiko kidogo cha chai
120 gram za maji (Usiweke maji yote inaweza zidi hii hutegemea na kiwango cha unga weka maji kidogo kidogo)
Changanya unga na chumvi katika bakuli
Weka maji katika unga kidogo kidogo endelea kukanda
Kanda pole poel mpaka unga wote uchanganyike. Hakikishs maji unaweka kidogo kidogo mpaka unga wote uchanganyike maana kiasi cha maji kitahitajika kutokana na kiwango cha unga. Pia unaweza ongezea kijiko kimoja cha mafuta moto uliyochemsha kwajili ya kuongeza ladha na ubora na uendelee kukanda na mchanganyiko wako usiwe laini sana wala mkavu sana uwe wastan.
Kanda vizuri kwa mara ya mwisho mchanganyiko wako uwe kama unavyoonekana katika picha.
Kisha kata vipande vidogo na zungusha miduara kama inavyoonyesha katika picha ukubwa wa miduara utategemea na ukubwa wa kikaango chako. Hakikisha hupotezi muda kata na sukuma haraka haraka kisha choma ili mkate wako utoke vizuri.
Sukuma kwa saizi ya wastani kama inavyonekana katika picha. Usisukume nyembamba sana zitakakamaa sana na hazitakua nzuri.
Hakikisha unarudia kwa kila miduara yote iliyobaki. Wakati huo huo hakikisha mafuta yanamoto na uanze kukaanga mkate wako.
Kata kipande kidogo cha unga na tupia katika mafuta kuangalia kama mafuta yamepata moto kama mafuta yanamoto kipande hicho kitachemka na kuja juu haraka. Mafuta yawe yamoto lakini sio moto wa kutoa moshi yataunguza mkate wako. Kama ukiweka kwenye mafuta ambayo hayana moto mkate wako utabaki flat na hautavimba na utameza mafuta hautakua mzuri tena.
Baada ya kuhakikisha mafuta yanamoto sasa tupia mkate katika mafuta.
Wakati mkate unapanda juu, Hakikisha unaendelea kumwagia juu ya huo mkate mafuta inasaidia uweze kuvimba.
Kumwagia mafuta inasaidia sana unaona sasa mkate umeshavimba na kupendeza.
Hakikisha una geuza geuza mpaka upate rangi nzuri unayoipenda wewe kahawia ya kawaida au kahawia ya udhurungi.
Weka katika paper towel ili ichuje mafuta. Kama ulikaanga vizuri haita meza mafuta na utakua mzuri sana sana.
Unaweza mpatia mlaji mkate huu na aina yeyote ya chakula utakachopenda au anachopenda. Unaweza mpatia mlaji mkate huu pamoja na Potato Masala (masala ya viazi ulaya) au njegere za nazi. Pia inapendeza sana kusave na sauce za aina mbili mint sauce na tamarind sauce ( Mchuzi wa ukwaju).
MKATE HUU UNAWEZA KULA KWA CHAKULA NA MCHUZI WA AINA TOFAUTI ANGALIA MUONEKANO MZURI WA MKATE HUU KATIKA PICHA TENGENEZA FAMILIA YAKO IFURAHIE SIO KAZI NGUMU.
1/26/2011 08:19:00 PM
i love this blogMariam.
Thursday, January 27, 2011 11:01:00 AM
Halow tupe hicho kitu mapeme lieo na mapishi ya unga wa mchele tuinjoy kesho week edn Ahsante saaaaaaaaaaana mie najifunza mapishi kutoka katika blog yako BIG UP
Friday, January 28, 2011 6:56:00 AM
tuambie mahitaji tukitaka kuupika mkate huo
Monday, January 31, 2011 10:09:00 AM
Kaka shida ni muda au hivyo vitu ni vigumu sana kupika ni wiki sasa tunahamu!!!!Friend
Monday, January 31, 2011 5:23:00 PM
kaka Bado umetoa vitu nusu nusu huo mkate wa PUTO hujamaliza tunafanyaje uwe umekamilika
Wahindi huita huu mkate PULL.mama yangu alinifundsha kutumia maji ya dafu kama unataka uzidi kuwa na ladha nzuuuri na pia ukishaukanda unaweza kuufunika kwa plasticfoil hewa isipite, uuuh ukija kusukuma na kuchoma utapenda mwenyewe!!ni mkate wa rahisi na haraka sana kutengeneza. Asante kaka Issa.tweety
Wednesday, February 09, 2011 7:39:00 AM
Mee too, looh!
Wednesday, February 09, 2011 2:13:00 PM
kaka naipenda sana blog yako, naomba utufundishe jinsi ya kupika biliani. yaani natamani sana kujua hicho kitu.
| 2017-03-30T14:37:16 |
http://activechef.blogspot.com/2011/01/jifunze-kutengeneza-mkate-huu-aina-ya.html
|
[
-1
] |
HEKIMA ZA BADI: Aggrey Mwanri Atimuliwa na Nyoka Kanisani
Aggrey Mwanri Atimuliwa na Nyoka Kanisani
NAIBU Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Aggrey Mwanri
NAIBU Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Aggrey Mwanri, juzi alitimua mbio kunusuru maisha yake pamoja na waumini wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini Usharika wa Sanja Juu Mtaa wa Kilingi, baada ya nyoka kuibuka ghafla kanisani humo.
Tukio hilo la kushangaza lilitokea juzi katika ibada ya saa nne iliyokuwa ikiongozwa na Askofu wa Dayosisi ya Kaskazini, Dk. Martin Shao ya kuweka jiwe la msingi pamoja na harambee ya ujenzi wa kanisa hilo.
Mwanri aliyekuwa mgeni rasmi kwa ajili ya kuendesha harambee hiyo ya ujenzi wa Kanisa la Kilingi, akiwa na mkewe katika meza kuu, aliwashangaza waumini alipokimbia huku na kule akiwa amenyanyua mikono yake. Kutokana na kuibuka kwa nyoka huyo, waumini walikimbizana na kiumbe huyo kwa mawe na viti bila kujali walikuwa ibadani, huku Askofu na wachungaji wengine wakiendelea kusali ambapo waumini walitakiwa kurudisha utulivu katika ibada.
Hata hivyo, jitihada za waumini za kumkimbiza nyoka huyo kutaka kumuua hazikufanikiwa, baada ya nyoka huyo kutoweka na kutooneka tena, jambo lililoacha simulizi ni kwa jinsi gani alifika mahali hapo.
Katika harambee hiyo, alitazamiwa Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, kuwa mgeni rasmi, lakini kutokana na kubanwa na shughuli za sherehe za miaka 35 ya kuzaliwa CCM, alishindwa kufika.
'Habarileo' lilishuhudia Mwanri ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Siha akikimbia huku akitoa sauti kubwa akisema ‘shindwa kwa jina la Yesu wewe shetani, shetani shindwa kwa jina la Yesu,’ huku wageni wengine waalikwa wakianguka chini wakati wakikimbia kujiokoa.
Akizungumza na 'Habarileo', Mwanri alisema tukio hilo ni la kushangaza zaidi, kwani nyoka huyo alipita nyuma ya watu wote, lakini hakuonekana hadi kufika katika meza yake huku akiwa ameweka kichwa chake juu akitema sumu.
“Inashangaza sana kwani lazima ujiulize kalifikafikaje hapo mbele, wakati nyuma yangu kulikuwa na watu wengi...alikuwa na hasira sana kwani alikuwa tayari kung'ata, kwa kweli hadi sasa mimi sielewi ni mambo gani haya,” alisema Mwanri.
Posted by AMANI BILA YA HESHIMA NA KIPATO NI KAZI BURE at Monday, February 06, 2012
| 2018-06-20T09:32:51 |
http://darusi2008.blogspot.com/2012/02/aggrey-mwanri-atimuliwa-na-nyoka.html
|
[
-1
] |
Kagua Packages ya Utalii wa India | Wasiliana nasi kwenye + 91-993.702.7574
Kagua Packages ya Utalii wa India
India ya ajabu - Nchi ya utofauti ni taifa la kupiga kelele na maisha. Pata charm ya kweli ya Uhindi, pamoja na Vipande vya Mchanga Vumbua Vifurushi vya Utalii India. Kila barabara na barabara, pombe na kamba zina na quintessence ambayo haiwezi tu kupotea. Kila jimbo la Uhindi lina utamaduni wake wa kipekee na mila ambayo hutoa roho ya nguvu roho. Hifadhi yetu ya Utalii ya Uhindi ya India inajumuisha kila anasa ambayo unaweza kuitamani. Aina nzuri ya ustawi wa India imesimama kuvuta kwa watafiti kutoka duniani kote. Kuingiza milima ya theluji, maziwa ya ajabu na majini, majumba mazuri, ishara za usanifu za kimapenzi, kuzingatia maisha ya asili na kadhalika ... kila kitu ambacho unaweza kufikiri kuchunguza India, unaweza kufikiri kuchunguza India. Vituo vya Wetu vya Utalii wa Uhindi vinatengenezwa kwa kuchunguza tofauti.
Kihindi cha Hindi kinaweza kuchunguzwa vizuri na kanda.
Kaskazini ya India: Kama marudio ya kusafiri, India Kaskazini ina mengi ya kutoa, yanafaa kutoka kwa vituo vilivyovutia vya kilima hadi mahali pa kidini. Inapatikana na mahekalu ya kale, maziwa ya shimmering, alama za kukumbukwa, maji ya ajabu, North India inalenga tukio la ajabu kwa wageni.
Uhindi wa Mashariki: Eneo la utawala la mamlaka mbalimbali ya zamani, Uhindi ya Mashariki ina utamaduni thabiti wa kikabila na mizizi ya dini. Alama za kihistoria na hekalu nzuri sana, vituo vya vilima na bustani za chai, vikwazo vya maisha ya asili na misitu ya kijani, mito na vijiko visivyo na rangi ni salama bora kwa wasafiri waliokomaa.
Kaskazini Mashariki mwa India: Kidogo cha kuchunguza, ardhi ya siri ya kaskazini mashariki ni halali kuwa mahali pa fumbo kutembelea. Kwa hakika mbinguni haijatambulika. Imefichwa katika mabonde ya mlima yasiyo na msimamo na ya kusonga ya Himalaya, Kaskazini ya Mashariki mwa India ni uchunguzi wa chini, wengine wa kidunia na kusimama kati ya maeneo mazuri sana India.
Uhindi wa Magharibi: Tajiri katika historia, kiroho, aina nzuri na utamaduni, Uhindi Magharibi hutoa mbadala mbalimbali kwa usafiri unaofaa wa kusafiri. Eneo hili linajumuisha mito ya milima yenye kupendeza, vituo vyema vilima vya milima, safari za ustadi, makao makuu ya kifalme ya kifalme, tamaduni zenye nguvu, vituo vya safari, alama za kale na maisha ya asili ya kusisimua.
South India: Uhindi wa Kusini ni ujuzi na kila kitu cha utafutaji wa wageni. Ina vituo vyema vya vilima vilivyovutia, vijiji vya maji, vumbi vya wanyamapori, makaburi ya kihistoria ya kale, mabwawa ya kupendeza, maji ya maji ya kushangaza na maeneo yanayopamba.
Uhindi wa Kati: Uhindi wa Kati, unaojulikana kwa aina mbalimbali za ufanisi, ni kitovu cha maeneo ya wanyamapori na viwanja vya kitaifa. Mbali na wanyamapori, ina nguvu kubwa na makaburi, mikoa ya kikabila, vivutio vya anasa, na maeneo ya kale ya safari; kwa kweli India kuu hutoa kwa wageni wake sahani iliyopangwa ya vivutio.
Chagua yoyote ya yetukuchunguza India Tour Packages kufanya likizo yako ikumbuke.
Ziara ya India Kusini
Uhindi wa Kati
Mashariki ya India India
Kivutio cha Utalii wa Hindi
Ziara ya Kaskazini ya India
Mashariki ya Uhindi ya Uhindi
| 2018-09-20T13:43:45 |
https://sw.sandpebblestours.com/explore-india-tour-packages
|
[
-1
] |
#TWEETS zilizobeba stori zote kubwa mchana wa leo May 2, 2017 – Millardayo.com
#TWEETS zilizobeba stori zote kubwa mchana wa leo May 2, 2017
Twitter ni moja ya mitandao ya kijamii ambayo hutumiwa na watu wengi katika kufikisha habari, taarifa, mawazo na maoni ambapo huwafikia watu wengi kwa wakati mmoja.
Kama ulipitwa na stori kubwa mchana wa leo May 2, 2017 kupitia twitter, basi hauna sababu ya kuwa na wasiwasi zaidi wa kuzikosa kwani nimekukusanyia hapa tweets sita zilizobeba stori kubwa mchana wa leo.
Maafisa wa Korea Kusini wamesema ndege 2 za Marekani za kuangusha mabomu zimefanya mazoezi kwenye anga la rasi ya Korea ili kuwapa taarifa. pic.twitter.com/A2A5pDdLua
— millard ayo (@millardayo) May 2, 2017
Jeshi la Marekani limesema mfumo wake wa THAAD unaotoa kinga dhidi ya makombora umeanza kufanya kazi ya ulinzi nchini Korea Kusini. #BBC pic.twitter.com/KHMXkK152k
Mamlaka inayosimamia vyombo vya habari Sudan Kusini imezifunga ofisi za televisheni ya Al-Jazeera, imetakiwa kutofanya kazi zake nchini humo pic.twitter.com/2uujh1ahWc
Kamati ya Bunge imemsamehe Mwenyekiti wa Kambi ya Upinzani Bungeni Freeman Mbowe baada ya kukiri kutoa kauli za kudharau Bunge April 4, 2017 pic.twitter.com/ZRdW7zgEjd
Himid Mao wa AzamFC ameondoka alfajiri ya Mei 2 kwenda kufanya majaribio ya siku 15 katika timu Randers FC ya Ligi Kuu Denmark. pic.twitter.com/I0oJ1rAPAL
Bunge limeazimia kumsamehe Halima Mdee MB aliyepewa adhabu ya kutohudhuria vikao vya bajeti baada ya Wabunge wa pande zote kumuombea msamaha pic.twitter.com/KTMMBVoNJG
VIDEO: Binadamu mzee zaidi duniani anayepatikana Tanzania. Bonyeza play kutazama…
Related Itemsfacebook Twitter na Inta
← Previous Story Wabunge wamepitisha msamaha juu ya adhabu ya Halima Mdee
Next Story → Alichokisema Bob Manecky kuhusu Studio za Wanene
VIDEO: Shamsa Ford kumsomea Al-badil aliyeiba account yake ya Instagram
Zisikupite Stori kubwa kutoka kwenye Magazeti ya leo April 27 2016
| 2019-03-23T10:24:48 |
http://millardayo.com/twitts25x/
|
[
-1
] |
UTEKAJI MWANZA: Mama asimulia kila kitu Mtoto kutekwa, Mtekaji ataka Mil 3 M-Pesa – Millardayo.com
UTEKAJI MWANZA: Mama asimulia kila kitu Mtoto kutekwa, Mtekaji ataka Mil 3 M-Pesa
Mwishoni mwa August 2017 huko Mwanza kulikuwa na mtoto ambaye ni mwanafunzi wa Darasa la Kwanza mwenye umri wa miaka 8 ambaye alitekwa na mtu asiyefahamika kisha Mama yake akapigiwa simu na Mtekaji huyo akitaka amtumie Tsh Milioni 3 ili arudishiwe mtoto wake.
Ayo TV na millardayo.com zimemtafuta mama huyo ambaye anasimulia mkasa mzima kuanzia mwanzo wa tukio hadi pale alipopata ujumbe kutoka kwa mtekaji uliomtaka atume fedha Tsh Milioni 3 ili amkomboe mtoto wake.
>>>”Kama mama iliniumiza sana. Siku mbili mtoto hajapatikana nyumbani, sikula wala kulala…alinitumia text majira ya saa sita siku hiyo hiyo baada ya kufanya juhudi za kumtafuta tumemkosa, tumeenda kituoni tukaambiwa baada ya saa 24 tukarudi nyumbani.
“Tumekaa mida ya saa sita ndiyo akatuma hiyo meseji kwamba ‘mtoto wako ninaye, tuma hela Milioni 3 tukupe mtoto wako’.” – Mama wa Mtoto.
SHAMBULIZI LA CHUI: Majeruhi asimulia alivyonusurika kuuawa
← Previous Story FURSA 2017!! “Mtu mvivu nitamfukuza” – Dr Tulia baada ya kuzindua Fursa 2017
Next Story → Rais Magufuli atinga Kanisani kwa Wasabato Magomeni, awapa pesa
| 2019-07-16T12:58:44 |
http://millardayo.com/po24x/
|
[
-1
] |
1x14- Crimson Casanova - The Mentalist Image (28791645) - fanpop
This The Mentalist screencap might contain herder, mchungaji, drover, mihogo, casava, muhogo, na kukamata, wanaovuliwa, na kupata, and uvuvi wa kasa usiokusudiwa.
| 2019-09-22T02:04:05 |
http://sw.fanpop.com/clubs/the-mentalist/images/28791645/title/1x14-crimson-casanova-screencap
|
[
-1
] |
Abhishek | ESD | Swahili | Page 8
India imetia saini makubaliano na Shirikisho la Ushirikiano na Maendel...
Wizara ya Maendeleo ya Rasilimali Jumatatu ilisaini makubaliano na Shirikisho la Ushirikiano na Maendeleo ya Uchumi (OECD) kwa Ushirikishwaji wa India katika Mpango wa Tathmini ya Kimataifa ya Wana...
Rais wa Afghanistan ametoa mwito Kwa Kundi la Talibani kuingia katika ...
Rais wa Afghanistan Bw Ashraf Ghani amesema, wafuasi wa Kundi la Talibani wanapaswa kuingilia mazungumzo makubwa na serikali yake. Katika anwani ya kitaifa Jumatatu, Bw Ghani alisema, Taliban lazima ...
Seneta wa Marekani asili wa India Bi Kamala Harris alizindua jitihada ...
Seneta wa Marekani asili wa India Bi Kamala Harris amezindua jitihada zake za urais mwaka 2020. Katika upinzani mbaya wa sera za Rais wa Marekani Bw Donald Trump, Bi Harris Jumatatu alisema Marekani ...
| 2019-07-20T08:00:55 |
http://airworldservice.org/swahili/archives/author/abhishek/page/8
|
[
-1
] |
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Sikilizeni Kero Hii | kero Yako Popote
Home Uncategories Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Sikilizeni Kero Hii
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Sikilizeni Kero Hii
Mimi kama mzazi kero yangu kubwa ni ongezeko la ombaomba hasa watoto wadogo wa kuanzia miaka 4 -13 barabarani tena wakiwa wamebeba watoto wenzao wadogo zaidi yao. Hili ni tatizo na ni aibu kwa Tanzania hasa ofisi husika Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, kama sijakosea ofisi hii inamilikiwa na Mh Sophia Simba ambaye ni mwanamke tena kama sikosei ni mzazi, hivi hili jambo halioni au ndio kulifumbia macho??
Mimi ninachojua wizara kama wizara lazima iwe na fungu la kuwasaidia au kuwafanya hao watoto au ombaomba wasiwepo tena kwenye barabara zetu, kwanza ni risk sana magari yanapita kwa kasi na yanaweza kusababisha hata ajali, hata hivyo vipi suala la watoto kufanyiwa vitendo viovu kama kubakwa na kunajisiwa nyakati za usiku hili waziri halioni au ndio kaziba masikio??. Naamini kabisa fungu lipo tena la kutosha kuwawezesha hawa watu wasiwepo tena mabarabarani.
Sitaki kuamini kwamba wizara imeshindwa kuwaondoa hawa watoto nilichokiona ni kwamba wazazi wa hawa watoto huwa wanakaa sehemu na kuwatuma watoto wao waende kuomba, sasa kama mzazi ni mzima tena anaweza kufanya chochote kwa nini wizara isitunge sheria ya kuwaadhibu hao wazazi wanao watuma watoto kuomba pesa nyakati ambazo wanatakiwa kwenda shule au kuwa mahala salama??
Mh Waziri mwenye mamlaka ya wizara husika jitume kuondoa hili bomu la watoto wa mitaani tunaona ni jinsi gani watoto wadogo wanavyoingia kwenye vitendo viovu na hasa hili janga la makundi ya kigaidi na mengineyo je wakijiunga huko kwa malipo ya chakula na malazi watanzania tutasema wameisaliti nchi? maana baadae lazima watakuja kufanya unyama kwenye nchi wanayotoka, hebu tuache kujibweteka kama unapopewa ofisi basi jitahidi kuifanyia haki na sio vinginevyo.
Mimi kama mzazi nitaendelea kuilaumu ofisi husika maana sioni kama imewajibika vya kutosha kuhusu swala hili.
kwakweli ili limeshakuwa tatizo haswa
| 2017-09-26T21:31:59 |
http://www.keroyako.com/2015/04/wizara-ya-maendeleo-ya-jamii-jinsia-na.html
|
[
-1
] |
www.bongostarlink.com - bongostarlink - domstat.net
mossmo87tehua.hi5.com
shop.hvw.be
dinegen.se
popcelebs.com
beautymits.com
oviedosuena.es
direkfilm.com
last data update: 2011/10/18, 01:01
cable connection (average): 2.35 s
Location: http://www.bongostarlink.com/
Date: Tue, 18 Oct 2011 08:01:51 GMT
Expires: Tue, 18 Oct 2011 08:01:51 GMT
Last-Modified: Tue, 18 Oct 2011 07:52:40 GMT
ETag: "ba5851f2-2f78-4dfe-8d48-c5baa6d0ad3d"
bongostarlink.com A 216.239.34.21 IN 1800
bongostarlink.com A 216.239.36.21 IN 1800
bongostarlink.com A 68.178.232.99 IN 1800
bongostarlink.com A 216.239.32.21 IN 1800
bongostarlink.com MX 50 ASPMX3.GOOGLEMAIL.com IN 1800
bongostarlink.com MX 10 ASPMX.L.GOOGLE.com IN 1800
bongostarlink.com MX 20 ALT1.ASPMX.L.GOOGLE.com IN 1800
bongostarlink.com MX 30 ALT2.ASPMX.L.GOOGLE.com IN 1800
bongostarlink.com MX 40 ASPMX2.GOOGLEMAIL.com IN 1800
bongostarlink.com TXT google-site-verification=G4mYVCRrgYDLJmFP1_WnWTbqBRcWd57QZdlbqMQNv6A Array IN 1800
bongostarlink.com SOA ns51.domaincontrol.com dns.jomax.net 2011101300 28800 7200 604800 86400 IN 43200
bongostarlink.com NS ns52.domaincontrol.com IN 3600
bongostarlink.com NS ns51.domaincontrol.com IN 3600
Request to the server "bongostarlink.com"
HEADER opcode: REQUEST, status: NOERROR, id: 25762
bongostarlink.com. IN ANY
bongostarlink.com. 86400 IN SOA ns51.domaincontrol.com. dns.jomax.net. 2011101300 28800 7200 604800 86400
bongostarlink.com. 3600 IN NS ns51.domaincontrol.com.
bongostarlink.com. 3600 IN NS ns52.domaincontrol.com.
bongostarlink.com. 1800 IN TXT "google-site-verification=G4mYVCRrgYDLJmFP1_WnWTbqBRcWd57QZdlbqMQNv6A"
bongostarlink.com. 1800 IN MX 10 ASPMX.L.GOOGLE.com.
bongostarlink.com. 1800 IN MX 20 ALT1.ASPMX.L.GOOGLE.com.
bongostarlink.com. 1800 IN MX 30 ALT2.ASPMX.L.GOOGLE.com.
bongostarlink.com. 1800 IN MX 40 ASPMX2.GOOGLEMAIL.com.
bongostarlink.com. 1800 IN MX 50 ASPMX3.GOOGLEMAIL.com.
bongostarlink.com. 1800 IN A 68.178.232.99
bongostarlink.com. 1800 IN A 216.239.36.21
bongostarlink.com. 1800 IN A 216.239.32.21
bongostarlink.com. 1800 IN A 216.239.34.21
Received 433 bytes from address 208.109.255.26#53 in 20 ms
HEADER opcode: REQUEST, status: NOERROR, id: 27747
flag: qr aa REQUEST: 1, ANSWER: 13, AUTHORITY: 0, ADDITIONAL: 0
Received 433 bytes from address 216.69.185.26#53 in 14 ms
vongostarlink.com
nongostarlink.com
hongostarlink.com
gongostarlink.com
bingostarlink.com
bkngostarlink.com
blngostarlink.com
bpngostarlink.com
b0ngostarlink.com
b9ngostarlink.com
bobgostarlink.com
bomgostarlink.com
bojgostarlink.com
bohgostarlink.com
bonfostarlink.com
bonvostarlink.com
bonbostarlink.com
bonhostarlink.com
bonyostarlink.com
bontostarlink.com
bongistarlink.com
bongkstarlink.com
bonglstarlink.com
bongpstarlink.com
bong0starlink.com
bong9starlink.com
bongoatarlink.com
bongoztarlink.com
bongoxtarlink.com
bongodtarlink.com
bongoetarlink.com
bongowtarlink.com
bongosrarlink.com
bongosfarlink.com
bongosgarlink.com bongosyarlink.com
bongos6arlink.com
bongos5arlink.com
bongostzrlink.com
bongostsrlink.com
bongostwrlink.com
bongostqrlink.com
bongostaelink.com
bongostadlink.com
bongostaflink.com
bongostatlink.com
bongosta5link.com
bongosta4link.com
bongostarkink.com
bongostarpink.com
bongostaroink.com
bongostarlunk.com
bongostarljnk.com
bongostarlknk.com
bongostarlonk.com
bongostarl9nk.com
bongostarl8nk.com
bongostarlibk.com
bongostarlimk.com
bongostarlijk.com
bongostarlihk.com
bongostarlinj.com
bongostarlinm.com
bongostarlinl.com
bongostarlino.com
bongostarlini.com
ongostarlink.com
bngostarlink.com
bogostarlink.com
bonostarlink.com bongstarlink.com
bongotarlink.com
bongosarlink.com
bongostrlink.com
bongostalink.com
bongostarink.com
bongostarlnk.com
bongostarlik.com
bongostarlin.com
obngostarlink.com
bnogostarlink.com
bognostarlink.com
bonogstarlink.com
bongsotarlink.com
bongotsarlink.com
bongosatrlink.com
bongostralink.com
bongostalrink.com
bongostarilnk.com
bongostarlnik.com
bongostarlikn.com
bbongostarlink.com
boongostarlink.com
bonngostarlink.com
bonggostarlink.com
bongoostarlink.com
bongosstarlink.com
bongosttarlink.com
bongostaarlink.com
bongostarrlink.com
bongostarllink.com
bongostarliink.com
bongostarlinnk.com
bongostarlinkk.com
IP: 216.239.32.21, 216.239.34.21, 216.239.36.21, 68.178.232.99
code weight: 120.3 KB
title: BONGO STAR LINK
BONGO STAR LINK.
Producer Max.
Kifo Jela au Taasis
E-mail address ya Langa
Download here and listen for promo ONLY
Kati ya vitu ambavyo navijaribu kuvifanya ni moja wako hii track ambayo sio track yakupiga radioni bali ni kama ya wadau wote wa BONGO STAR LINK. Hii ni yakwenu ndugu zangu, kaeni mkao wa kula kwa kazi zingine kama Official kwaajili ya radio na video pia, mungu aendelee kutupa uzima tu. Kazi hii nimeifanya pale Mbezi Beach AUTHENTIC STUDIOS chini ya mtu mzima Producer Max.
K-Style, Saju & Gosby
"This track is officially released. The remix of Bomboklat. I called it Kifo Jela au Taasis -- meaning Death, Jails or Institutions -- because when you use drugs you end up in one of those places. The track was produced by Hermy B and video done by Karabani. Please support this song and help me fight drug addiction. I am seven months clean now. Kete moja ni nyingi, kete elfu hazitoshi. Second chance for African addicts. God bless you!!"
Party pple! its Bikini party on Saturday 22 Oct .Get ready 4 Zanzest beach party ever! DJ side aka Pilot will rock u til late, Nonstop beat...Music all around the world.. Its Saturday nite on 22 Oct the roof is on-fire, Don't miss it in Zanzest beach bungalow east n of Zanzibar ...Jambian mfumbwi Entrc/ 5000/ drink as u can .. special buffet at beach age for 20000... Drink and dance til sun rise! Karibu sana
hapa ni katika makazi ya wazee wasiojiweza wanaosumbuliwa na ugonjwa wa ukoma katika kjiji cha Nunge...jana baadhi ya wasanii walipata nafasi hiyo na kuwa nao, pichani ni msanii kutoka THT Ditto akiwa na mzee Chambuso.
Jana nilikuwa pande za Mwanza kuwapa burudani wanavyuo wa Mwanza, nawashukuru sana washkaji wote tuliokura raha na waliojitokeza pale Lips Club
bongo%2Blog.jpg BONGO STAR LINK
skbanner.jpg DJ CHOKA
Shaa.jpg INGIA HAPA KUANGALIA VIDEO.
vote%2Bfor%2BAY.jpg
nyeusi%2Bcopy.jpg
choka.JPG
286803_218666131513353_110576862322281_564315_2574509_o.jpg
DJ+Choka+ft+Saju%252C+Gozby%252C+K-Style%252C+Fred+%2526+Mucky+-+Bongo+Star+Link.jpg
301275_10150885091115525_544075524_21482617_38096624_n.jpg
324821_2394642512870_1455160737_2531173_361441653_o.jpg
Zigua+a.k.a+Big+Z.jpg
291141_10150411623815709_718360708_10670455_479613107_o.jpg
326531_10150411622335709_718360708_10670435_208260587_o.jpg
338472_10150411624110709_718360708_10670459_1601058638_o.jpg
339853_10150411621885709_718360708_10670430_924355070_o.jpg
294654_2298984567288_1629361345_2254992_1453548391_n.jpg
320186_2298195747568_1629361345_2254281_1745553971_n.jpg
AdvertisingMarketing.jpg
entretaiments.jpg
NEW EAST AFRICA SONG.
DJ CHOKA Facebook Fans
FOLLOW DJ CHOKA ON TWITTER
INGIA HAPA KUANGALIA VIDEO.
http://www.bongostarlink.com/feeds/posts/default Posts (RSS)
http://www.bongostarlink.com/feeds/comments/default Comments (RSS)
http://www.bongostarlink.com/2011/10/kagomaz-biography.html Kagomaz Biography
http://www.bongostarlink.com/2011/10/kagomaz-biography.html Read more...
http://www.bongostarlink.com/2011/10/kagomaz-biography.html 6:24 PM
http://www.bongostarlink.com/2011/10/vida-mahimbo-azindua-beachwear.html VIDA MAHIMBO AZINDUA "BEACHWEAR COLLECTION" @ MEDITERRANEO HOTEL.
http://www.bongostarlink.com/2011/10/vida-mahimbo-azindua-beachwear.html Read more...
http://www.bongostarlink.com/2011/10/vida-mahimbo-azindua-beachwear.html 4:56 PM
http://www.bongostarlink.com/2011/10/dj-choka-presents-saju-gozby-k-style.html DJ CHOKA Presents SAJU, GOZBY, K-STYLE, FRED & MUCKY "Bongo Star Link"
http://www.bongostarlink.com/2011/10/dj-choka-presents-saju-gozby-k-style.html Read more...
http://www.bongostarlink.com/2011/10/dj-choka-presents-saju-gozby-k-style.html 4:36 PM
http://www.bongostarlink.com/search/label/dj%20choka dj choka
http://www.bongostarlink.com/search/label/Fred Fred
http://www.bongostarlink.com/search/label/Gosby Gosby
http://www.bongostarlink.com/search/label/K-Style K-Style
http://www.bongostarlink.com/search/label/Mucky Mucky
http://www.bongostarlink.com/search/label/Saju Saju
http://www.bongostarlink.com/2011/10/langas-new-track-kifo-jela-au-taasis.html Langa's new track - Kifo, Jela au Taasis
mailto:[email protected] [email protected]
http://www.bongostarlink.com/2011/10/langas-new-track-kifo-jela-au-taasis.html Read more...
http://www.bongostarlink.com/2011/10/langas-new-track-kifo-jela-au-taasis.html 4:08 PM
http://www.bongostarlink.com/search/label/Langa Langa
http://www.bongostarlink.com/2011/10/rip-dickson-sekwao.html R.I.P DICKSON SEKWAO
http://www.bongostarlink.com/2011/10/rip-dickson-sekwao.html Read more...
http://www.bongostarlink.com/2011/10/rip-dickson-sekwao.html 12:15 AM
http://www.bongostarlink.com/2011/10/new-track-night-crawlers-get-some-spend.html NEW TRACK: NIGHT CRAWLERS - GET SOME SPEND SOME
http://www.bongostarlink.com/2011/10/new-track-night-crawlers-get-some-spend.html Read more...
http://www.bongostarlink.com/2011/10/new-track-night-crawlers-get-some-spend.html 11:10 PM
http://www.bongostarlink.com/2011/10/ungalimi-2-queens.html UNGALIMI 2 QUEENS
http://www.bongostarlink.com/2011/10/ungalimi-2-queens.html Read more...
http://www.bongostarlink.com/2011/10/ungalimi-2-queens.html 10:19 PM
http://www.bongostarlink.com/2011/10/new-track-prezzo-for-sho-for-shizzle.html BRAND NEW TRACK KUTOKA KWA "CMB PREZZO" FEAT: ULOPA- 4 SHO 4 SHIZZY
http://www.bongostarlink.com/2011/10/new-track-prezzo-for-sho-for-shizzle.html Read more...
http://www.bongostarlink.com/2011/10/new-track-prezzo-for-sho-for-shizzle.html 10:08 PM
http://www.bongostarlink.com/search/label/Prezzo Prezzo
http://www.bongostarlink.com/2011/10/new-song-from-sns-records-ny.html New Song From SnS Records-NY ( PLAYEEERRRR !! - ZIGUA a.k.a BIG Z )
mailto:[email protected] [email protected]
http://www.bongostarlink.com/2011/10/new-song-from-sns-records-ny.html Read more...
http://www.bongostarlink.com/2011/10/new-song-from-sns-records-ny.html 9:32 PM
http://www.bongostarlink.com/2011/10/bikini-party.html BIKINI PARTY
http://www.bongostarlink.com/2011/10/bikini-party.html Read more...
http://www.bongostarlink.com/2011/10/bikini-party.html 8:27 PM
http://www.bongostarlink.com/2011/10/tanzania-to-denmark-tour-part-1-fid-q.html Tanzania to Denmark tour Part 1 - Fid Q & Mzungu Kichaa LIVE at Panu
http://www.bongostarlink.com/2011/10/tanzania-to-denmark-tour-part-1-fid-q.html Read more...
http://www.bongostarlink.com/2011/10/tanzania-to-denmark-tour-part-1-fid-q.html 8:06 PM
http://www.bongostarlink.com/2011/10/wazee-wanaoishi-na-ugonjwa-wa-ukoma.html WAZEE WANAOISHI NA UGONJWA WA UKOMA WATEMBELEWA NA WASANII.
http://www.bongostarlink.com/2011/10/wazee-wanaoishi-na-ugonjwa-wa-ukoma.html Read more...
http://www.bongostarlink.com/2011/10/wazee-wanaoishi-na-ugonjwa-wa-ukoma.html 7:50 PM
http://www.bongostarlink.com/2011/10/jiachie-na-camera-ya-djchoka-club-lips.html Jiachie na camera ya DJCHOKA @CLUB LIPS Mwanza
http://www.bongostarlink.com/2011/10/jiachie-na-camera-ya-djchoka-club-lips.html Read more...
http://www.bongostarlink.com/2011/10/jiachie-na-camera-ya-djchoka-club-lips.html 7:06 PM
http://www.bongostarlink.com/2011/10/show-ya-madj-wakongwe-maisha-club.html SHOW YA MADJ WAKONGWE @MAISHA CLUB
http://www.bongostarlink.com/2011/10/show-ya-madj-wakongwe-maisha-club.html Read more...
http://www.bongostarlink.com/2011/10/show-ya-madj-wakongwe-maisha-club.html 9:09 PM
http://www.bongostarlink.com/2011/10/yaliojiri-jana-kwenye-bongo-star-search.html YALIOJIRI JANA KWENYE BONGO STAR SEARCH @Diamond Jubilee
http://www.bongostarlink.com/2011/10/yaliojiri-jana-kwenye-bongo-star-search.html Read more...
http://www.bongostarlink.com/2011/10/yaliojiri-jana-kwenye-bongo-star-search.html 3:42 PM
http://www.bongostarlink.com/search?updated-max=2011-10-15T15%3A42%3A00%2B03%3A00&max-results=200 Older Posts
http://www.bongostarlink.com/feeds/posts/default Posts (Atom)
http://www.bongostarlink.com/ BONGO STAR LINK
http://ay.co.tz/ AY
http://www.bongocelebrity.com/#axzz1ZHKMk5DN Bongo Celebrity
http://bongo5.com/ Bongo5
http://www.cloudsfm.co/ Clouds FM
http://www.diva255.com/ Diva255
http://fullbata.com/ Full Bata
http://g5click.com/ G5 Click
http://www.globalpublishers.info/ Global Publishers
http://gongamx.com/ GongaMX
http://www.hiphopdx.com/ Hip Hop DX
http://www.itsdar.net/ Its Dar
http://noninimusic.com/ Nonini
http://swahilioriginaltz.com/ Swahili Original TZ
http://teentz.com/ Teen TZ
http://tzhiphop.com/ TZ Hip Hop
http://www.u-turn.co.tz/ U-Turn
http://www.worldstarhiphop.com/videos/ World Star Hip Hop
http://8020fashions.blogspot.com/ 8020 Fashions
http://www.abc-otuck.blogspot.com/ ABC-Otuck
http://chiniyacarpet.blogspot.com/ Chini Ya Carpet
http://www.dinamarios.blogspot.com/ Dina Marios
http://www.djfetty.blogspot.com/ DJ Fetty
http://fullshangwe.blogspot.com/ Full Shangwe
http://michuzijr.blogspot.com/ Jiachie
http://www.kabelelejr.blogspot.com/ Kabelelejr
http://kajunason.blogspot.com/ KajunaSON
http://kanumbathegreat.blogspot.com/ Kanumba The Great
http://www.artsfede.blogspot.com/ Katuni Zetu
http://kingkapita.blogspot.com/ King Kapita
http://www.ladyjaydee.blogspot.com/ Lady JayDEE
http://www.mkandamizaji.blogspot.com/ Masanja Mkandamizaji
http://mateja20.blogspot.com/ Mateja 20
http://othmanmichuzi.blogspot.com/ Mtaa Kwa Mtaa
http://mvutokwanza.blogspot.com/ Mvuto Kwanza
http://nuruthelight.blogspot.com/ Nuru The Light
http://pro-24.blogspot.com/ Pro 24
http://raythegreatest.blogspot.com/ Ray The Greatest
http://shaffih.blogspot.com/ Shaffih Sports
http://modotz.blogspot.com/ U-Modo
http://wajanjaclub.blogspot.com/ Wajanja CLUB
http://3.bp.blogspot.com/-T7bMVSIjxaY/TpxH7t10KlI/AAAAAAAAUvA/_YXzthibN_c/s1600/286803_218666131513353_110576862322281_564315_2574509_o.jpg img
http://www.reverbnation.com/kagomaz http://www.reverbnation.com/kagomaz
http://3.bp.blogspot.com/-i6WAMTAWLZ0/TpwylzG4YyI/AAAAAAAAUuA/9rXUrbM2Rck/s1600/1.JPG img
http://2.bp.blogspot.com/-sQ9kuZKDDWw/Tpwym5vx8mI/AAAAAAAAUuI/9djzxumZ2DI/s1600/2.JPG img
http://1.bp.blogspot.com/-w4yhtb2eUI0/TpwynnUB4UI/AAAAAAAAUuQ/p4F89CYO7L0/s1600/3.JPG img
http://1.bp.blogspot.com/-NBLBpDH76Gc/TpwyrQGI7cI/AAAAAAAAUuY/Hyjb6dPWkz4/s1600/4.JPG img
http://3.bp.blogspot.com/-4AIc0GxZWQI/TpwyvXcqb9I/AAAAAAAAUug/sTPQ1oUMvoA/s1600/5.JPG img
http://3.bp.blogspot.com/-83Scfa-2FaU/TpwzJzWtZlI/AAAAAAAAUuo/uzL7Pd0nxdo/s1600/6.JPG img
http://4.bp.blogspot.com/-mo6FfPAvR9g/TpwzSnQqCrI/AAAAAAAAUuw/16smTys1DV4/s1600/7.JPG img
http://2.bp.blogspot.com/-3m421L2k-uY/TpwzT4M9ZBI/AAAAAAAAUu4/dLF0We1f17g/s1600/8.JPG img
http://4.bp.blogspot.com/-jPIm0Yq0iMg/TpwsHK1QE9I/AAAAAAAAUtw/IO-tDXXoiZg/s1600/DJ+Choka+ft+Saju%252C+Gozby%252C+K-Style%252C+Fred+%2526+Mucky+-+Bongo+Star+Link.jpg img
http://hulkshare.com/d82n2epnm723 DJ Choka ft Saju, Gozby, K-Style, Fred & Mucky - Bongo Star Link
http://4.bp.blogspot.com/-pbOw4odxh4o/Tpwu7kKk1eI/AAAAAAAAUt4/Q_w3XULwSuE/s1600/IMG_1108.jpg img
http://1.bp.blogspot.com/-BAsRAxkZreQ/TpwoIJ2MVrI/AAAAAAAAUto/obIKx2Oyga4/s1600/167.jpg img
http://hulkshare.com/cn6bmj646dge Langa - Kifo Jela au Taasisi
http://4.bp.blogspot.com/-MCcTl5T3BdM/TptHUKI2tnI/AAAAAAAAUtQ/ktxIIO4uyNc/s1600/301275_10150885091115525_544075524_21482617_38096624_n.jpg img
http://4.bp.blogspot.com/-m2mz1ChkudY/TptHZR5y_vI/AAAAAAAAUtY/cPIPqW-Rdlc/s1600/DSCN0460.JPG img
http://3.bp.blogspot.com/-mI1BIBTMfEc/TptHa2GOkaI/AAAAAAAAUtg/eskPXsHsV5A/s1600/DSCN0466.JPG img
http://2.bp.blogspot.com/--_06ZBA2qCs/Tps5KqvGSnI/AAAAAAAAUtI/O80fYm2Kbgk/s1600/Downloads2.jpg img
http://hulkshare.com/a057tievpa79 Night Crawlers - Get Some Spend Some
http://3.bp.blogspot.com/-a9tynxTyTbU/Tpst0ikeDeI/AAAAAAAAUtA/atc2SYfQ6aU/s1600/324821_2394642512870_1455160737_2531173_361441653_o.jpg img
http://3.bp.blogspot.com/--5kglNG20bg/TpsqYT2HQrI/AAAAAAAAUs4/ag2EJcQIDsw/s1600/prezzo.jpg img
http://hulkshare.com/4s5bib26i9sw Prezzo - For Sho For Shizzle
http://2.bp.blogspot.com/-qcU-VyDLLFg/TpsilDqXqpI/AAAAAAAAUsw/B-u1gP1gM9c/s1600/Zigua+a.k.a+Big+Z.jpg img
http://www.snsrecordsny.com/ www.snsrecordsny.com
http://2.bp.blogspot.com/-7DPmwxPABdU/TpsTqcUy7jI/AAAAAAAAUso/tZ9EoWaGh_E/s1600/Bikini.jpg img
http://1.bp.blogspot.com/-9NbxUJJmjeA/TpsNVlZh8qI/AAAAAAAAUsI/m19zDrWskhA/s1600/291141_10150411623815709_718360708_10670455_479613107_o.jpg img
http://2.bp.blogspot.com/-k0wTZqqv3Bs/TpsNYxXKarI/AAAAAAAAUsQ/2jTDgVvPwjg/s1600/326531_10150411622335709_718360708_10670435_208260587_o.jpg img
http://2.bp.blogspot.com/-q6scdaAUUcM/TpsNbqiZimI/AAAAAAAAUsY/BFoYPHQStvE/s1600/338472_10150411624110709_718360708_10670459_1601058638_o.jpg img
http://2.bp.blogspot.com/-x3jzqWsFERA/TpsNeX_zsMI/AAAAAAAAUsg/CkYDsmAyn1I/s1600/339853_10150411621885709_718360708_10670430_924355070_o.jpg img
http://3.bp.blogspot.com/-3uzQgDyLOHY/TpsJVwKllaI/AAAAAAAAUr4/QZMZEk_b21M/s1600/294654_2298984567288_1629361345_2254992_1453548391_n.jpg img
http://1.bp.blogspot.com/-R7_GkDp2W9Y/TpsJXOABv-I/AAAAAAAAUsA/1w-Hr8Rrieo/s1600/320186_2298195747568_1629361345_2254281_1745553971_n.jpg img
http://3.bp.blogspot.com/-yrl6BpkdK08/Tpr8mYW3zvI/AAAAAAAAUqA/6vNqudHZ8YA/s1600/1.JPG img
http://3.bp.blogspot.com/-gMGGcbuM8fo/Tpr8n5IlArI/AAAAAAAAUqI/UQQvXe6xS5A/s1600/2.JPG img
http://1.bp.blogspot.com/-SxPUID_F0bA/Tpr8qk1psII/AAAAAAAAUqQ/FHII7jt2aEc/s1600/3.JPG img
http://4.bp.blogspot.com/-cJerrjuj1gg/Tpr83eDycGI/AAAAAAAAUqY/AQ-GFJ8ycdE/s1600/4.JPG img
http://2.bp.blogspot.com/-LpNHHSdo8_c/Tpr84kF4bpI/AAAAAAAAUqg/s_ARPiRnpjo/s1600/5.JPG img
http://1.bp.blogspot.com/-iA5jgBTKY7M/Tpr85c6aOpI/AAAAAAAAUqo/ex-uXf8_iQI/s1600/6.JPG img
http://3.bp.blogspot.com/-B4z29RboknE/Tpr86RFtXLI/AAAAAAAAUqw/zkMgxJR-HvM/s1600/7.JPG img
http://3.bp.blogspot.com/-gtlcqzj7qbs/Tpr87fM2ovI/AAAAAAAAUq4/uogj_mEzggM/s1600/8.JPG img
http://3.bp.blogspot.com/-36h8vyM6QeA/Tpr9AnSk34I/AAAAAAAAUrA/8P7oYPJIrO8/s1600/9.JPG img
http://4.bp.blogspot.com/-9f7BDRfP_yg/Tpr9BbdcBgI/AAAAAAAAUrI/nW958nAkqos/s1600/10.JPG img
http://3.bp.blogspot.com/-RqaX9TCvpsc/Tpr9CXmM7iI/AAAAAAAAUrQ/k4a6FgRrk28/s1600/11.JPG img
http://2.bp.blogspot.com/-3MnKwBDEfSk/Tpr9DDaz2JI/AAAAAAAAUrY/JFCPfJfd1zA/s1600/12.JPG img
http://1.bp.blogspot.com/-O93U_TWvanw/Tpr9ED_0JBI/AAAAAAAAUrg/csz4daiP6_E/s1600/13.JPG img
http://1.bp.blogspot.com/-AZK3b-9f7pU/Tpr9EqgRNtI/AAAAAAAAUro/0r0GNx7ZV1o/s1600/14.JPG img
http://3.bp.blogspot.com/-qUxUDgk3qu4/Tpr9FmMH2HI/AAAAAAAAUrw/JkUFL2N9_dY/s1600/15.JPG img
http://www.blogger.com/comment.g?blogID=1569412817012086223&postID=4924654638940114355&isPopup=true 1 Comments
http://2.bp.blogspot.com/-_9DNdbYVfqA/TpnGAXClONI/AAAAAAAAUpY/6VH0QNKO3Yo/s1600/IMG_5977.JPG img
http://4.bp.blogspot.com/-MfvbUoP3NAw/TpnGDBIO9wI/AAAAAAAAUpg/HYiSMtkTMtE/s1600/IMG_5983.JPG img
http://1.bp.blogspot.com/-0mViH_ToO-s/TpnGHvOMtxI/AAAAAAAAUpo/mHrsmQEWsGU/s1600/IMG_5990.JPG img
http://4.bp.blogspot.com/-tnU-vLp4ed8/TpnGK05-KmI/AAAAAAAAUpw/xVqwc00D5SM/s1600/IMG_5992.JPG img
http://2.bp.blogspot.com/-93zV6RQkQPM/TpnGSVrZEiI/AAAAAAAAUp4/oK80oHiviRM/s1600/IMG_5980.JPG img
http://3.bp.blogspot.com/-guTlxZVbi0o/Tpl6LPNC_YI/AAAAAAAAUnY/91b_scoUCgY/s1600/1.JPG img
http://2.bp.blogspot.com/-7K0qCARaFEI/Tpl6OmUPMtI/AAAAAAAAUng/FNqTCYCdP_g/s1600/2.JPG img
http://2.bp.blogspot.com/-i7S6HpAiHCg/Tpl6S7c7XsI/AAAAAAAAUno/riiqbDOMJfQ/s1600/3.JPG img
http://1.bp.blogspot.com/-4SyioMmIJ2k/Tpl6-CtvosI/AAAAAAAAUnw/HgYK4Z-7EA8/s1600/4.JPG img
http://3.bp.blogspot.com/-46iV6rIx7CM/Tpl7T-0RKWI/AAAAAAAAUn4/AzE9Wof0ixQ/s1600/5.JPG img
http://1.bp.blogspot.com/-69BpkXnUyuc/Tpl7Xe0CqTI/AAAAAAAAUoA/yCZx19Z7eSk/s1600/6.JPG img
http://3.bp.blogspot.com/-5MjcQSqEYoM/Tpl7Z-5zUqI/AAAAAAAAUoI/vUbFBRibn8E/s1600/7.JPG img
http://1.bp.blogspot.com/-CqNjSsNUK0w/Tpl7dq7frlI/AAAAAAAAUoQ/8OYmGOQWkJ4/s1600/8.JPG img
http://4.bp.blogspot.com/-zzyUJY5J9DY/Tpl7f-_pKoI/AAAAAAAAUoY/QhyZu0iVbMM/s1600/9.JPG img
http://3.bp.blogspot.com/-LjXAvSdzxQg/Tpl7kYXo4_I/AAAAAAAAUog/Of1_9YIECag/s1600/10.JPG img
http://2.bp.blogspot.com/-oTF7MYK1U44/Tpl7m-oEZCI/AAAAAAAAUoo/i0lhWX94Zps/s1600/11.JPG img
http://2.bp.blogspot.com/-mQ6RAUkl0bM/Tpl8CIiGcpI/AAAAAAAAUow/ilyUNOF3mKs/s1600/12.JPG img
http://2.bp.blogspot.com/-LXGTTgd_VgE/Tpl8FHPNbjI/AAAAAAAAUo4/vL39_Qd-ofI/s1600/13.JPG img
http://1.bp.blogspot.com/-JAtw4_KTlEk/Tpl8Ha_506I/AAAAAAAAUpA/MdZMWXtG6L4/s1600/14.JPG img
http://1.bp.blogspot.com/-50ySDxs9TDc/Tpl8LrJqTPI/AAAAAAAAUpI/ZfYgy1Ys3aE/s1600/15.JPG img
http://4.bp.blogspot.com/-rdaNs6xQB3Y/Tpl8QWD15yI/AAAAAAAAUpQ/tjlVtETyujs/s1600/16.JPG img
http://www.Tanzanianblogawards.com/ img
| 2019-11-15T18:50:52 |
http://domstat.net/bongostarlink.com.html
|
[
-1
] |
Serikali Yakabidhi Pikipiki 32 kwa Maafisa Elimu Kata Wilayani Moshi | JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Serikali Yakabidhi Pikipiki 32 kwa Maafisa Elimu Kata Wilayani Moshi
Maafisa Elimu kata wakiwa wamevalia kofia ngumu tayari kuanza safari mara baada ya kukabidhiwa pikipiki kwa ajili ya kurahisisha utendaji kazi wao.
← Waziri Kalemani Awatoa Hofu Wananchi Kuhusu Matumizi ya REA
Serikali Yafuta Baadhi ya Tozo za Kikanuni zilizokuwa Zikitozwa na OSHA Kuvutia Wawekezaji →
| 2019-06-17T17:10:50 |
http://blog.maelezo.go.tz/serikali-yakabidhi-pikipiki-32-kwa-maafisa-elimu-kata-wilayani-moshi/
|
[
-1
] |
KINANA, CCM WANAPANGA NJAMA ZA KUMVUA LISSU UBUNGE MAHAKAMANI!!! | Politiksi Kurunzini
Home HABARI POLITIKSI KINANA, CCM WANAPANGA NJAMA ZA KUMVUA LISSU UBUNGE MAHAKAMANI!!!
Dr. Slaa alisema kwamba lengo la njama za Kinana na CCM ni kuhakikisha kwamba Mh. Lissu anafutiwa Ubunge ili asiweze kushiriki katika mchakato wa Katiba Mpya kama mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba litakalojadili na kupitisha rasimu ya Katiba Mpya baadaye mwaka huu. Dr. Slaa alisema: “Kwa kipindi kifupi ambacho amekuwa Mnadhimu Mkuu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Mbunge, Mheshimiwa Lissu amekuwa mwiba mkali kwa CCM na Serikali yake ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano.
Amefumbua macho ya mamilioni ya Watanzania kuhusu masuala makubwa ya kikatiba na kisheria kwa hoja zake Bungeni. Uelewa wake mpana wa masuala hayo na wa Kanuni za Bunge umekuwa kikwazo kikubwa kwa CCM na Serikali yake pamoja na uongozi wa Bunge kupitisha mambo yao kinyume cha sheria, Kanuni za Bunge na maslahi ya nchi yetu. Uwepo wake ndani ya Bunge na ujasiri wake katika kutetea hoja mbali mbali umemzuia Spika wa Bunge na uongozi mzima wa Bunge kuwaonea Wabunge wa Upinzani na hasa CHADEMA. Mtu huyu amekuwa adui mkubwa wa CCM ndio maana Kinana anataka aondolewe Bungeni ili asiwepo kabisa katika mjadala wa Katiba Mpya Bungeni.”
Ijapokuwa rufaa hiyo inaonyesha kufunguliwa na Shabani Itambu Selema na Paschal Marcel Hallu waliokuwa walalamikaji katika kesi iliyotupwa na Mahakama Kuu, Dr. Slaa alidai kwamba watu hao hawahusiki kwa namna yoyote ile na kufunguliwa kwa rufaa hiyo.
“CCM na mawakili wao wanawatumia tu wanakijiji hawa bila hata kuwapa taarifa au kuwashirikisha kwa namna nyingine yoyote. Huyu Shabani Itambu Selema amekula kiapo mahakamani Dodoma kwamba yeye na mwenzake ambaye bado ni Katibu Kata wa CCM huko kwao, hawakuambiwa chochote juu ya kufunguliwa kwa rufaa hiyo. Hawakutoa maagizo yoyote kwa Wakili Wassonga kufungua rufaa kwa niaba yao dhidi ya Lissu; hawajamruhusu Wakili huyo kupinga maamuzi ya Mahakama Kuu iliyoridhika kwamba uchaguzi wa Mbunge Lissu ulikuwa halali; hawajamlipa Wakili Wassonga kwa ajili hiyo. Huyu Wakili anafunguaje kesi au rufaa bila kuambiwa au kulipwa na ‘wateja’ wake? Kama huku sio kukosa maadili ya kiuwakili ni kitu gani?”, amehoji Dr. Slaa.
Kuhusu ushiriki wa Kinana katika sakata hilo, Dr. Slaa alisema kwamba mara baada ya rufaa hiyo kufunguliwa, Wakili Wassonga alimwandikia Katibu Mkuu huyo wa CCM barua yenye kumbu kumbu Na. NO/KM/CCM/01/2013 kwa ajili ya “MADAI YA MALIPO YA AWALI YA SHAURI LA RUFAA KESI YA UCHAGUZI JIMBO LA SINGIDA MASHARIKI SHABANI ITAMBU SELEMA NA MWENZAKE DHIDI YA MH. TUNDU LISSU.” Barua hiyo inamkumbusha Kinana juu ya ‘makubaliano’ kati ya Wassonga Associates Advocates na CCM kuhusu kusimamia kesi ya wanachama hao wa CCM dhidi ya Mh. Lissu ambayo baadae ilitupiliwa mbali na Mahakama Kuu.
“Baada ya shauri husika nilipata maelekezo kutoka kwa wanasheria wa CCM kwamba tukate rufaa Mahakama ya Rufaa kazi ambayo tumekamilisha.” Wakili Wassonga anamweleza Kinana “... katika shauri la mwanzo nilikuwa nalipwa na CCM Singida Mkoa na hawakumalizia malipo.” Barua hiyo imeambatana na hati ya madai ya malipo (invoice) kwa ajili ya ‘malipo ya awali’ ya shilingi milioni mbili.
Dr. Slaa alidai kwamba kazi ya Lissu na wabunge wa CHADEMA ndani ya Bunge inawatisha CCM na Serikali yake ndio maana sasa Kinana anataka Lissu aenguliwe kwa kutumia Mahakama ya Rufaa ya Tanzania. “CCM inatapatapa, Bungeni hapakaliki kwa sababu ya hoja za Lissu na Wabunge wengine wa CHADEMA. Kila siku Bunge linaahirishwa ili kukwepa mijadala mikubwa juu ya matukio muhimu yanayoisibu nchi yetu.
Njama za kuizima CHADEMA kwa kuipunguzia muda wa kuzungumza Bungeni zimeshindikana; mikakati ya kuvuruga hoja za CHADEMA kwa kuingilia hotuba za Kambi Rasmi ya Upinzani na kutaka sehemu za hotuba hizo zifutwe zimegonga mwamba; vitisho vya Spika Makinda na Naibu Spika Ndugai kuwasimamisha wabunge wetu hazijafua dafu. Sasa tuna taarifa kwamba Kinana anataka kuwahonga majaji ya Mahakama ya Rufaa ya Tanzania mamilioni ya fedha ili wamfutie Kamanda wetu Lissu ubunge. Naye atashindwa pia.”
Akizungumzia hati ya kiapo ya Shabani Itambu Selema ambaye alihama CCM na kujiunga na CHADEMA baada ya kesi yao kutupiliwa mbali na Mahakama Kuu mwaka jana, Dr. Slaa amesema:
“Tutaishangaa sana Mahakama ya Rufaa kama itaisikiliza rufaa hiyo hata baada ya aliyekuwa mhusika wa kesi ya msingi kusema kwa kiapo kwamba yeye na mwenzake hawajakata rufaa bali ni mambo ya Kinana na CCM yake!”
Dr. Slaa alisema itakuwa ajabu kwa Mahakama ya Rufaa kusikiliza rufaa iliyofunguliwa zaidi ya mwaka mmoja tangu Mahakama Kuu ilipotupilia mbali kesi ya msingi. “Kwa mujibu wa kifungu cha 115 cha Sheria ya Uchaguzi, Sura ya 343, Mahakama ya Rufaa inatakiwa kusikiliza rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama Kuu ndani ya kipindi cha mwaka mmoja tangu rufaa ilipofunguliwa. Huyu Kinana na CCM yake wamesubiri mwaka umepita tangu Mahakama Kuu ilipokataa kufuta matokeo ya Lissu ndio wafungue rufaa. Kama huku sio kukanyaga spirit ya Sheria hiyo ni kitu gani?”, amehoji Dr. Slaa.
Aliongeza kuwa katika kesi ya Mbunge wa Arusha Mjini (CHADEMA), Mh. Godbless Lema aliyekuwa anashtakiwa na wanaCCM pia, Mahakama ya Rufaa ilipiga marufuku wapiga kura ambao hawakunyimwa haki zao za kupiga kura kufungua malalamiko ya kupinga matokeo ya uchaguzi mahakamani.
“Hata wino wa Mahakama ya Rufaa katika hukumu ya Lema haujakauka Kinana na CCM yake wanataka Mahakama ya Rufaa iyale matapishi yake kwa kusikiliza rufaa ya wapiga kura wanaodai kwa kiapo kwamba walielekezwa na wakubwa wao katika CCM kufungua kesi iliyokataliwa na Mahakama Kuu na sasa rufaa imefunguliwa kwa maelekezo ya Kinana bila hata wao kujulishwa au kushirikishwa kwa namna yoyote ile," amesema Dkt. Slaa.
Dr. Slaa alisema kwamba rufaa ya sasa inathibitisha kauli inayodaiwa kutolewa na Rais Jakaya Kikwete juu ya Tundu Lissu wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu uliopita ambapo Kikwete alidaiwa kuwaambia wanaCCM mjini Singida kwamba ni afadhali Dr. Slaa achaguliwe kuwa Rais kuliko Tundu Lissu kuwa Mbunge.
“Kwa kazi zake ndani na nje ya Bunge Lissu amethibitisha umahiri na uzalendo wake kwa Tanzania na kwa chama chetu. Ametetea wabunge na viongozi wetu dhidi ya njama za CCM kuwachafua kwa kuwafungulia mashtaka ya uongo mahakamani; ametetea Watanzania kila mahali nchini, na ameelimisha wananchi kwa hoja zake Bungeni. Ni mmoja wa Wabunge hodari, jasiri na wachapa kazi katika Bunge hili. Huyu ndiye Mbunge ambaye Kinana na CCM wanataka aondolewe Bungeni kwa mbinu za kishetani za aina hii. Hatutakubali na tunawataka Watanzania wasikubali!”
| 2018-07-17T21:30:27 |
https://arusha255.blogspot.com/2013/05/kinana-ccm-wanapanga-njama-za-kumvua.html
|
[
-1
] |
VIJIMAMBO: RAIS DKT MAGUFULI AENDA KENYA KWA ZIARA YA KISERIKALI YA SIKU MBILI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipokea saluti toka kwa Inspekta jenerali wa Polisi (IGP) Ernest Mangu katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akiwa tayari kwa safari ya kwenda Nairobi, Kenya kwa ziara ya kiserikali ya siku mbili leo Oktoba 31, 2016. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiagana na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akiwa tayari kwa safari ya kwenda Nairobi, Kenya kwa ziara ya kiserikali ya siku mbili leo Oktoba 31, 2016
| 2017-06-24T15:42:37 |
http://lukemusicfactory.blogspot.com/2016/10/rais-dkt-magufuli-aenda-kenya-kwa-ziara.html
|
[
-1
] |
Man United yailaza Barcelona 2-1 - BBC Swahili
Man United yailaza Barcelona 2-1
http://www.bbc.com/swahili/habari/2011/07/110731_manu_barca
Bao la ushindi alilofunga Michael Owen dakika ya 76 liliiwezesha Manchester United kuwalaza mabingwa soka wa bara la Ulaya Barcelona 2-1 katika mchezo wa kirafiki wa kujiandaa kwa patashika za Ligi Kuu, uliofanyika mjini Washington DC.
Image caption Michael Owen baada ya kufunga bao la ushindi
Mbele ya mashabiki karibu 82,000, Nani alitangulia kuipatia Manchester United bao la kuongoza katika dakika ya 22.
Barcelona, ikicheza bila ya Lionel Messi, ilisawazisha katika dakika ya 70 kwa mkwaju wa Thiago Alcantara.
Owen alimiminiwa pande la Tom Cleverley na kupachika bao la ushindi wakati United wakikamilisha ziara ya Amerika Kaskazini na kushinda mechi zake zote tano ilizocheza.
Owen aliandika katika mtandao wa kijamii wa tweeter baada ya mchezo huo: "Kama ilivyo kawaida ya Barca, upande wa upinzani unapata shida sana kumiliki mpira! Na ndivyo ilivyokuwa katika mchezo wa leo! Nashukuru nimefanikiwa kufunga bao."
United walifungwa na Barcelona katika fainali ya Kombe la Ubingwa wa Ulaya katika uwanja wa Wembley mwezi wa Mei, ilionekana mabingwa hao wa soka wa England wakipata nafasi ndogo ya kulipiza kisasi.
Kikosi hicho cha Sir Alex Ferguson kitarejea nyumbani kujiandaa kwa mchezo wa kuwania Ngao ya Jumuia dhidi ya washindi wa Kombe la FA, Manchester City siku ya Jumapili ijayo katika uwanja wa Wembley.
Meneja msaidizi wa Manchester United Mike Phelan alisema: "Mechi ya usiku huu haikuwa ya kuwania kitu chochote. Ilikuwa muhimu kwamba wachezaji tuliowapanga walikuwa wanaelewa nini kinachohitajika unapopambana na timu bora duniani.
Pamoja na Messi kutocheza, Barcelona iliamua kutomchezesha Xavi, Carlos Puyol na Gerard Pique katika kikosi chao kilichoanza.
| 2018-02-24T13:08:24 |
http://www.bbc.com/swahili/habari/2011/07/110731_manu_barca
|
[
-1
] |
(showing articles 34481 to 34500 of 65667)
06/02/17--03:42: _RC PAUL MAKONDA AMK...
06/02/17--03:57: _PSPF YAWAPIGA MSASA...
06/02/17--04:17: _SPIKA NDUGAI AMTOA ...
06/02/17--04:29: _MWIGULU AKABIDHI AM...
06/02/17--04:44: _RAIS DKT. MAGUFULI ...
06/02/17--05:51: _MFUMO WA TAIFA WA T...
06/02/17--06:29: _MAMLAKA YA KUDHIBIT...
06/02/17--07:07: _BRIGEDIA JENERALI F...
06/02/17--07:11: _Kiwanja Kinauzwa - ...
06/02/17--07:14: _wakala wa Vipimo nc...
06/02/17--07:15: _WAZIRI MKUU KASSIM ...
06/02/17--07:38: _Vijana wampongeza R...
06/02/17--07:55: _HALI YA HEWA ILIVYO...
06/02/17--07:55: _BARAZA LA WAGANGA W...
older | 1 | .... | 1723 | 1724 | (Page 1725) | 1726 | 1727 | .... | 3284 | newer
06/02/17--03:42: RC PAUL MAKONDA AMKABIDHI MWENGE WA UHURU RC NDIKILO WA PWANI
06/02/17--03:57: PSPF YAWAPIGA MSASA WASTAAFU WATARAJIWA ZAIDI YA 300 KUTOKA WILAYA ZOTE MKOANI MWANZA
06/02/17--04:17: SPIKA NDUGAI AMTOA NJE NA KUMFUNGIA SIKU SABA MBUNGE WA KIBAMBA JOHN MNYIKA KWA UTOVU WA NIDHAMU
Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai leo ameendelea kuwaadhibu wabunge ambao wamekwenda kinyume na taratibu na ukosefu wa nidhamu baada ya kumuamuru Mbunge wa Kibamba , Mhe. John Mnyika wa CHADEMA kutoka nje ya bunge kwa utovu wa nidhamu.
Spika Ndugai aliamuru walinzi wa Bunge kumtoa nje mbunge huyo na kusema hataruhusiwa kushiriki katika vikao vya bunge kwa siku 7, jambo ambalo limepelekea wabunge wengine wa upinzani kutoka nje ya ukumbi wa Bunge kupinga kitendo hicho.
06/02/17--04:29: MWIGULU AKABIDHI AMBULANCE NA KUSISITIZA LISITUMIKE VIBAYA.
06/02/17--04:44: RAIS DKT. MAGUFULI AFUNGUA KIKAO CHA MAAFISA WAANDAMIZI, MAKAMANDA WA MIKOA NA VIKOSI WA JESHI LA POLISI JIJINI DAR ES SALAAM LEO
06/02/17--05:51: MFUMO WA TAIFA WA TAKWIMU WASAIDIA KUBORESHA TAKWIMU RASMI NCHINI
06/02/17--06:29: MAMLAKA YA KUDHIBITI NA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA YAKAMATA KONTENA MBILI ZA KEMIKALI BASHIRIFU
06/02/17--07:07: BRIGEDIA JENERALI FADHIL OMAR NONDO AJITAMBULISHA KWA RAIS DK.SHEIN
06/02/17--07:11: Kiwanja Kinauzwa - Kigamboni Kibada
06/02/17--07:14: wakala wa Vipimo nchini wahakiki mizani 3,070, matayarisho ya ununuzi wa pamba kwa msimu wa 2017/2018
06/02/17--07:15: WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA ASHIRIKI SALA YA IJUMAA KWENYE MSIKITI WA AL - GADDAF
06/02/17--07:38: Vijana wampongeza Rais Dk. John Pombe Magufuli kwa kushitukia unyonyaji uliokuwepo katika sekta ya Nishati na Madini
06/02/17--07:55: HALI YA HEWA ILIVYOCHAFULEWA LEO BUNGENI
06/02/17--07:55: BARAZA LA WAGANGA WAIOMBA WIZARA YA AFYA KUWAPA ELIMU YA UGONJWA WA EBOLA.
| 2019-12-13T09:40:03 |
http://michuzi2.rssing.com/chan-7007653/all_p1725.html
|
[
-1
] |
Subsets and Splits
No community queries yet
The top public SQL queries from the community will appear here once available.